Kwa lolote utakalolisema leo halitakuwa na faida wala maana zaidi ya upumbavu, uuaji na udanganyifu tena ule unachora usoni pako picha ya ujuha, kukosa uzalendo njaa na kukosa mwelekeo katika maisha. Zaidi ya hapo hakuna mtu atakayekuamini na ndiyo maana hata polisi hawajayafanyia kazi maneno yako.
Mimi sifahamu unachotaka kusema ni kwa masilahi yako na nani. Lakini mtu yeyote mwenye akili timamu ataridhika ukijibu maswali yanayoibuka yakiwemo yafuatayo
1. Wewe Mzee Wangwe amesemekana kapata ajali ukiwa naye wewe. Na kwa hakika wewe ndiye unaufahamu ukweli sahihi, kwa nini hukusema wakati ule ule? Au polisi hawakuwepo?
2. Ni miaka mingi sasa imepita kama kweli wewe ni kiumbe mwenye dhamira safi, uliwezaje kuishi na jambo zito hilo moyoni?
3. Watu wengi wamefanya dhambi za kuwaza na kunena kila mtu alivyohisi. Leo hii utakaposema, utawafungua wengi sana lakini vipi walio kufa na dhambi ya kuwawazia watu mabaya kwa sababu wewe ulificha ukwel?
4. Kuna watu wamegombana na hata kupotezeana utu na hata kuvunja mahusiano yao yaliyokuwa na maslahi na faida kubwa kiasi kwa kuvunjika uhusiano waom maisha yao yameharibika permanently, kwa sababu tu uliwa mislead. Unawafidiaje hawa?
5. Kama unania safi na ya kweli, ulipaswa kwenda kwenye vyombo halali ili ukajisafishe na kuwatengenezea haki zao wanaostahili akiwemo Marehemu Wangwe. Lengo lako la kutaka kuandika hapa ni nini? JF ni mahakama kwamba itatoa tamko la kisheria ili kutoa haki inapostahili?
6. Unachotaka kusema hapa ni kwamba ulipotosha ukweli makusudi. Na hili lazima ni kwa maslahi makubwa sana ambayo uliyaona yanafaida kwako kuliko madhara uliyowasababishia watu wengine. That is inhuman. Na kama hiyo ndiyo tabia yako, kwa nini tusiamini kwamba unakuja na motive ile ile kama ya mwanzo ya kutokuwa mkweli kwa maslahi zaidi?
7. Kitu gani kitatutanabaishia kwamba wakti ule ulificha ukweli kwa sababu ulikuwa mnyama na sasa umekuwa binadamu kwamba utasema ukweli?
8. Wewe siyo minor na wakati ule hukuwa miro. Ninaomba utakalolisema lisikuache, uambatane nalo hadi mwisho wake hata kama ni kwa Divine Justice!. Tumechoka na mazingaombwe.
Salaam!
Kwa muda Mrefu nimekuwa nikipata msukumo unaonitaka kuzungumzia maneno yaliyosambaa mitandaoni na kwenye vyombo vya habari hivi karibuni kutoka kwa ndugu ma makundi mbali mbali.
Kimsingi sintajibu wanayotaka kwa sababu nimeendelea kupokea jumbe za Matusi na kejeli hata kuvamiwa na wanaodai ni wafuasi wa CHADEMA wakitaka niendelee kuwa Kimya!. Wapo walioamua kujitaja majina yao ili nijue ni kiasi gani wako 'Serious' kwenye kile wasemacho!.
Japo nilishatoa taarifa Polisi, kwa sasa nimechoka kuishi maisha ya kuwindwa ndani ya Nchi yangu. Nimechoka. Nitakachofanya ni KUONGEA na si KUJIBU kilichosemwa na yeyote kuhusu Mimi na 'Ajali ya Pandambili'
Naamini kwa Mungu siku zote
Naamini nikifa ni kwa Mpango wake
Nikifa ukweli Utaishi hadi vizazi vijavyo.
Deus Mallya
Dar es Salaam.