Wageni wa 'ghafla' majumbani mwetu.....

Wageni wa 'ghafla' majumbani mwetu.....

Kwanza tabia ya kwenda kushinda kwa watu ni mbaya kweli! Walau mtembeleane kwa 3hrs afu watu waondoke,unless mko close kweli!
Mie nikijiwa na wageni wavamizi inategemea kama nataka kuwa na muda nao,otherwise nawadanganya tuna mualiko very important, na kuwapa muda wa like 1 hrs. Aisee ukiwa hauko kwenye mood ya ku-entertain don't act up! Unless ni mgeni kutoka 1000 kms away na hakua na simu yangu!otherwise sie twajiandaa tutoke or else kama wanafaa kuwaachia nyumba poa.
 
Hapo sasa, kama unatabia ya kukataa wageni sababu ya msosi kinakushuka shu!

Mbona umekamia sana msosi? Ishu siyo msosi tu. Kuna mambo mengine pia kama matumizi ya umeme, maji, na kadhalika.

Binafsi sipingi wageni. Napinga wale wageni wanaokuja bila taarifa. Kumtaarifu mtu kuwa utamtembelea ni ustaarabu ambao hauna gharama yoyote. Au wewe unaona ni vigumu mno kumtaarifu mtu kuwa utamtembelea? Au unaona kuwa ni vibaya?
 
Hapo sasa, kama unatabia ya kukataa wageni sababu ya msosi kinakushuka shu!

RR kuna makabila huwa sijui ni utamaduni wao akikutembelea haji mikono mitupu regardless wewe ni tajiri kiasi gani. Wengine wanafungasha mpaka unamwuliza kulikuwa na haja gani ya kuleta vitu vyote hivi. Wengine ni wajanja wanakusoma mapema wanakuja na vitu ile roho inapenda. Wakati anaondoka utatamani kuwmuliza lini utakuja kututembelea tena? Mgeni njoo mwenyeji apone. lol
 
Samahani sijasoma posters zilizotangulia zote. Mnaongelea ugeni wa ghafla ama ugeni wa kuhamia? Kama mtu anakuja kutembelea kwa sababu maalum kama kazi,ugonjwa n.k. Inaweza isilazimu sana kuja na ndizi na mchele manake ukiangalia bajeti ya one extra head ni zaidi ya hivyo. Ila wa kuhamia nadhani atapata za uso,like let's talk abt ur visit na mipangilio yako...

RR, more than 90% of them huwa wanakuja mikono mitupu....na vijizawadi ambavyo kwa kweli havimalizi hata wiki halafu wanategemea kuwepo kwa mwezi au hata zaidi.
 
Ustaarabu haujalishi mtu unaishi wapi bana. Kwenda tu kwa watu bila kuwapa taarifa mapema si ustaarabu. Binafsi mimi ni mtu private sana na ninaithamini sana privacy yangu. Ukiniibukia tu bila taarifa naona kama umei-invade privacy yangu.

Mmh,na ww privacy ipi hiyo sasa?!ama ndo muda mwingi na maprivacy ya ngono tu!!!
 
RR, more than 90% of them huwa wanakuja mikono mitupu....na vijizawadi ambavyo kwa kweli havimalizi hata wiki halafu wanategemea kuwepo kwa mwezi au hata zaidi.
Hao wakukaa for a long time nao NO, NO, NO! comments zangu hapo juu ni kuhusu wale wanakuja kushinda siku za sikukuu bila taarifa. ila kwa siku zingine, or kwa muda mrefu hapo ni issue tofauti kabisa and I can't compromise on that. Simfukuzi ila naweka wazi kua he can stay for just XXX day(s)
 
Samahani sijasoma posters zilizotangulia zote. Mnaongelea ugeni wa ghafla ama ugeni wa kuhamia? Kama mtu anakuja kutembelea kwa sababu maalum kama kazi,ugonjwa n.k. Inaweza isilazimu sana kuja na ndizi na mchele manake ukiangalia bajeti ya one extra head ni zaidi ya hivyo. Ila wa kuhamia nadhani atapata za uso,like let's talk abt ur visit na mipangilio yako...
Dear tunaongelea wageni wakuja kushinda siku za sikukuu au weekend hivi. Ila hiyo dimention ya wenye kuja kwa siku kadhaa pia inaweza kua explored (with permission ya mtoa maada)
 
Hao ni wastaarabu maana at least walikuwa considerate. Wouldn't you say so?

Which means wakiwa considerate then hawana haja ya kukutaarifu kabala ya kuja? Kwa wale ambao sio wastaarabu unaweza kuwabadili wakawa wastaarabu either kwa kuwaleza kwa maneno au kwa vitendo. Mie akiwa anazuka hasa toka mbali bila taarifa and without anything in their hands, nikiwazukia kwao I carry something in my hands. Ikifanya mara tatu hivyo nexti ataona kuja mikono mitupu so hatakuja kabisa. Japokuwa wako wengine vichwa ngumu.
 
Which means wakiwa considerate then hawana haja ya kukutaarifu kabala ya kuja? Kwa wale ambao sio wastaarabu unaweza kuwabadili wakawa wastaarabu either kwa kuwaleza kwa maneno au kwa vitendo. Mie akiwa anazuka hasa toka mbali bila taarifa and without anything in their hands, nikiwazukia kwao I carry something in my hands. Ikifanya mara tatu hivyo nexti ataona kuja mikono mitupu so hatakuja kabisa. Japokuwa wako wengine vichwa ngumu.

Hapana, kwangu information is paramount and that's why I said 'at least'. Just inform me beforehand that you are going to visit me and I'm good even if you don't bring anything.

Sasa unakuja bila taarifa ukinikuta sipo nyumbani je? Utanisubiri hadi nirudi huku hujui nitarudi saa ngapi? Kuna faida nyingi sana unapomtaarifu mtu kuwa utamtembelea. And it is not that hard! Or is it?
 
Lazma utakua huishi peke yako!hakuna starehe kama unakaa nyumbani kwako na kujifanyia utakavyo bila kuwaza utamkwaza nani! Hata wageni wa kuja toka saa mbili asubuhi ni so invading!
Mmh,na ww privacy ipi hiyo sasa?!ama ndo muda mwingi na maprivacy ya ngono tu!!!
 
Samahani sijasoma posters zilizotangulia zote. Mnaongelea ugeni wa ghafla ama ugeni wa kuhamia? Kama mtu anakuja kutembelea kwa sababu maalum kama kazi,ugonjwa n.k. Inaweza isilazimu sana kuja na ndizi na mchele manake ukiangalia bajeti ya one extra head ni zaidi ya hivyo. Ila wa kuhamia nadhani atapata za uso,like let's talk abt ur visit na mipangilio yako...

Wote tu Dr wale wanaozuka siku za mwisho wa wiki/siku za sikukuu bila taarifa na huja karibu na saa za mlo na wale wanaokuja kama wageni bila taarifa na kutaka kuwepo kwa wiki chache au hata zaidi.
 
Asante kwa kunijuza mamii. Well,unless umealikwa for bfast, for which u arnt expected to stay for lunch, muda mzuri wa kwenda kwa watu baada ya kuwasiliana nao ni saa tisa jioni! Mambo ya kutembeleana saa mbili asubuhi hadi 4 usiku,wageni wakiondoka unaskia homa kwa uchovu!
Dear tunaongelea wageni wakuja kushinda siku za sikukuu au weekend hivi. Ila hiyo dimention ya wenye kuja kwa siku kadhaa pia inaweza kua explored (with permission ya mtoa maada)
 
Wiki chache!? Unless ni ugonjwa ama something really logical, mazungumzo yakinifu yanatakiwa
Wote tu Dr wale wanaozuka siku za mwisho wa wiki/siku za sikukuu bila taarifa na huja karibu na saa za mlo na wale wanaokuja kama wageni bila taarifa na kutaka kuwepo kwa wiki chache au hata zaidi.
 
Wote tu Dr wale wanaozuka siku za mwisho wa wiki/siku za sikukuu bila taarifa na huja karibu na saa za mlo na wale wanaokuja kama wageni bila taarifa na kutaka kuwepo kwa wiki chache au hata zaidi.

BAK ..
natamani nikuone 'uso wako'
wkati wageni wamevamia house yako na vifurushi vyao lol....
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Privacy ni privacy. Kwenda kwa mtu bila taarifa si ustaarabu.

Inategemea. Kwa tamaduni za West and wale wanaozifuata sio ustaarabu kumtembelea mtu even your next door neighbor bila taarifa. Labda ndio maana unakuta mtu amefia na kuozea nyumbani na hakuna anayejua even after a month?

Lakini kwa jamii nyingi za Kiafrika na hasa vijijini hawana utamaduni wa kutoa taarifa kabla ya kumtembelea mtu. Wanaishi as a community, not individually. It is simply their culture that "nyumbani kwangu ni kwako" so hakuna haja ya kutoa taarifa kabla ya kwenda "nyumbani" kwako. Sidhani kama kufanya hivyo ni kukosa ustaarabu.

Sidhani kama nitakuwa mstaarabu zaidi kama nikimtaarifu babu yangu kijijini kuwa nakuja kumtembelea siku fulani. In fact anaweza kunishangaa. Hata kama nikimkosa atakuwa ameacha ufunguo wa nyumba kwa jirani. Na hata kama alisahau kuacha ufunguo nitajibanza kwa jirani yake mpaka arudi.

Sidhani kama jirani zake wataniacha nirudi nilikotoka simply because hayupo. Kwao huo utakuwa sio ustaarabu.
 
BAK ..
natamani nikuone 'uso wako'
wkati wageni wamevamia house yako na vifurushi vyao lol....

hahahahaha lol! we acha tu 🙂🙂....Unarudi home halafu na mambo ya mgao wa umeme na ukosefu wa maji unakuta mtu nne zimezuka bila taarifa zimekuja kutembea zitakuwepo kwako kwa wiki sita, na hawana nauli ya kurudia walikotoka hivyo uanze kujipigapiga kuwatafutia na nauli na pia uongeze bajeti ili kuhakikisha nao wanaongezwa kwenye milo husika ya kila siku hapo nyumbani....halafu ndugu wenyewe si wa karibu kihivyo.
 
mimi nakumbuka tulivyokuwa wadogo
mna arrange na mdingi 'mtoke out after lunch siku za sikukuu'
wakisha kuja wageni ndo imetoka hiyo lol
ni home na kuzurura around the neighbourhood tu....
wageni wa ghafla wanaharibu mipangilio mingi tu...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom