Jamani tuache utani baadhi ya Wabongo (waTanzania) waishio nje ya nchi wanamisifa usipime.
Yaani kama umebahatika kutembelea nchi za UK na USA au nchi zinazofanana na hizo nchi basi
utanielewa ninachotaka kuongelea hapa…wakiwa wabongo kwa wabongo wanapenda sana kuzu
ngumza kiswahili na sana sana wakikutana na mtu wa nyumbani (Tanzania) ambaye amekwenda
au umekwenda kwa shughuli zako maramoja basi ndiyo kabisaaa yaani wakikuona tu wanapenda
sana kuzungumza au kuongea kiswahili na wewe.
Ila cha ajabu na kushangaza mtu huyo huyo au watu hao hao warudipo bongo kuja kusalimia ndugu
au kwa majukumu fulani fulani basi hawataki au hataki kabisa kuzungumza kiswahili na badala yake
anaongea ung'eng'e kuanzia mwanzo hadi mwisho au maneno 10 ung'eng'e na mawili kiswahili.
Sasa mimi najiuliza inakuwaje unapokuwa nchi za ung'eng'e unapenda kuongea lugha ya nyumbani
kwenu Tanzania alafu ukirudi Bongo kwa mapumziko ya wiki mbili au mwezi hutaki kuongea kiswahili.
Ukienda shopperz plaza unajifanya yes no,mlimani city yes no,kwenye daladala yes no ukikutana na
washikaji zako wa kitambo yes no nk nk nk.
Sasa hii yote ni nini? ni ushamba au ndiyo unataka tujue kuwa unatoka USA au Ulaya?
Ama kweli baadhi ya wabongo waishio majuu kwa misifa!!?