Waafrika ndivyo tulivyo?

Waafrika ndivyo tulivyo?

Africans have about 5000 years of evolution to catch up with the rest of the world. Lives of many (I dare say most) Africans today are comparable or worse in quality to the lives of Asians or Europeans 5000 years ago. Of course by quality I am not referring to intangible aspects of life such as happiness but more like general health, diet, life span, material possessions of the general population. The biggest obstacle in overcoming chronic African problems is the low average IQ among Africans (approximately 70 points). Average IQ of 70 points makes it almost impossible to function and compete in the modern world.

Important: It is also good to note that average of 70 IQ points also means that there are many Africans who score well above 70 points and some even fall into the genius category. This is what Dr. James Watson was referring to in his controversial statements.

Ukweli,

If I read you correct, then you are stating to us that "our lower IQ" points is the cause of "ndivyo tulivyo"!

In what terms or criteria of the lower IQ makes us to be "ndivyo tulivyo"? is it on our thinking, life style, hard working, desire to be successful, class room or what?
 
Mzee mwanakijiji,
Mkuu maelezo mazito sana na umegusia sehemu nyingi zinazozungumzia Sivyo tulivyo ktk fikra na pengine matendo ya wale wachache ktk kundi la kondoo. Lakini ktk utawala wa leo utakuta wameajiriwa mbwa maalum kwa kazi ya kuhakikisha kondoo hao wachache pia huishia zizini. Mwisho wa yote sote huingia ktk zizi moja pamoja na jitihada zote ambazo wengi huwa hawaelewi kwa nini Mwanakijiji hapendi kwenda zizini baada ya malisho. Na kwamtazamaji nje ya juhudi zote humwona Mwanakijiji pia akiwa zizini kundi moja na kondoo wengine kiasi kwamba hawezi kuona tofauti.
Jitihada hizi zote hapa JF ni ktk mapinduzi ya Kifikra na ndivyo changamoto analolitoa Nyani Ngabu ktk hatua nyingine, bila shaka ni muhimu ikienda sambamba na fikra za mapinduzi. Pengine yawezekana ndio mwanzo unaotakiwa tukubali kwanza Ndivyo tulivyo ili tuweze sote kupata tiba kwani kuukataa ugonjwa tukiwa ndani ya zizi kwa sababu kuna baadhi kati yetu wana ugonjwa huo wa kuambukiza itakuwa nje ya kutafuta solution. Hapa JF hatupo nje ya zizi mkuu wangu tumo ndani.

Binafsi namwelewa sana Rev. Kishoka na nimekuwa nikijiuliza kwa muda mrefu sana na kama utakumbuka niliwahi sema solution ktk swala la Siasa ni kuwepo kwa Chama kimoja tu - CCM kisha sote tubanane humo humo. Mfumo wa kumchagua rais uwe kama wanavyofanya Marekani leo hii ktk vyama kumpata mgombea sisi iwe ndio imetoka hiyo. Nina hakika kina Salim, JK, Mbowe, Lipumba, Lowassa wote watapata nafasi sawa chini ya mwavuli mmoja kuliko huu utaratibu wa vyama vingi hali kimoja kati yao kimejengwa na Taifa zima.
Ndivyo tulivyo ni utamaduni ambao hutumia scare tactic na hakika mwafrika hasa Mdanganyika anavyoogopa kufa njaa hawezi kuona Chadema ama CUf inaweza vipi kuondoa adha hiyo ikiwa wao kupewa mlo wa siku moja tu imekuwa nongwa, itakuwaje mwaka mzima!
Kumbuka una deal na watu wenye njaa, hayo maswala ya kwenda kulima tumbo halina kitu mkuu wangu watu wengi hawafahamu. Harusi iliyofana husifiwa kwa chakula kilichokuwepo mengine yote ya hotuba na kadhalika (helikopta) ni majivuno ya mwenye nacho kwa Mdanganyika. Huongeza chuki na maseng'enyo kwani ndvyo tulivyo hatupendi maendeleo ya mtu kama yatapitia gharama ama maamuzi yetu hata kama ni kwa faida yetu sisi.
 
Ulemhola nkwingwa?

Nalimhola Nkoi.

nobhese ku detroit huku tulimhola! tuliko tukulyaga mbuta; bhasukuma twitanagaka chengu menule!

Ubing'we pye mule basaji douho, anguh ng'walobela kule... nzhogi khokaya, shokagi gete bagheshi, eliseh leneleh lile bhalindelah !! 🙂


Back to topic....
Hoja nimeipenda, naona Rev. Kishoka ume preempt hoja yangu ya jibu la Dr. Watson. No harm though! Peace bruv!


SteveD.
 
" Mimi ni mzabibu wa kweli, tawi langu lisilozaa nitaliondoa na kulitupa"Yesu Kristo

Je sisi ambao "ndivyo tulivyo" ni tawi lile lisilozaa?
 
" Mimi ni mzabibu wa kweli, tawi langu lisilozaa nitaliondoa na kulitupa"Yesu Kristo

Je sisi ambao "ndivyo tulivyo" ni tawi lile lisilozaa?

Watu wanaoishi jangwani mfano huo hau apply kwao!! I think it is a localised philosophy ya wakati huo...
 
Napenda niukuu ile slogan ya Nyani Ngabu na kuurudisha mjadala ambao ulishafungwa na labda tukipata wakti kuuangalia upya tunaweza kubadili fikira zetu na kuulizana jee sisi ndivyo tulivyo? matendo yetu, tabia zetu, fikira zetu, hulza zetu, utamaduni wetu, kufanya kazi kwetu, kuridhika kwetu, kulalamika kwetu, utegemezi wetu, uvivu wetu?

Jambo lililonisukuma kuanza jiuliza swali hili tena ingawa sikushiriki mjadala uliopita au kupitia kitabu cha Bundala kama kilivyoletwa na Zanaki wa Radio Butiama ni mambo kadhaa na tabia za "kawaida" katika jamii yetu na hata hapa kijiweni.

Wenzetu wazungu, ugumu wa maisha kutokana na hali yeyote, milele umekuwa ni kichocheo cha wao kuwa wachapa kazi, wavumbuzi, watafiti na kuendelea kutafuta suluhisho la matatizo yao au kuongeza ufanisi kupunguza ugumu na makali ya maisha au uchapa kazi. Mafanikio yao si kabisa au kamili (absolute/perfect), lakini husaidia sana kuleta mabadiliko na maendleo katika maisha na jamii zao na hivyo kuendelea kuwa na hali nzuri za maendeleo mpaka tunawanyeyekea na kuwaita "Nchi Matajiri".

Sisi tumedumaa, je ndivyo tulivyo?

Sasa hivi tumeletewa Mjapani yupo Ikulu kutushauri na kutufundisha jinsi ya kuachana na jembe la mkono, je Aisco, UFi, Ushirika, SUA, TFA, Kilimo wako wapi? je hawaoni umuhimu wa kuleta maendeleo na kuleta zana mpya za kuongeza ufanisi na uzalishaji mali mpaka tuletemwe taarishi kutoka Ajemi au Mashariki ya mbali? je sisi ni wavivu wa ubunifu na hatuna wataalamu wa kutosha au ndivyo tulivyo twashukuru kusaidiwa mpaka Chandarua?

Hujuma; ATC, BOT, Richmond, TISCAN na sehemu nyingine, jami tunapiga kelele na kushindana kutoa mapovu, lakini hakuna hata mmoja wetu ambaye yupo tayari kusema ngoja niende mahakamani na kudai haki kama Katiba inavyosema. Tumeachia Serikali "ifanye kazi huku tukiendelea kufaidi kupiga kelele na kutoa matusi na kashfa, "Chenge fisadi, Lowassa mhujumu, Screw Muungwana, Riziwani, Manji, Rostam, Othman, Bangusilo" na majina kibao kulia hujuma, ufisadi, Sisiemu, je hii ndio tabia yetu kuishia kulalama na kuendelea kunyanyaswa? je ni hali yetu ya ndivyo tulivyo inayofanya tuendelee kuhujumiwa?

Wakati wa sakata la maji Chuo Kikuu, niliuliza kwa nini Idara ya Uhandisi pale Chuo isiwe ya kimapinduzi na kufanya utafiti wa kina (utumike kama somo kwa wanafunzi na wapeme maksi kwa kushiriki) na kutafuta suluhisho la uhaba wa maji ambalo limetawala Chuo Kikuu kwa miaka mingi? Majibu yakaja Sisiemu, UDSM sio chuo tafiti, ooh Msola na lawama kibao! Je ndivyo tulivyo?

I would have thought kwamba Idara na wanafunzi wa Uhandisi wangekutana na Chuo cha maji, chuo cha ardhi na idara ya Jiolojia pale UDMS na kusema, jamani tutumie "talanta" (kama in Maryam anavyosema) tutafute mbinu za kuleta maji, iwe ni kuchimba visima, kuweka mabomba ya kiwango fulani, kutengeneza pampu au hata kutumia nyezno zote kutafuta namna ya kutumia lita 10 kupata mafanikio ya kutumia lita 30 za maji(efficiency)! Lakini kama Tulivyo, tunailaumu Dawasco, Azimio, CCM na Mafisadi!

NI lini basi tutaacha kuwa "ndivyo tulivyo"? Je tuna hata nia ya kuachana na dhana na fikira hizo za "Ndivyo Tulivyo"? maana ni mentality ya namna hii imetufanya tuendeleel kuwa tegemezi, kuhitimu katika uvivu, kuendelea kunyonywa na kupunjwa na mwishowe tumeanza kudhulumiana na kutafuna njia panya na za haraka kujipatia marudufu.

Huu Ufisadi, Uhujumu, Uzembe na Kunyonywa kungeendelea kutoea kama tungeamka na kusema "hivi sivyo tulivyo" na kuanza kufanya mambo kwa njia za maendeleo kama Wazungu, Waasia na Wamarekani kusini?

"Ndivyo Tulivyo" wikiendi njema kwenye kupata Kilauri, nyama choma, Ikibinda nkoi na Poozeo la kugombea baa (bamedi kama si changudoa)! Ndivyo tulivyo!

Rev Kishoka:

Nili-draft kitabu cha kumjibu Bundala na niliweka mada fulani hapa hili niweze kujenga hoja fulani lakini kwa kipindi hicho watu walikuwa wamebadilika rangi na kushupalia matukio ya BOT na uFisadi mwingine. Na niliposhindwa kupata Inputs niliweka kazi hiyo pembeni na kuendelea kubeba mabokisi.

Dr. Bundala ni mhandisi na analiangalia tatizo letu kutokana na mtazamo wa maendeleo ya kihandisi au sayansi. Na ukitumia huo mtazamo hakuna kitu kitakachoonyesha nini tumekifanya. Lakini mtazamo huu nao una kasoro zake. Moja ya kasoro hizo ni kuchukua ufahamu wa sayansi au uhandisi kama ufunguo wa matatizo yetu.

Wiki iliyopita katika jarida linaloitwa Discover kuna mtu alizungumza kuhusu Dr. Watson. Baada ya Dr. Watson kutoa mawazo yake, kuna magazeti mbalimbali ya mkondo wa kushoto yaliotoa hoja mbalimbali za kumpinga Dr. Watson. Mwandishi mmoja akawatetea waafrika kwa kusema kuwa Pamoja na waafrika kutokuwa na trick za kufikiri kama wazungu, lakini wanaweza kutumia nguvu zao katika kazi za shamba.

Mwandishi wa Discover akashangazwa kuwa Dr. Watson anayesema kuwa tuna matatizo alifukuzwa kazi lakini yule anayetutetea na kutoa mifano ya kuwa tunaweza kufanya kazi za mitulinga shambani anaendelea kufanya kazi.

Hawa wote wawili kwa namna moja au nyingine wanakutukana. Mmoja anakwambia genetic yako sio nzuri na unakasirika. Na mwingine anakutetea kuwa wewe ni human being lakini kazi zao ni za shambani au kusafisha vyoo.

Na hapa ndipo tunapokuja kwenye mada. Watanzania kwa miaka mingi tunapokea misaada kutoka nchi za Scandinavia na kuna watu wamo humu JF anaoamini kuwa nchi hizi ni kama kaka zetu. Ukweli wa mambo ni kuwa wanatupa misaada kwa kuamini kuwa sisi ni binadamu lakini moyoni mwao hawaamini kuwa tunaweza kufanya vile wanavyofanya wao. Hivyo misaada yao ni kutufanya tuishi kwa amani na kuendeleza kazi zetu za shambani na sio kufikiri zaidi ya hapo.

Na kumjibu Dr. Bundala ni kuwa mazingira yanachangia sana maendeleo ya uchumi na kisayansi ya nchi. Kuna maeneo ambayo naturally yalimpa binadamu advantage ya kuanzisha maendeleo katika kipindi kifupi. Na kuna maeneo ambayo ni hostilities kwa maendeleo ya binadamu. Na hili maendeleo yapatikane katika maeneo hayo, breakthrough fulani ni lazima zipatikane.

Kwa mfano wazungu walipokuwa wanatafuta makoloni Afrika, walitafuta sehemu zenye kuweza kuendesha kilimo. Juhudi zao za mwanzo za kwenda kwenye delta za mto Niger zilikwama kwa sababu ya malaria na walikufa wengi. Na ugunduzi wa KWININI uliwafanya warudi kwa nguvu zote kutawala. Sasa mfikirie mtu ambaye anapambana na Malaria kila siku, je ana muda wa kupata nafasi ya kufikiria technologia zingine?
 
Nyani.
Ulimpinga na kumdhibiti sana Raj Patel enzi hizo kwa ku-advocate huu usemi, lakini naona mwishowe umekuwa muumini wake. Ukiondoa lugha mbaya ya Raj, na badala yake kuangalia substance na arguments za maneno yake, itabidi ukubaliane naye kuwa kuna kitu si sahihi kuhusu sisi watu weusi.

Chief,
Hahahaaaa...unajua hii topic Raj anaiweza kweli..si umemuona karudi kwa jina jingine..

Kaka, nilichokuwa napinga ni lugha yake hususan pale alipokuwa akituita sisi watu weusi wanyama as in terms of not being human beings. But on substance he was/ is absolutely right. Let me also make one thing clear. Just because I say Ndivyo Tulivyo it doesn't mean I say we deserve less than anybody. I just wanted to make that clear because I see some people have gotten the wrong impression.

Kuna watu humu watasema wao Sivyo Walivyo. Maybe that's true. Lakini kwa ujumla ukiangalia jamii zetu sisi watu weusi popote pale tulipo kimaendeleo tuko nyuma sana. Unyuma huu ungekuwa uko isolated ktk baadhi ya nchi au sehemu tu hapo tungeweza kusema labda kuna kitu hao watu hawafanyi sawa ndio maana walivyo jinsi walivyo. Afrika nzima kusini mwa jangwa la sahara inafanana. Kuanzia Ghana hadi Zimbabwe mambo ni yale yale. Exception hapa ni Afrika Kusini....mimi sijui kwa nini Afrika Kusini imeendelea kuliko nchi nyingine za Afrika...labda wewe unajua na kama unajua nisaidie kuelewa maendeleo yao wameyapataje.

Tukiwa tunazungumzia watu binafsi basi hata mimi nitaangukia kwenye kundi la Sivyo Nilivyo. Lakini mimi nazungumzia picha kubwa. Swali lingine la kujiuliza, hivi wengi wetu humu tusingekuwa ughaibuni tungekuwa tunafikiria kama tunavyofikiria sasa hivi?
 
Mzee mwanakijiji,
Mkuu maelezo mazito sana na umegusia sehemu nyingi zinazozungumzia Sivyo tulivyo ktk fikra na pengine matendo ya wale wachache ktk kundi la kondoo. Lakini ktk utawala wa leo utakuta wameajiriwa mbwa maalum kwa kazi ya kuhakikisha kondoo hao wachache pia huishia zizini. Mwisho wa yote sote huingia ktk zizi moja pamoja na jitihada zote ambazo wengi huwa hawaelewi kwa nini Mwanakijiji hapendi kwenda zizini baada ya malisho. Na kwamtazamaji nje ya juhudi zote humwona Mwanakijiji pia akiwa zizini kundi moja na kondoo wengine kiasi kwamba hawezi kuona tofauti.
Jitihada hizi zote hapa JF ni ktk mapinduzi ya Kifikra na ndivyo changamoto analolitoa Nyani Ngabu ktk hatua nyingine, bila shaka ni muhimu ikienda sambamba na fikra za mapinduzi. Pengine yawezekana ndio mwanzo unaotakiwa tukubali kwanza Ndivyo tulivyo ili tuweze sote kupata tiba kwani kuukataa ugonjwa tukiwa ndani ya zizi kwa sababu kuna baadhi kati yetu wana ugonjwa huo wa kuambukiza itakuwa nje ya kutafuta solution. Hapa JF hatupo nje ya zizi mkuu wangu tumo ndani.

Binafsi namwelewa sana Rev. Kishoka na nimekuwa nikijiuliza kwa muda mrefu sana na kama utakumbuka niliwahi sema solution ktk swala la Siasa ni kuwepo kwa Chama kimoja tu - CCM kisha sote tubanane humo humo. Mfumo wa kumchagua rais uwe kama wanavyofanya Marekani leo hii ktk vyama kumpata mgombea sisi iwe ndio imetoka hiyo. Nina hakika kina Salim, JK, Mbowe, Lipumba, Lowassa wote watapata nafasi sawa chini ya mwavuli mmoja kuliko huu utaratibu wa vyama vingi hali kimoja kati yao kimejengwa na Taifa zima.
Ndivyo tulivyo ni utamaduni ambao hutumia scare tactic na hakika mwafrika hasa Mdanganyika anavyoogopa kufa njaa hawezi kuona Chadema ama CUf inaweza vipi kuondoa adha hiyo ikiwa wao kupewa mlo wa siku moja tu imekuwa nongwa, itakuwaje mwaka mzima!
Kumbuka una deal na watu wenye njaa, hayo maswala ya kwenda kulima tumbo halina kitu mkuu wangu watu wengi hawafahamu. Harusi iliyofana husifiwa kwa chakula kilichokuwepo mengine yote ya hotuba na kadhalika (helikopta) ni majivuno ya mwenye nacho kwa Mdanganyika. Huongeza chuki na maseng'enyo kwani ndvyo tulivyo hatupendi maendeleo ya mtu kama yatapitia gharama ama maamuzi yetu hata kama ni kwa faida yetu sisi.

Mkandara bob....wewe na Kishoka nadhani ndio mnanielewa zaidi ya wengi humu ndani. Thanks bro
 
Tukiwa tunazungumzia watu binafsi basi hata mimi nitaangukia kwenye kundi la Sivyo Nilivyo. Lakini mimi nazungumzia picha kubwa. Swali lingine la kujiuliza, hivi wengi wetu humu tusingekuwa ughaibuni tungekuwa tunafikiria kama tunavyofikiria sasa hivi?

Jibu ni hapana, wengi wetu tungelikuwa hivo hivyo kama wenzetu walio wengi ambao tuko nao hapa Bongo/Afrika. Ambao kama utawaambia au kuwauliza kuwa waafrika ndivyo tulivyo, basi watakubali na au kukujibu kwa kusema ni kweli ndivyo tulivyo bila kuonesha au ku argue the other side ya kuwa sivyo tulivyo!!


SteveD.
 
Ninaelewa vizuri kinachojaribu kusemwa na pole pole kwa mbali mmeanza kukipata ninachosema. Nitajaribu kukileta karibu zaidi.

Je Watanzania wote "ndivyo walivyo"? je weusi wote "ndivyo walivyo". Mada hii inasema "Watanzania ndivyo tulivyo" na imedokezea kidogo kuwa "waafrika" ndivyo tulivyo. Ina maana wote? Hili ninalikataa kwani hata wakati wa utumwa si wazungu wote walishughulika na utumwa na si wazungu wote waliamini watumwa siyo binadamu. Wapo katika fikra zao walipinga. Hata kina Jefferson wenyewe waliona ubaya wa utumwa kifikra ingawa na wenyewe walikuwa nao.

Sasa wale ambao wako kwenye kundi la "ndivyo tulivyo" hawawezi kutoka humo na kuanza kutenda na kuleta mabadiliko bila ya kubadilisha fikra zao. Kuna baadhi ya timu huendelea kufungwa na timu nyingi kwa sababu kwenye fikra zao wamekubali kuwa wa ni medebweda! Wachezaji wa timu hiyo licha ya mazoezi na utaalamu wa viungo hawawezi kusonga mbele kwa sababu hawajiamini na wamekubali kuwa wao ndivyo walivyo.

Mwenye macho haambiwi kodoa! Je, watanzania wote wamekubali utawala dhaifu, usio na mwelekeo wa CCM? Je Watanzania wote kwa kukubali "ndivyo tulivyo" wameshindwa kuonesha kupinga kwao hali ilivyo na kuchagua tofauti? Tukisikiliza mawazo ya wateteo "ndivyo tulivyo" tunaweza kushawishika kuamini kuwa hakuna Watanzania wenye kwenda kinyume na status quo.

Niwape mfano; uchaguzi wa 2005 Kigoma Kaskazini chama cha Demokrasia ambacho kilimsimamisha mgombea kijana Bw. Zitto Kabwe kilishinda jimbo hilo kwa Zitto kupata kura 28,198 na mgombea wa CCM kupata kura 21,822. Zitto akashinda kwa kura 6376. Kwa maneno mengine karibu watu thelathin elfu walikataa "ndivyo tulivyo" na leo hii tunakubaliana kuwa walifanya uchaguzi sahihi! Hili hamlioni?

Niwape mfano mwingine; Jimbo la Ubungo mgombea wake ambaye nusura abwagwe na bwana mdogo mwingine Bw. Charles Keenja alishinda jimbo hilo kwa kupata kura 98,473 na mpinzani wake bwana mdogo John Mnyika kupata kura 45,164. Leo hii wangapi mmelisikia jina la Mnyika zaidi kuliko Keenja? Leo sitoshangaa wakazi wengine wa Ubungo ambao walimpigia Keenja wanajuta kufanya uchaguzi huo kwa sababu walikubali mawazo ya "ndivyo tulivyo". Lakini hata kama hakushinda tuna ushahidi wa wazi kuwa watu 45,000 jijini Dar walikataa status quo, walikataa ndivyo tulivyo! kweli hawa hamuwaoni? mnaona wale walioshinda tu?

Hebu tuangalie Moshi Mjini. Mgombea wa Chadema Moshi Mjini mzee Phillemon Ndesamburo alishinda kwa kupata kura 32,025 na yule wa CCM Bi. Elizabeth Minde alipata kura 23,773. Mzee Ndesa alimbwaga kwa kura 8252. Mtu wa kawaida hawezi kuona hilo kwa sababu haamini kuwa wakazi wa Moshi wamekataa "ndivyo tulivyo" na wakaamua kuonesha bila chembe ya shaka kuwa wao sivyo walivyo! Hatuwaoni hawa kwa sababu tunaamini kuwa "ndivyo tulivyo".

Twende Kiteto kwenye uchaguzi huu uliopita. Mgombea wa CCM Bw. Benedict Nangoro alishinda kwa kupata kura 21,506 na mpinzani wake (niliyempigia debe kwa mbali) Bw. Victor Kimesera alipata kura 12,561. Kwa yule anayeamini kuwa "ndivyo tulivyo" yeye anaangalia zile kura 21,506 na kuona watu wamekubali status quo na kwa haraka atasema unaona "mbona Kiteto wameichagua tena CCM". Ingawa anachosema ni kweli lakini anashindwa kuona (a.k.a hataki kuona) kuwa kuna wana Kiteto elfu kumi na mbili hivi ambao wakionesha uhuru wa fikra zao na maamuzi ya kukataa hali "ilivyo" wakaamua kupiga kura kinyume na status quo! Kwanini hawa hamuwaoni kuwa wanaonesha kwa vitendo vyao kuwa "sivyo tulivyo".

Katika mifano hiyo minne utaona kuwa watanzania wenzetu zaidi ya laki moja na kumi na saba elfu wamekataa kuwekwa kwenye kundi la "ndivyo tulivyo". Hawakusema, hawakuimba, na hawakutangazwa magazetini bali kwa vitendo vyao wameonesha kuwa wanaweza kuwa tofauti!

Lakini tuachane na mambo ya kura kwa sekunde chache; Hapa JF tumepata bahati ya kupata taarifa ambazo vyanzo vyake ni ndani ya serikali. Kuna watu serikalini amba wamekataa kabisa kuwa "ndivyo tulivyo" na kutokana na wanayoyaona wameanza pole pole kupinga kwa kuonesha uozi na uchafu serikali. Ripoti zilizokwisha bandikwa na ile itakayobandikwa Jumatatu (kama mipango yao haitabadilika kwa kuamini ndivyo tulivyo) ni ushahidi wa wazi kuwa hata kwenye utumishi wa umma watu wameanza kukataa kwa vitendo "ndivyo tulivyo".

Hawa sitaki kuwakatisha tamaa kuwa "jamani ndivyo tulivyo, kwanini mnafunua mambo haya wakati hakuna lolote litakalobadilika?". Kwanini watu hawa warisk kazi zao, majina yao, na hadhi zao in a loosing battle? Kwanini, tuwatie moyo kufanya na kusimamia mambo ambayo tunajua hayatabadilisha lolote? Kama ndivyo tulivyo, kwanini tunapoteza muda kujadiliana na kukosoa wakati tumeshaamini kuwa "watanzania ndivyo tulivyo"?

If we were to agree to your proposition, we would have fundamentally, agreed to inferiority of mind and purpose. Tutaonekana tumekubali kuwa siyo tu Watanzania hatuwezi kubadilisha, bali pia hatustahili kubadilisha kwa sababu hakuna kati yetu mwenye uwezo wa kubadilisha kitu kwani "wote" ndivyo tulivyo.

Hivyo katika mifano hiyo tunaweza kuhitimisha mambo machache. Kwanza si wote "ndivyo walivyo" kwa sababu tuna ushahidi wa kiimpiriko kuwa kuna zaidi ya watanzania laki moja ambao wamekataa kuichagua CCM. Na pili kama kuna Mtanzania zaidi ya mmoja ambaye ameonesha kuwa hayuko kwenye kundi la "ndivyo tulivyo" basi kauli kuwa "Watanzania ndivyo tulivyo" inadondoka kifudifudi na kuvunja pua!

Kitu ambacho kinanifanya nitangaze pasipo shaka. Bado binafsi niko upande wa wale wote wanaokataa status quo na ambao hawakubali kupiga magoti kwenye altare ya washindwao na ambao wamenyosha mikono ya kusalimu mbele ya wale watubezao kama kina watson!

I categorically and singularly as an individual and part of a movement deny, despise, disagree, reject, unequivocally and perpertually the thoughts, ideas, sentiments, and everything else that says directly or indirectly that I, a black man, born of a black parents or of mixed race in a country called Tanzania that I'm inferior to anybody in the world or in any shape, manner, or form that I'm unequal in dignity, abilities, possibilities and opportunities just because I'm of a difference race or geographic origin. This I denounce without hesitation and unambiguously!

To this, I sign!

M. M. Mwanakijiji on this date of the year of Our Lord March 8th, 2008

And that is my final thought on the subject. Thank your friends!!
 
Ninaelewa vizuri kinachojaribu kusemwa na pole pole kwa mbali mmeanza kukipata ninachosema. Nitajaribu kukileta karibu zaidi.

Je Watanzania wote "ndivyo walivyo"? je weusi wote "ndivyo walivyo". Mada hii inasema "Watanzania ndivyo tulivyo" na imedokezea kidogo kuwa "waafrika" ndivyo tulivyo. Ina maana wote? Hili ninalikataa kwani hata wakati wa utumwa si wazungu wote walishughulika na utumwa na si wazungu wote waliamini watumwa siyo binadamu. Wapo katika fikra zao walipinga. Hata kina Jefferson wenyewe waliona ubaya wa utumwa kifikra ingawa na wenyewe walikuwa nao.

Sasa wale ambao wako kwenye kundi la "ndivyo tulivyo" hawawezi kutoka humo na kuanza kutenda na kuleta mabadiliko bila ya kubadilisha fikra zao. Kuna baadhi ya timu huendelea kufungwa na timu nyingi kwa sababu kwenye fikra zao wamekubali kuwa wa ni medebweda! Wachezaji wa timu hiyo licha ya mazoezi na utaalamu wa viungo hawawezi kusonga mbele kwa sababu hawajiamini na wamekubali kuwa wao ndivyo walivyo.

Mwenye macho haambiwi kodoa! Je, watanzania wote wamekubali utawala dhaifu, usio na mwelekeo wa CCM? Je Watanzania wote kwa kukubali "ndivyo tulivyo" wameshindwa kuonesha kupinga kwao hali ilivyo na kuchagua tofauti? Tukisikiliza mawazo ya wateteo "ndivyo tulivyo" tunaweza kushawishika kuamini kuwa hakuna Watanzania wenye kwenda kinyume na status quo.

Niwape mfano; uchaguzi wa 2005 Kigoma Kaskazini chama cha Demokrasia ambacho kilimsimamisha mgombea kijana Bw. Zitto Kabwe kilishinda jimbo hilo kwa Zitto kupata kura 28,198 na mgombea wa CCM kupata kura 21,822. Zitto akashinda kwa kura 6376. Kwa maneno mengine karibu watu thelathin elfu walikataa "ndivyo tulivyo" na leo hii tunakubaliana kuwa walifanya uchaguzi sahihi! Hili hamlioni?

Niwape mfano mwingine; Jimbo la Ubungo mgombea wake ambaye nusura abwagwe na bwana mdogo mwingine Bw. Charles Keenja alishinda jimbo hilo kwa kupata kura 98,473 na mpinzani wake bwana mdogo John Mnyika kupata kura 45,164. Leo hii wangapi mmelisikia jina la Mnyika zaidi kuliko Keenja? Leo sitoshangaa wakazi wengine wa Ubungo ambao walimpigia Keenja wanajuta kufanya uchaguzi huo kwa sababu walikubali mawazo ya "ndivyo tulivyo". Lakini hata kama hakushinda tuna ushahidi wa wazi kuwa watu 45,000 jijini Dar walikataa status quo, walikataa ndivyo tulivyo! kweli hawa hamuwaoni? mnaona wale walioshinda tu?

Hebu tuangalie Moshi Mjini. Mgombea wa Chadema Moshi Mjini mzee Phillemon Ndesamburo alishinda kwa kupata kura 32,025 na yule wa CCM Bi. Elizabeth Minde alipata kura 23,773. Mzee Ndesa alimbwaga kwa kura 8252. Mtu wa kawaida hawezi kuona hilo kwa sababu haamini kuwa wakazi wa Moshi wamekataa "ndivyo tulivyo" na wakaamua kuonesha bila chembe ya shaka kuwa wao sivyo walivyo! Hatuwaoni hawa kwa sababu tunaamini kuwa "ndivyo tulivyo".

Twende Kiteto kwenye uchaguzi huu uliopita. Mgombea wa CCM Bw. Benedict Nangoro alishinda kwa kupata kura 21,506 na mpinzani wake (niliyempigia debe kwa mbali) Bw. Victor Kimesera alipata kura 12,561. Kwa yule anayeamini kuwa "ndivyo tulivyo" yeye anaangalia zile kura 21,506 na kuona watu wamekubali status quo na kwa haraka atasema unaona "mbona Kiteto wameichagua tena CCM". Ingawa anachosema ni kweli lakini anashindwa kuona (a.k.a hataki kuona) kuwa kuna wana Kiteto elfu kumi na mbili hivi ambao wakionesha uhuru wa fikra zao na maamuzi ya kukataa hali "ilivyo" wakaamua kupiga kura kinyume na status quo! Kwanini hawa hamuwaoni kuwa wanaonesha kwa vitendo vyao kuwa "sivyo tulivyo".

Katika mifano hiyo minne utaona kuwa watanzania wenzetu zaidi ya laki moja na kumi na saba elfu wamekataa kuwekwa kwenye kundi la "ndivyo tulivyo". Hawakusema, hawakuimba, na hawakutangazwa magazetini bali kwa vitendo vyao wameonesha kuwa wanaweza kuwa tofauti!

Lakini tuachane na mambo ya kura kwa sekunde chache; Hapa JF tumepata bahati ya kupata taarifa ambazo vyanzo vyake ni ndani ya serikali. Kuna watu serikalini amba wamekataa kabisa kuwa "ndivyo tulivyo" na kutokana na wanayoyaona wameanza pole pole kupinga kwa kuonesha uozi na uchafu serikali. Ripoti zilizokwisha bandikwa na ile itakayobandikwa Jumatatu (kama mipango yao haitabadilika kwa kuamini ndivyo tulivyo) ni ushahidi wa wazi kuwa hata kwenye utumishi wa umma watu wameanza kukataa kwa vitendo "ndivyo tulivyo".

Hawa sitaki kuwakatisha tamaa kuwa "jamani ndivyo tulivyo, kwanini mnafunua mambo haya wakati hakuna lolote litakalobadilika?". Kwanini watu hawa warisk kazi zao, majina yao, na hadhi zao in a loosing battle? Kwanini, tuwatie moyo kufanya na kusimamia mambo ambayo tunajua hayatabadilisha lolote? Kama ndivyo tulivyo, kwanini tunapoteza muda kujadiliana na kukosoa wakati tumeshaamini kuwa "watanzania ndivyo tulivyo"?

If we were to agree to your proposition, we would have fundamentally, agreed to inferiority of mind and purpose. Tutaonekana tumekubali kuwa siyo tu Watanzania hatuwezi kubadilisha, bali pia hatustahili kubadilisha kwa sababu hakuna kati yetu mwenye uwezo wa kubadilisha kitu kwani "wote" ndivyo tulivyo.

Hivyo katika mifano hiyo tunaweza kuhitimisha mambo machache. Kwanza si wote "ndivyo walivyo" kwa sababu tuna ushahidi wa kiimpiriko kuwa kuna zaidi ya watanzania laki moja ambao wamekataa kuichagua CCM. Na pili kama kuna Mtanzania zaidi ya mmoja ambaye ameonesha kuwa hayuko kwenye kundi la "ndivyo tulivyo" basi kauli kuwa "Watanzania ndivyo tulivyo" inadondoka kifudifudi na kuvunja pua!

Kitu ambacho kinanifanya nitangaze pasipo shaka. Bado binafsi niko upande wa wale wote wanaokataa status quo na ambao hawakubali kupiga magoti kwenye altare ya washindwao na ambao wamenyosha mikono ya kusalimu mbele ya wale watubezao kama kina watson!

I categorically and singularly as an individual and part of a movement deny, despise, disagree, reject, unequivocally and perpertually the thoughts, ideas, sentiments, and everything else that says directly or indirectly that I, a black man, born of a black parents or of mixed race in a country called Tanzania that I'm inferior to anybody in the world or in any shape, manner, or form that I'm unequal in dignity, abilities, possibilities and opportunities just because I'm of a difference race or geographic origin. This I denounce without hesitation and unambiguously!

To this, I sign!

M. M. Mwanakijiji on this date of the year of Our Lord March 8th, 2008

And that is my final thought on the subject. Thank your friends!!

Nakuunga mkono kwa kuyaweka wazi mawazo yako Mkjj, ila kuna moja nitakuja nalo ambalo ni more holistic kwani linajumisha baadhi ya binadamu wa asili nyingine pia, katika hilo naomba uchangie maana naona umeanza kuweka ultimatums za kiaina.. lol
 
The coloniser's mentality:WAAFRIKA NDIVYO WALIVYO
The colonized's mentality:WAAFRIKA NDIVYO TULIVYO.
Laiti waliopigania kufika hapa tulipo wangekuwa na attitudes za kuchoka namna hiyo,basi wengi wetu tusingekuwa hapo tulipo sasa (talking of you guys mlio nje).Maana,kama tungeafikiana na mkoloni kuwa sie ndivyo tulivyo,basi tusingepata uhuru (utafsiri kwa mtzamo wako),na kama tusingepata uhuru basi nyie wote mliopo hapa JF mkichangia kutoka ughaibuni mngekuwa ni watoto wa machifu wanaoshiriki kwenye indirect rule.Bado,mnasema ndivyo tulivyo!?

Ndivyo mlivyo?Mbona mna mawazo tofauti na yale yanayopigiwa kelele?Mbona hamtetei ifisadi,kama ndivyo mlivyo?We are not homogenious guys,we vary because we differ.Mtizamo wa Mmakonde uko shaped kwenye historia yake ambayo kiaina flani ni tofauti na Mchagga ambaye Mkoloni alipendezewa na weather ya mahala hapo,akajenga shule lukuki,hospitals,etc.Sivyo tulivyo,kwa maana hatukuumbwa kuwa hivi bali kwa sababu moja au nyingine ndio tunajikuta tunajiuliza maswali kama haya.Hata hivyo kujiuliza "hivi mie ni mjinga?" is not the same as ku-concede kuwa "kwa hakika mimi ni mjinga".

Nimalizie kwa kusema,labda AKINA FLANI NDIVYO MLIVYO,wala sio mie.Mmefika nchi za watu,mmeona historia ngumu walizopitia hadi kufika hapo walipo,lakini hamtaki kujifunza wamefikaje hapo,mna-resign na attitude ya kushindwa kwamba ndivyo tulivyo!I wish Aborigines wangesikia habari hizi,au genuine civil right acitivists (wale walioonja adha ya utumwa,na sio hawa wanaotafuta ulaji) wangetuhurumia laiti wangesikia "kilio" hiki.

Ni uzembe wa hali ya juu kuwa na mawazo kama haya tukiwa huru,ilhali Mandela alipokuwa gerezani hakuamini kuwa "weusi ndivyo walivyo...yaani wao ni tabaka la kupelekeshwa"

Kwa Watanzania wenzangu mnaoamini kwenye ukweli kwamba mabadiliko ni kwa hatua,then tukumbuke kuwa tulipata uhuru 1961,hata nusu karne haijafika tangu tuwe huru.Tukifanya reference kwenye historia ya mabadiliko duniani,tutagundua kuwa wote waliofanikiwa hawakuwa na fikra stagnant kwamba hapo walipo ndipo wanapopaswa kuwa.Watumwa hawakukubali kuwa wanapaswa kuwa watumwa milele,ndio maana leo tuna akina Condi hapo WH,na Obama running for the Dem's ticket.Akina John Barnes wangekubali kuwa nafasi ya mtu mweusi katika soka ni ushangiliaji tu,basi tusingekuwa na akina Ashley Cole,Rio Ferdinand,David James,etc na kama Lewis Hamilton angeamini kuwa kazi ya mtu mweusi ni kuosha tu magari,BASI asingefika hapo.

Na kama "Waafrika ndivyo tulivyo",so what?Tusubiri kifo?Tusisome?Tusije JF?Anayedhani Waafrika/watz ndivyo walivyo,hilo lake,by the way huo ni uhuru wa mawazo...mie binafsi naangalia wapi nilipotoka,wapi nilipo na wapi naenda,na naamini kuna wenzangu chungu mbovu wanaofanya inventory kama hiyo na kugundua kuwa change is possible.Nyie mlio "wazima" mkiwa na mawazo hayo,je walioathirika na majanga kama ukimwi nao wafikirie nini?Pamoja na kutopatikana tiba,watafiti na wagonjwa bado wana matumaini kuwa iko siku...na sio "ndivyo tulivyo".Hope should be the last thing to lose,guys....especially katika age hii tuliyonayo (40s in independence,20s-40s kwa most members,na vigezo vingine)
 
Nakuunga mkono kwa kuyaweka wazi mawazo yako Mkjj, ila kuna moja nitakuja nalo ambalo ni more holistic kwani linajumisha baadhi ya binadamu wa asili nyingine pia, katika hilo naomba uchangie maana naona umeanza kuweka ultimatums za kiaina.. lol

no huwa naona mbali kuwa tofauti hiyo ya mawazo haiwezi kubadilika sasa kuendelea kuzungumzia kitu ambacho najua siwezi kubadili mawazo kwa sababu hakuna hoja yenye nguvu naona ni kutumia muda wangu sivyo vilivyo. Ila of course kama kuna hoja zaidi ya kuwa sisi ni "weusi na watanzania" niko macho kuiangalia. Nimejifunza kukubali kutofautiana na kuendelea na mambo mengine. Ultimatum, what altimatum? LOL!
 
Mimi ningependa kufahamishwa ni kitu gani ambacho ni particular kwa waafrika ambacho hao wengine hawana? Wizi, uvivu, uzinzi, uzembe, uoga, kupenda rushwa n.k? Nini hasa tunachozungumzia hapa? Kutuambia tukuthibitishie kuwa sivyo tulivyo ni kuwa 'disingenuous' maana lazima katka jamii yeyote atapatikana mtu au watu watakao'disprove' chochote nitakachosema.

Miaka ya 1800s, mtu mweusi hakuruhusiwa kupigana masumbwi kwa sababu walidai wakubwa kuwa huyo mtu mweusi hana uwezo huo wa kupigana kiufundi. Wakina joe jackson wakawathibitishia kuwa sio hivyo. Leo wanatushitaki waafrika kwa kusema tumeumbwa kuwa wanamasumbwi.

Mpaka 1950s walisema mtu mweusi hawezi kuwa mrembo wa marekani. Kuna vijana wengi weusi waliuawa marekani kwa kuambiwa kuwa walimwangalia vibaya, walimpigia mluzi mwanamke mweupe kwa hiyo walikuwa wana nia ya kumbaka kwa sababu NDIVYO watu weusi walivyo.

Hao wakina Watson na wengine wanaosema kuwa I.Q. za waafrika ziko chini walitumia vigezo gani? Kuna hata mmoja wao anayeweza ku'survive hata siku mbili katika mazingira ya wahadzabe? Kuna hata mmoja wao anawajua tabia na mienendo ya wanyama kama hao wahadzabe? wana haki gani basi kuwaona hawa kuwa ni primitive kwa sababu hawajawahi kuiona monitor ambayo haitawasaidia lolote katika mazingira yao?

Nyani Nguba swali lako ni kama lile ambalo wagiriki wa kale walilokuwa wakiwauliza wakristu, " Kama huyo Mungu wenu ni muweza vyote, je anaweza kuumba jiwe asiloweza kubeba?" Kama ni jinsi unavyoamini, kuwa wewe umeumbwa inferior na watu wengine hakuna kitu tutakachokuambia kitakachobadili msimamo wako.
 
Mzee Mwanakijiji,
Hata wazungu naweza sema Ndivyo Walivyo lakini ktk objective manner maanake hao waliopinga Utumwa hawakufanya lolote kuhakikisha unakwisha as a fact walikuwa na mtumwa akifanya kazi majumbani mwao za kuosha nguo ama kulima wakidai wanam treat kama ndugu yao.. Uongo mtupu. Kwa hiyo walifikiria kuwa wao sio Ndivyo Walivyo lakini waliishi kama ndivyo walivyo na pengine ndio shina la maendeleo yao wakati sisi ndio dimbwi la umaskini wetu.
Na ndio maana hadi leo kina Livingstone ni sehemu ya historia yao na wanaipokea kwa mikono miwili.
 
Hii dhana ya kwa vile Ndivyo Tulivyo basi sisi ni inferior sijui mmeitoa wapi. Haina maana hata kidogo kama wewe ndivyo ulivyo basi uko chini zaidi ya watu wengine kwenye mambo ya msingi. Ndivyo Tulivyo kwangu mimi ni dhana inayoelezea uwezo wa jamii nzima kutawala mazingira yake na si watu binafsi au watu wachache ktk jamii na mafanikio yao kimaisha.

Halafu hii mifano ya kisiasa wala haileti maana yoyote. Hao watu waliowachagua wagombea wa CCM na wenyewe wanaweza wakawanyooshea vidole watu wa upinzani na kusema wapinzani ndivyo walivyo na hawaelewi nini kinachoendelea.

Maisha ya jamii za kiafrika au watu weusi kwa kweli bado yako nyuma kiujumla ukilinganisha na jamii zingine bila sababu yoyote ile ya msingi kwa mtazamo wangu. Hivi mmejiuliza ni kwa nini? Niwape mfano mmoja au miwili. Nianze na usafi. Pale Kipawa kuna magenge na mama ntilie kibao. Katika eneo hilo hilo kuna majalala na mitaro ya maji machafu iliyoziba na kusababisha harufu mbaya. Iwe asubuhi, mchana au jioni utakuta watu kibao wamefunga kwa hao mama ntilie wakipata msosi. Hivi ni kwa nini watu wale chakula ktk mazingira kama hayo? Yaani watu kwa umoja na ujumla wanashindwa kuhakikisha angalau mazingira ya panapopikwa chakula ni masafi? Jamani hivi ni mimi tu nionaye kwamba kwenye jambo kama hili hatuhitaji chama chochote cha kisiasa kuja kutusafishia?

Aisee nina mambo kibao ninayoweza kuyataja hapa lakini ngoja ninyamaze tu maana anayetaka kukubali na akubali atayekataa na akatae. Ukweli uko palepale.
 
Hii dhana ya kwa vile Ndivyo Tulivyo basi sisi ni inferior sijui mmeitoa wapi. Haina maana hata kidogo kama wewe ndivyo ulivyo basi uko chini zaidi ya watu wengine kwenye mambo ya msingi. Ndivyo Tulivyo kwangu mimi ni dhana inayoelezea uwezo wa jamii nzima kutawala mazingira yake na si watu binafsi au watu wachache ktk jamii na mafanikio yao kimaisha.

Halafu hii mifano ya kisiasa wala haileti maana yoyote. Hao watu waliowachagua wagombea wa CCM na wenyewe wanaweza wakawanyooshea vidole watu wa upinzani na kusema wapinzani ndivyo walivyo na hawaelewi nini kinachoendelea.

Maisha ya jamii za kiafrika au watu weusi kwa kweli bado yako nyuma kiujumla ukilinganisha na jamii zingine bila sababu yoyote ile ya msingi kwa mtazamo wangu. Hivi mmejiuliza ni kwa nini? Niwape mfano mmoja au miwili. Nianze na usafi. Pale Kipawa kuna magenge na mama ntilie kibao. Katika eneo hilo hilo kuna majalala na mitaro ya maji machafu iliyoziba na kusababisha harufu mbaya. Iwe asubuhi, mchana au jioni utakuta watu kibao wamefunga kwa hao mama ntilie wakipata msosi. Hivi ni kwa nini watu wale chakula ktk mazingira kama hayo? Yaani watu kwa umoja na ujumla wanashindwa kuhakikisha angalau mazingira ya panapopikwa chakula ni masafi? Jamani hivi ni mimi tu nionaye kwamba kwenye jambo kama hili hatuhitaji chama chochote cha kisiasa kuja kutusafishia?

Aisee nina mambo kibao ninayoweza kuyataja hapa lakini ngoja ninyamaze tu maana anayetaka kukubali na akubali atayekataa na akatae. Ukweli uko palepale.

Kwa hiyo kimsingi dhana yako ya "ndivyo tulivyo" doesn't carry or imply any negative connotation? Kwa hiyo inaweza kuwa ni positive trait siyo?
 
Kwa hiyo kimsingi dhana yako ya "ndivyo tulivyo" doesn't carry or imply any negative connotation? Kwa hiyo inaweza kuwa ni positive trait siyo?

Could be both...

If I say Africans are more gregarious than whites because that is just the way they are....is that a good or bad thing?
 
Back
Top Bottom