Waafrika ndivyo tulivyo?

Waafrika ndivyo tulivyo?

NN, hivi kile kilichotokea Dodoma hukukiona?... yaani huoni dalili za watu kukataa kwa vitendo mawazo ya "ndivyo tulivyo"? hatujafika tunakotaka kufika na labda itachukua muda kidogo lakini vitendo vya watu kukataa mazoea hayo vimeanza kuonekana. Sasa siwezi kushangaa wengine inachukua muda kidogo kuona na ndio maana wengine inabidi tuvae contacts kuongeza uwezo wetu wa kuona. So, give it time my friend..


I wish ingekuwa hivi ndugu yangu. Lakini kuna kila dalili kwamba kilichotokea Dodoma ni kwa ajili yao sio kwa ajili yetu sisi wananchi. Hatuna cha kushangilia pale na wala hakuna dalili ya mwanga pale zaidi ya sisi kuliwa. Tatizo moja kubwa sana tulilonalo watanzania ukilinganisha na wenzetu ktk Afrika yetu hii ni wepesi mno wa kuridhika na kudanganywa hasa na viongozi wetu. Tena Kikiwete ndio katupata hasa, anafanya blunder lukuki halafu anafanikiwa kuisawazisha kwa mzaha rahisi kabisa, basi nasi twamchekelea kama mazuzu, hapa ndipo ninapokubaliana na NN kwamba Ndivyo Tulivyo until further notice!
 
I wish ingekuwa hivi ndugu yangu. Lakini kuna kila dalili kwamba kilichotokea Dodoma ni kwa ajili yao sio kwa ajili yetu sisi wananchi. Hatuna cha kushangilia pale na wala hakuna dalili ya mwanga pale zaidi ya sisi kuliwa. Tatizo moja kubwa sana tulilonalo watanzania ukilinganisha na wenzetu ktk Afrika yetu hii ni wepesi mno wa kuridhika na kudanganywa hasa na viongozi wetu. Tena Kikiwete ndio katupata hasa, anafanya blunder lukuki halafu anafanikiwa kuisawazisha kwa mzaha rahisi kabisa, basi nasi twamchekelea kama mazuzu, hapa ndipo ninapokubaliana na NN kwamba Ndivyo Tulivyo until further notice!

Kaka Kitila unanichekesha sana siku hizi...Loh!!

On a serious note, huu mjadala kwa kweli ni mzuri na naomba watu wasinielewe vibaya kwa kung'ang'ania kusema ndivyo tulivyo. You never know...this may very well bring the best out of us....
 
Ikitokea kwamba tumeelewana lugha na mjapan, website hii itawasaidi wale wanao taka kununua matrekta mtumba toka hapa Marekani.

http://www.tractorhouse.com/listing...ERGUSON&guid=F98150D505734447AF39832D1B8F4AC6

Mengine bei zake zimo ndani ya uwezo wetu tulio wengi.

Sasa sijui ile sheria ya kuzuia mitumba yenye uzee wa zaidi ya miaka 10 ni kwa magari tu au hata kwa matrekta, ndege, Mashine za umeme kama za RDC, meli na vichwa vya train?

Pikipiki je?

Maana kuna vichwa vya train toka India ni vya mwaka 1890.
http://www.tractorhouse.com/listing...mdl=250&guid=F98150D505734447AF39832D1B8F4AC6
 
Mtaji mkubwa wa kupiga hatua yoyote ile hapa duniani ni matatizo.

Udhaifu wetu Watanzania ni moja kati ya matatizo makubwa yanayo tukabiri kama taifa pia kama jamii ya watu.

Tunatakiwa kutumia udhaifu wetu kama reference ya kutafuta na kutengeneza njia sahihi za kuondoka hapa tulipo na kusonga mbele.

Kila tatizo kwa kawaida huja likiwa na package ya solution, wakati mwingine huwa na solution zaidi ya moja.

Solution nyingi ziambatanazo na tatizo kwa kawaida huwa ni zile ambazo hatuzikubali, hatuko tayari kuzichukua kama ushauri na kibaya zaidi ni ile tabia ya kuzipiga vita ili kudumisha kawaida.

Kwa mfano tatizo la mmomonyoko wa udongo unaosababishwa na over grazing huja na solution ya kupunguza mifugo au kufanya zero grazing.
Wafugaji wangapi wako tayari kwa solution hizo?

Tatizo la uchafu utokanao na uingizaji wa bidhaa toka mashambani huja na solution ya kudesign reusable packaging.
Nani yuko tayari kwa ufumbuzi kama huo?

Msongamano wa Mgari na tatizo la usafiri katika mji wa Dar huja na solution ya kupiga marufuku Town basi za abiria chini ya 60.
Au kutandaza light truck kwaajili ya light eletric train

Solution kama hizi zitawafagia wote wenye vipanya na Coastal wangapi wapo tayari kwenda na solution hiyo?

Tukiongelea matatizo na ufumbuzi wake tunaongelea kuachana na kawaida tuliyo izoea ili kutoa nafasi ya kuendeleza aina nyingine ya utaratibu tusio uzoea. Kwa asili binadamu wote tunapenda kufanya jambo tulilo lizoea kuliko lile ambalo ni geni.

Kutatua tatizo lolote maana yake ni kukubali kubadirika wewe kama mtu binafsi, kama familia na kama jamii. Hili si tu, suala la kuwaambia viongozi wabadirike, ni suala la kuiambia jamii nzima ikubali kubomoa ukale na kuvaa upya.

Maandishi yetu mengi hapa JF yanadhihirisha wazi hisia zetu za kutamani jamii ya watu fulani au kundi fulani la Watanzania wabadirike ili sisi wote tufaidike na mwelekeo mpya.
kam tunaongelea mabadiriko ya tabia au mazoea wa kwanza kubadirika ni lazima tuwe sisi tunaoshikia bango vitabia.

Waafrika ndivyo tulivyo ni hatua ya awali na muhimu ya utambuzi wa udhaifu wetu.
Waafrika tutabadirika vipi ni suala la pili ambalo linatakiwa kuunganishwa na hili tunalo lijadiri ili kuanza kupata mwanga wa kujenga mazoea mapya.
Tumetambua tatizo sasa ni muda wa kuchambua kiini cha tatizo na kutafuta njia za kupambana na tatizo katika lengo la kujenga mwelekeo mpya wa mawazo na matendo.

Next time usinunue gari kuu kuu nunua Trekta kuu kuu.
 
Waafrika ndivyo tulivyo!... haina Ubishi ndivyo tulivyo...

Madela wa Madilu kaandika hivi:-
Mtaji mkubwa wa kupiga hatua yoyote ile hapa duniani ni matatizo. Udhaifu wetu Watanzania ni moja kati ya matatizo makubwa yanayo tukabiri kama taifa pia kama jamii ya watu.
Tunatakiwa kutumia udhaifu wetu kama reference ya kutafuta na kutengeneza njia sahihi za kuondoka hapa tulipo na kusonga mbele.
Kila tatizo kwa kawaida huja likiwa na package ya solution, wakati mwingine huwa na solution zaidi ya moja.

Nae Rev. Kishoka katupa hoja hii:-
Wenzetu wazungu, ugumu wa maisha kutokana na hali yeyote, milele umekuwa ni kichocheo cha wao kuwa wachapa kazi, wavumbuzi, watafiti na kuendelea kutafuta suluhisho la matatizo yao au kuongeza ufanisi kupunguza ugumu na makali ya maisha au uchapa kazi. Mafanikio yao si kabisa au kamili (absolute/perfect), lakini husaidia sana kuleta mabadiliko na maendleo katika maisha na jamii zao na hivyo kuendelea kuwa na hali nzuri za maendeleo mpaka tunawanyeyekea na kuwaita "Nchi Matajiri".

Sisi tumedumaa, je ndivyo tulivyo?

Kwa mtazamo huo hapo juu bila shaka Nyani Ngabu katupa mtihani huu na hakika jibu lake tunalo na linauma sana kulisema...Hapa JF tunayaweka bayana matatizo yetu, udhaifu wa viongozi pamoja na sisi wenyewe umeshindikana kupatiwa ufumbuzi isipokuwa kwa msaada toka nje iwe hata kuwaondoa viongozi wabaya bado tunategemea uwezo wa Mungu kama tulivyookoka wakati wa Utumwa. Bila UN kupiga marufuku Utumwa pengine hadi leo Mwarabu mwenye tumbo la pilau na gobole lake angeweza kabisa kukusanya watumwa 1000 na kuwafunga minyororo tena mijitu iliyosimama fupi sita kwenda juu. As a fact wapo watu kati yetu wanaopongeza waarabu, wazungu na kadhalika kwa matendo yao wakisema haikutokea hivyo....Hii inatokana na Kusahau machungu. Waafrika wepesi sana wa kusamehe na kusahau hali Watu kama wazungu ama wayahudi hawatasahau wala kusamehe Hitler na watu wake hadi mwisho wa dunia hii. Historia itafundishwa kizazi hadi kizazi lakini sio sisi.
Hivyo tunatumia muda mwingi kubishana na siku zote hatuwezi fikia solution kwa sababu sisi wote ni wavivu wa kutafuta solution ama sii kipaji tulichopewa. Mfano mdogo ni hayo yaliyotokea Dodoma, Je, baada ya kuachishwa kazi Lowassa tumepata solution kweli ya Ufisadi?... hivi kweli kuna mtu anaweza kunambia kuachishwa kazi kwa hao viongozi ama kurudishwa fedha za EPA ni somo kwa mafisadi wote nchini?... Je, mmesahau Mkapa alipoingia pia alihakikisha fedha zote za malimbikizo ya kodi za wahujumu Uchumi wetu zinarudishwa! Sasa tafuta list ya vigogo wote waliotakiwa kurudisha fedha hizo kisha fuatilia kesi zao ziiko wapi... wengi wao kama sii wote leo hii ni mabillionea yaani ndio kwanza walichukua mikopo zaidi na kuboresha uhusiano wao na viongozi waliokuwa madarakani. Halikuwa somo wakati ule na tumerudia tena leo ktk kufuata nyayo zile zile...kuuzunguka mbuyu.

Tazamani viongozi wanavyogawana mali za Umma, majumba ya msajiri na kadhalika utadhani babu zao waliwaachia urithi, nani kati yetu kaweza kusimama kuhakikisha mchezo huu unakoma. Sii viongozi ndani ya chama wala wastaafu wote kimyaaa! wakute migahawani utafikiri watu wa maana jinsi wanavyopingana na mwelekeo wa nchi yetu lakini wakishafika Bungeni.. makofi kwa wingi.
Lowassa tayari kisha pata wapambe pamoja na yote aloyafanya, haya na hao wanaompinga humu utawakuta wakisherehekea msaada wa Bush hali wanafahamu fika kuwa fedha hizo zinaenda mfuko wa mtu. Sasa tunachoshangilia ni kipi hasa ikiwa watu hawa hawa walisema hawana confidence na utawala wa JK kwa sababu umejaa mafisadi, leo Utawala huo huo wapewe dollar millioni 700 kisha watu wamesahau matatizo yote ya confidence, tunashangilia hali hakuna solution iliyokwisha patikana ama wekwa dhidi ya Ufisadi. Jamani kweli hii sio breakdown of confidence yenyewe?..
Rev. Kishoka ngona ya Mdanganyika ipo hapa:- Kuna kufikiria kuwa "ndivyo tulivyo" na kuna matendo ya kuthibitisha "ndivyo tulivyo" na hatimaye kuishi "kama tulivyo"

Hapa mkubwa Wadanganyika tunaondoka na yote isipokuwa wengi hawapendi kufikiria ndivyo tulivyo hali matendio yetu na maisha yetu yanathibitisha - Ndivyo tulivyo!

Mkuu Nyani Ngabu na Rev. Kishoka nipo nanyi ktk hili na nipo tayari kupokea maelezo yoyote tofauti kwa mifano hai isiwe mazungumzo na kunyoosheana vidole. Mimi mwenyewe ni matunda ya kizazi cha watumwa yaani tupo ktk inherited cycle ya Utumwa na Ethics zake.
 
Kuna kufikiria kuwa "ndivyo tulivyo" na kuna matendo ya kuthibitisha "ndivyo tulivyo" na hatimaye kuishi "kama tulivyo"

Je kuendelea kuwa na viongozi Mafisadi na Serikalii butu ni makosa ya nani? Y a Raisi, Mwenyekiti wa Chama au ni makosa ya Rev, Bubu, Mwk na Mwanakijiji?

Ni makosa ya viongozi wa vyama vya upinzani ambao wanadhani watashinda viti vingi vya ubunge na Urais kwa kujitangaza mijini tu badala ya vijijini ambako ndiko asilimia kubwa ya Watanzania wanakoishi.

Ni makosa ya viongozi wa vyama vya upinzani ambao pamoja na kilio cha Watanzania kwamba waungane na kuunda chama kimoja chenye nguvu ili kuking'oa chama cha mafisadi madarakani, wao bado wameweka mbele ubinafsi. Wanaogopa wakiungana basi watapoteza madaraka katika vyama vyao ambavyo mpaka sasa hivi havijawa na mafanikio makubwa kwenye chaguzi za vyama vingi.

Tuendelee kuvishinikiza vyama vya upinzani, labda vitasikia vilio vya Watanzania na kuunda chama kimoja chenye nguvu kitakachokuwa na matawi na wanachama wengi katika kila kona ya Tanzania na hatimaye kuking'oa nambari one kwa ufisadi madarakani.
 
Bubu ataka Kusema,
Mkuu uchaguzi wa Kiteto ni mfano mmoja safi sana. Umetokea wakati wa mafisadi na Tanzania nzima walijua habari za serikali hii, mikutano kibao imefanyika huko Kiteto na hakuna asiyefahamu, yet wananchi wamechagua CCM tena kwa kura nyingi sana.
Nasema wamechagua CCM kwa sababu hata kama CCM wameiba kura ama wametumia njama fulani lakini haiwezekani kabisa wangefikia nafasi ya kutegemewa kukaribia ama kupata ushindi kama ingekuwa nchi nyingine. ONLY in Tanzania na ndivyo tulivyo!..
 
Waafrika ndivyo tulivyo!... haina Ubishi ndivyo tulivyo....

Inanikumbusha Waamerika weusi walio wengi ambao wako vyuoni lakini wanayakacha masomo ambayo yana ajira nyingi. Wao vitu kama engineering, accounting, mathematics hawavitaki kuvisikia kabisa. Wanataka vitu kama Black American history, African history. Pamoja na kuwa wanaona wenzao waliomaliza wanahangaika kupata kazi za maana au kupata kazi tu, bado asilimia kubwa wanajikita kwenye masomo hayo. Waafrika wanalala mbele na masomo hayo hayo 'magumu' na wakimaliza wengi wao wanaonja "American Dream" wao wanabaki kulalama oohhh! Waafrika wanajiona wana akili kuliko sisi bla bla bla zisizokwisha. Wameshabweteka na akilini mwao ni kwamba masomo hayo wao hawayawezi, hata kujaribu na kuwauliza 'waafrika' siri yenu katika kufanikiwa katika masomo haya ni ipi, hawataki !

Afrika tuna rasilimali chungu nzima, na sio kweli kwamba waafrika ndio tulivyo ndio maana pamoja na Mwalimu Nyerere kung'atuka mwaka 1985 lakini bado anakumbukwa na waafrika wengi kwa mazuri mengi aliyoyafanya Tanzania na Afrika. Kwa nini waafrika hawa wanamkumbuka Mwalimu na siyo Mwinyi au Mkapa ambao ni wajuzi juzi tu!? Ni kwa sababu wengi waliyapenda aliyofanya mwalimu pamoja na kuwa hakufanikiwa kama alivyotaka yeye, lakini wengi wanamuona alikuwa na mapenzi ya kweli kwa Tanzania na Afrika.

Hapa JF tunapambana na mafisadi ndani ya CCM na SK. Tungekuwa waafrika ndio tulivyo si tungenyamaza tu tuendelee na maisha yetu ya kila siku? Ya nini kuwapigia kelele na kuwashinikiza viongozi mafisadi ili wafilisiwe na hatimaye kufunguliwa mashtaka? 😕

Kinatuuma nini na sisi waafrika ndivyo tulivyo! We don't care for anything, even for our beloved countries. NO I am not that type of African. I do care for my country as well as my countrymen and women that's why I am trying my level best to get rid of those fisadis who are stealing and looting day and night billions of shillings while the majority of Tanzanians are suffering. Na sisi tukibweteka na hii dhana potofu "Watanzania/Waafrika ndio tulivyo" basi hata hii vita dhidi ya mafisadi haitafanikiwa maana conclusion itakuwa 'ndivyo tulivyo, why should we bother wasting our precious time'
 
Bubu ataka Kusema,
Mkuu uchaguzi wa Kiteto ni mfano mmoja safi sana. Umetokea wakati wa mafisadi na Tanzania nzima walijua habari za serikali hii, mikutano kibao imefanyika huko Kiteto na hakuna asiyefahamu, yet wananchi wamechagua CCM tena kwa kura nyingi sana.
Nasema wamechagua CCM kwa sababu hata kama CCM wameiba kura ama wametumia njama fulani lakini haiwezekani kabisa wangefikia nafasi ya kutegemewa kukaribia ama kupata ushindi kama ingekuwa nchi nyingine. ONLY in Tanzania na ndivyo tulivyo!..

Hujui rushwa inayofanywa na CCM wakati wa chaguzi? Pamoja na kuwa wananchi wamesikia story chungu nzima za ufisadi, uchaguzi ukikaribia CCM wanagawa rushwa, wenyewe wanaita 'takrima' kila kona vikiwemo mifuko ya cement, vyakula na pesa pia. Sasa ukichukulia asilimia kubwa ya wapiga kura wanaishi maisha ya dhiki nani unadhani akishapewa vitu kama hivyo hatakuwa tayari kuichagua tena CCM.

Kama sikosei waliopiga kura walikuwa 77,000 na mwisho wa kupiga kura ni 12 jioni. Je kuhesabu kura 77,000 inabidi kufanyike mpaka usiku wa manane? Wanaporuhusu hili la kuhesabu kura liendelee mpaka usiku wa manane au kesho yake basi hapo ndipo upinzani huwa unafungwa goli la kisigino na CCM.
 
Jamani hii dhana ya Waafrika Ndivyo Tulivyo inaweza ikatupa changamoto kubwa sana ya kudhihirisha kuwa Sivyo Tulivyo. Udhihirishaji huo utatokana na matendo yetu na matokeo yake na si maneno matamu. Kwa hiyo nawaombeni tusikate tamaa...tujitahidi kama jamii kudhihirisha kwamba sivyo tulivyo kwa matendo na si maneno. Lakini kama tukiwa tunaongea tu wakati maneno yetu hayalingani na matendo yetu hatutakuwa na jinsi zaidi ya kukiri kweli labda ndivyo tulivyo and we can't help it....
 
Bubu ataka kusema,
uchaguzi ukikaribia CCM wanagawa rushwa, wenyewe wanaita 'takrima' kila kona vikiwemo mifuko ya cement, vyakula na pesa pia. Sasa ukichukulia asilimia kubwa ya wapiga kura wanaishi maisha ya dhiki nani unadhani akishapewa vitu kama hivyo hatakuwa tayari kuichagua tena CCM.

Tunarudi pale pale kuwa NDIVYO TULIVYO... nchi nyingine wasingempa kura CCM hata kama angetoa magari na pengine ingekuwa ushahidi tosha kutengua/kuwaondoa ktk uchaguzi. Haya baada ya kufahamu yote haya tumefanya nini?...Hiyo dhiki si ndiyo ingekuwa fundisho kwa mwananchi kutochagua CCM, leo T shirt moja itakupa chakula cha mwaka?..Sisi wavivu wa kifikiri kupata solution!
Tunasubiri mwaka 2010 tumwone Freeman ktk Helikopta kisha tukapokee Tshirt zetu na kofia maneno CCM. Mkuu hii imesha andikwa kama inavyosema Biblia haina changes toka kwa mwanadamu na tutaendelea kuwa hivyo hadi kizazi kipya chenye mchanganyiko wa damu tofauti...Hilo agano jipya!
 
Bubu ataka kusema,


Tunarudi pale pale kuwa NDIVYO TULIVYO... nchi nyingine wasingempa kura CCM hata kama angetoa magari na pengine ingekuwa ushahidi tosha kutengua/kuwaondoa ktk uchaguzi. Haya baada ya kufahamu yote haya tumefanya nini?...Hiyo dhiki si ndiyo ingekuwa fundisho kwa mwananchi kutochagua CCM, leo T shirt moja itakupa chakula cha mwaka?..Sisi wavivu wa kifikiri kupata solution!
Tunasubiri mwaka 2010 tumwone Freeman ktk Helikopta kisha tukapokee Tshirt zetu na kofia maneno CCM. Mkuu hii imesha andikwa kama inavyosema Biblia haina changes toka kwa mwanadamu na tutaendelea kuwa hivyo hadi kizazi kipya chenye mchanganyiko wa damu tofauti...Hilo agano jipya!

Sivyo tulivyo! Kwa mfano katika uchaguzi unaokuja wa 2010, Kama JF tukiamua kulivalia njuga hili la rushwa aka 'takrima' kwa kukusanya pesa na kutoa elimu through majarida na matangazo katika TV na redio ya athari za kupokea rushwa ili kiongozi asiyefaa achaguliwe tena wakati hastahili kuchaguliwa, basi tutakuwa tumetoa mchango mkubwa wa kupambana na hii dhana kwamba waafrika ndivyo tulivyo. MOST OF US DO CARE.
 
Kungekuwa na jinsi ya kuongeza "thank you" kwenye post moja ningekupa nyingi sana Bubu! you just nailed it!

Ndugu zangu;

Ngoja niende kwenye falsafa kidogo(rector wangu pale Peramiho atafurahi LOL)

Kuna vitu ambavyo tunaweza kuchagua na vitu ambacho hatuna uwezo wa kuchagua hata kama tungetaka vipi. Vitu hivi ambavyo tunavyo lakini hatukuvichagua ni vitu ambavyo sheria za fizikia, kemia, na elimuviumbe zinakataza. Vitu hivi ambavyo hatukuwa na uchaguzi navyo mara nyingi tunajikuta hatuvipendi na tunatamani tungepewa uchaguzi wa aina fulani. Lakini kanuni zijulikanazo ambazo zinatawala ulimwengu zinatukatalia uchaguzi huo.

Ni kwa sababu hiyo basi hatuna uchaguzi wa wapi tutazaliwa. Ni wengine na mazingira yanayochagua wapi tutazaliwa. Tungekuwa na uchaguzi wengine tusingependa kuzaliwa nyumbani ingekuwa bora hospitalini; wengine tungependa kuzaliwa angalau nyumbani kuliko ndani ya basi (I witnessed one of those); lakini katika hali zote ni watu wengine waliamua au mazingira yaliamua tukazaliwa tulikozaliwa; Sisi wenyewe hatukuwa na uchaguzi.

Hatukupewa uchaguzi wa mji na nchi gani tungezaliwa au Taifa gani tungezaliwa. Labda wengine tungetamani "angalau" tungezaliwa watu weusi hivi hivi lakini tungezaliwa Marekani au Ulaya. Lakini tusingependa kuzaliwa weusi huko India au China! Wengine tunaona ingekuwa bora kama tungezaliwa tukiwa wazungu maana kuwa mzungu kuna "kaujiko" na "ubora" wa aina fulani. Bahati mbaya, hatukupewa uchaguzi huo.

Ningeweza kuorodhesha mengine mengi ambayo yanathibitisha kuwa kuna mambo katika maisha yetu ambayo hatuwezi au hatukuweza kuyachagua na tunajua kuwa kama tungekuwa na uchaguzi basi tungechagua kitu tofauti.

Ukweli huo kuwa kuna vitu ambavyo mwanadamu hana uwezo wa kuchagua (ingawa anaweza kumchagulia mwingine) ni ukweli ambao unakubalika kuwa ni kweli ukienda China, Alaska au Amazoni. Lakini pia kuna vitu vingine ambavyo mtu mwingine anaweza kutuamulia nacho ni kama tuko huru au la, tunaishi vipi n.k

Hata hivyo kuna kitu kimoja ambacho mwanadamu ana uchaguzi nacho na hakuna pingu, au mawingu yoyote yanayoweza kumuondolea. Kitu hakijalishi kama huyo mtu yuko Sahara au Kalahari. Kitu hicho ambacho mwanadamu anaumiliki kamili hakijalishi kama huyo mtu ni mtumwa au huru, mweusi au mweupe, msomi au simsomi. Kitu hicho ni uwezo wake wa kufikiri na kuamua yeye anajitambuaje (self perception)

Mtu anaweza kujiona duni na mnyonge; anaweza kujiona hafai na hastahili, anaweza kujiona dhaifu na asiyeweza. Kujiona huko kunatokana siyo na matendo ya nje lakini na fikara zake za ndani. Katika mfano wa Kunta Kinte hapo juu utaona kuwa Kunta hakukubali kuitwa "Toby" licha ya mijeredi mingi. Yeye alijitambua kama "Kunta Kinte". Lakini baada ya kufanywa duni na vitendo vingine alizisalimisha fikara zake kwa kukubali kuwa yeye ni "Toby". Kwa kufanya hivyo alizisaliti fikara zake kwa ajili ya kukwepa maumivu.

Mtu anayekubali fikra za kujiona duni hujikuta anajenga hisia ya ya kujiona duni (inferiority complex). Mtu anayejiona duni anakubali vitu jinvi "vilivyo" na anaona chochota anachokipata (chema au kibaya)) kuwa ni mastahili yake. Akiona barabara mbaya anasema "ndivyo tulivyo"; bodi ya mikopo iliyo mbovu anasema "ndivyo tulivyo"; wanaiba EPA anasema "ndivyo tulivyo"; n.k yaani mtu mwenye fikra za kujiona duni haoni mwanga mbele yake bali giza tu! Huyo ukimpa watu awaongoze atawaongoza shimoni kwani hivyo ndivyo ilivyo!

Mtu huyo mwenye fikra hizo za "ndivyo tulivyo" hawezi kuongoza na siyo tu hawezi kuongoza hastahili kuongoza. Kwani na yeye ni mtu ambaye hawezi kubadili kitu. Kwanini abadili kitu wakati "ndivyo tulivyo"? Mtu mwenye mawazo ya kukubali hali halisi na ambaye anaona kuwa siyo tu ni vigumu kubadilika bali amechagua kukaa pembeni na kuona wengine wabadili hali hiyo ili aone "proof" kuwa sivyo tulivyo!

Ni kweli kuwa baadhi ya viongozi tulionao leo hii katika utumishi wa umma na hata sekta binafsi wana mawazo hayo yaliyosalimu amri. Mawazo ya mtumwa aliyekubali kuitwa Toby!

Lakini mimi ndugu zangu sijasalimisha mawazo yangu kwenye kambi ya waishio katika ulimwengu wa "ndivyo tulivyo". Mawazo yangu na fikra zangu ziko huru na hazitegemei matukio nje yake kuweza kuulinda uhuru wake. Mimi na nyinyi bila ya shaka tunaangalia vitu vile vile lakini tunafikia mahitimisho tofauti. Ya kwenu ni ya ya watu waliokubali kushindwa na kusalimu amri. Ni mawazo ya watu waliokata tamaa kuwa situ vitu jinsi vilivyo bali kuwa "ndivyo sisi tulivyo".

Na hapa suali la Bubu hapo juu lina uzito wake. Kama sisi ndivyo tulivyo kwanini tunasimama kukosoa na kutoa mapendekezo ya kufanya vitu tofauti? Kwanini tunasisitisha kuona mabadiliko wakati tumeshasema kuwa "ndivyo tulivyo". One can not predict the obvious! You can not prophecy and go out to fullfil that prophecy. Kama ndivyo tulivyo juhudi zetu zote na mazungumzo yetu yote na mijadala yetu yote hapa hasa ile inayohusu mabadiliko ya uongozi ni bure tu!

Na hapa naweza kuyasikia maneno ya Lowassa kuwa "nimeonewa" yanapokuwa na ukweli. Kama ndivyo tulivyo kwanini Lowassa kajiuzulu na Baraza kuvunjika? Kama ndivyo tulivyo kwanini tunataka watu wa EPA wasiishie kurudisha fedha tu bali pia watiwe pingu? Kama ndivyo tulivyo kwanini tunataka Balali arudi na kutiwa pingu asimame Kisutu?

Nyinyi mliokubali kuwa ndivyo mlivyo hiyo ni haki yenu na hizo ni fikra zenu ambazo kama nilivyosema hapo juu mmezichagua na kuzikubali. Ni haki yenu kuzitetea na kuzisimamia kwa sababu kama hivyo ndivyo mlivyo hamuwezi kubadilika na hivyo mnathibitisha wenyewe kwa kauli zenu kuwa ndivyo mlivyo.

Kwa vile hivyo ndivyo mlivyo hakuna mtu anayeweza kuwashawishi vinginevyo au kusababisha mtazame vitu kwa namna nyingine ya matumaini zaidi na ya kutaka mabadiliko ya kweli. Hakuna hoja au vioja vinavyoweza kusababisha mabadiliko ya fikra ndani yenu isipokuwa nyinyi wenyewe mtakapoona kwenye ushawishi wa fikra zenu kuwa vitu vinaweza kubalishwa na kama vinaweza kubadilishwa basi sivyo tulivyo!

Mimi, Fundi, Bubu, na wengine ambao tumekataa maxim hiyo ya "ndivyo tulivyo" tumechagua katika fikra zetu kutowekwa kwenye chupa na kufungiwa humo! Tumekataa kuwekwa kwenye kisanduku kibovu cha "ndivyo tulivyo" na kuambiwa ati hatutoki humo. Kwa ghadhabu na makelele, na kama watu walio na kisasi tunakataa, tunapinga, tunakejeli, na kudharau fikra hizo dhaifu ambazo hazina msingi katika ukweli.

Hatuwezi kuwa wazungu, hatuwezi kubadili nasaba zetu. Lakini tunachagua fikra zetu kuwa na sisi ni watu sawa, wenye haki sawa. Ndiyo maana mapambano haya yanaitwa mapambano ya kifikra siyo mapambano ya nani mzuri, nani anaweza n.k Ndiyo maana nilisema huko nyuma kabla ya kuwashinda kwenye sanduku la kura ni lazima tuwashindwe kwenye fikra!

Lakini kama wapo watu wengi wenye mawazo ya "ndivyo tulivyo" basi ni rahisi kuelezea kilichotokea Kiteto; ni rahisi kuelezea vijana pale barabara ya Nyerere karibu na Scania watu wanafanya biashara hadi barabarani na hakuna Polisi anayeweza kuwaondoa; ni rahisi kuelezea kwanini badala ya kuwafikisha wahalifu mahakamani tunakaa meza moja na kujadiliana nao ni adhabu gani tunaweza kuwapa!

Ni lazima tushinde kwenye fikra kwanza kabla hatujaweza kushinda kwenye ofisi zao na kubadili mikataba; ni lazima tushinde kwenye fikra kwanza kabla hatujadhaminiwa kuongoza nchi. Kabla hamjaona vitendo vinavyoonesha mabadiliko ni lazima mabadiliko ya fikra yatangulie kwanza kwa sababu wazo hutangulia kitendo!

Msitarajie kuona mabadiliko ya utendaji kama hakuna mabadiliko ya fikra. Ninatoa mwaliko huru na kwa wote ambao bado wamefungwa na minyororo ya "ndivyo tulivyo" kuivunja na kuikana na kuungana na fikra za "sivyo tulivyo" ili kwa pamoja tuweze kuanza kubadili mtu mmoja baada ya mwingine!

Ninawakaribisha kwenye mapambano ya kifikra ambako hakuna kusalimu amri wala kurudi nyuma ni mbele kwa mbele hadi Watanzania wote wanajiamini, wanatambua kuwa wanaweza, na wanaanza kutenda wakijua kuwa wanastahili vitu vizuri na viongozi wazuri!!!

M. M.
 
Mwanakijiji bana....maneno meeengi utadhani sijui nini....aaaah

Haya bana...kwa maneno tu hakuna anayekuweza...but I still maintain that I'll believe it when I see it...
 
Hili halina ubishi, watu weusi ndivyo tulivyo kuanzia Haiti mpaka Papua New Guinea, Canada mpaka Fiji, dunia nzima!
 
Africans have about 5000 years of evolution to catch up with the rest of the world. Lives of many (I dare say most) Africans today are comparable or worse in quality to the lives of Asians or Europeans 5000 years ago. Of course by quality I am not referring to intangible aspects of life such as happiness but more like general health, diet, life span, material possessions of the general population. The biggest obstacle in overcoming chronic African problems is the low average IQ among Africans (approximately 70 points). Average IQ of 70 points makes it almost impossible to function and compete in the modern world.

Important: It is also good to note that average of 70 IQ points also means that there are many Africans who score well above 70 points and some even fall into the genius category. This is what Dr. James Watson was referring to in his controversial statements.
 
Me, I consider myself a world citizen kama mhindi. Yaani popote nilipo.....jibu sivyo nilivyo kwasababu najua uwezo wangu, mawazo yangu na malengo yangu kimaisha. Yaani naweza kushindana na mtu yeyote.

Sasa ukiniweka katika mazingila ya kikwetu kwetu, ukaning'ang'aniza nifikirie kibongo bongo.....au uniweke pale kijijini, uniletee na ka kadi ka CCM, ingawa akili itakuwa inakataa niwasikilize kina Chadema na wanaJF, ila nikiangalia minjemba wenzagu wanafakamia liubwabwa la uchaguzi....mmh yaani hapo naishiwaga manguvu yote (utafikili wamenilimisha matuta gambushi)...ninajikuta mawazo ya kijamaa yananigandamiza kabisa mwanawane. Basi hapo ninakuwa nakataa sivyo nilivyo, lakini mienendo inanifanya niwe mzalendo, nami nakuwa ndivyo nilivyo. Ila siwezi kukubali.

Ninachosema, yaani tuko wachache wenye kuamini 'sivyo tulivyo'...ila kwavile wengi wetu wako upande wa 'ndivyo tulivyo' historia inatuhukumu sana sana tukija kwenye mambo ya collective decision making and moving forward as people (ukizingatia ni rahisi kuwa manipulated as individuals). Mkandara amevivunjilia vunjilia vipengele kama michembe iliyokauka.

Tofauti moja niliyojifunza kati yetu na hawa wenzetu walioendeleaga, ni kwamba, sisi huwa wepesi kuona vikwazo na ku-give up, lakini wao ndio akili inachemkaga kama mvuke wa gongo. Na hilo ni somo moja kubwa nililojifunza na kuishi nalo, yaani 'There is always another way/alternative'. And so long I believe that....basi, 'sivyo nilivyo'. Ila hiyo ya wingi, naona mtu kaamua wikiendi achemshe vichwa vibaya.
 
Okay...I just want to be shown more than I can be told...

Kilichotokea Dodoma ni mazingaombwe kaka...jamaa anapeta na kapata mafao kibao like he's a king or something...

And I want to take this opportunity to make a pledge that if and when I'm proven wrong, I will change my signature to Waafrika Sivyo Tulivyo, Samahani kwa kuwatusi.....

Nyani.
Ulimpinga na kumdhibiti sana Raj Patel enzi hizo kwa ku-advocate huu usemi, lakini naona mwishowe umekuwa muumini wake. Ukiondoa lugha mbaya ya Raj, na badala yake kuangalia substance na arguments za maneno yake, itabidi ukubaliane naye kuwa kuna kitu si sahihi kuhusu sisi watu weusi.
 
Bubu ataka kusema,
Maelezo yako mazuri sana lakini kidogo unakosea kuitazama hiyo shilingi.
Umezungumzia swala la Waamerika weusi, hapa mkuu unaondoa Uraia wao na kuichukua rangi yao - meaning weusi. Hivyo unajaribu kuipanua hoja ama Mada ya Nnyani Ngabu kuwa ni swala la rangi sio tena Waafrika - I mean Watanzania ndivyo tulivyo.
Sasa ukisha vuka mipaka ya ramani na kuwa rangi hii inatuweka ktk nafasi ngumu zaidi kwani tutazungumzia tofauti kati ya minority na wapi wameendelea zaidi ya wenzao. Tofauti kama hizo tunaweza zipata hata ndani ya Watanzania, Mchagga anaweza sema hivyo hivyo lakini haiondowi ukweli kuwa sisi Wadanganyika pamoja na Wachagga Ndivyo tulivyo.
Mkuu population ya weusi US ni kitu kama 10% ambayo inaweza lingana na population nzima ya Tanzania. Lakini lazima ukubali kuna wasomi wengi weusi US kuliko TZ na uwezo wa mwafrika mweusi Marekani ni mkubwa kuliko mwafrika wa Afrika-Tanzania kwa kila sekta unayofikiria wewe. Na pengine margin ya Utajiri, middle class na umaskini kwa watu weusi Marekani ni 10-40-50 wakati hapa kwetu tunazungumzia 5 -15-80, hapa mkuu unapima mbingu na ardhi. Na ni ktk kuitukuza historia yao imeweza kuwakumbusha kule walikotoka hivyo kuongeza struggle zaidi kuhakikisha yale yaliyowakuta babu zao hayatarudiwa tena...Sisi na elimu zetu tunaishi ktk utumwa tena tunatawaliwa na ndugu zetu wenyewe.

Pili, umezungumzia swala la Nyerere kukumbukwa.. Mkuu wangu Nyerere anakumbukwa kwa sababu ailikuwa akisisitiza kuiweka Identity yetu mbele, nafasi ya Tamaduni zetu, lugha na Utanzania mbele ya kuiga. Ni ktk kumkumbusha Mtanzania kila siku kulinda hadi yake ndiko kulikompa sifa Nyerere na hata kina Nkurumah, Mandela na kadhalika hawa ndio madereva.

Kina Mwinyi na Mkapa ni viongozi madereva wa treni wanaofuata reli ya uongozi hivyo hakuna jipya ambalo wananchi wanaweza kuliwekea kumbukumbu kwani watu kama hawa wapo dunia nzima. Marais madereva wa reni yaani hawana kazi kubwa zaidi ya ku keep time, huko tuendako wameisha jengewa reli.
 
Hujui rushwa inayofanywa na CCM wakati wa chaguzi? Pamoja na kuwa wananchi wamesikia story chungu nzima za ufisadi, uchaguzi ukikaribia CCM wanagawa rushwa, wenyewe wanaita 'takrima' kila kona vikiwemo mifuko ya cement, vyakula na pesa pia. Sasa ukichukulia asilimia kubwa ya wapiga kura wanaishi maisha ya dhiki nani unadhani akishapewa vitu kama hivyo hatakuwa tayari kuichagua tena CCM.

Kama sikosei waliopiga kura walikuwa 77,000 na mwisho wa kupiga kura ni 12 jioni. Je kuhesabu kura 77,000 inabidi kufanyike mpaka usiku wa manane? Wanaporuhusu hili la kuhesabu kura liendelee mpaka usiku wa manane au kesho yake basi hapo ndipo upinzani huwa unafungwa goli la kisigino na CCM.

Bubu,

Who is to be blamed on rushwa na takrima kwenye uchaguzi Kiteto? Je ni Mtoa rushwa pekee? what about mpokea rushwa?

Kwa nini mpokea rushwa alikubali kupokea hongo? Kwa nini alimchagua yule aliyempa hongo na si yule ambaye hakutoa hongo?

Je hii si dhahiri kuwa mtoa hongo katumia mazoea na tabia za mpokea hongo ya kuwa "ndivyo alivyo" huku akijua wazi nikitoa hongo atanipa kura na tukuzo?

Umekiri kuwa kila mtu anajua yaliyosemwa kuhusu Ufisadi, je ni kwa nini basi mpiga kura alikubali hongo kutoka kwa fisadi na kumpa fursa ya kuendelea kutumbua na kuhujumu hazina ya Taifa kwa kuimarisha ufisadi?

Hata tukisema tuende kwa wahesabu kura na waratibu kama tutadai faulo ilitumika, je ni kwa nini wote walikubaliana na mtoa hongo na kudhihirishia umma na dunia kuwa wao "ndivyo walivyo"? wepesi kurubuniwa, wasio na msimamo wa kukataa kuburuzwa, wenye kufuata kila wanachoambiwa kufanya bila kufikiri, walion na dhamira zilizolala au wanakataa kusutwa na dhamira kwa kufanya makosa?

Swali linakuwa ni vipi huyu mtu ambaye "ndivyo alivyo" atabadilika na kuachana na kufanya mambo "kama ndivyo alivyo"?

Ni mbinu gani ambazo sisi tunaosema hapana "hivyo sivyo tulivo" kama Yunic, Mwanakijiji na wewe Bubu mnaweza kuzileta kwa jamii ili kuondokana na mazoea ya tabia na utegemezi wa kufanya mambo, kufikiri na kuishi kwa kudai "hivi ndivyo tulivyo"?
 
Back
Top Bottom