Waafrika ndivyo tulivyo?

Waafrika ndivyo tulivyo?

poverty.jpg


Sio Afrika hiyo....
 
3488%20Poverty%20Brazil%20Boy%20scavenging%20for%20recyclables%20in%20the%20garbage%20dump%20Recife.jpg


Hii Ulaya,nchi inayoitwa Romania

image011.jpg

Hii nayo ni Ulaya,nchini Bulgaria

Kama ndivyo tulivyo kwa sababu ya uchafu,umasikini,nk then picha hizi chache zinathibitisha tofauti,na images za Katrina zilituonyesha taswira kama zile za Kipawa kuashiria kuwa suala si rangi au asili bali mfumo.
 
oh.. ok naogopa you might be able to convince me kuwa ndivyo tulivyo!! LoLest!

Actually I don't have to convince anybody...nobody convinced me. I just looked, observed, then reached a conclusion based on what I see/ saw. And don't worry...it's not that bad to think ndivyo tulivyo....
 
Katika kuperuze hii mada ninaona kuna kutofautiana kimaana kwenye hii hoja

'NDIVYO TULIVYO' tunamaanisha nini hasa.....kama watanzania, kama waafrika, watu weusi....katika 'abstract' level, ndivyo tulivyo haipaswi kuwa na mtizamo hasi wowote ule. Kwa nini nasema hivo? kwa sababu pia hata yaho 'maendeleo' ambayo sisi tunaoan wengine 'wameendelea', nini maana yake? tunakubaliana kuhusu maana ya maendeleo?

Walioendelea, walau katika maana ya kawaida tunategemea wawe na maisha flani ya kuwa na furaha, etc, lakini labda tujiulize, je wenzetu pamoja na kuendelea, are they 'warm' au 'cold'?

Ni kitu gani kinatufanya sisi tutake kuwa 'kama walivyo' na sio kama 'tulivyo', nikistick kwenye dhana kuwa 'ndivyo tulivyo' haina mtizamo hasi?

Nasema hivi kwa sababu naona tatizo linakuja pale tunapoichukulia hii 'ndivyo tulivyo' kwa mtizamo hasi. Naweza kuona kuwa hoja za Mzee Mwanakijiji zinaanzia hapa, na Nyani Ngabu akimaanisha kinyume chake.

Hivi tumeshawahi kujiuliza, kama kusingekuwa na mwingiliano na jamii nyingine, sisi kama waafrika tungekuwa wapi na tungekuwa na 'matatizo' yepi? Tungekuwa tunajiuliza kama hivi 'ndivyo tulivyo'?
 
Katika kuperuze hii mada ninaona kuna kutofautiana kimaana kwenye hii hoja

'NDIVYO TULIVYO' tunamaanisha nini hasa.....kama watanzania, kama waafrika, watu weusi....katika 'abstract' level, ndivyo tulivyo haipaswi kuwa na mtizamo hasi wowote ule. Kwa nini nasema hivo? kwa sababu pia hata yaho 'maendeleo' ambayo sisi tunaoan wengine 'wameendelea', nini maana yake? tunakubaliana kuhusu maana ya maendeleo?

Walioendelea, walau katika maana ya kawaida tunategemea wawe na maisha flani ya kuwa na furaha, etc, lakini labda tujiulize, je wenzetu pamoja na kuendelea, are they 'warm' au 'cold'?

Ni kitu gani kinatufanya sisi tutake kuwa 'kama walivyo' na sio kama 'tulivyo', nikistick kwenye dhana kuwa 'ndivyo tulivyo' haina mtizamo hasi?

Nasema hivi kwa sababu naona tatizo linakuja pale tunapoichukulia hii 'ndivyo tulivyo' kwa mtizamo hasi. Naweza kuona kuwa hoja za Mzee Mwanakijiji zinaanzia hapa, na Nyani Ngabu akimaanisha kinyume chake.

Hivi tumeshawahi kujiuliza, kama kusingekuwa na mwingiliano na jamii nyingine, sisi kama waafrika tungekuwa wapi na tungekuwa na 'matatizo' yepi? Tungekuwa tunajiuliza kama hivi 'ndivyo tulivyo'?

Mwanakijiji yeye anafikiri kuwa "ndivyo tulivyo" ku-imply mabaya tu wakati sio hivyo hata kidogo ingawa mabaya yanaweza kuyazidi mazuri.
 
Bubu ataka kusema,
Maelezo yako mazuri sana lakini kidogo unakosea kuitazama hiyo shilingi.
Umezungumzia swala la Waamerika weusi, hapa mkuu unaondoa Uraia wao na kuichukua rangi yao - meaning weusi. Hivyo unajaribu kuipanua hoja ama Mada ya Nnyani Ngabu kuwa ni swala la rangi sio tena Waafrika - I mean Watanzania ndivyo tulivyo.
Sasa ukisha vuka mipaka ya ramani na kuwa rangi hii inatuweka ktk nafasi ngumu zaidi kwani tutazungumzia tofauti kati ya minority na wapi wameendelea zaidi ya wenzao. Tofauti kama hizo tunaweza zipata hata ndani ya Watanzania, Mchagga anaweza sema hivyo hivyo lakini haiondowi ukweli kuwa sisi Wadanganyika pamoja na Wachagga Ndivyo tulivyo.

Naomba tusilete usanii ambao tunaoutumia katika suala la uzawa. Nyani Nguba aliposema hivi hakumaanisha wahindi waishio Afrika au makaburu pengine hata wale waarabu wa kaskazini kwetu hawakuwemo kwenye ramani yake. Kinachozungumziwa hapa ni Mwafrika Mmatumbi. Ndio maana wale wengine walio wazi katika kutetea hoja hii waliingiza neno Nyani!

Mkuu population ya weusi US ni kitu kama 10% ambayo inaweza lingana na population nzima ya Tanzania. Lakini lazima ukubali kuna wasomi wengi weusi US kuliko TZ na uwezo wa mwafrika mweusi Marekani ni mkubwa kuliko mwafrika wa Afrika-Tanzania kwa kila sekta unayofikiria wewe. Na pengine margin ya Utajiri, middle class na umaskini kwa watu weusi Marekani ni 10-40-50 wakati hapa kwetu tunazungumzia 5 -15-80, hapa mkuu unapima mbingu na ardhi. Na ni ktk kuitukuza historia yao imeweza kuwakumbusha kule walikotoka hivyo kuongeza struggle zaidi kuhakikisha yale yaliyowakuta babu zao hayatarudiwa tena...Sisi na elimu zetu tunaishi ktk utumwa tena tunatawaliwa na ndugu zetu wenyewe.

Statistics zinaonyesha kuwa mtu mweusi anayetoka Afrika anafanya vizuri kuliko wamarekani weusi marekani na wale wanaotoka katika visiwa vya karibian huko uingereza. Hawa waafrika wanajitahidi mashuleni na kwenye maisha ni wahangaikaji kuliko wenyeji wao. Kwa bahati mbaya hii imewafanya waafrika kuwa na tabia ya kuwadharau weusi wenyeji. Si mara moja nimemsikia mswahili akiwazungumzia 'niggas' kwa dharau. tunasahau mzigo wa historia. Ingawa sisi nasi tulitawaliwa lakini hatukuwa dehumanised kama walivyo fanywa hao ndugu zetu. Afrika ya kusini tunaona wanavyohangaika na hali hii. Sisi tulikuwa kwetu, tukapata uhuru kwetu na katika sehemu nyingi, pamoja na juhudi za wageni, asili yetu ilibaki pale pale na ndiyo iliyoweza kutupa confidence.


Pili, umezungumzia swala la Nyerere kukumbukwa.. Mkuu wangu Nyerere anakumbukwa kwa sababu ailikuwa akisisitiza kuiweka Identity yetu mbele, nafasi ya Tamaduni zetu, lugha na Utanzania mbele ya kuiga. Ni ktk kumkumbusha Mtanzania kila siku kulinda hadi yake ndiko kulikompa sifa Nyerere na hata kina Nkurumah, Mandela na kadhalika hawa ndio madereva.

Nadhani hapa tatizo ni kuwa hatujaweza hasa ku'define' utanzania wetu. Sidhani kama mtu unaweza kusema kweli kuna tamaduni ya kitanzania bali ni tamaduni mchanganyiko wa makabila na watu wote wanaoishi Tanzania. Kujenga identity sio kitu kidogo. Hao wazungu mpaka leo wanahangaika katika kujaribu kuji'define'. Hii kazi wasingeweza kuifanya hao unaowataja peke yao. Mchango wa watu kama Shaaban Robert, Mwinyimila, Salum Abdallah, Mathias Tinga Tinga na wengine wengi wote wamechangia. Kazi ni yetu wote kuwaenzi katika huu mradi wa kujenga utaifa wetu.

Kina Mwinyi na Mkapa ni viongozi madereva wa treni wanaofuata reli ya uongozi hivyo hakuna jipya ambalo wananchi wanaweza kuliwekea kumbukumbu kwani watu kama hawa wapo dunia nzima. Marais madereva wa reni yaani hawana kazi kubwa zaidi ya ku keep time, huko tuendako wameisha jengewa reli.

Mkuu, kumbuka kuwa kuanzisha ni rahisi kuliko kuendeleza.

Mimi ninachopinga kwenye dhana hii ni matumizi yake katika kuwakebehi waafrika na kuwakatisha tamaa. Hayo yote yanayotolewa mifano ni tabia, tamaduni ambazo zinaweza kubalika. Ulaya kulikuwa hakuishi na magonjwa yanayotokana na uchafu hadi hivi karibuni tu. Nchi/Mji wa Singapore ulipopata uhuru ulikuwa mchafu kupindukia wenye vibiashara vya ajabu na hivi sasa ni moja ya miji safi duniani! Tunawalaumu watanzania kwa kuendelea kuikumbatia CCM, mbona wamarekani wamemchagua George W mara mbili?

Tusikate tamaa, na tusikubali kukatishwa tamaa.

Amandla!!!
 
Mwaka 1994, huko Rwanda mfanyakazi mmoja wa ubalozi wa Marekani aliwapelekea ujumbe wakubwa wake kwamba hali inaelekea kubaya kutokana na matangazo ya chuki na taarifa anazozipata kutoka kwa wenyeji. Akatahadharisha kuwa kuna uwezekano mkubwa wa umwagaji damu. Wakubwa wake kule Washington wakamwabia " haujui waafrika ndivyo walivyo? Vita vya kikabila ni sehemu ya hulka yao." Wamarekani na wenzao wakaondoa raia zao wakaangalia hao waafrika wakitimiza destiny yao maana ndivyo walivyo! Si wahutu wote waliokuwa na nia ya kuua watutsi lakini hawa hawakupewa nafasi maana waafrika ndivyo walivyo. Wakafa watu karibu milioni moja ili kuthibitisha dhana hiyo. Mbona yalipotokea kwao hawakukunja mikono na kusema waserbia ndivyo walivyo?
 
Could be both...

If I say Africans are more gregarious than whites because that is just the way they are....is that a good or bad thing?

NN, I beg to differ. In my opinion "waafrika ndivyo tulivyo" does not have any positive connotation. Kwa watanzania kusema msemo huu ni kunyoosha mikono juu na kukubali kushindwa. Na kuwapa mafisadi ushindi mkubwa na kuwaacha wakikenua gego mpaka gego maana tumewaruhusu waendelee kufanya ufisadi kwa sababu hatuwezi kufanya chochote cha kupambana na ufisadi wao. Tunakubali kwamba direction ambayo nchi yetu inaelekea si nzuri na wengi hatuipendi na hatuna chochote tunachoweza kufanya ili kubadilisha hali hiyo labda hatuna uwezo wa kubadili hali tusiyoipenda au we just don't care about our beloved country anymore.

Watanzania ndio tulivyo! maybe some of you ndivyo mlivyo, but I know that majority of Tanzanians are not happy about the direction of our beloved country and they would like to do something to bring a positive change, because THEY DO CARE ABOUT TANZANIA.
 
Bagosha ne Basungu Kinehe, Ulimhola wa mamishago!

Baada ya kusikiliza pande zote mbili za waliomo na wasiomo, naomba wote mrudie bandiko la kwanza nililolitoa liwe mwongozo wa kujua mwelekeo huu ni wapi!

Nilifanya kwa makusudi kabisa kwa kuanzia Waafrika nikaongeza kwa kubadilisha na kusema I mean Watanzania ndivyo tulivyo!

Lengo langu ni kujichangua sisi Watanzania kama Taifa na kama Wananchi. Naomba tusianze kukimbilia kujifananisha na Wamarekani Weusi au Watogo maana hata kama wao wanamitabia inayofanana fanana, suluhisho la kusahihisha dhana ya "hivi ndivyo tulivyo" kwa Tanzania ni jukumu letu na tujipime ni vipi tutajisahihisha kama tutasema ni dhana potofu. Tukisema ni dhana jenzi na marudufu, ni vipi tutaifanya iwe yetu wote?

Mimi nitaendela kuhoji kama nilivyohoji awali, ni kwa nini tunaendelea kulea na kuishi katika tabia ambazo si endelevu? Zaidi ni ule uvivu wa kujituma, kuchacharika na kufikiri! Mbaya zaidi ni ule utashi wa urahisi kujifanyia mambo tunavyotaka kwa kukiuka sheria au kuzipuuzia, Angamizi zaidi ni kule kutaka kupata mapato na manono bila kutoka jasho au kutumika!

Ndio maana nikauliza, je ndivyo tulivyo? je ndio tabia zetu hizo na tumeridhika nazo? je kelele zetu hapa ni mazoea na kawaida kulalamika tuu bila kuchukua hatua ya kupanga mawazo yetu, kutafakari ni nini tunakipigia kelele na kufanya utafiti wa kupatia ufumbuzi au ni kawaida kupiga domo kulalama na kuendelea kulalama kwa kila jipya?

Suala la nani ni sawa ni subjective, kutokana na utashi wako. Nyani kahoji tabia za watu kula pale Kipawa mbele ya uchafu, je "hivyo ndivyo walivyo"?

Mwanakijiji ananena, wale waliopiga kura dhidi ya CCM "sivyo walivyo" lakini machoni pa CCM, "ndivyo walivyo", je lini Mtanzania atapiga kura yake kwa kutafuta mtu wa kumpa haki na tumaini na si mazoea? Je Wapiga kura wetu wengi "ndivyo walivyo" na wameridhika "jinsi walivyo"?

Je kupiga kwetu kelele kudai haki, heshima, uwajibikaji, kupiga vita ufisadi na uhujumu kunapokelewa na Watanzania kama "JF ndivyo walivyo" na kupuuzwa?
 
Watanzania ndio tulivyo! maybe some of you ndivyo mlivyo, but I know that majority of Tanzanians are not happy about the direction of our beloved country and they would like to do something to bring a positive change, because THEY DO CARE ABOUT TANZANIA.

Bubu,

Kiteto folks had a chance and they blew it, the question is why? why did they find comfort to vote back Mtu wa CCM? Even if huyo Mbunge could have been a Saint, but he belongs to a party of Thieves, why in the heck did they give him a mandate and increase the dominance of Chama cha Mafisadi? Isn't it "ndivyo walivyo" wameridhika na Zimwi liwajualo?
 
Bubu,

Kiteto folks had a chance and they blew it, the question is why? why did they find comfort to vote back Mtu wa CCM? Even if huyo Mbunge could have been a Saint, but he belongs to a party of Thieves, why in the heck did they give him a mandate and increase the dominance of Chama cha Mafisadi? Isn't it "ndivyo walivyo" wameridhika na Zimwi liwajualo?

We don't have all the facts yet. Maybe CCM stole another election. They have done that before and they have the ability to do it many more times
 
Naomba tusilete usanii ambao tunaoutumia katika suala la uzawa. Nyani Nguba aliposema hivi hakumaanisha wahindi waishio Afrika au makaburu pengine hata wale waarabu wa kaskazini kwetu hawakuwemo kwenye ramani yake. Kinachozungumziwa hapa ni Mwafrika Mmatumbi. Ndio maana wale wengine walio wazi katika kutetea hoja hii waliingiza neno Nyani!
Statistics zinaonyesha kuwa mtu mweusi anayetoka Afrika anafanya vizuri kuliko wamarekani weusi marekani na wale wanaotoka katika visiwa vya karibian huko uingereza. Hawa waafrika wanajitahidi mashuleni na kwenye maisha ni wahangaikaji kuliko wenyeji wao. Kwa bahati mbaya hii imewafanya waafrika kuwa na tabia ya kuwadharau weusi wenyeji. Si mara moja nimemsikia mswahili akiwazungumzia 'niggas' kwa dharau. tunasahau mzigo wa historia. Ingawa sisi nasi tulitawaliwa lakini hatukuwa dehumanised kama walivyo fanywa hao ndugu zetu. Afrika ya kusini tunaona wanavyohangaika na hali hii. Sisi tulikuwa kwetu, tukapata uhuru kwetu na katika sehemu nyingi, pamoja na juhudi za wageni, asili yetu ilibaki pale pale na ndiyo iliyoweza kutupa confidence.

Nadhani hapa tatizo ni kuwa hatujaweza hasa ku'define' utanzania wetu. Sidhani kama mtu unaweza kusema kweli kuna tamaduni ya kitanzania bali ni tamaduni mchanganyiko wa makabila na watu wote wanaoishi Tanzania. Kujenga identity sio kitu kidogo. Hao wazungu mpaka leo wanahangaika katika kujaribu kuji'define'. Hii kazi wasingeweza kuifanya hao unaowataja peke yao. Mchango wa watu kama Shaaban Robert, Mwinyimila, Salum Abdallah, Mathias Tinga Tinga na wengine wengi wote wamechangia. Kazi ni yetu wote kuwaenzi katika huu mradi wa kujenga utaifa wetu.
Mkuu, kumbuka kuwa kuanzisha ni rahisi kuliko kuendeleza.

Mimi ninachopinga kwenye dhana hii ni matumizi yake katika kuwakebehi waafrika na kuwakatisha tamaa. Hayo yote yanayotolewa mifano ni tabia, tamaduni ambazo zinaweza kubalika. Ulaya kulikuwa hakuishi na magonjwa yanayotokana na uchafu hadi hivi karibuni tu. Nchi/Mji wa Singapore ulipopata uhuru ulikuwa mchafu kupindukia wenye vibiashara vya ajabu na hivi sasa ni moja ya miji safi duniani! Tunawalaumu watanzania kwa kuendelea kuikumbatia CCM, mbona wamarekani wamemchagua George W mara mbili?

Tusikate tamaa, na tusikubali kukatishwa tamaa.

Amandla!!!


Fundi Mwenzangu:

Afu unasema ulikimbia umande. Kwa points unazoweka kwa nini basi tujenge shule? Tuambie tu ulipokuwa unakimbia umande, ulikuwa unakwenda wapi hili tuwapeleke watanzania wengine.

Kuna kasoro fulani katika mijadala yetu na anayeshinda mara nyingi anafikiri kuwa point zake ni za kweli kwa asilimia 100 na kusahau anayosema mpinzani wake. Na akiwa kiongozi wa nchi mara nyingi anaishia kufanya wrong things badly.

Kwa kuongezea mjadala wa waMarekani weusi. Mwanzo wa karne ya 20 kulikuwa na mashuhuri wawili Booker T. Washington na W.E.B Dubois.

Booker T. Washington alifanya kazi kubwa ya kuanzisha Tuskegee Institute na sasa ni University. Huyu bwana alipigania weusi wasome mambo ufundi stadi na aliona ni lazima watu weusi wajifunze mambo hayo hili wapate heshima na uwezo wa kufanya kazi za mikono kama wazungu.

Na aliona ni muhimu mtu mweusi akiwa shuleni ajifunze kuzalisha. Na haya yalitokana na background yake akiwa shuleni (Hampton institute).

Na umaarufu wake ulipoongezeka aliweza kushawishi wazungu kubadili mitaala ya vyuo vingine vya weusi. Kwa mfano Howard University ambayo tayari ilikuwa na mtaala kama university kubwa ilibidi kubadili mitaala yake na kuanza kufundisha kazi za mikono.

Ukisoma kitabu cha Booker T. Washington kuhusu kazi za mikono, utaona ni sawa na vitabu vya Nyerere kuhusu elimu ya kujitegemea.

Kitu kimoja ambacho Booker T. Washington hakukiona ni matumizi ya mashine. Unamfundisha mtu useremala wakati watu wanaanza kununua furniture sokoni kama wananunua nyanya. Unamfundisha mtu kazi za kushona nguo wakati nguo zitauzwa sokoni kama unanunua vitunguu.

Ushauri wa Booker T. Washington wa kufundisha watu weusi skill za nyumbani na shambani tu ulidumaza vyuo vya watu weusi kwa miaka mwingi.

Kwa upande wake W.E.B DuBois alisema kama nadharia ni muhimu kwa mtu mweupe basi ni muhimu kwa mtu mweusi pia. Ni lazima jamii iwe na watu wataoweza kufikiri katika abstract terms na kutoa critical analysis.
 
Bagosha ne Basungu Kinehe, Ulimhola wa mamishago!

Baada ya kusikiliza pande zote mbili za waliomo na wasiomo, naomba wote mrudie bandiko la kwanza nililolitoa liwe mwongozo wa kujua mwelekeo huu ni wapi!

Nilifanya kwa makusudi kabisa kwa kuanzia Waafrika nikaongeza kwa kubadilisha na kusema I mean Watanzania ndivyo tulivyo!

Lengo langu ni kujichangua sisi Watanzania kama Taifa na kama Wananchi. Naomba tusianze kukimbilia kujifananisha na Wamarekani Weusi au Watogo maana hata kama wao wanamitabia inayofanana fanana, suluhisho la kusahihisha dhana ya "hivi ndivyo tulivyo" kwa Tanzania ni jukumu letu na tujipime ni vipi tutajisahihisha kama tutasema ni dhana potofu. Tukisema ni dhana jenzi na marudufu, ni vipi tutaifanya iwe yetu wote?

Mimi nitaendela kuhoji kama nilivyohoji awali, ni kwa nini tunaendelea kulea na kuishi katika tabia ambazo si endelevu? Zaidi ni ule uvivu wa kujituma, kuchacharika na kufikiri! Mbaya zaidi ni ule utashi wa urahisi kujifanyia mambo tunavyotaka kwa kukiuka sheria au kuzipuuzia, Angamizi zaidi ni kule kutaka kupata mapato na manono bila kutoka jasho au kutumika!

Ndio maana nikauliza, je ndivyo tulivyo? je ndio tabia zetu hizo na tumeridhika nazo? je kelele zetu hapa ni mazoea na kawaida kulalamika tuu bila kuchukua hatua ya kupanga mawazo yetu, kutafakari ni nini tunakipigia kelele na kufanya utafiti wa kupatia ufumbuzi au ni kawaida kupiga domo kulalama na kuendelea kulalama kwa kila jipya?

Suala la nani ni sawa ni subjective, kutokana na utashi wako. Nyani kahoji tabia za watu kula pale Kipawa mbele ya uchafu, je "hivyo ndivyo walivyo"?

Mwanakijiji ananena, wale waliopiga kura dhidi ya CCM "sivyo walivyo" lakini machoni pa CCM, "ndivyo walivyo", je lini Mtanzania atapiga kura yake kwa kutafuta mtu wa kumpa haki na tumaini na si mazoea? Je Wapiga kura wetu wengi "ndivyo walivyo" na wameridhika "jinsi walivyo"?

Je kupiga kwetu kelele kudai haki, heshima, uwajibikaji, kupiga vita ufisadi na uhujumu kunapokelewa na Watanzania kama "JF ndivyo walivyo" na kupuuzwa?

Rev:

Kitu kimoja tunachoweza kufanya ni ku-set standards kwa Tanzania. Haya mambo ya kuangalia Mkenya ameshindwa kitu fulani na sisi tuwe na kisingizio cha kushindwa ni upuuzi mtupu.

Ni lazima tuwe na standards na sisi wenyewe tuwe tunafanya juhudi za kuvuka standards hizo.

Na kuanzia, tuanze na vitu vichache tu. Kwa miaka mingi tunajitahidi kufuta ujinga lakini nadhani kabla ya kujua kusoma na kuandika ni lazima mtu ashibe. Tukiweza kutatua matatizo ya chakula kuna uwezekano wa mambo mengine ku-solve yenyewe.
 
Wajameni

Mimi naona kwamba idea kubwa hapa ni "Ndivyo tulivyo" na "Ndivyo nilivyo" VS "Sivyo tulivyo" na "Sivyo nilivyo"

Pande zote mbili zinaweza kutoa mifano kibao ya kudhihirisha wanayoyajadili, hivyo basi mimi sinta taja kwamba nipo upande gani, nitaacha mawazo yangu yajieleze.

Mimi nakubaliana na wale wote ambao wanasema kwamba the fact that we are discussing this, ni proof kwamba "Sivyo nilivyo". Sisi hapa kama individuals, ukatuweka katika familia ya JF, sivyo tulivyo. Ila ukituweka kama kundi la Watanzania hapo mmmnnhhhh...

Watanzania miaka mingapi tunachagua viongozi, wanaboronga, wanaendelea na business as usual. Tumlaumu nani kwa kuendelea kuwa na mafisadi na wazembe katika uongozi? Kama kweli watu tunaanza kubadilika, iko wapi list ya wale waliorudisha billioni 50? Kwa nini iwe just 80% will be recovered? kwa nini isiwe 100% ? Na sisi wananchi tunafanya nini ili kubadili huu mfumo wa ufisadi? Je Ndivyo tulivyo? Je ndivyo nilivyo?

Tanzania kuna opportunities nyingi sana, nafikiri tunakubaliana katika hili. Lakini hata hivyo bado wako watu wetu wengi sana ambao wanatumia vibatari kwa mwanga usiku, hawaja move up even kutumia chemli. Je ndivyo tulivyo? Je hatuwezi?

Mimi naamini kwamba kama kuna kibaya wazungu walichotutenda zaidi ya kutubeba utumwani, ni kutukandamiza fikra. Kule kuamini kwamba "Tamaduni zenu ni za kishenzi" etc, ndiko kunakotufanya tu "look up to them" kama vile ndio kipimo cha direction ya maendeleo yetu. Wakati ambapo, laba tungeyasukuma maendeleo yetu sisi wenyewe labda tungechukua direction tofauti kabisa. Who knows, ingezekana kusafiri kwa ungo! Wao wanaita "Teleportation" inawezekana teleportation inaweza kuwa implemented kwa ungo!! But Noooooo, hayo ni ya kishenzi!!!

Je ndivyo tulivyo? Kwamba Watanzania tuko tayari na tunashukuru kupokea misaada na ufadhili kutoka nje bila hata kuwa na Pride? Iko wapi pride yetu ya kufanya kazi? Kwa nini tuko tayari "kununuliwa"? Wangapi kati yetu leo hii akipewa dola 10000, (For nothing, no strings attached) anaweza kuikataa just kwa sababu he didnt work for it? Je ndivyo tulivyo?

Je ndivyo nilivyo? Hapana hapana hapana!! Je ndivyo tulivyo? Ndiyo. Mimi naungana na Mzee mwanakijiji kuzipiga vita hizi fikra na kujaribu kuleta fikra za "self worth" na kuwa proud kujitegemea. Tujenge shule zetu wenyewe, tujenge barabara zetu wenyewe, tuwafundishe watoto wetu kuipenda elimu sisi wenyewe, tupige vita rushwa na adha za kijamii sisi wenyewe, tubadilishe serikali yetu sisi wenyewe, tujitosheleze kwa chakula sisi wenyewe, tufanye R&D za kwetu na tuzi fund wenyewe! Hakuna cha "aah sisi hayo mambo hatuwezi" hao walioweza wamewezaje??

Tuondoe fikra za "Ndivyo tulivyo" kwamba "hatuwezi", "sisi ni masikini", "tuna matatizo ya malaria" etc etc etc. Tuwe na fikra za kwamba tunaweza, au tujaribu tuone!! Inawezekana "mchunga" na "mnavu" ni dawa ya kasa!! Mtu hata hujajaribu unaanza kusema its impossible!!! Unabisha!

Tubadilike na tujaribu kubadilisha jamii yetu. Mimi nina imani kuwa wengi wetu humu JF kama individuals tunaangukia kwenye "Sivyo nilivyo", basi ni wajibu wetu sisi kuiambukiza jamii ili tuelekee wote kwenye "Sivyo tulivyo"

Nahavache.
 
Unasema kitu kibaya wazungu walichotutenda zaidi ya kutubeba utumwani, ni kutukandamiza fikra. Sasa kwa nini walitukandamiza na sisi tukakubali tu huku tukijua kwa hivyo wanavyofanya si sahihi? Kama tulikuwa tunatambua kosa hilo kwa nini hatukulikataa au kwa vile Ndivyo Tulivyo tulishindwa hata kukataa?

Na kwa nini hatukuwabeba wao utumwani au kwenda kuwatawala kwao kama walivyotutawala sisi wakati wa ukoloni?

Kwa nini nchi kama Zimbabwe iliyokuwa nuru ya matumaini barani Afrika wakati inapata uhuru sasa hivi imekuwa kichekesho na kutia huruma? Wananchi wake wanakula panya...wengine wengi tu wanakimbilia hadi Msumbiji....mfumuko wa bei umefikia asilimia 66,000...kwa nini?
 
Bubu,

Kiteto folks had a chance and they blew it, the question is why? why did they find comfort to vote back Mtu wa CCM? Even if huyo Mbunge could have been a Saint, but he belongs to a party of Thieves, why in the heck did they give him a mandate and increase the dominance of Chama cha Mafisadi? Isn't it "ndivyo walivyo" wameridhika na Zimwi liwajualo?

wale 21 elfu or so ndivyo walivyo, wale 12,000 hivi sivyo walivyo!
 
Unasema kitu kibaya wazungu walichotutenda zaidi ya kutubeba utumwani, ni kutukandamiza fikra. Sasa kwa nini walitukandamiza na sisi tukakubali tu huku tukijua kwa hivyo wanavyofanya si sahihi? Kama tulikuwa tunatambua kosa hilo kwa nini hatukulikataa au kwa vile Ndivyo Tulivyo tulishindwa hata kukataa?

Na kwa nini hatukuwabeba wao utumwani au kwenda kuwatawala kwao kama walivyotutawala sisi wakati wa ukoloni?

Kwa nini nchi kama Zimbabwe iliyokuwa nuru ya matumaini barani Afrika wakati inapata uhuru sasa hivi imekuwa kichekesho na kutia huruma? Wananchi wake wanakula panya...wengine wengi tu wanakimbilia hadi Msumbiji....mfumuko wa bei umefikia asilimia 66,000...kwa nini?

soma kitabu cha Walter Rodney, How Europe Underdeveloped Africa...
 
soma kitabu cha Walter Rodney, How Europe Underdeveloped Africa...

All he does in his book is whine about white people...he doesn't offer any solutions or anything...to him the problem is white people

Oh so how did Europe underdevelop South Africa..?
How did Europe underdevelop Ethiopia?...they were never colonized. How did Europe underdevelop Liberia?
 
Back
Top Bottom