Vyuo vikuu nchini haviwatendei haki wasabato??

Vyuo vikuu nchini haviwatendei haki wasabato??

Pia haviwatendei haki Waislamu kwa kuendelea na shughuli zake kama kawaida siku za Ijumaa??

Tume ya uchaguzi pia haiwatendei haki wakristo kwa kufanya uchaguzi siku za Jumapili?

Kwahiyo Serikali pia haitutendei haki wanandoa maana tulipaswa tupumzike siku ya Jumatatu??

Visabato masalia vina lalamika kama makalio ya konki konki...
Je kuna andiko lolote kwenye Koran linakukataza kufanya kazi siku ya sita ya juma (Ijumaa) maana inakukataza kufanya kazi siku ya Jumamosi (Sabato) au hauna habari?
 
Je kuna sehemu yoyote ktk Biblia Yesu alifanya/zungumzia (kuhusiana na Sabato) kazi tofauti zaidi ya kuokoa uhai (mfano : kuponya, kula n. k)?
Tutende yaliyo mema!!! Alisema hvyo, je mema ni kuponya tu? Mema ni kula tu?
 
Hapo na mm najiuliza sana kwanini padri Martin Luther alipojitoa RC, kwanini hakuanzisha utaratibu wa kusali siku nyingne tofaut na jpl? Nazan aliona SIKU haina shida bali MAFUNDISHO ya kanisa
Martin Luther, mwasisi wa kanisa la Kilutheri, aliandika katika ungamo la Augusiburgi (Augusburg Confession), sharti la imani la 28, aya ya 9, maneno haya: "Wao [Wakatoliki wa Roma] wanadai kwamba Sabato ilibadilishwa na kuwa Jumapili, siku ya Bwana, kinyume na ile sheria ya Amri kumi,.. wala hakuna mfano wanaojivunia sana kama huo wa kuibadili siku ya Sabato. Ni mkuu, wasema wao, uwezo na mamlaka ya Kanisa, kwa kuwa liliiondoa mojawapo ya zile Amri kumi."

Wanatheolojia wa Kimethodisti Amosi Binney na Danieli Steele walitoa maoni yao haya:
"Ni kweli, hakuna amani dhahiri ya ubatizo wa watoto wachanga….wala hakuna yo yote ya kuitakasa siku ya kwanza ya juma." Theological Compend (New York: Methodist Book Concern, 1902), Kurasa 180,181.

Dk. N. Summerbell, mwanahistoria wa wanafunzi wa Kristo (Disciples of Christ) au Kanisa la Kikristo (Christian Church), aliandika, alisema:
"Kanisa la Roma lilikuwa limeasi kabisa…..Liliigeuza Amri ya Nne kwa kuiondoa Sabato ile ya Neno la Mungu, na kuiweka Jumapili kama siku takatifu" A True History of the Christian and the Christian Church, kurasa za 417,418.
 
"'Kama ukigeuza mguu wako usihalifu sabato, usifanye anasa yako siku ya utakatifu wangu; ukiita sabato siku ya furaha, na siku takatifu ya Bwana yenye heshima; ukiitukuza, kwa kutokuzifanya njia zako mwenyewe, wala kuyatafuta yakupendezayo, wala kusema maneno yako mwenyewe'' Isa.58:13

Ikumbuke siku ya sabato uitakase,Siku sita fanta kazi, utende mambo yako yote. Lakini siku ya saba ni sabato ya bwana Mungu wako.Kutoka 20 :8-11
 
Je kuna sehemu yoyote ktk Biblia Yesu alifanya/zungumzia (kuhusiana na Sabato) kazi tofauti zaidi ya kuokoa uhai (mfano : kuponya, kula n. k)?
Yakobo, kiongozi wa kwanza wa kanisa lile la mwanzo, aliandika maneno haya kuhusu zile Amri kumi:


"Anayevunja amri mojawapo ya sheria, atakuwa na hatia ya kuivunja sheria yote. Maana yule yule aliyesema: "USIZINI, "alisema pia" "USIUE." Kwa hiyo, hata ikiwa hukuzini, lakini umeua, wewe umeivunja sheria" - (Yakobo 2:10, 11).

Luka, tabibu na mwinjilisti katika kanisa lile la kwanza, anatoa taarifa hii.

"Siku ya Sabato tukatoka nje ya mji, tukaenda kando ya mto, ambapo tulidhani kuwa mahali pa kusali. Tuliketi, tukiongea na wanawake waliokusanyika mahali hapo" - (Matendo 16:13).

Kitabu cha Matendo cha Agano Jipya kinataja mara 84 ilipotunzwa. Sabato hiyo na wafuasi wa Kristo, zote hizo zilikuwa zikitunzwa zaidi ya miaka 14 baada ya ufufuo wa Yesu: Sabato 2 pale Antiokia (Matendo 13:14,42,44); 1 pale Filipi (Matendo 16:13), 3 pale Thesalonike (Matendo 17:2,3), Sabato 78 pale Korintho (Matendo 18:4,11).

Yohana, wa mwisho kufa miongoni mwa wale mitume kumi na wawili, aliitunza Sabato. Aliandika hivi:
"Siku ya Bwana nilikuwa katika Roho" - (Ufunuo 1:10).

Kulingana na maneno ya Yesu, siku ya Bwana ni Sabato:
"Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa Sabato" - (Mathayo 12:8).
 
mm nna ushauri tu,

hoja zinazohusisha dini hua haziishi coz kila mtu anaamini ktk kile anachoamini, so tuwaacheni tu hawa ndugu waamue ya kwao ilomradi tu hawaingilii Uhuru wetu.

pia kwa mnaopenda mabishano kuwen makini maana hawa jamaa ata ukibishana nao mpaka kesho hamna utakachoambulia; ni watu wanaojaribu kujitetea siku zote na Mara zote atataka muongelee kile anachokijua.

mfano,
angalia comment ya hapo juu ya attachment ya gazeti,
then jiulize,

upapa una uhusiano gani na mahafari ya vyuo vikuu Tz kama Uzi unavyoeleza.

utagundua kua anataka mjadili anachokijua yeye.

so please,

speak only when your words are more important than your silence

ni ushauri tu
Una mahusiaano makubwa sana , kwakuwa upo kama nyumbu hivo huwez kuelewa,

Hivi unajua anayeipinga IBADA YA sabato ni UPAPA aliyepewa nguvu na JOKA

JE UNAJUA IBADA YA JUMAPILI MNAYOIPIGIA DEBE ,ni pando kutoka ROMA?
FB_IMG_1540766508618.jpeg
 
Pia haviwatendei haki Waislamu kwa kuendelea na shughuli zake kama kawaida siku za Ijumaa??

Tume ya uchaguzi pia haiwatendei haki wakristo kwa kufanya uchaguzi siku za Jumapili?

Kwahiyo Serikali pia haitutendei haki wanandoa maana tulipaswa tupumzike siku ya Jumatatu??

Visabato masalia vina lalamika kama makalio ya konki konki...
Si jambo jema hata kidogo kudharau imani ya mtu mwingine hata katiba ya nchi hii inatamka hivyo, sasa matusi uloyasema yanaonesha huna ustarabu.
 
Habari wana jamii!

Zikiwa zimebaki siku chache tu kabla ya kufanyika kwa mahafari ya kuhitimu chuo kikuu, nina sikitika kuona kwamba rafiki zangu wengi wasabato hawachangamki kabisa.

Jana tumetoka kulipia majoho lakini nikashangaa kuona rafiki zangu wasabato hawalipii (siowote) na sababu kubwa ya kutolipia ni kwamba sherehe hiyo ya kuhitimu chuo inafanyika siku ya jumamosi ambayo ni siku yao ya kuabudu.

Idadi kubwa ya vyuo vikuu nchini hapa hufanya sherehe hizi siku ya jumamosi hivyo kuwanyima nafasi ya kushiriki ndg zetu hawa wasabato.

Na ninyi wasabato mje hapa mtuambie ubaya wa kushiriki siku ya jumamosi maana kwa mtizamo wangu siku hiyo hufanyi kazi ni sawa na kupumzika kabisa huku ukifrahia kujumuika na wenzako.

Karibuni tueleweshane.
Kwani Jumamosi walikuwa hawaingii darasani kusoma?
 
Hapo na mm najiuliza sana kwanini padri Martin Luther alipojitoa RC, kwanini hakuanzisha utaratibu wa kusali siku nyingne tofaut na jpl? Nazan aliona SIKU haina shida bali MAFUNDISHO ya kanisa
Wewe huna akili na unafata mkumbo,

Martin luther mwenyewe katoka RC lkn alikuwa bado anachunguza maandiko, na bado kuna upagani mwingi alikuwa anaurekebisha ,amekufa bado hajamaliza kazi

Na ndio wafuasi wake wakaishia hapo alipoishia yeye,

Ndio maana Leo WARUTHER bado wana upagani kutoka roma ,

Na sasa wamerudi tena kwa MAMA YAO KANISA KATOLIKI
FB_IMG_1540123502299.jpeg
 
Acha kutisha watu wewe! Jibu hoja!!!

Nimisema Wazungu na Wasabato walileta Ukiristo kama chombo cha kukutawala sisi Waafika!! Sasa wewe kwa nini unatisha watu?
Wahindi, Wajapani wana dni zao hadi lei hii.. ila Mwafrika aliacha dini zake akakubali kutumia dini ya Mzungu na Mwarabu!

Nini hapo huelewei!!

Jibu hoja na acha kutisha watu!
😀 😀 😀 Mimi ni nani hadi nitishe mtu aisee kama unaamini ililetwa na wazungu fine take it as yours.
 
Propaganda
Luka, tabibu na mwinjilisti katika kanisa lile la kwanza, anatoa taarifa hii.

"Siku ya Sabato tukatoka nje ya mji, tukaenda kando ya mto, ambapo tulidhani kuwa mahali pa kusali. Tuliketi, tukiongea na wanawake waliokusanyika mahali hapo" - (Matendo 16:13).

Kitabu cha Matendo cha Agano Jipya kinataja mara 84 ilipotunzwa. Sabato hiyo na wafuasi wa Kristo, zote hizo zilikuwa zikitunzwa zaidi ya miaka 14 baada ya ufufuo wa Yesu: Sabato 2 pale Antiokia (Matendo 13:14,42,44); 1 pale Filipi (Matendo 16:13), 3 pale Thesalonike (Matendo 17:2,3), Sabato 78 pale Korintho (Matendo 18:4,11).

FB_IMG_1540120406498.jpeg
 
  • Thanks
Reactions: HDP
Si jambo jema hata kidogo kudharau imani ya mtu mwingine hata katiba ya nchi hii inatamka hivyo, sasa matusi uloyasema yanaonesha huna ustarabu.
Nioneshe tusi nililotukana hapo...
 
Hakuna anayeabudu siku, kama ni hivo bas wa kwanza ni Mungu , maana hata YESU alitunza sabato, luka 4:16 ,sasa niambie ALIABUDU SIKU?

WEWE biblia gan imekupa mandate ufanye ibada jumapili?

HUO NDIYO UKWELI! SOMA BIBLIA UPATE MAARIFA,ASANTE MTUMISHI
 
Luka, tabibu na mwinjilisti katika kanisa lile la kwanza, anatoa taarifa hii.

"Siku ya Sabato tukatoka nje ya mji, tukaenda kando ya mto, ambapo tulidhani kuwa mahali pa kusali. Tuliketi, tukiongea na wanawake waliokusanyika mahali hapo" - (Matendo 16:13).

Kitabu cha Matendo cha Agano Jipya kinataja mara 84 ilipotunzwa. Sabato hiyo na wafuasi wa Kristo, zote hizo zilikuwa zikitunzwa zaidi ya miaka 14 baada ya ufufuo wa Yesu: Sabato 2 pale Antiokia (Matendo 13:14,42,44); 1 pale Filipi (Matendo 16:13), 3 pale Thesalonike (Matendo 17:2,3), Sabato 78 pale Korintho (Matendo 18:4,11).

View attachment 926328
Yani wewe mtu anakujibu na sentensi moja wewe unakuja na essay khaaa endelea na essay zako
 
  • Thanks
Reactions: etb
Yani wewe mtu anakujibu na sentensi moja wewe unakuja na essay khaaa endelea na essay zako
Kwakuwa umezoe , kuburuzwa na kusomewa maandiko na mapadri na manabii fake ,ndio maana hizo paragraph 3 zilizojaa MAANDIKO YA MUNGU , unaona ni ESSAY
 
Kwakuwa umezoe , kuburuzwa na kusomewa maandiko na mapadri na manabii fake ,ndio maana hizo paragraph 3 zilizojaa MAANDIKO YA MUNGU , unaona ni ESSAY
Nabii feki ni wewe na unaye muabudu. Mungu wangu ninaye muabudu ni tofauti na wako
 
  • Thanks
Reactions: etb
Back
Top Bottom