Vyuo vikuu nchini haviwatendei haki wasabato??

Vyuo vikuu nchini haviwatendei haki wasabato??

Ila yesu alisema sio vibaya kutenda yaliyo mema siku ya sabato. Kuna vyuo kama tumaini na sauti hivi ni vya dini kabisa tena vina dressing code kwahyo huwez kukuta mavazi mabaya wala pombe hadi maaskofu wana hudhuria. Kwanini msishiriki?
Siku ya Sabato ni Mali ya BWANA hatupaswi kufanya chochote ila kinacholeta Utukufu kwa Muumbaji wetu. Kwa nionavyo Graduation haileti Utukufu wowote kwa Mungu zaidi ni kwa ajiri kujifurahisha sisi wenyewe.
'"lakini siku ya saba ni Sabato ya Bwana, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yo yote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako"" Kut.20:10.
 
Pia haviwatendei haki Waislamu kwa kuendelea na shughuli zake kama kawaida siku za Ijumaa??

Tume ya uchaguzi pia haiwatendei haki wakristo kwa kufanya uchaguzi siku za Jumapili?

Serikali pia haitutendei haki wanandoa maana tulipaswa tupumzike siku ya Jumatatu.

Visabato masalia vina lalamika kama makalio ya konki konki...
umejibu vizuri japo umemaliza vibaya
 
Pia haviwatendei haki Waislamu kwa kuendelea na shughuli zake kama kawaida siku za Ijumaa??

Tume ya uchaguzi pia haiwatendei haki wakristo kwa kufanya uchaguzi siku za Jumapili?

Serikali pia haitutendei haki wanandoa maana tulipaswa tupumzike siku ya Jumatatu.

Visabato masalia vina lalamika kama makalio ya konki konki...
nimejikuta nimetoa chozi la kicheko
 
Tembea uone, usingoje kuambiwaa.. Watu tumesali Ijumaa badala ya j.pili kisa Ijumaa ndo siku ya kuabudu. Hatukupinga, Tukaenda Israel ambapo J.mosi ni siku ya ibada tukasali siku hiyo ingawa J. pili vile inaheshimia. Tumeenda nchi ambayo Buddhism ndo dini na wenyewe hata J.pili ni siku ya kazi ila kama kuna Full moon, likizo siku tatu. Sasa mwenzetu wewe unaweza mudu kuzunguka dunia? Ji tune kila unapoenda ili ulingane na mazingira. Mbona Jeshini tulikuwa tunaambiwa kwenda kusali tukirudi tunadaiwa mizigo ya kuni. Maafande hawakujua siku ya J.pili ni siku ya kupumzika?? Kaa na dini kichwani mwako maisha yanasonga. Imani yako siyo ya jirani yako.
 
Siyo lazima kufanya graduation furaha yako siku moja haipaswi kututenganisha na Mungu wetu sabato ni siku maalumu ya Mungu haipaswi kuhalifiwa kwa ajili ya chochote kile,

Bwana awabariki hao walioamua kutii na kumuheshimu katika sabato yake Amina
 
Pia haviwatendei haki Waislamu kwa kuendelea na shughuli zake kama kawaida siku za Ijumaa??

Tume ya uchaguzi pia haiwatendei haki wakristo kwa kufanya uchaguzi siku za Jumapili?

Serikali pia haitutendei haki wanandoa maana tulipaswa tupumzike siku ya Jumatatu.

Visabato masalia vina lalamika kama makalio ya konki konki...
suala la imani ni mtambuka sana....
kama imani yako inayokuelekeza kusali jumatano haikuelekezi kupumzika siku hiyo ni tofauti sana na mwingine anayesali jumamosi na imani yake kumuelekeza kupumzika na kutojishughulisha kwa chochote siku hiyo..

Ikumbuke siku ya sabato uitakase. Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote; lakini siku ya saba ni sabato ya BWANA, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yo yote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya mlango yako. Maana kwa siku sita BWANA alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo akastarehe siku ya saba; kwa hiyo BWANA akaibarikia siku ya sabato akaitakasa.
 
Ila hawa watu mm siwaelewi. Pale udsm kunaticha walimgomea kufanya pepa Jumamosi nayeye akagoma kutunga pepa mbili. Wakaenda hadi kwenye uongozi, so ticha akasema poa haina shida ntatunga pepa mbili. Unaambiwa hiyo jumamosi aliyepata nyingi ni 2. Na wote walirudi September. Siku nyingine ,second year, ticha akaweka tena pepa Jumamosi wote wakaja bila kubisha.
Nikagundua hawa jamaa hawana msimo.
 
Back
Top Bottom