Kiranga
Platinum Member
- Jan 29, 2009
- 85,949
- 146,195
Waanzishe chuo chao tu.Habari wana jamii!
Zikiwa zimebaki siku chache tu kabla ya kufanyika kwa mahafari ya kuhitimu chuo kikuu, nina sikitika kuona kwamba rafiki zangu wengi wasabato hawachangamki kabisa.
Jana tumetoka kulipia majoho lakini nikashangaa kuona rafiki zangu wasabato hawalipii (siowote) na sababu kubwa ya kutolipia ni kwamba sherehe hiyo ya kuhitimu chuo inafanyika siku ya jumamosi ambayo ni siku yao ya kuabudu.
Idadi kubwa ya vyuo vikuu nchini hapa hufanya sherehe hizi siku ya jumamosi hivyo kuwanyima nafasi ya kushiriki ndg zetu hawa wasabato.
Na ninyi wasabato mje hapa mtuambie ubaya wa kushiriki siku ya jumamosi maana kwa mtizamo wangu siku hiyo hufanyi kazi ni sawa na kupumzika kabisa huku ukifrahia kujumuika na wenzako.
Karibuni tueleweshane.
Wakatoliki wameweza.
Ikiwa kila mtu atataka siku yake watu wasifanye kazi,kutakuwa hakuna siku ya kufanya kazi.