Vyuo vikuu nchini haviwatendei haki wasabato??

Vyuo vikuu nchini haviwatendei haki wasabato??

Habari wana jamii!

Zikiwa zimebaki siku chache tu kabla ya kufanyika kwa mahafari ya kuhitimu chuo kikuu, nina sikitika kuona kwamba rafiki zangu wengi wasabato hawachangamki kabisa.

Jana tumetoka kulipia majoho lakini nikashangaa kuona rafiki zangu wasabato hawalipii (siowote) na sababu kubwa ya kutolipia ni kwamba sherehe hiyo ya kuhitimu chuo inafanyika siku ya jumamosi ambayo ni siku yao ya kuabudu.

Idadi kubwa ya vyuo vikuu nchini hapa hufanya sherehe hizi siku ya jumamosi hivyo kuwanyima nafasi ya kushiriki ndg zetu hawa wasabato.

Na ninyi wasabato mje hapa mtuambie ubaya wa kushiriki siku ya jumamosi maana kwa mtizamo wangu siku hiyo hufanyi kazi ni sawa na kupumzika kabisa huku ukifrahia kujumuika na wenzako.

Karibuni tueleweshane.
asante kwa swali lako zuri , kufanya kazi siku ya j mosi ni dhambi kwa sababu mungu alifanya uumbaji ndani ya siku sita na siku ya saba[j mosi ] alipumzika siku hiyo aliitakasa na kuibariki , siku hiyo hautakiwi kufanya kazo yoyote ile mbali na kuabudu 222222222222222
 
Ila hawa watu mm siwaelewi. Pale udsm kunaticha walimgomea kufanya pepa Jumamosi nayeye akagoma kutunga pepa mbili. Wakaenda hadi kwenye uongozi, so ticha akasema poa haina shida ntatunga pepa mbili. Unaambiwa hiyo jumamosi aliyepata nyingi ni 2. Na wote walirudi September. Siku nyingine ,second year, ticha akaweka tena pepa Jumamosi wote wakaja bila kubisha.
Nikagundua hawa jamaa hawana msimo.
olewake huyo lecture angekutana na mimi angemjua mwenye Sabato ni nani,chuoni nilikuwa na msimamo kumtii Mungu kuliko mwanadamu kwa kiburi na madharau hayohayo ya malecture kufanya mitihani siku ya Sabato kutukomoa WASDA na nilitoka na first class,mwanzoni wenzangu walikata tamaa nikawatia moyo kwamba wasiogope hata wakitunga pepa mbili, tulitoboa hawatasahau. Mungu alitufanya vichwa
 
Kuna mambo ukikurupuka unageuka kuwa mtumwa..maandiko yako wazi ..Yesu aliuliza ni nani kwenu ng'ombe wake akitumbukia shimoni siku ya sabato hata mtoa?

Imani zingine ni mateso makubwa kwakweli...wana heri wa Muabudio Mungu ktk roho na kweli na wala si kwa siku wala muandamo wa mwezi
elewa maandiko wewe umsukume ng`ombe shimoni halafu usingizie katumbukia,Mungu hadhihakiwi
 
Hii ilitokeaga chuo kimoja waislamu walienda omba mtiani usongezwe masaa mbele ili wapate time ya kwenda swali walivyorudi chuo wanakuta tangazo lingine mtiani ni juma 3 maana wasabato nao kwanzia SAA 12 wanaanza sabato yao
 
2- Serikali yetu haina dini lkn jamii inawwza kuweka utaratibu kwa ajiri ya kuwapa watu Uhuru wa kuabudu kufuatia na kile wanachoamini. Hivyo usitwambie kuhusu upapa, twambie/ tupe ushauri ambao unahisi kua utasaidia sabato japo unapotoa ushauri kumbuka kua sabato sio kipaumbele cha jamii na si chochote kwa jamii bali dini kama dini zingine hivyo usilazimishe jamii ikufuate wewe.

Watu wamelewa mvinyo wa kidini. Habari za kwamba serikali haina Dini kwao hazina mashiko. They are more obsessed to their religious principles than government principles.

Binadamu hutoonekana mkamilifu kwakua umeweza kuonesha udhaifu wa mwenzio.
Point noted. You are good.
 
Back
Top Bottom