Vyama vya siasa ya Upinzani kushambulia vyama vya wafanyakazi ni mkakati au Heche na Nondo wanatumika?

Adharusi

JF-Expert Member
Jan 22, 2012
14,402
7,310
Msingi wa vyama vyote siasa Duniani umezaliwa ubavuni mwa vyama vya wafanyakazi. Kwa sababu kundi la vyama vya wafanyakazi wote wanakua wamesoma na werevu, ndio kundi la kwanza kuona ukandamizaji katika jamii, na kuanza kutoa elimu kwa jamii.

Vyama vya wafanyakazi mara nyingi kazi ngumu ya kupambana na muajiri, wakiwa wameweka rehani ajira yao. Ndio maana viongozi wengi wa vyama vya wafanyakazi wanapoteza ajira zao kwa sababu ya kupigania ustawi wa wanaowapigania, wanapoteza mahusiano na muajiri katika mazingira ya kazi.

Kuna tofauti kubwa kati ya vyama vya wafanyakazi na vyama vya siasa. Viongozi wa vyama vya siasa wapo huru kupambana na dola kwasababu hawako ndani ya ajira ,na hawana cha kupoteza.

Viongozi wa vyama vya wafanyakazi ni waajiriwa yaani wanapambana muajiri ambae anaweza kuwa serikali au sekta binafsi lakini ni muajiriwa tofauti kubwa sana.

Kuna tofauti kubwa sana ufanyaji wa kazi vyama vya siasa na vyama vya wafanyakazi, ukiona mtu kiongozi wa chama cha wafanyakazi hata kama ni ngazi ya Tawi mpe heshima yake, maana amejitoa muhanga kwa ajili ya wenzake.

Kwahiyo Abdul Nondo na Heche labda hawajui historia ya vyama vya wafanyakazi, wakae na waombe hitoria sio kudharau na kushambulia vyama vya wafanyakazi sitaki kuamini kuwa wamekodiwa kwa mradi maalumu kushambulia vyama vya wafanyakazi.

Vyama vya wafanyakazi vipo kwa mujibu wa sheria ya ajira na mahusiano kazini,sheria ya majadiliano. Kwahiyo wananjia za kupita katika majadiliano kabla ya kupiga kelele.

Nimeona Heche akishambulia vyama vya wafanyakazi Mara ya kwanza nilidhani bahati mbaya, juzi nimemuona ameshambulia chama walimu Tanzania, na kudharau kabisa CWT kwangu inaniambia hana taarifa za kutosha namna vyama vinavyofanya kazi, akae atafute watu wamuelimishe na asome sheria ya ajira na mahusiano kazini sasa huyu ni kijana kutoka chadema alikua kiongozi wa vijana chadema

Nimemuona tena kijana wa ACT Wazalendo Abdul Nondo, huyu ameandika hadithi nyingi akishambulia viongozi wa CWT, na kumpigania aliekua katibu mkuu 2020 mpaka June 28 ,2022.

Nondo anaonekana kabisa kanunuliwa kumpigia chapuo Aliekua Katibu mkuu Thefu, ambae alifungwa miezi sita kwa uchepushaji wa fedha ,ni kweli amekata rufaa ni haki yake lakini kimaadili tu peke yake hastahili hata kusogelea CWT.

Kipindi cha Thefu na mtandao wake CWT ilijaa udikteta, waliondoa viongozi wote waliokua na mawazo ya kuwajali walimu, walifuta mkono wa kwaheri, walifuta Tshirt kwa walimu ,walinyima uhuru wa wanachama kutoa maoni yao.

Sasa baada ya kuingia Katibu mkuu mpya ,anarudisha fedha wilayani, Thefu alikataa kupeleka fedha wilayani, sasa hivi chama kimeandaa mikutano mikuu bila kukopa fedha ,wananunuaa Tshirt za walimu wote ,ambayo Thefu alishafuta na genge lake, Thefu alinunua media zote na watu maarufu wakiwepo Thadeo Mushi kumpamba kwenye mitandao ya kijamii.

Niwaambie Heche na Nondo kama wametumwa kushambulia vyama vya wafanyakazi, wajiandae kundi wanalolishambulia ndio kubwa na werevu kuanzia katika vijiji.

Pia wanatakiwa kujua bila vyama vya wafanyakazi, wafanyakazi wnagekua wanyonge sana kwa muajiri

Jukumu la vyama vya siasa ni kutetea makundi yote kwenye jamii na kuungana makundi yote yanayopigania haki ya jamii ikiwepo kundi la vyama vya wafanyakazi sio kuwabeza.
 
Vyama vya wafanuakazi kwa ufupi havina tija yoyote kwa mfanyakazi!
Angalia mafao yao yanavyopunjwa! Vikokotoo vya unyonyaji mkubwa!yanavyokatwa kodi wakati kodi zililipwa! inavyochukua muda mrefu kulipwa mafao yao!
dawa ni kujitoa kuchangia hivi vyama kwani havina msaada wowote!
 
Vyama vya wafanuakazi kwa ufupi havina tija yoyote kwa mfanyakazi!
Angalia mafao yao yanavyopunjwa! Vikokotoo vya unyonyaji mkubwa!yanavyokatwa kodi wakati kodi zililipwa! inavyochukua muda mrefu kulipwa mafao yao!
dawa ni kujitoa kuchangia hivi vyama kwani havina msaada wowote!
Umenena ukweli mtupu. Ubarikiwe sana. Hivi vyama vya wafanyakazi havina msaada wowote zaidi ya kuendeleza unyonyaji kwa wafanyakazi.
 
Adharus,inawezekana una macho lakini hayaoni.CWT imeshapoteza sifa ya kuwa chama cha wafanyakazi!Wanachama wake ndio wanaongoza kwa kuwa na masilahi duni,hakuna posho Wala marupurupu ya maana,lakini chama hakiwezi kuitisha mgomo Wala kushinikiza kwa njia yoyote kudai masilahi bora.Kwanini hawawezi?Kwa sababu chama kimetekwa na CCM!Hata baadhi ya makada wa CCM ni viongozi wa CWT.Kwahiyo Heche kuishambulia CWT ni kama anashaishambulia ccm,mpinzani wake wa siku zote.
 
UWT ni zaidi ya Chadema

UWT ina Wabunge zaidi ya 150 wakati Chadema ina mbunge mmoja tena naye yuko UWT
chadema haitegemei ubunge ni mpumbavu tu ndio anaweza kufikria ubunge kwa chadema by the way hao wabunge 150 wa uwt mbona hawawez hata kuitisha hata mkutano kuprove kuwa wako active au ni ubunge wa mchongo wa kuliletea Taif a hasara ambazo CAG amekuwa akitoa taarifa.
NB, ccm na wafuas wao ni mapumbavu hayana reasoning capacity kama yamekatwa shingo.
 
Adharus,inawezekana una macho lakini hayaoni.CWT imeshapoteza sifa ya kuwa chama cha wafanyakazi!Wanachama wake ndio wanaongoza kwa kuwa na masilahi duni,hakuna posho Wala marupurupu ya maana,lakini chama hakiwezi kuitisha mgomo Wala kushinikiza kwa njia yoyote kudai masilahi bora.Kwanini hawawezi?Kwa sababu chama kimetekwa na CCM!Hata baadhi ya makada wa CCM ni viongozi wa CWT.Kwahiyo Heche kuishambulia CWT ni kama anashaishambulia ccm,mpinzani wake wa siku zote.
Inawezekana huna elimu ya kutosha kuhusu vyama vya wafanyakazi ,uwepo wa vyama vya wafanyakazi una tija kubwa sana kwa wafanyakazi

Stahiki mbalimbali katika maeneo ya kazi zinatolewa kwa hofu ya vyama vya wafanyakazi bila vyama vya wafanyakazi watumishi wataonea sana
 
Umenena ukweli mtupu. Ubarikiwe sana. Hivi vyama vya wafanyakazi havina msaada wowote zaidi ya kuendeleza unyonyaji kwa wafanyakazi.
Huna elimu ya kutosha kuhusu vyama vya wafanyakazi, yako mengi yanafanyika kwa njia majadiliano katika ya serikali na vyama vya wafanyakazi, usione stahiki unazopata zinakuja kwa kutaka tu muajiri, muajiri hatekelezi bila kusukumwa
 
Ngoja tuone

Kwani hiyo CWT na Chadema Wana tofauti gani?

Au CWT na ACT Wazalendo mbona zinafanana sana!
Bora umeuliza swali ,je kutokana na chadema na ACT kuungana na serikali, wananchi wawafukuze viongozi wa vyama vya upinzani, ila kwa kuheshimu kuwa msemo wa " saa mbovu kuna muda inasema ukweli"
Kwahiyo uwepo wao hata kama hawana makali wanasaidia kupunguza uonevu kwa Raia
 
Vyama vya wafanuakazi kwa ufupi havina tija yoyote kwa mfanyakazi!
Angalia mafao yao yanavyopunjwa! Vikokotoo vya unyonyaji mkubwa!yanavyokatwa kodi wakati kodi zililipwa! inavyochukua muda mrefu kulipwa mafao yao!
dawa ni kujitoa kuchangia hivi vyama kwani havina msaada wowote!
Nataka nikuambie vyama visingekuwepo serikali ilikua inaleta kikokotoo cha 25% badala ya hiki ya 33% kwahiyo uwepo wao kidogo inapunguza maumivu kwa watumishi wa Umma

Naomba upokee elimu ya vyama vya wafanyakazi

Vyama vya wafanyakazi viliidhibiti serikali kuondoa watoto kwenye bima ya afya waliofika miaka 19,mpaka serikali ilibadilisha kanuni na kusogeza umri
 
Msingi wa vyama vyote siasa Duniani umezaliwa ubavuni mwa vyama vya wafanyakazi. Kwa sababu kundi la vyama vya wafanyakazi wote wanakua wamesoma na werevu, ndio kundi la kwanza kuona ukandamizaji katika jamii, na kuanza kutoa elimu kwa jamii.

Vyama vya wafanyakazi mara nyingi kazi ngumu ya kupambana na muajiri, wakiwa wameweka rehani ajira yao. Ndio maana viongozi wengi wa vyama vya wafanyakazi wanapoteza ajira zao kwa sababu ya kupigania ustawi wa wanaowapigania, wanapoteza mahusiano na muajiri katika mazingira ya kazi.

Kuna tofauti kubwa kati ya vyama vya wafanyakazi na vyama vya siasa. Viongozi wa vyama vya siasa wapo huru kupambana na dola kwasababu hawako ndani ya ajira ,na hawana cha kupoteza.

Viongozi wa vyama vya wafanyakazi ni waajiriwa yaani wanapambana muajiri ambae anaweza kuwa serikali au sekta binafsi lakini ni muajiriwa tofauti kubwa sana.

Kuna tofauti kubwa sana ufanyaji wa kazi vyama vya siasa na vyama vya wafanyakazi, ukiona mtu kiongozi wa chama cha wafanyakazi hata kama ni ngazi ya Tawi mpe heshima yake, maana amejitoa muhanga kwa ajili ya wenzake.

Kwahiyo Abdul Nondo na Heche labda hawajui historia ya vyama vya wafanyakazi, wakae na waombe hitoria sio kudharau na kushambulia vyama vya wafanyakazi sitaki kuamini kuwa wamekodiwa kwa mradi maalumu kushambulia vyama vya wafanyakazi.

Vyama vya wafanyakazi vipo kwa mujibu wa sheria ya ajira na mahusiano kazini,sheria ya majadiliano. Kwahiyo wananjia za kupita katika majadiliano kabla ya kupiga kelele.

Nimeona Heche akishambulia vyama vya wafanyakazi Mara ya kwanza nilidhani bahati mbaya, juzi nimemuona ameshambulia chama walimu Tanzania, na kudharau kabisa CWT kwangu inaniambia hana taarifa za kutosha namna vyama vinavyofanya kazi, akae atafute watu wamuelimishe na asome sheria ya ajira na mahusiano kazini sasa huyu ni kijana kutoka chadema alikua kiongozi wa vijana chadema

Nimemuona tena kijana wa ACT Wazalendo Abdul Nondo, huyu ameandika hadithi nyingi akishambulia viongozi wa CWT, na kumpigania aliekua katibu mkuu 2020 mpaka June 28 ,2022.

Nondo anaonekana kabisa kanunuliwa kumpigia chapuo Aliekua Katibu mkuu Thefu, ambae alifungwa miezi sita kwa uchepushaji wa fedha ,ni kweli amekata rufaa ni haki yake lakini kimaadili tu peke yake hastahili hata kusogelea CWT.

Kipindi cha Thefu na mtandao wake CWT ilijaa udikteta, waliondoa viongozi wote waliokua na mawazo ya kuwajali walimu, walifuta mkono wa kwaheri, walifuta Tshirt kwa walimu ,walinyima uhuru wa wanachama kutoa maoni yao.

Sasa baada ya kuingia Katibu mkuu mpya ,anarudisha fedha wilayani, Thefu alikataa kupeleka fedha wilayani, sasa hivi chama kimeandaa mikutano mikuu bila kukopa fedha ,wananunuaa Tshirt za walimu wote ,ambayo Thefu alishafuta na genge lake, Thefu alinunua media zote na watu maarufu wakiwepo Thadeo Mushi kumpamba kwenye mitandao ya kijamii.

Niwaambie Heche na Nondo kama wametumwa kushambulia vyama vya wafanyakazi, wajiandae kundi wanalolishambulia ndio kubwa na werevu kuanzia katika vijiji.

Pia wanatakiwa kujua bila vyama vya wafanyakazi, wafanyakazi wnagekua wanyonge sana kwa muajiri

Jukumu la vyama vya siasa ni kutetea makundi yote kwenye jamii na kuungana makundi yote yanayopigania haki ya jamii ikiwepo kundi la vyama vya wafanyakazi sio kuwabeza.
Zaidi ya kununua t shirts mmefanya nini cha zaidi kusaidia wafanyakazi?
Wakati wa Magu mtu atadhani nyie ni UVCCM
 
Zaidi ya kununua t shirts mmefanya nini cha zaidi kusaidia wafanyakazi?
Wakati wa Magu mtu atadhani nyie ni UVCCM
Kipindi cha Magu vyama vya wafanyakazi vilikomaa na kikokotoo mpaka Magu akasitisha kikokotoo
 
Back
Top Bottom