Vyama vya siasa ya Upinzani kushambulia vyama vya wafanyakazi ni mkakati au Heche na Nondo wanatumika?

Umeandika vizuri ila kama ni CWT basi Heche yuko sahihi. Hiyo CWT haina msaada wowote kwa mwalimu. Kugawa Tshirt kwa hela ulizomkata mwalimu ni upuuzi mtupu. Kutotetea waalimu wanapokatwa hela za mwenge ni upuuzi mwingine wa CWT. Ingekuwa sio CWT ningeunga mkono hoja yako.
 
Inawezekana huna elimu ya kutosha kuhusu vyama vya wafanyakazi ,uwepo wa vyama vya wafanyakazi una tija kubwa sana kwa wafanyakazi

Stahiki mbalimbali katika maeneo ya kazi zinatolewa kwa hofu ya vyama vya wafanyakazi bila vyama vya wafanyakazi watumishi wataonea sana
Elimu juu ya vyama vya wafanyakazi ninayo kwakuwa mie pia ni mwanachama.Lakini natambua pia kuwa chama cha wafanyakazi chaweza kuwepo na kisitekeleze malengo ya kuanzishwa kwake.Hii ndiyo hoja yangu ya msingi.CWT kwa sasa haiwezi kutekeleza malengo ya kuanzishwa kwake kwa asilimia miamoja kwasababu ya kutekwa na ccm.Inapofika kwenye kufanya au kutekeleza maazimio magumu kama kuitisha mgomo(silaha kuu ya trade unions)CWT hawawezi tena.
Ni watu wachache wanauona huu muunganiko wa CWT na CCM na jinsi ambavyo unaathiri utekelezaji wa malengo ya kuanzishwa kwa CWT.Inawezekana wewe pia hauoni,na sikulaumu.
 
CWT nilichama la hovyo kuliko lichana lolote nililowahi kulishuhudi. Viongozi pandikizi toka sisiem kwa maslai yao na binafsi.
Walimu wangekuwa wanaskili wangeandamana kukipinga hikichama nyonyaji!!
Wanadanganya kurudisha hela lkn kimsingi hiyo ni fitna na unafiki hata matishet wanayogawa ni uzuzu wa danganya toto!
 
Msingi wa vyama vyote siasa Duniani umezaliwa ubavuni mwa vyama vya wafanyakazi. Kwa sababu kundi la vyama vya wafanyakazi wote wanakua wamesoma na werevu, ndio kundi la kwanza kuona ukandamizaji katika jamii, na kuanza kutoa elimu kwa jamii.

Vyama vya wafanyakazi mara nyingi kazi ngumu ya kupambana na muajiri, wakiwa wameweka rehani ajira yao. Ndio maana viongozi wengi wa vyama vya wafanyakazi wanapoteza ajira zao kwa sababu ya kupigania ustawi wa wanaowapigania, wanapoteza mahusiano na muajiri katika mazingira ya kazi.

Kuna tofauti kubwa kati ya vyama vya wafanyakazi na vyama vya siasa. Viongozi wa vyama vya siasa wapo huru kupambana na dola kwasababu hawako ndani ya ajira ,na hawana cha kupoteza.

Viongozi wa vyama vya wafanyakazi ni waajiriwa yaani wanapambana muajiri ambae anaweza kuwa serikali au sekta binafsi lakini ni muajiriwa tofauti kubwa sana.

Kuna tofauti kubwa sana ufanyaji wa kazi vyama vya siasa na vyama vya wafanyakazi, ukiona mtu kiongozi wa chama cha wafanyakazi hata kama ni ngazi ya Tawi mpe heshima yake, maana amejitoa muhanga kwa ajili ya wenzake.

Kwahiyo Abdul Nondo na Heche labda hawajui historia ya vyama vya wafanyakazi, wakae na waombe hitoria sio kudharau na kushambulia vyama vya wafanyakazi sitaki kuamini kuwa wamekodiwa kwa mradi maalumu kushambulia vyama vya wafanyakazi.

Vyama vya wafanyakazi vipo kwa mujibu wa sheria ya ajira na mahusiano kazini,sheria ya majadiliano. Kwahiyo wananjia za kupita katika majadiliano kabla ya kupiga kelele.

Nimeona Heche akishambulia vyama vya wafanyakazi Mara ya kwanza nilidhani bahati mbaya, juzi nimemuona ameshambulia chama walimu Tanzania, na kudharau kabisa CWT kwangu inaniambia hana taarifa za kutosha namna vyama vinavyofanya kazi, akae atafute watu wamuelimishe na asome sheria ya ajira na mahusiano kazini sasa huyu ni kijana kutoka chadema alikua kiongozi wa vijana chadema

Nimemuona tena kijana wa ACT Wazalendo Abdul Nondo, huyu ameandika hadithi nyingi akishambulia viongozi wa CWT, na kumpigania aliekua katibu mkuu 2020 mpaka June 28 ,2022.

Nondo anaonekana kabisa kanunuliwa kumpigia chapuo Aliekua Katibu mkuu Thefu, ambae alifungwa miezi sita kwa uchepushaji wa fedha ,ni kweli amekata rufaa ni haki yake lakini kimaadili tu peke yake hastahili hata kusogelea CWT.

Kipindi cha Thefu na mtandao wake CWT ilijaa udikteta, waliondoa viongozi wote waliokua na mawazo ya kuwajali walimu, walifuta mkono wa kwaheri, walifuta Tshirt kwa walimu ,walinyima uhuru wa wanachama kutoa maoni yao.

Sasa baada ya kuingia Katibu mkuu mpya ,anarudisha fedha wilayani, Thefu alikataa kupeleka fedha wilayani, sasa hivi chama kimeandaa mikutano mikuu bila kukopa fedha ,wananunuaa Tshirt za walimu wote ,ambayo Thefu alishafuta na genge lake, Thefu alinunua media zote na watu maarufu wakiwepo Thadeo Mushi kumpamba kwenye mitandao ya kijamii.

Niwaambie Heche na Nondo kama wametumwa kushambulia vyama vya wafanyakazi, wajiandae kundi wanalolishambulia ndio kubwa na werevu kuanzia katika vijiji.

Pia wanatakiwa kujua bila vyama vya wafanyakazi, wafanyakazi wnagekua wanyonge sana kwa muajiri

Jukumu la vyama vya siasa ni kutetea makundi yote kwenye jamii na kuungana makundi yote yanayopigania haki ya jamii ikiwepo kundi la vyama vya wafanyakazi sio kuwabeza.
Wewe tafuna michango ya wafanyakazi mnayoshirikiana na serikali KUIBA mishahara yao kwa Makato ya LAZIMA.


Usifikiri wafanyakazi ni wajinga.

Hizi stori mchoko kadanganye madhumati wenzio siku ipite.
 
Msingi wa vyama vyote siasa Duniani umezaliwa ubavuni mwa vyama vya wafanyakazi. Kwa sababu kundi la vyama vya wafanyakazi wote wanakua wamesoma na werevu, ndio kundi la kwanza kuona ukandamizaji katika jamii, na kuanza kutoa elimu kwa jamii.

Vyama vya wafanyakazi mara nyingi kazi ngumu ya kupambana na muajiri, wakiwa wameweka rehani ajira yao. Ndio maana viongozi wengi wa vyama vya wafanyakazi wanapoteza ajira zao kwa sababu ya kupigania ustawi wa wanaowapigania, wanapoteza mahusiano na muajiri katika mazingira ya kazi.

Kuna tofauti kubwa kati ya vyama vya wafanyakazi na vyama vya siasa. Viongozi wa vyama vya siasa wapo huru kupambana na dola kwasababu hawako ndani ya ajira ,na hawana cha kupoteza.

Viongozi wa vyama vya wafanyakazi ni waajiriwa yaani wanapambana muajiri ambae anaweza kuwa serikali au sekta binafsi lakini ni muajiriwa tofauti kubwa sana.

Kuna tofauti kubwa sana ufanyaji wa kazi vyama vya siasa na vyama vya wafanyakazi, ukiona mtu kiongozi wa chama cha wafanyakazi hata kama ni ngazi ya Tawi mpe heshima yake, maana amejitoa muhanga kwa ajili ya wenzake.

Kwahiyo Abdul Nondo na Heche labda hawajui historia ya vyama vya wafanyakazi, wakae na waombe hitoria sio kudharau na kushambulia vyama vya wafanyakazi sitaki kuamini kuwa wamekodiwa kwa mradi maalumu kushambulia vyama vya wafanyakazi.

Vyama vya wafanyakazi vipo kwa mujibu wa sheria ya ajira na mahusiano kazini,sheria ya majadiliano. Kwahiyo wananjia za kupita katika majadiliano kabla ya kupiga kelele.

Nimeona Heche akishambulia vyama vya wafanyakazi Mara ya kwanza nilidhani bahati mbaya, juzi nimemuona ameshambulia chama walimu Tanzania, na kudharau kabisa CWT kwangu inaniambia hana taarifa za kutosha namna vyama vinavyofanya kazi, akae atafute watu wamuelimishe na asome sheria ya ajira na mahusiano kazini sasa huyu ni kijana kutoka chadema alikua kiongozi wa vijana chadema

Nimemuona tena kijana wa ACT Wazalendo Abdul Nondo, huyu ameandika hadithi nyingi akishambulia viongozi wa CWT, na kumpigania aliekua katibu mkuu 2020 mpaka June 28 ,2022.

Nondo anaonekana kabisa kanunuliwa kumpigia chapuo Aliekua Katibu mkuu Thefu, ambae alifungwa miezi sita kwa uchepushaji wa fedha ,ni kweli amekata rufaa ni haki yake lakini kimaadili tu peke yake hastahili hata kusogelea CWT.

Kipindi cha Thefu na mtandao wake CWT ilijaa udikteta, waliondoa viongozi wote waliokua na mawazo ya kuwajali walimu, walifuta mkono wa kwaheri, walifuta Tshirt kwa walimu ,walinyima uhuru wa wanachama kutoa maoni yao.

Sasa baada ya kuingia Katibu mkuu mpya ,anarudisha fedha wilayani, Thefu alikataa kupeleka fedha wilayani, sasa hivi chama kimeandaa mikutano mikuu bila kukopa fedha ,wananunuaa Tshirt za walimu wote ,ambayo Thefu alishafuta na genge lake, Thefu alinunua media zote na watu maarufu wakiwepo Thadeo Mushi kumpamba kwenye mitandao ya kijamii.

Niwaambie Heche na Nondo kama wametumwa kushambulia vyama vya wafanyakazi, wajiandae kundi wanalolishambulia ndio kubwa na werevu kuanzia katika vijiji.

Pia wanatakiwa kujua bila vyama vya wafanyakazi, wafanyakazi wnagekua wanyonge sana kwa muajiri

Jukumu la vyama vya siasa ni kutetea makundi yote kwenye jamii na kuungana makundi yote yanayopigania haki ya jamii ikiwepo kundi la vyama vya wafanyakazi sio kuwabeza.
Umeandika ujinga sana humu baada ya kuleta hoja za maana unakuja kusema issue za T-shirt kweli walimu wanahitaji sana izo t-shirt ...stupid
Watu wakisema chama cha walimu hakina msaada kwa walimu wanamaanisha
1.walimu ndo kundi la watumishi wanaofanya kazi mpaka muda wa ziada remedial class bila kulipwa "overtime "
2.walimu ndo kundi la watumishi ambao hawana allowance yoyote salary to salary
3.walimu ndo kundi la watumishi ambao wanaishi kwenye mazingira magumu vijijini huko walimu wamegawana vyumba kwenye nyumba moja na wanaishi na familia zao.
4.walimu ndo mtumishi ambae ananyaswa na kusumbuliwa hata sehemu ambayo alitakiwa kupewa stahiki zake mf. Uhamisho n.k lkn CWT Ipo kimya.
5.walimu wanapitia nyakati ngumu sana ndo maana wanaingia kwenye mikopo isiyokua na tija wajinasue na hali ya maisha kwaio walikua wanahitaji msaada wa CWT hatua kwa hatua kwenye utetezi wa maslahi yao.
Matokeo yake viongozi CWT wamekua wabinafsi wameacha kabisa kujadili agenda za walimu na wamejikita kwenye ugomvi,kubambikiana kesi ,kuondoana kwenye chama,kuhamishana kwa kukomoana .
Kukosana baadhi ya viongozi na kutokuwepo kwa umoja ndani ya chama cha walimu hatutegemei kama kero za walimu zitakuja kufanyiwa kazi kwaio ni bora hiki chama kifutwe walimu wajue hawana mtetezi kuliko waendelee kukatwa michango yao iendelee kuliwa na wajanja wachache.
 
Mwl analazimishwa kuchangia mwenge wakati mwenge una bageti yake CWT wako kimya
 
Vyama vya wafanuakazi kwa ufupi havina tija yoyote kwa mfanyakazi!
Angalia mafao yao yanavyopunjwa! Vikokotoo vya unyonyaji mkubwa!yanavyokatwa kodi wakati kodi zililipwa! inavyochukua muda mrefu kulipwa mafao yao!
dawa ni kujitoa kuchangia hivi vyama kwani havina msaada wowote!
100%
 
Kukosana baadhi ya viongozi na kutokuwepo kwa umoja ndani ya chama cha walimu
Migogoro ipo kila sehemu ,hakuna sehemu isio kuwa na Migogoro hata mawaziri wana Migogoro na mandibu wao au makatibu wao
 
Back
Top Bottom