Vyama vya Siasa nchini huu ndio wakati sahihi wa kutafuta ushindi wa kura za Uchaguzi wa Mkuu wa 2025, amkeni!

mama D

JF-Expert Member
Nov 22, 2010
19,760
35,205
Habari za asubuhi

Siku zinakwenda, mambo mengi yanabadilika, watanzania wanabadilika lakini hatari ni kwamba mifumo na miongozo ya vyama vingi vya siasa inabaki ileile ya kufanya mambo kwa mazoea.

Hivi, viongozi wa vyama vya siasa pinzani mlishawahi kujiuliza ni nini kipya mnaweza ambia wananchi au kufanya ili kuongeza thamani ya vyama vyenu huku mitaani? Mlishawahi kufanya tafiti kujua ni vitu gani wananchi wakipata watakua loyal kiasi cha kusimama kidedea na kuwalinda viongozi wao kwa hali na gharama yoyote na kuhakikisha msukumo wa kushinda uchaguzi unatoka kwao na sio kwenu?

Badala ya kutenga budget ya kwenda kutembea na kuwapa wananchi maneno matupu huko majimboni ili mjinufaishe nyie na familia zenu kwa hizo per diem, nufaikeni kidogo na wananchi mnaowatembelea wanaufaike kidogo. Mkono mtupu haulambwi. Watanzania wala hawataki mambo makuuuubwa, wnataka mambo madogomadogo yenye muendelezo

Msikurupuke makaendelea kufanya vitu vilivyokwishafanyika, sera zenu zinaweza kuwa nzuri sana ila sasa wekeni mipango itakayowapa wananchi imani kwamba sera zenu zinatekelezeka either kwa kuwashirikisha kwa vitendo au kuwapa connections muhimu au miongozo itakayogusa maisha yao.

Hakuna nchi nyepesi kuongoza na ngumu kuongoza kama Tanzania, ila kizuri na rahisi ni kwamba wepesi wa kuwaongoza watanzania unatokana na mahusiano ya kidugu mtakayokuwa mmeyajenga .

Msikurupuke mkawageza chama tawala CCM. Wenzangu hawa wana pa kusimamia tena sio padogo.... hawa wana cha kusemea sababu ndio wenye serikali na ndio watekelezaji wa mipango ya serikali.
Ingieni gharama kujenga vyama vyenu leo na baadae vyama hivi vitawajenga ninyi.

Halafu msilalamike kwamba hamna pesa ya kufanya mambo ya msingi sababu hata hayati Mwalimu Nyerere na Karume hawakuwa na pesa lakini walieweza kujenga vyama imara vilivyowaondoa wakoloni na vinavyowasumbua wapinzani hadi leo

Kama kweli mko kwaajili ya maendeleo ya taifa Amkeni ndugu zangu. Mkiendelea kufanya kilekile kinachowakoseshaga kila uchaguzi mtaendelea kukosa ushindi milele.

Rais wetu na mwenyekiti wa chama tawala ameshawaambia msisubirie msisubirie 2025 anzeni sasa. Mkumbuke pia na yeye ameshaanza kutetea kiti

Upinzani kwa afya ya taifa💥

Mungu ibariki Tanzania😍🇹🇿🤝
 
Kwa hali ya maisha ilivyo kama watanzania wanahitaji kuelimishwa na chadema basi CCM inaongoza watu waliokufa.

Sijaitaja chadema nimeongelea siasa za vyama pinzani kwa ujumla
Halafu sijasema watanzania wanahitaji kuelimishwa nimesema wanaotaka kushika madaraka wanatakiwa kujiongeza sana

Vinginevyo KIDUMU chama tawala CCM
 
Sijaitaja chadema nimeongelea siasa za vyama pinzani kwa ujumla
Halafu sijasema watanzania wanahitaji kuelimishwa nimesema wanaotaka kushika madaraka wanatakiwa kujiongeza sana

Vinginevyo KIDUMU chama tawala CCM
Kwani chadema siyo chama cha upinzani?. Ndo na mimi nimekwambia mambo ya kuwaeleza watanzania siyo ya kutafuta kwa tochi kwa sababu sisi wenyewe wananchi tunaona hali halisi.

KIDUMU CHAMA CHA MAMBUZII.
 
Kwani chadema siyo chama cha upinzani?. Ndo na mimi nimekwambia mambo ya kuwaeleza watanzania siyo ya kutafuta kwa tochi kwa sababu sisi wenyewe wananchi tunaona hali halisi.

KIDUMU CHAMA CHA MAMBUZII.

Endeleeni kubishana muendelee kushindwa kwa sababu zilezile ili KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
😃😃😃
 
Siku zinakwenda, mambo mengi yanabadilika, watanzania wanabadilika lakini hatari ni kwamba mifumo na miongozo ya vyama vingi vya siasa inabaki ileile ya kufanya mambo kwa mazoea.
Mkuu mama D , naunga mkono hoja, umeshauri jambo kubwa sana la msingi.
Hivi, viongozi wa vyama vya siasa pinzani mlishawahi kujiuliza ni nini kipya mnaweza ambia wananchi au kufanya ili kuongeza thamani ya vyama vyenu huku mitaani? Mlishawahi kufanya tafiti kujua ni vitu gani wananchi wakipata watakua loyal kiasi cha kusimama kidedea na kuwalinda viongozi wao kwa hali na gharama yoyote na kuhakikisha msukumo wa kushinda uchaguzi unatoka kwao na sio kwenu?
Naunga mkono hoja, they have to come with something new
Badala ya kutenga budget ya kwenda kutembea na kuwapa wananchi maneno matupu huko majimboni ili mjinufaishe nyie na familia zenu kwa hizo per diem, nufaikeni kidogo na wananchi mnaowatembelea wanaufaike kidogo. Mkono mtupu haulambwi. Watanzania wala hawataki mambo makuuuubwa, wnataka mambo madogomadogo yenye muendelezo
Naunga mkono hoja, kahutubieni lakini jengeni local capacity ili hayo mnayohubiri yawe na muendelezo, sustainable, hivyo hata excuse ni umasikini wa chama, tugawane tuu hivyo hivyo huo umasikini, ruzuku ya Chadema ni zaidi ya TZS 100m monthy, then tugawane umasikini!.
Msikurupuke makaendelea kufanya vitu vilivyokwishafanyika, sera zenu zinaweza kuwa nzuri sana ila sasa wekeni mipango itakayowapa wananchi imani kwamba sera zenu zinatekelezeka either kwa kuwashirikisha kwa vitendo au kuwapa connections muhimu au miongozo itakayogusa maisha yao.
Hii inaitwa SMART politics ni hoja zinazotekelezeka, with smart objectives.
Hakuna nchi nyepesi kuongoza na ngumu kuongoza kama Tanzania, ila kizuri na rahisi ni kwamba wepesi wa kuwaongoza watanzania unatokana na mahusiano ya kidugu mtakayokuwa mmeyajenga .
Hili neno!.
Msikurupuke mkawageza chama tawala CCM. Wenzangu hawa wana pa kusimamia tena sio padogo.... hawa wana cha kusemea sababu ndio wenye serikali na ndio watekelezaji wa mipango ya serikali.
Hili ni somo kubwa sana kwa wapinzani, CCM sio wenzao, CCM ndio wenye nchi na ukifika wakati wa uchaguzi, CCM wana cha kuonyesha, hili nililisema ile 2020 Oktoba 28 ni mashindano kati ya Reality vs Ahadi Hewa? Je, Watanzania watachagua nini kati ya visible, tangible Deliverables vs The Empty Promises? halafu huyu mtu mwenye empty promises asiye na chochote cha kuonyesha, anashindwa, anawahamasisha wafuasi wake kuwa alishinda akaibiwa ushindi!, hivyo hawakubali matokeo, hawamtambui rais, hawalitambui Bunge, hawapeleki majina ya viti maalum!. Mashujaa 19 wakagomea ujinga huu, majina yakapelekwa. Ikawa taabu!
Ingieni gharama kujenga vyama vyenu leo na baadae vyama hivi vitawajenga ninyi.
Ushauri huu niliwapa ile 2010 kwenye CCM Imechokwa, CHADEMA Haijajipanga! niliwashauri

Hakuna ubishi, Chadema imenyanyuka, toka wabunge 5 mpaka 22 wa kuchaguliwa tena majimbo ya haja yenye impact ikiwemo kuyashika majiji makubwa katika mikoa the big five!, huku sio kukua bali ni kupaa, tatizo kubwa la Chadema, bado hawajipanga mkao wa kichama tawala, ili kikabidhiwe nchi, kitawale, Chadema bado kimekaa kichama harakati, hivyo kuna wengi wanakiona kama bado hakijakomaa kiasi cha kukabidhiwa ikulu yetu!.

Kichama, wanachadema mkubali msikubali, chama chenu kwa sasa japo kipo juu, lakini bado hamjakomaa kufikia kiwango cha kukabidhiwa nchi, bado mko kiuana harakati zaidi kuliko ki chama tawala, na hamjajipanga kwa sura ya kitaifa na utayari wa kutawala nchi.

Kwa vile CCM imechokwa na imekaa mkao wa kifo, hii ndio opportunity yenu Chadema kuongeza offensive ili kuisindikiza CCM kaburini, kwa kujipanga kimkakati ili muwe na sura ya kitaifa, kwa kuonyesha Watanzania kuwa mmekomaa na mko tayari kutawala, hivyo Watanzania watawamini watawakabidhi nchi mwaka 2015.

Sehemu muhimu kabisa kwa Chadema to keep watch kuhakikisha hamuiachii ni hiyo Kanda ya Ziwa ambayo imeipokonya CCM na kuishika, hii ndio Kanda determinant ya nani anakuwa rais wa nchi hii. Aliyeishika Kanda ya Ziwa ndio rais wa Tanzania. Hivyo CCM imeumia sana kupoteza Kanda ya Ziwa na wataelekeza all it might powers to reclaim what it has lost, hivyo Chadema itumie uwezo wake wote kulinda what it has!.

Kwa upande wa Chadema, lazima kibadilike, first and foremost, anzeni na Mwenyekiti wenu Freeman Mbowe, he should go!. Ajiuzulu uenyekiti, ampishe more able person kama Dr. Slaa kwenye usukani wa chama, Katibu Mkuu mpeni Zitto strategically, hii itaifuta ile dhana ya nepotisim kwenye chama chenu, na kulivua lile koti la ukanda na ukabila ili walioichoka CCM wawafungulie mikono kwa kujitokeza kwa wingi kuwapigia kura 2015 kwa kujionyesha Chadema ni chama cha wote, dini zote na kanda zote.

Kupumzishwa kwa Freeman Mbowe sio kuwa hafai no, anafaa sana lakini kwa background yake na nature ya kazi zake, as a businessman, hapo alipoifikisha Chadema amaishafanya kazi kubwa na kufikia mwisho wa uwezo wake. Kwa background yake ya a former DJ na sasa ni mfanyabiashara, focus ya wafanyabiashara kote dunia nzima ni maximisation of profits, hivyo Mbowe atahitaji ruzuku ya Chadema itumike kuivest kwenye assets, kwenye vitu vya kuonekanika yaani assets kama magari, mavazi, etc

Ili Chadema kiweze kushika nchi 2015, it has to invest on people na sio ku invest kwenye vitu. Chadema must invest kwenye mass mobilisation na sio kutegemea mikutano ya hadhara na maandamano. Chadema needs to have able people kuiwezesha kushika dola five years to come kwa kutumia reaching out mechanism kuwafikia the mases kwa kumiliki media yake yenyewe. Chadema lazima ifanye recruitment ya able people, watakaokuja kuendesha serikali ya Chadema. Mbowe hawezi kukubali ruzuku ya Chadema itumike to invest on people, it's a loss making venture kwa mfanyabiashara na kuivest kwenye mass media sio profitable investment kwa business man ambaye ni in for profit making. Dr.Slaa na Zitto sio wafanyabiashara hawa ni ma technocrats. Chama kishikwe na wanasiasa watendaji sio wanasiasa wafanyabiashara. Chadema iwekeze kwenye watu na kupanua mtandao wake hadi vijijini, ili kwenda kuiongoa CCM kuanzia kule chini kabisa kwenye mizizi yake ambako ni kule kwenye mashina. Chadema imiliki media yake yenyeshe for mass mobilization na sio kutegemea mikutano na maandamano, huko ni kuendeleza uanaharakati, Chadema inatakiwa kukaa mkao wa kutawala, ikitangaza kitu, kinafika Tanzania nzima!.
Paskali
Halafu msilalamike kwamba hamna pesa ya kufanya mambo ya msingi sababu hata hayati Mwalimu Nyerere na Karume hawakuwa na pesa lakini walieweza kujenga vyama imara vilivyowaondoa wakoloni na vinavyowasumbua wapinzani hadi leo
Hili neno!
Kama kweli mko kwaajili ya maendeleo ya taifa Amkeni ndugu zangu. Mkiendelea kufanya kilekile kinachowakoseshaga kila uchaguzi mtaendelea kukosa ushindi milele.
Hili neno!
Rais wetu na mwenyekiti wa chama tawala ameshawaambia msisubirie msisubirie 2025 anzeni sasa. Mkumbuke pia na yeye ameshaanza kutetea kiti

Upinzani kwa afya ya taifa💥

Mungu ibariki Tanzania😍🇹🇿🤝
Naunga mkono hoja, Chadema wana mtindo wa kupuuza ushauri!, labda sasa watakusikia na kuzingatia ushauri
Hongera sana kuwashauri wapinzani.
P
 
Tanzania hakuna uchaguzi bali kuna maonyesho ya ujinga wa mtu mweusi kwenye box la kura. Sasa sijui ni ushindi gani unaongelea kwa wapinzani.


Nini kinashindikana kuondoa hicho unachokiita " maonyesho ya ujinga wa mtu mweusi kwenye box la kura. " kama kipo kweli????

Kama kweli CCM haifai itoeni. Vinginevyo acheni kujiita wapinzani kumbe ni wanaSACCOs

Wanaume Mkwawa aliwaweza kwa wajerumani, Karume akiweza, Nyerere aliweza tena bila kulialia kama nyie mnalialia kutafuta excuses za kitoto mnooo

Sio ajabu hata hamjui mnachotaka

ZIDUMU FIKRA ZA MWENYEKITI
 
Nini kinashindikana kuondoa hicho unachokiita " maonyesho ya ujinga wa mtu mweusi kwenye box la kura. " kama kipo kweli????

Kama kweli CCM haifai itoeni. Vinginevyo acheni kujiita wapinzani kumbe ni wanaSACCOs

Wanaume Mkwawa aliwaweza kwa wajerumani, Karume akiweza, Nyerere aliweza tena bila kulialia kama nyie mnalialia kutafuta excuses za kitoto mnooo

Sio ajabu hata hamjui mnachotaka

ZIDUMU FIKRA ZA MWENYEKITI

Tunaitoa kwani iko madarakani kwa chaguzi halali? Labda tuwe na vikundi vya msituni maana yenyewe inawekwa madarakani na vyombo vya dola. Hivyo machafuko au mapinduzi ndio yataitoa maana hakuna uchaguzi Tanzania. Uchaguzi upo Kenya.
 
Mkuu

Vyama vya siasa hasa vya upinzani vinajua haviwezi CHUKUA DOLA coz DOLA ya Tanzania haijaamua kuwapa ushindi hata wakishinda!

Wanahisi JAMUHURI haitokuwa SALAMA kama wao wakichukua!

Hilo limedhihirika KWA chaguzi nyingi zilizopita!

Tanzania bado haijaandaa Chama Mbadala cha kushika dola bali vilivyoandaliwa ni vya kuisimamia ccm isiharibu Sana!

WAKATI mwafaka ukifika kitaandaliwa na kupewa DOLA!!

KWA Sasa vyama pinzani vilivyopo ni ubunge tu ndio una baraka za DOLA wao kupewa!

Usijichoshe ndivyo ilivyo Sasa labda Baada ya KATIBA mpya ndio kitazaliwa Chama Mbadala cha kupewa DOLA na sio KWA Sasa!!!
 
Kwani chadema siyo chama cha upinzani?. Ndo na mimi nimekwambia mambo ya kuwaeleza watanzania siyo ya kutafuta kwa tochi kwa sababu sisi wenyewe wananchi tunaona hali halisi.

KIDUMU CHAMA CHA MAMBUZII.
Na hapo ndio huwa mnakwama kila season!

Badala ya kujikita kwenye hoja mnabaki kukazania ujinga,Upumbavu na Upimbi!

Matokeo yake mnaendelea kuwa na wafuasi aina ya wapiga debe wa stendi za mabasi na Bodaboda wasiojitambua bali "wanaojitumbua" na viroba kwa bhange... kama wewe Waterloo
JamiiForums-355495924_remastered.jpg
20230113_080002.jpg
 
Habari za asubuhi

Siku zinakwenda, mambo mengi yanabadilika, watanzania wanabadilika lakini hatari ni kwamba mifumo na miongozo ya vyama vingi vya siasa inabaki ileile ya kufanya mambo kwa mazoea.

Hivi, viongozi wa vyama vya siasa pinzani mlishawahi kujiuliza ni nini kipya mnaweza ambia wananchi au kufanya ili kuongeza thamani ya vyama vyenu huku mitaani? Mlishawahi kufanya tafiti kujua ni vitu gani wananchi wakipata watakua loyal kiasi cha kusimama kidedea na kuwalinda viongozi wao kwa hali na gharama yoyote na kuhakikisha msukumo wa kushinda uchaguzi unatoka kwao na sio kwenu?

Badala ya kutenga budget ya kwenda kutembea na kuwapa wananchi maneno matupu huko majimboni ili mjinufaishe nyie na familia zenu kwa hizo per diem, nufaikeni kidogo na wananchi mnaowatembelea wanaufaike kidogo. Mkono mtupu haulambwi. Watanzania wala hawataki mambo makuuuubwa, wnataka mambo madogomadogo yenye muendelezo

Msikurupuke makaendelea kufanya vitu vilivyokwishafanyika, sera zenu zinaweza kuwa nzuri sana ila sasa wekeni mipango itakayowapa wananchi imani kwamba sera zenu zinatekelezeka either kwa kuwashirikisha kwa vitendo au kuwapa connections muhimu au miongozo itakayogusa maisha yao.

Hakuna nchi nyepesi kuongoza na ngumu kuongoza kama Tanzania, ila kizuri na rahisi ni kwamba wepesi wa kuwaongoza watanzania unatokana na mahusiano ya kidugu mtakayokuwa mmeyajenga .

Msikurupuke mkawageza chama tawala CCM. Wenzangu hawa wana pa kusimamia tena sio padogo.... hawa wana cha kusemea sababu ndio wenye serikali na ndio watekelezaji wa mipango ya serikali.
Ingieni gharama kujenga vyama vyenu leo na baadae vyama hivi vitawajenga ninyi.

Halafu msilalamike kwamba hamna pesa ya kufanya mambo ya msingi sababu hata hayati Mwalimu Nyerere na Karume hawakuwa na pesa lakini walieweza kujenga vyama imara vilivyowaondoa wakoloni na vinavyowasumbua wapinzani hadi leo

Kama kweli mko kwaajili ya maendeleo ya taifa Amkeni ndugu zangu. Mkiendelea kufanya kilekile kinachowakoseshaga kila uchaguzi mtaendelea kukosa ushindi milele.

Rais wetu na mwenyekiti wa chama tawala ameshawaambia msisubirie msisubirie 2025 anzeni sasa. Mkumbuke pia na yeye ameshaanza kutetea kiti

Upinzani kwa afya ya taifa

Mungu ibariki Tanzania
Unazijua hasira za mgagagigikoko aliyopo ikulu ? Kama uzijui basi tafuta kitabu cha buricheka kakisome upya vizuri kwa kutumia akili ....utajua kua buricheka ni mbara na wagagagigikoko ni kina nani ?
 
Back
Top Bottom