Mgawanyo wa Ruzuku za vyama vya siasa nchini

lord atkin

Senior Member
Sep 30, 2018
197
683
Kufuatia kuibuka kwa mjadala wa ruzuku za vyama vya siasa kufuatia kauli ya Makamu mwenyekiti wa CCM Mheshimiwa Kinana aliyonukuliwa akisema CHADEMA wamechukua ruzuku ya shilingi za kitanzania bilioni 2.7 nimeona ni vyema nikaleta mgawanyo wa ruzuku za vyama vya siasa kama ilivyoripotiwa kwenye gazeti la Mwananchi la Tarehe 15 Januari 2021 mwezi mmoja tu baada ya uchaguzi habari yenye kichwa "VYAMA SITA VYALAMBA SH 1.4 BILIONI ZA RUZUKU".

Ofisi ya Msajili wa vyama vya siasa Kila mwezi hutoa shilingi bilioni 1.4 kama ruzuku kwa vyama vya siasa. Na mgawanyo wa ruzuku hiyo kwa vyama vya siasa kwa Kila mwezi kutokana na mafanikio na kura za uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 ni kama ifuatavyo

1. CCM

Chama cha Mapinduzi hupokea ruzuku ya shilingi za kitanzania bilioni 1.33 kila mwezi. Kwa hesabu za haraka haraka mpaka sasa miaka 3 baada ya uchaguzi CCM wameshapokea shilingi Bilioni 47.88

2. CHADEMA

Chama cha Demokrasia na Maendeleo hupokea ruzuku ya shilingi za kitanzania Milioni 109.68 Kila mwezi.Mpaka sasa miaka 3 baada ya uchaguzi wameshapokea shilingi Bilioni 3.8.

3. ACT

Chama cha ACT wazalendo hupokea ruzuku ya shilingi za kitanzania Milioni 14 Kila mwezi. Mpaka sasa miaka 3 baada ya uchaguzi mkuu wamepokea shilingi Milioni 504

4. CUF

Chama cha Wananchi CUF hupokea ruzuku ya shilingi za kitanzania Milioni 5.7 kwa mwezi, na mpaka sasa miaka 3 baada ya uchaguzi mkuu wamepokea shilingi za kitanzania Milioni 205.2

5. NCCR Mageuzi

Chama cha NCCR MAGEUZI hupokea ruzuku ya shilingi za kitanzania 316,937/= kwa mwezi na mpaka sasa miaka 3 baada ya uchaguzi mkuu wamepokea shilingi za kitanzania Milioni 11.4

6. DP

Chama cha DP hupokea ruzuku ya shilingi za kitanzania 67,387/=, mpaka sasa miaka 3 baada ya uchaguzi mkuu wamepokea shilingi za kitanzania Milioni 2.3.

Source: Gazeti la Mwananchi la Tarehe 15 Januari 2021

 
Kufuatia kuibuka kwa mjadala wa ruzuku za vyama vya siasa kufuatia kauli ya Makamu mwenyekiti wa CCM Mheshimiwa Kinana aliyonukuliwa akisema CHADEMA wamechukua ruzuku ya shilingi za kitanzania bilioni 2.7 nimeona ni vyema nikaleta mgawanyo wa ruzuku za vyama vya siasa kama ilivyoripotiwa kwenye gazeti la Mwananchi la Tarehe 15 Januari 2021 mwezi mmoja tu baada ya uchaguzi habari yenye kichwa "VYAMA SITA VYALAMBA SH 1.4 BILIONI ZA RUZUKU".

Ofisi ya Msajili wa vyama vya siasa Kila mwezi hutoa shilingi bilioni 1.4 kama ruzuku kwa vyama vya siasa. Na mgawanyo wa ruzuku hiyo kwa vyama vya siasa kwa Kila mwezi kutokana na mafanikio na kura za uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 ni kama ifuatavyo

1. CCM

Chama cha Mapinduzi hupokea ruzuku ya shilingi za kitanzania bilioni 1.33 kila mwezi. Kwa hesabu za haraka haraka mpaka sasa miaka 3 baada ya uchaguzi CCM wameshapokea shilingi Bilioni 47.88

2. CHADEMA

Chama cha Demokrasia na Maendeleo hupokea ruzuku ya shilingi za kitanzania Milioni 109.68 Kila mwezi.Mpaka sasa miaka 3 baada ya uchaguzi wameshapokea shilingi Bilioni 3.8.

3. ACT

Chama cha ACT wazalendo hupokea ruzuku ya shilingi za kitanzania Milioni 14 Kila mwezi. Mpaka sasa miaka 3 baada ya uchaguzi mkuu wamepokea shilingi Milioni 504

4. CUF

Chama cha Wananchi CUF hupokea ruzuku ya shilingi za kitanzania Milioni 5.7 kwa mwezi, na mpaka sasa miaka 3 baada ya uchaguzi mkuu wamepokea shilingi za kitanzania Milioni 205.2

5. NCCR Mageuzi

Chama cha NCCR MAGEUZI hupokea ruzuku ya shilingi za kitanzania 316,937/= kwa mwezi na mpaka sasa miaka 3 baada ya uchaguzi mkuu wamepokea shilingi za kitanzania Milioni 11.4

6. DP

Chama cha DP hupokea ruzuku ya shilingi za kitanzania 67,387/=, mpaka sasa miaka 3 baada ya uchaguzi mkuu wamepokea shilingi za kitanzania Milioni 2.3.

Source: Gazeti la Mwananchi la Tarehe 15 Januari 2021

 

Attachments

  • IMG-20240204-WA0068.jpg
    IMG-20240204-WA0068.jpg
    90.5 KB · Views: 2
Samia naye anajenga kwao kama mwendazake alivyo jenga chat. Hivi hawajinga hawajifuzi kutokana na makosa ya watangulizi wao?
 
Sasa kama vyama vyote hivyo vinapata Ruzuku Kila Mwezi sasa mbona vinapigana majungu Kila Leo?

Wakiendekeza hayo, tutapitisha Sheria visiwe vinapata Ruzuku

Viwe vinaendeshwa na michango ya kujitolea
 
Hakuna haja ya hizo Pesa kupewa vyama, ilitakiwa ziende kwenye miradi ya maendeleo....kila chama kingetafuta funds chenyewe
 
Back
Top Bottom