Kuna waandishi wengine mahiri sana ambao watu wengi hawawafahamu, mfano mmoja wapo ni Mwandishi ajulikanae kwa jina la Muhamed Said Abdulla a.k.a bwana Msa (Marehemu), ana vitabu kama vile Kosa la Bwana MSA, Siri ya Sifuri, Mzimu wa Watu wa Kale, Kisiwa cha Giningi, Duniani Kuna Watu, Mke Mmoja Waume Watatu na Mwana wa Yungi Hulewa. Vile vile kuna huyu ajuliukanae kwa jina la Said Ahmed Mohamed na vitabu vyake ni Kiza katika Nuru, Utengano, Asali Chungu... Bila kumsahau Mzee Shafi Adam Shafi. Na Vitabu vyake vijulikanavyo kwa majina haya: Kasri Ya Mwinyi Fuad, Kuli, Haini na Vuta N' Kuvute.