Vitabu vya Willy Gamba (Elvis Musiba)

wakuu naombeni msaada wenu kama kuna anayejua ninakoweza kupata hivi vitabu ya Elvis Musiba, vikiwa na stellingi Willy Gamba.

Vitabu hivyo ni kama vile:
1.Kikosi cha Kisasi
2.Kufa na Kupona
3.Hofu.
4.Njama
5.Uchu

na vinginevyo. nimevisoma baadhi zamani lakini sasa hivi sina nakala tena ningependa kujua ninakoweza kuvipata.

shukrani!
mwenye ivyovitabu anijulishe 0715 555855
 
Nakumbuka shambulio lilofanyika pale Butiama hotel shinyanga, nakumbuka kuna mtu alikuwa anaitwa Skazwe, nakumbuka kuna mtu alikua anaitwa Kabwe makanika au Jitu kumbuka, nakumbuka kuna dada alikua anaitwa Amanda si mchezo kabisa bila kumsahau Inspector wa Polisi, nakumbuka ile ajari ambapo treni iligonga gari ambalo Gmaba alikuwa amekodi kisha yule mtu akalipwa toka serikalini. vile vitabu havisahauliki.ila kwa ufupi mmiliki wa vitabu vile sijui sio mjasiliamali? kwa sababu akivirudisha kwenye market vitalipa sana.
Mkuu kabwe makanika,aka jitu kumbuka au giant to remember alikuwa kwenye kitabu cha unyama wa mafia
 
stori za jamaa ni taaamu mnoo, inshort ukizisoma tu nikama unatizama kwa screen.

Kwa habari ya kuhuzunisha ni kuwa ELVIS A.MSIBA alifariki mwaka 2010.

POLENI SANA MASHABIKI WAKE.
 
'Willy Gamba kama unathamini maisha yako achana na hao watu wa gazeti la Africa.Kama ni rafiki zako basi waambie leo saa kumi na mbili wawe uwanja wa ndege.Vinginevyo yaliyompata Kamara Frank yatawapata nanyi.Subiani.' Hii ni kutoka njama halafu nyingine 'Aisee Mlambo iiiiji...mjukuu wa Chaka mwana wa Zulu fanya kazi yako'
Musiba sr ameshafariki.Mwanae anataka kugombea Ubunge huko Bunda pia aliwahi kuwa mtangazaji Ch. Ten
 
Kitabu cha njama kilikuwa kikitumika na wanafunzi wa A level miaka ya 90 - 2000
Jamaa alikuwa mtunzi mzuri ingawa yeye fani yake ilikuwa ni uhasibu.
 
"leo sijaja kula chochote bali ni kuwauwa wapinga mapinduzi wote,wewe ukiwa mmoja wao"

"Nguo aliyovaa Veronica Amadu ilikuwa na matundu madomadogo yaliyosababisha nione umbo la chuchu zake"

"Nilisimama nikiliangalia gari la Veronica Amadu mpaka taa za nyuma zilipofifia''

"sammy alikuwa na akili sana,aliweza kutafsiri mambo kwa haraka sana na alikuwa na uwezo mkubwa wa kutumia Kisu,alikuwa na uhakika wa kuua watu watatu kwa visu vitatu kuliko mimi nikiwa na risasi tano"

"tulikuta ujumbe umeandikwa KUONDOKA LEO NA MMOJA KATI YA WAONYESHA MAVAZI KUTOKA UADUINI TUNAMOFIKIRI,hapa tulikuja Kujua kuwa mshiriki kutoka south Afrika ambae alikuwa anaondoka siku hiyo,atakuwa amebeba nyaraka hizo"
 
"leo sijaja kula chochote bali ni kuwauwa wapinga mapinduzi wote,wewe ukiwa mmoja wao"

"Nguo aliyovaa Veronica Amadu ilikuwa na matundu madomadogo yaliyosababisha nione umbo la chuchu zake"

"Nilisimama nikiliangalia gari la Veronica Amadu mpaka taa za nyuma zilipofifia''

"sammy alikuwa na akili sana,aliweza kutafsiri mambo kwa haraka sana na alikuwa na uwezo mkubwa wa kutumia Kisu,alikuwa na uhakika wa kuua watu watatu kwa visu vitatu kuliko mimi nikiwa na risasi tano"

"tulikuta ujumbe umeandikwa KUONDOKA LEO NA MMOJA KATI YA WAONYESHA MAVAZI KUTOKA UADUINI TUNAMOFIKIRI,hapa tulikuja Kujua kuwa mshiriki kutoka south Afrika ambae alikuwa anaondoka siku hiyo,atakuwa amebeba nyaraka hizo"

umenikumbusha mbali sana,
 
wakuu naombeni msaada wenu kama kuna anayejua ninakoweza kupata hivi vitabu ya Elvis Musiba, vikiwa na stellingi Willy Gamba.

Vitabu hivyo ni kama vile:
1.Kikosi cha Kisasi
2.Kufa na Kupona
3.Hofu.
4.Njama
5.Uchu

na vinginevyo. nimevisoma baadhi zamani lakini sasa hivi sina nakala tena ningependa kujua ninakoweza kuvipata.

shukrani!
HUYU jamaa aliwahi kuwa mwandishi mzuri wa hadithi za kubuni (creative writting) hivi kwa nini siku hizi hawapo ? waandishi wengi ambao hata riwaya na tamthilia zao zinatumika mashuleni ni wale wasomi wa miaka ya 60 na 70 kwa sasa sijaona vitabu vipya, anyway hivi mkuu #Kaizer** ulifanikiwa kupata hivi vitabu lakini niliwahhi kusikia kuwa polisi wakikukamata navyo unakesi ya kujibu? hivi ni kweli?
 
Unfortunately sipo zanzibar muda mrefu sasa, lakini kama unavitaka kweli Masomo Bookshop, Darajani ni pahala pa uhakika zaidi, unaweza kuwasiliana na Farouk Karim mwenyewe anakuwepo dukani hapo, au unaweza kupata kontakti zake katika Ofisi yoyote ya ITV/Redio One, Dsm hapo,(yye ni mwandishi wa habari wa vituo hivyo), au mwandishi yeyote wa vituo hivyo anaweza akakupatia kontakti zake.Kama utaweza kufika zanzibar, ukifika soko kuu la Darajani, ukimuuliza mtu yeyote wapi Masomo Bookshop kwa Farouk Karim atakupeleka wala si mbali kutoka sokoni.
 
Mbona hivi vitabu vipo tele tu katika maduka ya kuuzia vitabu "book shops", ingekuwa upo visiwani ningekuelekeza kwa Farouk Karim, Masomo BookShop, Darajani.
Bytheway, Huyu muandishi wa Riwaya hizi yupo wapi siku hizi, na anafanya kazi gani?
Nilizipenda sana kazi zake kama hizo ulizozitaja, lakini iliyonisisimua zaidi ni ile ya KIKOMO.
Alishafariki musiba. Hapa dar hivi vitabu havipo jaribu visiwan
 
HUYU jamaa aliwahi kuwa mwandishi mzuri wa hadithi za kubuni (creative writting) hivi kwa nini siku hizi hawapo ? waandishi wengi ambao hata riwaya na tamthilia zao zinatumika mashuleni ni wale wasomi wa miaka ya 60 na 70 kwa sasa sijaona vitabu vipya, anyway hivi mkuu #Kaizer** ulifanikiwa kupata hivi vitabu lakini niliwahhi kusikia kuwa polisi wakikukamata navyo unakesi ya kujibu? hivi ni kweli?
Nadhani kuna kitabu kimoja kilikuwa kinaitwa HUJUMA, nasikia ndicho ilikuwa ni kosa la jinai kukisoma wala kuonekana nacho. Hiki nadhani ndicho kitabu cha E. Musiba ambacho sikupata kukiona kabisa enzi hizo niliposoma vitabu vyake vingine.
 
........... mwanangu usikubali kufa kama kondoo...... Willy Gamba kitabu Kufa na Kupona
 
Back
Top Bottom