Life starts at 45
JF-Expert Member
- Sep 22, 2015
- 1,002
- 1,004
Hope kesho kutakuwa na visa hapa vya kutosha
Tank nilikuwa namaanisha uwezo wa mtu kunywa na kulewaNadhani ishu hapo sio ujazo wa tank,bali Kichwa,watu tunatofautiana vichwa,kuna wale hata akisikia harufu ya pombe analewa chakali.
Mpaka kunya mkuu 😂😂😂Yaani mi binafsi sina wazo kabisa la kuiacha pamoja na yote inayonifanyiaga lakini haijanikomoa.
Ninakumbuka kiroba cha boss tangawizi hangover yake balaa,inafunga hamu ya kula,kunya mpaka kuoga na ukijilazimisha kunywa supu basi mchuzi mnaugawana na meza kwa jinsi mikono inavyotetemeka.
Sio kunya tuu cha kushangaza mi hata kulalaMpaka kunya mkuu 😂😂😂
Unaweza jikataa chief [emoji3]Pombe imeniletea visa vingi sana hapa duniani, nilikwenda Mbeya kikazi miaka tisa au kumi iliyopita. Kukawa kuna baa mpya inazunduliwa pale Uyole njia panda inaitwa Queen bar, nilikunywa pombe nakuja kuzinduka alfajiri nimelala kwenye mashamba ya mahindi ya chuo cha kilimo. Yaani badala ya kwenda guest niliyofikia nikaenda upande mwingine kabisa.
Ulikua unakata moto kisembe kabisa [emoji3]Ngoja niweke mkasa wangu mwingine ulitokea 2004, Jamaa zangu walitoka mgodini wana hela ya maana wamekuja na mshikaji wao watupambanishe kunywa pombe wanajua mimi kichwa ngumu kwenye bia. Nikawapa masharti kuwa nakunywa bia na si pombe kali. Wakaleta kreti moja ya Tusker na jamaa akapewa yakwake hiyo ni saa mbili asubuhi tumeshakula ugali kwa supu ya samaki. Kufika saa saba nimemaliza kreti jamaa kachemsha. Nikaaga nikaenda kulala, nakuja kushtuka kesho yake mchana majirani wanabomoa mlango wakijua nimekufa. Walichungulia dirishani wanaona mtu kalala chini wakajua nishaenda kwa Sir God. Niliugua siku 3 sijiwezi kabisa.
Dah nimecheka aisee [emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]Kipindi Niko chuo kikuu Cha Dar es Salaam miaka Ile. Tulikua tunakwenda kunywa wanzuki au mbege maeneo ya Riverside. Siku hiyo tulipata boom vzr Basi tukaona tukapate mbili tatu. Tukafika pale zilipo hostel za mabibo enzi hizo hazijajengwa kulikua na vibanda vya pombe za ovyo. Tukaanza kugida wanzuki. Wenzangu wakachoka wakaniacha na li barmeid Fulani umri umesogea. Kufika saa nne hivi nikaanza kuliona Ni beautiful Fulani. Basi nikalikokota Hadi hall one tower block kwa wale mliopitia shule za ukweli. Tukapanda mpaka kwa room na kufanya majambooz. Asubuhi naamka kwenda kukojoa nikaona ndala za yule mmama zilikua zimetoboka pale anapokanyagia na zimekarabatiwa na waya. Kumcheki kichwani ametia Ile kalkit ya muonekano Kama nywele zimetiwa maji au mafuta mengi. Kumbuka wanafunzi wameshaanza kukaa pale chini karibu na ofisi ya hall manager, wengine wanapiga stori wakitokea kafeteria kupata chai. Mimi Niko juu gorofani na msukule wangu unao dai lazima nimpeleke kituo Cha Basi. Madem wa chuo nao wapo pale stendi wanasubiri daladala. Mimi bado Nina msukule wangu anadai anataka kuwahi kutengeneza pombe mabibo. Aloo.
Nilimlaumu shetani na kazi zake zote. Nitampitishaje yule msukule mbele ya ma brazamen?
Tulia. Nakuletea kisa kingine utacheka mpaka meno yatoke.Dah nimecheka aisee [emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
Mkuu, habari za siku nyingi; Nimefanikiwa kumaintain na kujitoa kwenye hilo dubwasha la ulevi. JF ina msaada mkubwa sana kwa hili.vipi umeweza kumaintain??[emoji3][emoji3][emoji3]
Safi sana na hongera kwa hiloTarehe 20 nitatimiza miezi mitatu bila kunywa pombe....
Miezi mitatu bila kufanya ngono.
Miezi mitatu bila kula wanga (ugali na wali)
Itakua miezi mitatu natimiza kilo 75 kutoka kilo 96.....
Super....