Viongozi 9 kutoka Afrika waliotawala kwa muda mrefu zaidi na bado wapo madarakani

Wild Flower

Member
Jul 20, 2023
80
96
1. Teodoro Obiang Nguema Mbasogo - Miaka 44
Huyu anashikilia rekodi ya kuwa Mtawala aliyekaa muda mrefu zaidi madarakani. Ni Rais wa Equatorial Guinea ambaye ameshika madaraka tangu Agosti 1979 baada ya kumpindua Mjomba wake Francisco Macías Nguema.

Mbali na Afrika, Mbasogo anashikilia rekodi ya dunia pia kwa kukaa Ikulu kwa muda mrefu zaidi.

2. Paul Biya - Miaka 41
Amekuwa Rais wa Cameroon tangu Novemba 6, 1982. Anashika nafasi ya pili kwa kukaa madarakani kwa muda mrefu zaidi Barani Afrika, na ndiye Rais mzee zaidi duniani.

3. Denis Sassou Nguesso - Miaka 39
Ni Rais wa Jamhuri ya Congo kwa miaka 34 mfululizo lakini pia aliwahi kuwa Rais wa Taifa hilo kati ya mwaka 1979 hadi 1992 baadaye akarudi tena mwaka 1997 baada ya kumalizika kwa Mapigano ya Kiraia na kuendeleza utawala wake unaofikia miaka 39.

4. Yoweri Kaguta Museveni - Miaka 37
Unaweza kumuita Mzee au Babu, amekuwa Rais wa Uganda tangu mwaka 1986 muda unaomfanya kuwa kiongozi wa 4 aliyetawala kwa muda mrefu zaidi Afrika huku akishika nafasi ya kwanza kwa Afrika Mashariki.

Museveni aliingia madarakani Januari 1986 baada ya kushinda vita ya ndani iliyofuta utawala wa Milton Obote na makundi ya Idi Amin Dada Oumee.

5. Mfalme Mswati III - Miaka 37
Mswati III ni mtawala wa Eswatini (Zamani ilijulikana kama Swaziland), ndiye kiongozi mkuu wa Familia ya Kifalme ya Kiswazi.

Aliapishwa kuwa Mfalme Aprili 25, 1986 akiwa na miaka 18 na kumfanya kuwa kiongozi mwenye umri mdogo zaidi duniani kwa wakati huo.

Mswati anaiongoza Eswatini akiwa na Mama yake mzazi, Ntfombi Tfwala, ambaye ndiye Mama Malkia, unaweza kumwita Ndlovukati.

6. Isaias Afwerki - Miaka 37
Huyu ni Rais wa kwanza wa Eritrea ambaye amekuwa madarakani tangu taifa hilo lilipopata Uhuru kutoka Ethiopia, Aprili 1993.

Wengine ni

7. Ismaïl Omar Guelleh, Rais wa Djibouti kwa miaka Miaka 24.

8. Mfalme Mohammed VI
Huyu ni Mtawala wa Morocco amekuwa madarakani kwa miaka 24 tangu July 1999, alipokabidhiwa Mamlaka baada ya kifo cha baba yake, Mfalme Hassan II.

9. Paul Kagame - Miaka 23
Kagame aliingia rasmi Ikulu Aprili 2000 akiwa ni Rais wa 4 wa Rwanda. Lakini amekuwa kiongozi wa taifa hilo tangu mwaka 1994 ingawa alijielekeza zaidi kwenye masuala ya Kijeshi, Mambo ya Nje na Usalama wa Nchi.

Alitwaa madaraka baada ya Rais Bizimungu kujiuzulu.

 
Mimi.

Nimekua Rais wa Jamhuri ya kichwa changu kwa muda mrefu sana.
 
Dah! Kwa dunia kama elizabeth the second angekuwa hai angekuwa anaongoza 4 -0 first half
 
Kesho tujadili pia vile vyama vinganganizi kutoka madarakani - miaka 50 chama hakipendwi ila hakitaki kutoka madarakani yaani wanafanya kubadilishana tu utafikiri ni nchi ya kifalme.
 
Kuna wapenda madaraka na wamekaa madarakani muda mrefu na kuna wenye kupenda madaraka na kutaka hao waliyokaa muda mrefu madarakani watoke ili waingie wao.
 
1. Teodoro Obiang Nguema Mbasogo - Miaka 44
Huyu anashikilia rekodi ya kuwa Mtawala aliyekaa muda mrefu zaidi madarakani. Ni Rais wa Equatorial Guinea ambaye ameshika madaraka tangu Agosti 1979 baada ya kumpindua Mjomba wake Francisco Macías Nguema.

Mbali na Afrika, Mbasogo anashikilia rekodi ya dunia pia kwa kukaa Ikulu kwa muda mrefu zaidi.

2. Paul Biya - Miaka 41
Amekuwa Rais wa Cameroon tangu Novemba 6, 1982. Anashika nafasi ya pili kwa kukaa madarakani kwa muda mrefu zaidi Barani Afrika, na ndiye Rais mzee zaidi duniani.

3. Denis Sassou Nguesso - Miaka 39
Ni Rais wa Jamhuri ya Congo kwa miaka 34 mfululizo lakini pia aliwahi kuwa Rais wa Taifa hilo kati ya mwaka 1979 hadi 1992 baadaye akarudi tena mwaka 1997 baada ya kumalizika kwa Mapigano ya Kiraia na kuendeleza utawala wake unaofikia miaka 39.

4. Yoweri Kaguta Museveni - Miaka 37
Unaweza kumuita Mzee au Babu, amekuwa Rais wa Uganda tangu mwaka 1986 muda unaomfanya kuwa kiongozi wa 4 aliyetawala kwa muda mrefu zaidi Afrika huku akishika nafasi ya kwanza kwa Afrika Mashariki.

Museveni aliingia madarakani Januari 1986 baada ya kushinda vita ya ndani iliyofuta utawala wa Milton Obote na makundi ya Idi Amin Dada Oumee.

5. Mfalme Mswati III - Miaka 37
Mswati III ni mtawala wa Eswatini (Zamani ilijulikana kama Swaziland), ndiye kiongozi mkuu wa Familia ya Kifalme ya Kiswazi.

Aliapishwa kuwa Mfalme Aprili 25, 1986 akiwa na miaka 18 na kumfanya kuwa kiongozi mwenye umri mdogo zaidi duniani kwa wakati huo.

Mswati anaiongoza Eswatini akiwa na Mama yake mzazi, Ntfombi Tfwala, ambaye ndiye Mama Malkia, unaweza kumwita Ndlovukati.

6. Isaias Afwerki - Miaka 37
Huyu ni Rais wa kwanza wa Eritrea ambaye amekuwa madarakani tangu taifa hilo lilipopata Uhuru kutoka Ethiopia, Aprili 1993.

Wengine ni

7. Ismaïl Omar Guelleh, Rais wa Djibouti kwa miaka Miaka 24.

8. Mfalme Mohammed VI
Huyu ni Mtawala wa Morocco amekuwa madarakani kwa miaka 24 tangu July 1999, alipokabidhiwa Mamlaka baada ya kifo cha baba yake, Mfalme Hassan II.

9. Paul Kagame - Miaka 23
Kagame aliingia rasmi Ikulu Aprili 2000 akiwa ni Rais wa 4 wa Rwanda. Lakini amekuwa kiongozi wa taifa hilo tangu mwaka 1994 ingawa alijielekeza zaidi kwenye masuala ya Kijeshi, Mambo ya Nje na Usalama wa Nchi.

Alitwaa madaraka baada ya Rais Bizimungu kujiuzulu.

View attachment 2841575
Halafu wote hao ni madikteta wa kutupwa..

Tanzania, kwa zaidi ya nusu karne imepatwa na chama kimoja cha kidikteta badala ya mtu
 
1. Teodoro Obiang Nguema Mbasogo - Miaka 44
Huyu anashikilia rekodi ya kuwa Mtawala aliyekaa muda mrefu zaidi madarakani. Ni Rais wa Equatorial Guinea ambaye ameshika madaraka tangu Agosti 1979 baada ya kumpindua Mjomba wake Francisco Macías Nguema.

Mbali na Afrika, Mbasogo anashikilia rekodi ya dunia pia kwa kukaa Ikulu kwa muda mrefu zaidi.

2. Paul Biya - Miaka 41
Amekuwa Rais wa Cameroon tangu Novemba 6, 1982. Anashika nafasi ya pili kwa kukaa madarakani kwa muda mrefu zaidi Barani Afrika, na ndiye Rais mzee zaidi duniani.

3. Denis Sassou Nguesso - Miaka 39
Ni Rais wa Jamhuri ya Congo kwa miaka 34 mfululizo lakini pia aliwahi kuwa Rais wa Taifa hilo kati ya mwaka 1979 hadi 1992 baadaye akarudi tena mwaka 1997 baada ya kumalizika kwa Mapigano ya Kiraia na kuendeleza utawala wake unaofikia miaka 39.

4. Yoweri Kaguta Museveni - Miaka 37
Unaweza kumuita Mzee au Babu, amekuwa Rais wa Uganda tangu mwaka 1986 muda unaomfanya kuwa kiongozi wa 4 aliyetawala kwa muda mrefu zaidi Afrika huku akishika nafasi ya kwanza kwa Afrika Mashariki.

Museveni aliingia madarakani Januari 1986 baada ya kushinda vita ya ndani iliyofuta utawala wa Milton Obote na makundi ya Idi Amin Dada Oumee.

5. Mfalme Mswati III - Miaka 37
Mswati III ni mtawala wa Eswatini (Zamani ilijulikana kama Swaziland), ndiye kiongozi mkuu wa Familia ya Kifalme ya Kiswazi.

Aliapishwa kuwa Mfalme Aprili 25, 1986 akiwa na miaka 18 na kumfanya kuwa kiongozi mwenye umri mdogo zaidi duniani kwa wakati huo.

Mswati anaiongoza Eswatini akiwa na Mama yake mzazi, Ntfombi Tfwala, ambaye ndiye Mama Malkia, unaweza kumwita Ndlovukati.

6. Isaias Afwerki - Miaka 37
Huyu ni Rais wa kwanza wa Eritrea ambaye amekuwa madarakani tangu taifa hilo lilipopata Uhuru kutoka Ethiopia, Aprili 1993.

Wengine ni

7. Ismaïl Omar Guelleh, Rais wa Djibouti kwa miaka Miaka 24.

8. Mfalme Mohammed VI
Huyu ni Mtawala wa Morocco amekuwa madarakani kwa miaka 24 tangu July 1999, alipokabidhiwa Mamlaka baada ya kifo cha baba yake, Mfalme Hassan II.

9. Paul Kagame - Miaka 23
Kagame aliingia rasmi Ikulu Aprili 2000 akiwa ni Rais wa 4 wa Rwanda. Lakini amekuwa kiongozi wa taifa hilo tangu mwaka 1994 ingawa alijielekeza zaidi kwenye masuala ya Kijeshi, Mambo ya Nje na Usalama wa Nchi.

Alitwaa madaraka baada ya Rais Bizimungu kujiuzulu.

View attachment 2841575
Tukimaliza maraisi tugeukie wenyeviti wa maisha!
 
Rais wa Eritrea amekuwa madarakani kwa miaka 30 sasa na sio 37. Halafu hao madikteta wote ni majizi kupindukia
 
Back
Top Bottom