Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,341
- 51,907
Bila Shaka mpo Pouwa!
Kwa kweli Njia ya kujiajiri ni ngumu Sana. Kupitia ugumu huo waliofanikiwa kujiajiri huwa na heshima na umakini wao kiasi kwamba inawawia vigumu kuamini Watu kirahisi hasa wale wakuwasaidia.
Vijana wengi wanapenda Sana kushikwa Mkono, kusaidiwa iwe sehemu za kujishikiza na kufanya vikazi ili wapate riziki na Wakati mwingine uzoefu kazini. Lakini Kwa bahati Mbaya wenye biashara na makampuni hawaruhusu Jambo Hilo kutokea Kutokana na Baadhi ya tabia Mbaya ya Vijana waliowengi.
Tabia Mbaya zinazoripotiwa kujitokeza mara Kwa mara ni pamoja na;
1. Kukosa uaminifu.
Uaminifu unaposhikwa mkono ndio silaha namba moja ili upige hatua. Lakini Vijana wengi wamejikuta walikosa Sifa Hii.
Upo uaminifu wa Aina nyingi lakini mtego ambao wengi hushindwa ni uaminifu wa Pesa na kushindwa kujizuia kimwili.
Wizi WA Pesa pamoja na uzinzi(Kufanya ngono na watoto wa boss) imekuwa ni changamoto kubwa Kwa Vijana wengi.
2. Kukosa Subira.
Kijana anataka akishakuja kwako basi umsikilize hapohapo kisha umsaidie hapohapo.
Hata umempa nafasi ya kuja kufanya kazi ya kujishikisha humlipi chochote zaidi ya posho ya Kula na nauli. Lakini yeye ndani ya muda mfupi ataanza usumbufu,
Ni kama wanapenda mambo yote yafanyike Kwa Usiku mmoja.
Vijana unapotaka connection itakupasa uwe na Subira, subira itakupa matunda kuliko kujifanya unaharaka.
Kwani unaharakia kitu gani?
3. Kukosa Shukrani.
Vijana wengi wapewapo nafasi badala ya kuwa na shukrani matokeo yake wanakuwa Watu wa lawama. Ikiwezekana inakuwa vita baina ya kijana na boss wake aliyempa nafasi.
Kukosa Shukrani ni pamoja na kutotenda wajibu wako kama kijana.
Vijana wengi Zama za Leo suala la shukrani kwao ni kipengele.
Ni wepesi kuomba msaada na kujiliza huku wakitoa ahadi lukuki kuwa ukimpa nafasi atafanya vizuri lakini ukishampa nafasi ataishia kukuangusha.
Jambo hilo linafanya wengi wasitoe nafasi Kwa Vijana.
4. Vijana wengi ni Wavivu.
Wanahitaji wafanye kazi Kwa kusimamiwa. Iwe ni kazi ya Hospitalini, shuleni, shambani, dukani au popote. Vijana wengi wa kibongo ni Wavivu. Sio wachapakazi wakujituma wenyewe.
Mwanzoni watazuga kana kwamba Wana Ari ya kufanya kazi lakini ndani ya miezi mitatu nguvu ya soda itawaishia.
5. Vijana wengi Wana WIVU.
Vijana wengi ukiwapa nafasi alafu wakajua kiasi unachokiingiza wataingiza wivu. Wataanza jamaa anaingiza Pesa yote hiyo alafu anashindwa kunilipa Pesa nzuri. Hapo ndipo wengi huanza kujifunza kukuibia na usipoangalia biashara yako itaenda mrama.
Kijana atakachosahau ni nafasi yake.
6. Vijana wengi wanajiona wanaakili kukushinda pale unapowapa nafasi.
Moja ya tabia za Vijana wengi wa Kitanzania ni kufikiri wenye Pesa Hawana Akili 😂😂 sijajua hii dhana waliipata Kwa Nani lakini bila Shaka ni ujinga unaowachanganya.
Vijana wengi ukiwapa nafasi kadiri unavyomuweka karibu badala aone upendo unaomuonyesha yeye ataanza kukuona wewe ni mjinga na hizo Mali umezipata Kwa bahati tuu!
Taikon Kwa uzoefu wangu na chunguzi zangu, zinaonyesha kuwa Vijana wengi ukikaa nao wanafikiri wao wanamawazo yenye Akili sema Hawana Pesa ukilinganisha na wale Vijana waliofanikiwa. Na wengi kupitia mawazo Yao hayo ambayo ni Utopia wanafikiri ni kweli wanaakili Wakati Akili sio tuu kuwa na wazo Fulani Bali pia ni kutekeleza wazo Hilo Kwa ufanisi mkubwa.
Nawatakia jumapili njema!
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Kwa kweli Njia ya kujiajiri ni ngumu Sana. Kupitia ugumu huo waliofanikiwa kujiajiri huwa na heshima na umakini wao kiasi kwamba inawawia vigumu kuamini Watu kirahisi hasa wale wakuwasaidia.
Vijana wengi wanapenda Sana kushikwa Mkono, kusaidiwa iwe sehemu za kujishikiza na kufanya vikazi ili wapate riziki na Wakati mwingine uzoefu kazini. Lakini Kwa bahati Mbaya wenye biashara na makampuni hawaruhusu Jambo Hilo kutokea Kutokana na Baadhi ya tabia Mbaya ya Vijana waliowengi.
Tabia Mbaya zinazoripotiwa kujitokeza mara Kwa mara ni pamoja na;
1. Kukosa uaminifu.
Uaminifu unaposhikwa mkono ndio silaha namba moja ili upige hatua. Lakini Vijana wengi wamejikuta walikosa Sifa Hii.
Upo uaminifu wa Aina nyingi lakini mtego ambao wengi hushindwa ni uaminifu wa Pesa na kushindwa kujizuia kimwili.
Wizi WA Pesa pamoja na uzinzi(Kufanya ngono na watoto wa boss) imekuwa ni changamoto kubwa Kwa Vijana wengi.
2. Kukosa Subira.
Kijana anataka akishakuja kwako basi umsikilize hapohapo kisha umsaidie hapohapo.
Hata umempa nafasi ya kuja kufanya kazi ya kujishikisha humlipi chochote zaidi ya posho ya Kula na nauli. Lakini yeye ndani ya muda mfupi ataanza usumbufu,
Ni kama wanapenda mambo yote yafanyike Kwa Usiku mmoja.
Vijana unapotaka connection itakupasa uwe na Subira, subira itakupa matunda kuliko kujifanya unaharaka.
Kwani unaharakia kitu gani?
3. Kukosa Shukrani.
Vijana wengi wapewapo nafasi badala ya kuwa na shukrani matokeo yake wanakuwa Watu wa lawama. Ikiwezekana inakuwa vita baina ya kijana na boss wake aliyempa nafasi.
Kukosa Shukrani ni pamoja na kutotenda wajibu wako kama kijana.
Vijana wengi Zama za Leo suala la shukrani kwao ni kipengele.
Ni wepesi kuomba msaada na kujiliza huku wakitoa ahadi lukuki kuwa ukimpa nafasi atafanya vizuri lakini ukishampa nafasi ataishia kukuangusha.
Jambo hilo linafanya wengi wasitoe nafasi Kwa Vijana.
4. Vijana wengi ni Wavivu.
Wanahitaji wafanye kazi Kwa kusimamiwa. Iwe ni kazi ya Hospitalini, shuleni, shambani, dukani au popote. Vijana wengi wa kibongo ni Wavivu. Sio wachapakazi wakujituma wenyewe.
Mwanzoni watazuga kana kwamba Wana Ari ya kufanya kazi lakini ndani ya miezi mitatu nguvu ya soda itawaishia.
5. Vijana wengi Wana WIVU.
Vijana wengi ukiwapa nafasi alafu wakajua kiasi unachokiingiza wataingiza wivu. Wataanza jamaa anaingiza Pesa yote hiyo alafu anashindwa kunilipa Pesa nzuri. Hapo ndipo wengi huanza kujifunza kukuibia na usipoangalia biashara yako itaenda mrama.
Kijana atakachosahau ni nafasi yake.
6. Vijana wengi wanajiona wanaakili kukushinda pale unapowapa nafasi.
Moja ya tabia za Vijana wengi wa Kitanzania ni kufikiri wenye Pesa Hawana Akili 😂😂 sijajua hii dhana waliipata Kwa Nani lakini bila Shaka ni ujinga unaowachanganya.
Vijana wengi ukiwapa nafasi kadiri unavyomuweka karibu badala aone upendo unaomuonyesha yeye ataanza kukuona wewe ni mjinga na hizo Mali umezipata Kwa bahati tuu!
Taikon Kwa uzoefu wangu na chunguzi zangu, zinaonyesha kuwa Vijana wengi ukikaa nao wanafikiri wao wanamawazo yenye Akili sema Hawana Pesa ukilinganisha na wale Vijana waliofanikiwa. Na wengi kupitia mawazo Yao hayo ambayo ni Utopia wanafikiri ni kweli wanaakili Wakati Akili sio tuu kuwa na wazo Fulani Bali pia ni kutekeleza wazo Hilo Kwa ufanisi mkubwa.
Nawatakia jumapili njema!
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam