BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,376
- 8,118
Zaidi ya vijana 100 wa Programu ya Kuwezesha Ushiriki wa Vijana Katika Kilimo Biashara (BBT- YIA) wanadaiwa kuondoka katika kambi ya Chinangali, Dodoma, ambako vijana hao wamekusanywa, wakidai hakuna mwelekeo kambini hapo, huku wakiishutumu Serikali kwa kushindwa kwake kutimiza ahadi ilizotangaza awali.
Kwa mujibu wa taarifa ilizozifikia The Chanzo, mpaka kufikia jioni ya Machi 19, 2024, vijana waliokuwepo kambini hapo ni kati ya 120 na 128 kutoka vijana 268 ambao Serikali imekuwa ikidai kuwepo Chinangali kushiriki kwenye programu hiyo inayokusudiwa kuongeza ajira za vijana milioni tatu na kuongeza ukuaji wa kilimo nchini hadi kufikia asilimia kumi ifikapo mwaka 2030.
“Watu tulioko pale [kambini] mpaka sasa hivi tunafika 134, kati ya watu 268 tuliotakiwa kuripoti, lakini walioripoti ni 261,” alisema mmoja wa viongozi wa vijana hao ambaye The Chanzo imeamua kutotaja jina lake kulinda usalama wake. “Watu wengine waliobaki hawako kwenye kituo, hawako kwenye kituo kwa sababu pale hakuna kinachoeleweka.”
“Wengine wanakuja, wanakaa siku mbili, wanachungulia, wanaondoka, wale wenye uwezo wa kifedha,” aliongeza kijana huyo. “Kwa siku mbili hizi, [Machi 18 na 19], watu wengi wameondoka, tumebaki watu kama 120 hivi. Lakini muda mwingi tunacheza hapo 120 hadi 130. Wengi wamekimbia hali iliyoko pale [kambini].”
Mmoja kati ya vijana walioondoka kambini hapo ameiambia The Chanzo: “Mimi binafsi nimeondoka, kuna mambo yangu nimekuja kufuatilia. Unajua kipindi kile watu wengi tuliondoka kwa sababu hapakuwa panaeleweka hapo ila nitarudi muda si mrefu. Pale kambini kusema ukweli panaboa. Sasa ukae pale ufanye shughuli gani, sasa ukalime shamba la ushirika ambalo hujui hata utavuna nini?”
The Chanzo ilimuuliza Vumilia Zinkankuba, Mratibu wa Programu ya BBT, endapo kama taarifa za vijana kuondoka kambini hapo zina ukweli wowote, ambapo aliomba apewe kwanza chanzo cha taarifa hiyo ndiyo ajibu kama ni za kweli au la.
The Chanzo, hata hivyo, iligoma kufichua watoa taarifa wake kwani kufanya hivyo siyo tu kungewaweka hatarini bali pia ni kwenda kinyume na maadili ya uandishi wa habari yanayosisitiza umuhimu wa kuwaficha watoa taarifa.
The Chanzo
Kwa mujibu wa taarifa ilizozifikia The Chanzo, mpaka kufikia jioni ya Machi 19, 2024, vijana waliokuwepo kambini hapo ni kati ya 120 na 128 kutoka vijana 268 ambao Serikali imekuwa ikidai kuwepo Chinangali kushiriki kwenye programu hiyo inayokusudiwa kuongeza ajira za vijana milioni tatu na kuongeza ukuaji wa kilimo nchini hadi kufikia asilimia kumi ifikapo mwaka 2030.
“Watu tulioko pale [kambini] mpaka sasa hivi tunafika 134, kati ya watu 268 tuliotakiwa kuripoti, lakini walioripoti ni 261,” alisema mmoja wa viongozi wa vijana hao ambaye The Chanzo imeamua kutotaja jina lake kulinda usalama wake. “Watu wengine waliobaki hawako kwenye kituo, hawako kwenye kituo kwa sababu pale hakuna kinachoeleweka.”
“Wengine wanakuja, wanakaa siku mbili, wanachungulia, wanaondoka, wale wenye uwezo wa kifedha,” aliongeza kijana huyo. “Kwa siku mbili hizi, [Machi 18 na 19], watu wengi wameondoka, tumebaki watu kama 120 hivi. Lakini muda mwingi tunacheza hapo 120 hadi 130. Wengi wamekimbia hali iliyoko pale [kambini].”
Mmoja kati ya vijana walioondoka kambini hapo ameiambia The Chanzo: “Mimi binafsi nimeondoka, kuna mambo yangu nimekuja kufuatilia. Unajua kipindi kile watu wengi tuliondoka kwa sababu hapakuwa panaeleweka hapo ila nitarudi muda si mrefu. Pale kambini kusema ukweli panaboa. Sasa ukae pale ufanye shughuli gani, sasa ukalime shamba la ushirika ambalo hujui hata utavuna nini?”
The Chanzo ilimuuliza Vumilia Zinkankuba, Mratibu wa Programu ya BBT, endapo kama taarifa za vijana kuondoka kambini hapo zina ukweli wowote, ambapo aliomba apewe kwanza chanzo cha taarifa hiyo ndiyo ajibu kama ni za kweli au la.
The Chanzo, hata hivyo, iligoma kufichua watoa taarifa wake kwani kufanya hivyo siyo tu kungewaweka hatarini bali pia ni kwenda kinyume na maadili ya uandishi wa habari yanayosisitiza umuhimu wa kuwaficha watoa taarifa.
The Chanzo