Video: Tundu Lissu atoa ufafanuzi wa hoja aliyoitoa Babati Aprili 26, 2024 kumjibu Fatma Karume kuhusu 'Ubaguzi na Muungano wetu'

Naona kuna shida ya kuelewa point kuu ninayotaka kuzungumzia. Nilipoandika mfano wa Mafia, lengo kuu lilikuwa kwa ujumla, si Zzibar tu bali hata bara ubunge kati ya jimbo na jimbo haulinganishwi kwa idadi ya watu.
Nilichotaka kusema, Lissu kama anataka kuwa muwazi basi vile vile alaumu kwanini Mafia ina mbunge mwenye hadhi sawa na mbunge wa Kawe, kama idadi ya watu ndio vigezo?
Bado, hata Wilaya ya Mafia yenyewe, yenye wananchi zaidi ya 67,000; na ukubwa wa kilomita za mraba 640 huwezi ukailinganisha kwa vyovyote na jimbo la uchaguzi lolote toka Zanzibar; hata kwa vigezo hivyo pekee.
Suala la Muungano. Kwanza tukubaliane kuwa ni nchi 2 ndio zilizoungana, sio mikoa 2. Kumbuka Zanzibar ilkuwa na kiti umoja wa mataifa kilichokuwa na uzito sawa na Tanganyika. Tunaposema Tanzania imepiga kura umoja wa mataifa kupitisha suala fulani, kura hiyo ina uzito sawa na kura ya Burundi na Rwanda zenye watu chini ya 6 mil kila moja. Hivyo suala la nchi huheshimiwa kama nchi bila kujali kuna watu wangapi. Twende pamoja!
Sasa tuliungana ili iweje, Zanzibar ifaidi matunda ya Muungano bila ya yenyewe kupoteza chochote? Iendeshe mambo yake yenyewe bila ya kujali kuwa imo kwenye Muungano?
 
Mwaka 1964 Tanganyika ilikuwa na watu 12 milioni na Zanzibar takriban laki 3.5. Ni nchi mbili zenye uzito sawa kimataifa. Hivyo kulihitajika majadiliano yenye uzito sawa kwa kila upande. Katika kulinda hadhi ya watu wa Zanzibar ambao walikuwa 3.5 milioni, na Tanganyika Mengi yalifikiwa. Unaweza kukubaliana na baadhi ya mambo au hapana. Kwa maneno mengine Kila nchi ilitakiwa kuwa na kura ya Veto kwa kila nchi.
Zanzibar inatumia kura yake ya "Veto" kumsambaratisha mwenzake ndani ya muungano? Mbona huu utakuwa muungano wa hatari sana.
Mnapokubaliana kuungana, ni lazima mkubaliane kufanya mambo yenu kwa pamoja, vinginevyo hapatakuwa na muungano. Unapokwenda kujitengenezea Katiba yako itumike kwako na kuiweka pembeni ile iliyo waunganisha, unashiriki katika kuuvunja muungano wenu.
 
Tundu Hana wito wa siasa aendelee na shughuli za uwakili pamoja na Mwabukusi mwananchi wa kawaida hawezi kumuelewa Lisu wala Mwabukusi wana siasa ngumu sana hawana ushawishi zaidi ya kueneza chuki.
 
This is choir my friend...Hizi nyimbo mlizokaririshwa na mabeberu kama unaita knowledge basi pole...Hakuna kitu kibaya kama kutokujua hujui na Bado ukadhani unajua...All the best I have nothing to buy from your poems, jikomboe kwanza ki fikra Kisha utanishukuru baadaye
Mimi ndugu Ame NAJUA NITAKACHO na NINAJUA kuwa NAJUA..

Ona tu..

Nimekuuliza maswali specific kadhaa kwa kuzingatia hoja zako..

Lakini badala ujibu maswali, wewe umeanza kukimbia huku ukipiga mayowe..

Pole na kwaheri..
 
Tundu Hana wito wa siasa aendelee na shughuli za uwakili pamoja na Mwabukusi mwananchi wa kawaida hawezi kumuelewa Lisu wala Mwabukusi wana siasa ngumu sana hawana ushawishi zaidi ya kueneza chuki.
Ama kweli wewe ni Godo..

Kumbe sisi tunaowaelewa hawa jamaa ni wananchi special na sio wa kawaida..?

Umewaza kwa kutumia kiungo gani hata kuandika hii kitu hapa?
 
Mnapokubaliana kuungana, ni lazima mkubaliane kufanya mambo yenu kwa pamoja, vinginevyo hapatakuwa na muungano. Unapokwenda kujitengenezea Katiba yako itumike kwako na kuiweka pembeni ile iliyo waunganisha, unashiriki katika kuuvunja muungano wenu
Muungano wa kweli ni makubaliano kati ya pande mbili. Ni muhimu kufahamu kuwa muungano wa kweli hutanguliwa na kura za maoni kwa nchi zinazoungana. Hii inamaanisha kuwa Tanganyika wanapiga kura wenyewe na Zanzibar nao wanapiga kura wenyewe kama wanataka muungano. Hivyo kura za watanganyika 12 milioni (1964) uzito wake ni sawa na kura laki 3.5 za Zanzibar (Hapa ndio Lissu anafahamu wazi lakini anataka kudanganya watu na suala la Wabunge). Kama Zanzibar wakisema Hapana na Tanganyika wakasema Ndio, kisheria hapo hakuna Muungano.
Hakuna muungano wa aina moja, ni juu ya nchi mbili wamekubaliana nini. Hilo karatasi/contract ya Muungano ndio kila kitu na si maoni ya vijiweni. Kama karatasi limeandikwa kuwa Zanzibar itakuwa nchi yenye Rais wake na wawakilishi wake ndani ya Muungano itakuwa hivyo. Nawashangaa watu wanaolazimisha Zanzibar kuwa mkoa kwa kigezo cha idadi ya watu. Huu ni upotoshaji.
Kuna nchi zilizoungana kama Senegal na Gambia na kuitwa Senegambia. Lakini Muungano huo ulivunjika baadae baada ya Senegal kutaka kuifanya Gambia kama mkoa katika Muungano.
 
View attachment 2977398
Tazama na sikiliza kwa makini mwanzo mwisho video clip hii fupi ya dakika 16 Tundu Lissu akijibu hoja ya ubaguzi na matundu ya muungano wa Tanganyika & Zanzibar (1964) kwa kutumia katiba mbili za JMT (1977) na ile ya Zanzibar (1984) akihutubia maelfu ya wananchi Dodoma jana tarehe 29/4/2024.

Hakika utafunguliwa ufahamu wako na kila mtu atajua mjinga na mwerevu ni nani. Pengine ndiye mtawajua wabuguzi halisi ni kina nani...

Hii ni muhimu sana Nape Nauye na chama chake (CCM) wajitokeze kujibu hoja hizi na kuukanusha ukweli huu wa kikatiba kama unakanushika.

Mimi hata sijui mtu mwenye uelewa na ufahamu kama Tundu Lissu unaweza kumkamatia wapi ili umshitaki afungwe jela. Ni ngumu na pengine haiwezekani tu kabisa maana ni hakika kuwa: KNOWLEDGE IS POWER..!

Kila mtu anajua na kuelewa kuwa Samia Suluhu Hassan ni Mzanzibari. Yupo hapo kwa katiba hii ya 1977. HilI sina hakika kama lina ubishi wowote na kwwamba yupo mtu anaweza kulikanusha hili..

Na hivi inawezekana vipi kuwa kila ukweli unaojifunua kupitia kwa watu kama Tundu Lissu aliyejitoa kupigana kwa damu yake mwenyewe kwa ajili ya manufaa ya watu masikini wengi iwe ni ubaguzi na uchochezi? Really?

Mimi nadhani ifike wakati kila mtu wakiwemo watawala kupitia CCM waelewe kuwa nyakati za kuishi katika giza la ujinga wa kudanganywa na watawala umefika mwisho. Tunachosubiri kwa sasa ni justification tu kupitia "unyakuo"

Inashangaza kuwa kina Nape Nauye na CCM yake wanataka tuendelee kuishi ktk giza la ujinga na udanganyifu wa miaka 60..

Hapana. HII HAIWEZEKANI TENA... Watu wanataka kuishi katika Nuru ya haki na usawa...

Hebu nyie kina Dr Akili, ChoiceVariable, Tlaatlaah, Samiaagain2025 MamaSamia2025, Paul Makonda, @Nnape Nauye njooni mkanushe ukweli huu kwa hoja zenye ushahidi halafu mrudi tena kusema mbaguzi hapa ni nani. Pia mseme kama Rais Samia Suluhu Hassan sio mzanzibari, basi ni wa taifa lipi?

Na kuna ugumu gani wote kukiri kuwa kuna tatizo katika muungano huu wa 1964 kati ya Tanganyika na Zanzibar?

Kazi ya Tundu Lissu ni kuonesha matatizo lakini nyie mnamwita mbaguzi..!!

Looh!!, mna shida kwelikweli nyie

Pia soma: Tundu Lissu: Tuna Rais Mzanzibari anayeweza kwenda Ngorongoro na kutoa Amri kwa Wanajeshi wafukuze wamasai wote

View attachment 2978056
Tundu Lissu shida yake ni kuusema ukweli
 
Muungano wa kweli ni makubaliano kati ya pande mbili. Ni muhimu kufahamu kuwa muungano wa kweli hutanguliwa na kura za maoni kwa nchi zinazoungana. Hii inamaanisha kuwa Tanganyika wanapiga kura wenyewe na Zanzibar nao wanapiga kura wenyewe kama wanataka muungano. Hivyo kura za watanganyika 12 milioni (1964) uzito wake ni sawa na kura laki 3.5 za Zanzibar (Hapa ndio Lissu anafahamu wazi lakini anataka kudanganya watu na suala la Wabunge). Kama Zanzibar wakisema Hapana na Tanganyika wakasema Ndio, kisheria hapo hakuna Muungano.
Hakuna muungano wa aina moja, ni juu ya nchi mbili wamekubaliana nini. Hilo karatasi/contract ya Muungano ndio kila kitu na si maoni ya vijiweni. Kama karatasi limeandikwa kuwa Zanzibar itakuwa nchi yenye Rais wake na wawakilishi wake ndani ya Muungano itakuwa hivyo. Nawashangaa watu wanaolazimisha Zanzibar kuwa mkoa kwa kigezo cha idadi ya watu. Huu ni upotoshaji.
Kuna nchi zilizoungana kama Senegal na Gambia na kuitwa Senegambia. Lakini Muungano huo ulivunjika baadae baada ya Senegal kutaka kuifanya Gambia kama mkoa katika Muungano.
Wewe ni mtu mtulivu katika mijadala, nakupongeza kwa hilo.
Aya ya kwanza kuhusu kura ya maoni, ninakubaliana nawe kwamba wakati huu inafaa wananchi wahusishwe kuhusu huu muungano wetu; uendelee kuwepo, na kama uendelee uwe katika sura gani.

Najuwa unafahamu, kwamba wananchi hawakuhusishwa katika uamzi huo waasisi walpokubaliana pawepo na muungano. Hapa pia najuwa unaelewa kwa nini haikuwa hivyo.

Nafahamu pia kwamba, muungano ulivyo sasa, siyo ule uliokuwepo mwanzo. Maswala ya "kero nyingi za muungano" toka upande mmoja wa muungano ndizo zilizosababisha kwa kiasi kikubwa tukafikia hapa tulipo leo; kinyume kabisa na matarajio ya muungano walioutegemea waasisi; kwamba baada ya muda, tukisha zoeana vya kutosha na kuchanganyika kati yetu, hofu zilizokuwepo wakati ule zingekuwa zimepungua na kuruhusu muungano wa karibu zaidi. Badala yake, kero zilipo pamba moto, badala ya kuwa karibu, ndiyo tukawa tunatafuta njia ya kuua muungano.

Hili kundi linaloibua maswala ya kero kila mara, ni kundi lile lile lililokuwa haliutaki muungano toka mwanzo. Na kundi hili limepata nguvu zaidi walipopata wenzao waliokuwemo ndani ya CCM toka Zanzibar, ili wachochee kazi hiyo ya kuulegeza muungano ndani kwa ndani chamani.
Na kama nilivyokwisha sema huko nyuma, ndani ya CCM toka Tanganyika, kumekuwemo na ombwe la watu wanaoweza kusimama na kuutetea muungano. Huko kumejaa wanafiki tupu. Udhaifu huo ndio umetoa fursa kwa Zanzibar kuanza kufanya mambo yake ionavyo inawafaa wao badala ya kuangalia maslahi ya wote katika muungano
Watu wa CCM visiwani ndio walikuwa wamewashikiria kwa nguvu wenzao toka Tanganyika, kwa sababu tu za kulinda maslahi yao kwa jina la kuyaenzi Mapinduzi Tukufu. Na ni hawa, pamoja na kutekwa na lile kundi lisilo penda muungano, bado wanawang'ang'ania CCM wa Bara waendelee kuwakingia maslahi yao dhidi ya hao wasiotaka muungano.

Ni wakati mzuri sasa, huu muungano upekwe kwa wananchi, waamue wenyewe wanachotaka juu ya huu muungano.

Sasa hata hapa naona kuna shida, siyo hasa kwa upande wa Tanganyika; bali kwa upande wa Zanzibar. Pamoja na wingi wao ulivyo Tanganyika, hata wakiukataa muungano, kama lile kundi la CCM litapata waZanzibari wa kutosha kubaki kwenye muungano, Tanganyika hawezi kujitoa. Bila shaka hii ndiyo 'veto' uliyokuwa ukiizungumzia.

Hata ikitokea ikawa hivyo, maoni yangu ni kwamba kura hiyo ya maoni itatupatia fursa ya kuutazama upya muundo wa muungano wetu.
Kama kuna makosa ya kiuandishi humo ndani, naomba uniwie radhi, maana nilitiririka tu, yoka juu hadi mwisho.
 
Wewe ni mtu mtulivu katika mijadala, nakupongeza kwa hilo.
Aya ya kwanza kuhusu kura ya maoni, ninakubaliana nawe kwamba wakati huu inafaa wananchi wahusishwe kuhusu huu muungano wetu; uendelee kuwepo, na kama uendelee uwe katika sura gani.

Najuwa unafahamu, kwamba wananchi hawakuhusishwa katika uamzi huo waasisi walpokubaliana pawepo na muungano. Hapa pia najuwa unaelewa kwa nini haikuwa hivyo.

Nafahamu pia kwamba, muungano ulivyo sasa, siyo ule uliokuwepo mwanzo. Maswala ya "kero nyingi za muungano" toka upande mmoja wa muungano ndizo zilizosababisha kwa kiasi kikubwa tukafikia hapa tulipo leo; kinyume kabisa na matarajio ya muungano walioutegemea waasisi; kwamba baada ya muda, tukisha zoeana vya kutosha na kuchanganyika kati yetu, hofu zilizokuwepo wakati ule zingekuwa zimepungua na kuruhusu muungano wa karibu zaidi. Badala yake, kero zilipo pamba moto, badala ya kuwa karibu, ndiyo tukawa tunatafuta njia ya kuua muungano.

Hili kundi linaloibua maswala ya kero kila mara, ni kundi lile lile lililokuwa haliutaki muungano toka mwanzo. Na kundi hili limepata nguvu zaidi walipopata wenzao waliokuwemo ndani ya CCM toka Zanzibar, ili wachochee kazi hiyo ya kuulegeza muungano ndani kwa ndani chamani.
Na kama nilivyokwisha sema huko nyuma, ndani ya CCM toka Tanganyika, kumekuwemo na ombwe la watu wanaoweza kusimama na kuutetea muungano. Huko kumejaa wanafiki tupu. Udhaifu huo ndio umetoa fursa kwa Zanzibar kuanza kufanya mambo yake ionavyo inawafaa wao badala ya kuangalia maslahi ya wote katika muungano
Watu wa CCM visiwani ndio walikuwa wamewashikiria kwa nguvu wenzao toka Tanganyika, kwa sababu tu za kulinda maslahi yao kwa jina la kuyaenzi Mapinduzi Tukufu. Na ni hawa, pamoja na kutekwa na lile kundi lisilo penda muungano, bado wanawang'ang'ania CCM wa Bara waendelee kuwakingia maslahi yao dhidi ya hao wasiotaka muungano.

Ni wakati mzuri sasa, huu muungano upekwe kwa wananchi, waamue wenyewe wanachotaka juu ya huu muungano.

Sasa hata hapa naona kuna shida, siyo hasa kwa upande wa Tanganyika; bali kwa upande wa Zanzibar. Pamoja na wingi wao ulivyo Tanganyika, hata wakiukataa muungano, kama lile kundi la CCM litapata waZanzibari wa kutosha kubaki kwenye muungano, Tanganyika hawezi kujitoa. Bila shaka hii ndiyo 'veto' uliyokuwa ukiizungumzia.

Hata ikitokea ikawa hivyo, maoni yangu ni kwamba kura hiyo ya maoni itatupatia fursa ya kuutazama upya muundo wa muungano wetu.
Kama kuna makosa ya kiuandishi humo ndani, naomba uniwie radhi, maana nilitiririka tu, yoka juu hadi mwisho.
Upo sahihi Mkuu
Fact ni kuwa model ya Muungano iliyopo ni matokeo ya maamuzi yaliyotokana na utashi wa watu wasiozidi 20.

Na uwepo wake hadi sasa umetokana na low human capital hasa Bara. Wengi hawajui content ya muungano na implication zake katika maisha ya kila siku.

Fact nyingine ni kuwa muungano una faida kwa pande zote mbili kiuchumi, kijamii na zaidi kiusalama.

Tafiti zinatoa viashiria kuwa Zenji ipo salama na wamoja sasa kwa sababu ya Muungano. Mchonga aliwahi sema kwa lugha ya kidiplomasia ingawa wengi hawakuelewa kuhusu falsafa ya kumbagua mtu ukizani nyie ni wamoja kumbe ni simba na swala. Ishara zilizopo ni kuwa wakijitenga, Wapee watapaswa wapewe zenji au wajitenge na kuunda nchi ya Pembee kama ilivyo kwa njuani. Nje ya Muunganio wamakunduchi imekula kwao! Je bila Bara, CC ingekuwa inaongoza Zenji leo! Je bila Muungano 1995 na 2000 na 2015 nini kingetokea Zenji, nahisi hadi leo pangekuwa panachimbikai? Je wamakonde, wandengereko, wanyamwezi, wazaramo wangekuwa na hali gani leo bila muungano? Je ni nani anadhibiti hasira na kisasi cha watu waliopoteza nchi baada ya mapinduzi? Je zenji wamekomaa kiasi cha kuweza kudhibiti kilichomtokea Founder kisitokeee tena wakiachwa? Ukiyatafakari haya utaona kuwa ni muhimu kwa wamakunduchi kuung'ang'ania mfumo uliopo.

Kwa upande wa Bara, Zenji ikiondoka hali ya uchumi itakuwaje? athari ya kwanza ni Bandari za Bara kuporomoka kwani Zenji itakuwa huru kuwa eneo la magendo jambo ambalo litafanya bandari zake kuwa na mvuto kwa meli za kigeni. Kumbukeni hali ilivyokuwa wakati wa Komando, Kisiwa kilikomaa kwa rushwa, kutokusanya kodi na Magendo hali iliyofanya mizigo yote muhimu ikiwemo magari vishushwe zenji. Zenji ilikuwa Dubai ndogo watu walikuwa wanaenda kufunga mzigo Zenji. Aidha upo uwezekano wa Zenji kuwa changamoto ya kudumu ya kiusalama kwa Bara hasa wapembee wakichukua nchi. Tunaweza tukawa sawa na ilivyo kwa Rwanda na DRC baada ya Kagame kuchukua nchi. Au kama South Sudan na Sudan baada ya kutengana.

Kuhusu Takwimu za nzito, Zenji inachukua Bara haichangiii
 
Mi nadhani wewe na mimi tunakubaliana kwa kiasi kikubwa. Sioni sababu ya kutafuta visababu vinavyotutenganisha hapa.
Tuko sawa. Tatizo ni watu wa upande mmoja kuwa na mawazo ya kwamba wanawza kutawala upande mwingine kwa sababu yoyote iwayo. Hili halikubaliki na haikuwa azma ya muungano huu tokea awali.
 
Nafahamu pia kwamba, muungano ulivyo sasa, siyo ule uliokuwepo mwanzo. Maswala ya "kero nyingi za muungano" toka upande mmoja wa muungano ndizo zilizosababisha kwa kiasi kikubwa tukafikia hapa tulipo leo; kinyume kabisa na matarajio ya muungano walioutegemea waasisi; kwamba baada ya muda, tukisha zoeana vya kutosha na kuchanganyika kati yetu, hofu zilizokuwepo wakati ule zingekuwa zimepungua na kuruhusu muungano wa karibu zaidi. Badala yake, kero zilipo pamba moto, badala ya kuwa karibu, ndiyo tukawa tunatafuta njia ya kuua muungano
Ni kweli muungano wa sasa sio ule wa awali, na ndio maana ni dhambi hata kuiona ile contract ya muungano. Huu umekuwa ni muungano wa viongozi wa juu. Kujadili muungano imekuwa ni taboo. Kila kiongozi alioujadili muungano alionekana ni msaliti. Mawazo haya ndio dhambi iliyouua muungano.
Ni wakati mzuri sasa, huu muungano upekwe kwa wananchi, waamue wenyewe wanachotaka juu ya huu muungano.
Hili ni muhimu sana. Tusiwaburuze wananchi, tukadhani ni wajinga. Hawa ndio watatuhukumu kesho kama wao hawafaidiki. Na hapa ni muhimu kuelewa kuwa kura ya maoni lazima iwe 1+1, nikimaanisha Tanganyika (59 milioni-wakazi) wafanye wenyewe kura ya maoni yao na Zanzibar (1.88 milioni) wafanye yao peke yao. Kama kuna nchi moja itasema hapana, jibu litakuwa hapana kwa muungano mzima.
Sasa hata hapa naona kuna shida, siyo hasa kwa upande wa Tanganyika; bali kwa upande wa Zanzibar. Pamoja na wingi wao ulivyo Tanganyika, hata wakiukataa muungano, kama lile kundi la CCM litapata waZanzibari wa kutosha kubaki kwenye muungano, Tanganyika hawezi kujitoa. Bila shaka hii ndiyo 'veto' uliyokuwa ukiizungumzia.

Hata ikitokea ikawa hivyo, maoni yangu ni kwamba kura hiyo ya maoni itatupatia fursa ya kuutazama upya muundo wa muungano wetu
Shida hakuna. Cha msingi tuamini maoni ya wananchi.
Kama ulivyosema, inawezekana wakahitaji kuutazama upya muundo wa muungano au kuuvunja. Mimininaimani kwa hapa tulipofika wengi watahitaji muundo mpya wa muungano wenye haki sawa kwa wote na uliozingatia kila upande kufaidika na muungano.

My take: Lissu huwa ana point juu ya kero za muungano. Nisichokipenda kwake ni jinsi anavyoeleza kwa hisia za kiharakati na kutumbukia katika dimbwi la kubaguana na kuwa mbaguzi namba 1.
 
Na ukishayaelewa na kulewa hayo maneno ya Lissu, kinachofuata ni vita vya vyenyewe kwa wenyewe. Huko ndio Lissu anakotupeleka.

Sikia nikwambia, idiolojia za Lissu hazina afya kabisa katika nchi yeyote ile ya Afrika. Jirani yako ndio mtu utayefanya naye biashara kwa ustawi wa Afrika na nchi moja moja. Huwezi kujua Ethiopia waliingiaje kwenye vita za wenyewe kwa wenyewe. Ni kama hizi siasa za Lissu ndio mbolea nzuri sana ya kukupeleka katika nchi ya ahadi ya Lissu.

Baada ya maelezo yake, tuchukulie kesho mmetengana, na yeye ndio Rais, hivi atakwendaje kwa jirani kuomba ujirani mwema?
Hizi sasa ndio blaa blaa za kijinga zinazotumika kuwahadaa watanzania miaka nenda rudi ili wasia -dress mambo ya muhimu na kero mbali mbali za kiuongozi...
 
Tuko sawa. Tatizo ni watu wa upande mmoja kuwa na mawazo ya kwamba wanawza kutawala upande mwingine kwa sababu yoyote iwayo. Hili halikubaliki na haikuwa azma ya muungano huu tokea awali.
Kupishana kwetu kunaweza kuwa ni hapo; pa "...upande mmoja kuwa na mawazo ya kwamba wanaweza kutawala upande mwingine..."
Pamoja na ubovu wao mwingi uliomo CCM, upande wa Tanganyika, sioni hata mmoja kati yao mwenye uwezo wa kuwatawala Zanzibar,( kama maana yako ya upande mmoja) unawalenga waTanganyika.
Raia wa Tanganyika, wa kawaida huko vijijini na hata mjini, hakuna mwenye fikra za kumtawala mtu mwingine yeyote.
Hawa ndio wanaoupenda muungano bila ya hisia za kufanyiziana ujanjaujanja wowote. Hawategemei kufaidika kwa vyovyote kutokana na kuwanyanyasa wenzao wa upande wa pili, tofauti kabisa na hawa viongozi wa CCM wa pande zote mbili, wanaotumia muungano kwa faida zao.; CCM wa Zanzibar kuhakikisha wanabaki madarakani kwa kisingizio cha kulinda Mapinduzi Matukufu, na hawa CCM wa Tanganyika wakilinda maslahi ya wao pia kubaki madarakani; kwani wanajuwa, CCM Zanzibar ikitetereka, hata wao wataanza kutetereka huku bara.

Mwisho, nikuombe msaada, kama unaweza kutoa mfano halisi wa "...wanaweza kutawala upande mwingine..."; ni kipi hasa kilichofanywa na upande huo ambacho kinaitofautisha bayana na "...haikuwa azma ya muungano huu tokea awali."
Ukiweza kubainisha hili, pengine nitaanza kuelewa vizuri matatizo yetu ya muungano.

Binafsi, ninachoona, na ambacho ni tofauti kabisa na "...azma ya muungano wa mwanzo" ni hizi KERO mpya nyingi zilizoibuka kila mara toka upande mmoja. Hizi kero, kila ziliposhughulikiwa, ziliturudisha nyuma katika muungano wetu badala ya kutuimarisha ndani ya muungano huo.
Tofauti yetu mimi na wewe kimsingi ipo hapo.
 
Shida hakuna. Cha msingi tuamini maoni ya wananchi.
Kama ulivyosema, inawezekana wakahitaji kuutazama upya muundo wa muungano au kuuvunja. Mimininaimani kwa hapa tulipofika wengi watahitaji muundo mpya wa muungano wenye haki sawa kwa wote na uliozingatia kila upande kufaidika na muungano.
Mkuu 'Zawadi' tumejadili vya kutosha. Tumekubalina tulipo kubaliana; lakini la msingi kabisa naona ni hii dhana ya 50:50; bila kujali sifa zingine zote zinazotofautisha pande mbili.
Kwa maoni yako, nadhani; kwa mfano: Kama ni mgao wa mapato ya serikali; kila upande upate 50%! Kama ni utumishi katika serikali, kila upande upate nafasi 50%?, Jeshini, 50:50, n.k. Hili litawezekana vipi!

Hili la WaZanzibari wakikataa muungano, waTanganyika wakiukubali, Muungano uvunjike, kama unavyosema wewe! Una maana Tanganyika hawezi kuwa na sauti juu ya jambo lolote mZanzibari akilikataa? Huu utakuwa ni muungano, au kitu gani?

Muungano ni muhimu tufike mahali, sote tuseme hatuutaki, au tunautaka; na kama sote tunasema tunautaka tukae chini tujadili ni muungano wa aina gani. huu uliopo sasa siyo muungano tena. Na kwa mjibu wa unayosema wewe, huo wa pili wanaoutaka waZanzibari, ukiimarisha zaidi utaifa wao, kuliko uTanzania; hilo nalo halitufai.
Tuvunje hiki kiini macho tunachokiita Muungano.

Mimi sioni UBAGUZI wowote anaoueleza Tundu Lissu. Nashangaa sana wewe kumsema kwa ubaguzi wake, upi?
 
Mkuu 'Zawadi' tumejadili vya kutosha. Tumekubalina tulipo kubaliana; lakini la msingi kabisa naona ni hii dhana ya 50:50; bila kujali sifa zingine zote zinazotofautisha pande mbili.
Kwa maoni yako, nadhani; kwa mfano: Kama ni mgao wa mapato ya serikali; kila upande upate 50%! Kama ni utumishi katika serikali, kila upande upate nafasi 50%?, Jeshini, 50:50, n.k. Hili litawezekana vipi!
Hapa hukunielewa, nitafafanua. 50:50 ni katika vyombo vya maamuzi. Wale wanaoamua kukubalika au kutounga mkono hoja ndio wanatakiwa kuwa 50:50.
Hii inamaanisha kwamba kama kwa hoja zilizopo mezani, kwa mfano juu ya mapato- inaweza ikawa 75%-Bara na 25%Zzibar, au 97% bara na 3% Zzibar- maamuzi haya ili yapite yanahitaji kura 50:50. Hali kadhalika kwenye jeshi, utumishi maamuzi yanahitaji kura 50:50.
Kumbuka, muungano ni swala la hiari na si lazima. Ukilazimisha ndio matitizo yake ni kero tupu. Ifahamike kwamba ni nchi nyingi zina wakazi chini ya milioni 1 kama Qatar na haihitaji kuungana na nchi yoyote ile na maisha yanaendelea tena safi kabisa.
Chukulia Umoja wa ulaya- Uingereza ilipiga kura za maoni kujitoa na wala haikuhitaji kura nchi nyingine za Umoja huo. Ilipopata kura zaidi ya 50% wakajitoa. Hii ndio faida ya 50:50.
Hili la WaZanzibari wakikataa muungano, waTanganyika wakiukubali, Muungano uvunjike, kama unavyosema wewe! Una maana Tanganyika hawezi kuwa na sauti juu ya jambo lolote mZanzibari akilikataa? Huu utakuwa ni muungano, au kitu gani?
Hapana, hapa napo hukunielewa. Nilitolea mfano tu.
Katika 50:50 ipo hivi- Ili maamuzi ya jambo fulani yapite inahitaji pande zote mbili ziseme "ndio". Pande moja yeyote ile Tanganyika au Zzibar ikasema hapana, suala hilo halipiti. Vile vile kama pande zote zimesema Hapana jambo hilo halipiti. Hii ndio faida ya 50:50. Faida ya mtindo huu ni kuhakikisha wananchi wa kila upande wanakubaliana kufaidika na maamuzi yanayofanywa. Ikumbukwe, muungano ni wa nchi mbili na sio mikoa miwili.
Mwisho: Muungano wa nchi mbili si kitu rahisi- rahisi kama tunavyokichukulia, ni suala linalohitaji mazungumzo ya muda mrefu hata kama litakwenda polepole.
 
View attachment 2977398
Tazama na sikiliza kwa makini mwanzo mwisho video clip hii fupi ya dakika 16 Tundu Lissu akijibu hoja ya ubaguzi na matundu ya muungano wa Tanganyika & Zanzibar (1964) kwa kutumia katiba mbili za JMT (1977) na ile ya Zanzibar (1984) akihutubia maelfu ya wananchi Dodoma jana tarehe 29/4/2024.

Hakika utafunguliwa ufahamu wako na kila mtu atajua mjinga na mwerevu ni nani. Pengine ndiye mtawajua wabuguzi halisi ni kina nani...

Hii ni muhimu sana Nape Nauye na chama chake (CCM) wajitokeze kujibu hoja hizi na kuukanusha ukweli huu wa kikatiba kama unakanushika.

Mimi hata sijui mtu mwenye uelewa na ufahamu kama Tundu Lissu unaweza kumkamatia wapi ili umshitaki afungwe jela. Ni ngumu na pengine haiwezekani tu kabisa maana ni hakika kuwa: KNOWLEDGE IS POWER..!

Kila mtu anajua na kuelewa kuwa Samia Suluhu Hassan ni Mzanzibari. Yupo hapo kwa katiba hii ya 1977. HilI sina hakika kama lina ubishi wowote na kwwamba yupo mtu anaweza kulikanusha hili..

Na hivi inawezekana vipi kuwa kila ukweli unaojifunua kupitia kwa watu kama Tundu Lissu aliyejitoa kupigana kwa damu yake mwenyewe kwa ajili ya manufaa ya watu masikini wengi iwe ni ubaguzi na uchochezi? Really?

Mimi nadhani ifike wakati kila mtu wakiwemo watawala kupitia CCM waelewe kuwa nyakati za kuishi katika giza la ujinga wa kudanganywa na watawala umefika mwisho. Tunachosubiri kwa sasa ni justification tu kupitia "unyakuo"

Inashangaza kuwa kina Nape Nauye na CCM yake wanataka tuendelee kuishi ktk giza la ujinga na udanganyifu wa miaka 60..

Hapana. HII HAIWEZEKANI TENA... Watu wanataka kuishi katika Nuru ya haki na usawa...

Hebu nyie kina Dr Akili, ChoiceVariable, Tlaatlaah, Samiaagain2025 MamaSamia2025, Paul Makonda, @Nnape Nauye njooni mkanushe ukweli huu kwa hoja zenye ushahidi halafu mrudi tena kusema mbaguzi hapa ni nani. Pia mseme kama Rais Samia Suluhu Hassan sio mzanzibari, basi ni wa taifa lipi?

Na kuna ugumu gani wote kukiri kuwa kuna tatizo katika muungano huu wa 1964 kati ya Tanganyika na Zanzibar?

Kazi ya Tundu Lissu ni kuonesha matatizo lakini nyie mnamwita mbaguzi..!!

Looh!!, mna shida kwelikweli nyie

Pia soma: Tundu Lissu: Tuna Rais Mzanzibari anayeweza kwenda Ngorongoro na kutoa Amri kwa Wanajeshi wafukuze wamasai wote

View attachment 2978056
Ukishataja mtu anakotoka tayari ni ubaguzi
 
Hapa hukunielewa, nitafafanua. 50:50 ni katika vyombo vya maamuzi. Wale wanaoamua kukubalika au kutounga mkono hoja ndio wanatakiwa kuwa 50:50.
Hii inamaanisha kwamba kama kwa hoja zilizopo mezani, kwa mfano juu ya mapato- inaweza ikawa 75%-Bara na 25%Zzibar, au 97% bara na 3% Zzibar- maamuzi haya ili yapite yanahitaji kura 50:50. Hali kadhalika kwenye jeshi, utumishi maamuzi yanahitaji kura 50:50.
Kumbuka, muungano ni swala la hiari na si lazima. Ukilazimisha ndio matitizo yake ni kero tupu. Ifahamike kwamba ni nchi nyingi zina wakazi chini ya milioni 1 kama Qatar na haihitaji kuungana na nchi yoyote ile na maisha yanaendelea tena safi kabisa.
Chukulia Umoja wa ulaya- Uingereza ilipiga kura za maoni kujitoa na wala haikuhitaji kura nchi nyingine za Umoja huo. Ilipopata kura zaidi ya 50% wakajitoa. Hii ndio faida ya 50:50.

Hapana, hapa napo hukunielewa. Nilitolea mfano tu.
Katika 50:50 ipo hivi- Ili maamuzi ya jambo fulani yapite inahitaji pande zote mbili ziseme "ndio". Pande moja yeyote ile Tanganyika au Zzibar ikasema hapana, suala hilo halipiti. Vile vile kama pande zote zimesema Hapana jambo hilo halipiti. Hii ndio faida ya 50:50. Faida ya mtindo huu ni kuhakikisha wananchi wa kila upande wanakubaliana kufaidika na maamuzi yanayofanywa. Ikumbukwe, muungano ni wa nchi mbili na sio mikoa miwili.
Mwisho: Muungano wa nchi mbili si kitu rahisi- rahisi kama tunavyokichukulia, ni suala linalohitaji mazungumzo ya muda mrefu hata kama litakwenda polepole.
Nikushukuru hapa. Niseme kwamba unaelewa unachokizungumzia.

Muungano wetu ulipoanzishwa ulikuwa ni muungano wa mahitaji kwa wakati ule. Zanzibar walitaka kinga ya Tanganyika kulinda "Mapindzi" yao; na Tanganyika kwa wakati huo mahitaji ya viongozi wao ulikuwa ni msukumo wa kuwa na umoja;nchi za Africa kuungana.
Kumbuka, Tanganyika tulikuwa tayari kuahirisha uhuru wetu tuwasubiri Uganda na Kenya ili tuwe na Muungano. Kwa bahati mbaya wenzetu hawakuwa tayari. Na ni wakati huo huo ambapo Jumuia yetu ya Afrika Mashariki ilianza kutetereka. Kwa hiyo, Tanganyika kuungana na Zanzibar lilikuwa hitaji na tukio la kujivunia kwa wakati huo. Bila shaka ni kutokana na hali hiyo, ikaonekana maswala ya kuungana hayakuhitaji kuchukuwa muda mwingi kwa kulipeleka swala hilo kwa wananchi wakaamue.
Mimi sioni sababu sasa hivi ya kushindwa kuwashirikisha wananchi katika uamzi wa Muungano kuendelea au ukome.
Nakubaliana nawe katika 50:50. Zanzibar asili mia 50+1 wakisema Muungano hawautaki, itabidi mchakato ufanyike kwenye Bunge la Muungano kuruhusu jambo hilo. Hali kadhalika, hali itakuwa hivyo kwa Tanganyika.
Sasa nisichojua ni uhusika wa Bunge la Muungano katika hatua hiyo. Zanzibar wao kwa kuwa wana serikali yao na wawakilishi; bila shaka watakuwa na wakati mzuri wa kuamua hilo.Tanganyika haina serikali, wala Bunge, sasa sijui wao mchakato wao utakwenda vipi.

Umetoa mfano wa Britain kujitoa kwenye umoja wa Ulaya. Sijui kama mfano huo ni sahihi sana kwa hali yetu. Mfano mzuri ungekuwa ni kwa mfano Scotland wakitaka kujitoa kwenye Muungano wao na England, Wales na Ireland. Mchakato huu ungekuwa karibu zaidi na huu wetu.
 
Umetoa mfano wa Britain kujitoa kwenye umoja wa Ulaya. Sijui kama mfano huo ni sahihi sana kwa hali yetu. Mfano mzuri ungekuwa ni kwa mfano Scotland wakitaka kujitoa kwenye Muungano wao na England, Wales na Ireland. Mchakato huu ungekuwa karibu zaidi na huu wetu
Mazingira ni hayo hayo. Ona kura za maoni za Scotland kujitoa uingereza 2014.
"Results by council area of the 2014 Scottish independence referendum. The referendum on Scottish independence held on 18 September 2014 saw Scotland vote to remain part of the United Kingdom (UK), with 55% voting against the proposal for Scotland to become an independent country and 45% voting in favour"

Ukiangalia hapa si UK wote wliohusika katika kura ya maoni, bali ni waskottish tu na matokeo yake yalikuwa:
55%- wlitaka muungano uendelee.
45%- Walitaka wawe huru (muungano uvunjike)
Na ndio maana wakabaki na muungano. Majibu yangekuwa kinyume, muungano ungevunjika. Narudia, suala la muungano ni hiari na si kulazimisha.
 
Ukiangalia hapa si UK wote wliohusika katika kura ya maoni, bali ni waskottish tu na matokeo yake yalikuwa:
55%- wlitaka muungano uendelee.
Sawa kabisa.

Kwa maana hiyo hiyo, hapa kwetu, Zanzibar waweza kuweka 'referendum' yao ya kujitoa kwenye muungano. Kura Asili mia 50 +1 zikikataa muungano; basi inakuwa halali kwa Zanzibar kujiondoa katika muungano.
Lakini hapo hapo, tunajua kwa Tanganyika haiwezi kufanya hivyo; kuweka 'referendum', kwa sababu hakuna kitu kama hicho katika muundo wetu. Sasa hili utalizungumziaje? Huo mfano wa Scotland, kumbe hata kwetu haukubaliani.

Hata hivyo, kwa maoni yangu, ningetamani waZanzibari wapewe fursa hiyo ya kupiga kura waamue wanachokitaka wenyewe bila kujali wananchi wa muungano wa upande wa pili wanasemaje. WaZanzibar wakiamua kubaki ndani ya muungano, kwa masharti yaliyopo sasa au yatakayokubaliwa baadae, basi hizi kelele za wanaotaka kutoka zisisumbue watu mara kwa mara na marekebisho ya mara kwa mara mambo ya upande mmoja bila kujali upande wa pili.
Na ndio maana wakabaki na muungano. Majibu yangekuwa kinyume, muungano ungevunjika. Narudia, suala la muungano ni hiari na si kulazimisha.
Katika hili la" kulazimishana" ni muhimu kulifafanua. Ni nani hasa katika muungano wetu anayemlazimisha mwingine abaki?
Ukiniambia ni Tanganyika, hapo nitakataa. Ukisema ni Tanzania, ambayo Zanzibar nayo imo hapo tutakubaliana.
Sasa sielewi katika Tanzania ni nani hasa analazimisha Zanzibar ibaki; na kwa upande wa pili, kwa vile Tanganyika haipo hatuwezi kuihusisha na huko kulazimisha.
Mimi nitasema hivi: anayelazimisha muungano, wala hata siyo aliyebatizwa jina la Tanzania Bara. Tanzania Bara ni jina tu, haina serikali wala haina Bunge.
Hili jambo la kuwalaumu Tanzania Bara kulazimisha muungano siyo sahihi hata kidogo. Wanaolazimisha muungano ni hao Tanzania (CCM) ikiwa na serikali pande zote za muungano.
Muungano unainufaisha CCM; kwa kuwapa nafasi ya kuwa madarakani milele.
Sasa basi, ukitaka kupata ufumbuzi sahihi, ni lazima uanze huko huko CCM. CCM wa Zanzibar wakisema hawataki muungano, sina shaka yoyote kuwa itakuwa rahisi kwa Zanzibar kujitoa kwenye muungano.

Kwa hiyo nimalize kwa kusema: kumbe hata mfano wa Scotland na UK hauendani na hali tuliyo nayo sisi. Miundo yao na yetu ni tofauti kabisa.
 
Ahojiwe kwa kupotosha umma wa Watanzania na kusambaza chuki kwa wananchi dhidi ya viongozi wao wa nchi
 
Back
Top Bottom