tukio hili kwa kweli linasikitisha sana na la kikatili mno.
Embu itazame tena hiyo video mwishomwisho,muangalie vizuri godbless lema,uzito wa jambo na alivyo.kuna kitu utagundua
kama wewe ndo tabia yako kutafuta wanaume humu jf nakupa pole sana. humu watu wapo kikazi zaidi. uzalendo ndo unaotutuma
Bila kusahahau nani aliyempandikizia sumu mwalimu nyerereMungu wangu, hii yoote kuwatisha watu wasiende kwenye mikutano ya wapinzani, ikiwezekana CCM iendelee kuwa madarakani, kwani wakiondolewa, siri zoote zitakuwa wazi kwa mfano:-
1. Kifo cha Sokoine hakitakuwa fumbo tena.
2. Kifo cha Holace kolimba wahusika watafahamika na wananchi watajua ni nani aliyewatuma wafanye mauaji yale.
3. Kifo cha Imrani Kombe kitaangaliwa upya, na kutakuwa na fursa ya kohoji kwanini wauaji waliachiwa huru na kwa maslahi ya nani
4. Ufisadi wa melemeta utahojiwa, kupata ukweli kama kweli ulikuwa ni mradi wa Usalama wa Taifa na kama kweli Usalama wa Taifa wanafanya biashara.
5. Kutakuwa na fursa ya kuwabana wale wezi wa Pesa za EPA ambao walisamehewa na Kikwete na kuwaomba warudishe ilihali, kuna watu wamebainika kuiba Baiskeli wanaozea jera.
6. Kutakuwa na fursa ya kujua kama kweli Pesa ya EPA imerudishwa yoote au ilikuwa ni funika Kombe Chadema ipite.
7. Kutakuwa na fursa za kuhoji uhusika wa Kikwete katika ishu ya Richmond, japo Lowassa alitaka kutudokeza lakini alisita.
.
.
.
.
.
.
.
.
6548. Kutakuwa na fursa ya kujua kuna siri gani ya kuendelea na watu kama akina Kamuhanda japo ametajwa katika mauaji ya Songea na Iringa?
6549. Itafahamika kama Balali alifariki kweli au yupo hai, na kama yupo hai kwanini afichwe?
Lakini katika mkusanyiko kama huo watoto wako kwenye risk ya kupoteza uhai wao.
Children are vulnerable na wakati wa vurumai kama hiyo hakuna atakayemjali mtoto.
Wataishia kukanyagwa kanyagwa tuu.
damu mumwage nyie halafu lawama tupate sisi! punde si punde mtaumbuka na ni lazima muipate fresh mwaka huu. haiwezekani chama kinalea magaidi, mnapoteza maisha ya watu na wengine wanabaki vilema halafu tuwachekelee tu. tutapambana humu jf na polisi watapambana nanyi huko nje
wacheni upuuzi hizi ni siasa tu, mimi naamini kabisa kuwa hata hao chadema wenyewe inaweza kuwa ndio walorusha bomu hilo kwa kumtumilia polisi (kama ni kweli) wanaweza kuwa wamevaa uniform za polisi, au munadhani hao polisi hakuna wafuasi wa chadema????? Na kwa nini bomu hilo lirepuliwe karibu na hicho kiriri cha kutoa hutuba tena pale alipopanda muheshimiwa aliyetaka kuhutubia watu wa arusha????
Kama lengo ilikuwa ni huyo muheshimiwa basi huyo muheshimiwa angelipigwa risasi 1 tu ya kichwa bila ya hata kujulikana aliyefanya tukio, ila hili bomu nina imani kabisa kuwa mfanyaji na wapangaji wa hili tukio na shambulizi ni wenyewe chadema, msidanganywe na hizi siasa na hawa wanasiasa, kwani walofanya september eleven attack marekani ni osama kweli???? Amkeni nyinyi wachaga
tanzania sasa imekalia time bomb niliwaambia zamani haya maneno tokea 2010 tusubiri hiyo 2015 time bomb iripuke pasikalike tena hapa ndio lilobakia, hivi unadhani chadema watakubali kushindwa 2015? Hivi unadhania ccm watakubali kushindwa 2015 basi ujue tanzania ipo katika time bomb, ndio maana huku zanzibar tunataka kujitoa na mapemaaaaa katika muungano na hii time bomb yenu munayotegeshewa muirepuwe wenyewe.....mwenye remote hayupo hasaaaa.
Dah! jamani! nimeangalia na kutokwa machozi.
Yaani nikiangalia yule mtoto mdogo alivyokuwa anajithaidi kunyanyuka, nimetokwa machozi sana
Sina la kusema, mwenyezi wapunzishe kwa amani! dah