viongozi wa dini wako wapi? mbona hakuna anayetoa tamko la kulaani haya? mimi siyo nabii wala mtume ila ni maombi yangu iwe hivi:- Mungu aliyesema kila atakayemwaga damu ya mwenzie na yake itamwagwa, auwaye kwa upanga naye atakufa kwa upanga. aliyehusika na haya kama ni serikali au ni maagizo ya viongozi wa serikali kila aliyehusika haki haitamuacha kuishi!!! tutashuhudia vifo vya wahusika iwe ni kwa ajaliau shinikizo la damu au vifo vya ghafla ili mradi kila aliyehusika katika hili haki haitamuacha kuishi! na alaaniwe kila aliyehusika kwenye tukio hili kuanzia aliyeagiza mapaka waliotekeleza unyama huu! wasomaji wa bible mnamkumbuka mfalme ahabu, aliwahi kuagiza kwa mkono wa mkewe yezebeli kumuua naboth myezreeli kwa sababu ya shamba tu. lakini mungu alimtuma nabii wake eliya kutoa laana kwenye nyumba ya mfalme na alisema hivi,"mahali pale mbwa walipoilamba damu ya naboth,mbwa watailamba na damu yako naam damu yako............2wafalme 21:1-24. na mimi ninasema tena kila aliyehusika na tukio hili kuanzia aliyeagiza mpaka aliyetekeleza lazima atakufa kifo kibaya kama alivyowaua wenzake na kila anayependa haki na aseme AMINA!