Jabali la Siasa
JF-Expert Member
- Jul 10, 2020
- 2,551
- 2,184
Hivi wanazengo wenzangu mnafahamu ni kwanini Rais wetu Mhe Samia Suluhu Hassan aliamua kupanda ndege ya Emirates na kuacha ndege 11 mpya zimepaki?
" Hakuna kama Samia "
Kutoka Dar es salaam kwenda New York Marekani ni Jumla ya Km 12,050 sawa na jumla ya Km 24,100 two ways,ikiwa ni sawa na safari ya masaa 21 na dk 31 Mchana na Usiku nanisawa na masaa 43 kwenda na kurudi,
Boing 787-8 engine inatumia lita 5,400 za mafuta kwa lisaa limoja yaani ( 5,400L/h )
Fanya hivi, chukua lita 5,400 za mafuta zidisha kwa masaa 21.31 utapata jumla ya Lita 115,074 za mafuta ili kufika New York Marekani yaani ( one way)
Tunafahamu,bei ya Lita moja ya mafuta ya ndege (Jet fuel) hapa Tanzania kama trh 24|09|2021 ni $0.501/lita sawa na Tshs 1,162
Ilikupata gharama ya mafuta Dar es salaam to New York ,Chukua lita hizi 115,074 zidisha kwa bei ya lita moja ambayo ni Tsh 1,162 utapata jumla ya Tshs 133,653,240 kwa Safari moja tu ( One way)
Ilikupata gharama ya safari zote mbili yaani kwenda New York na kurudi,Zidisha gharama ya mafuta ya kwenda Tshs 133,653,240 X 2 ilikupata gharama halisi ya mafuta ya Dar es Salaam to New York two ways ,Utapata Jumla ya Tsh267,306,480 hii ni pesa ya mafuta tu yakwenda New York na kurudi Dar es salaam,
Hapa hatujazungumzia rate ya landing fees, Parking fees nanyinginezo watu wa aviation wanafahamu hizi gharama vizuri, kwakuwa Mimi si mtaalum wa mambo Aviation naomba niishie hapa kwenye mathematical calculation ya gharama ya mafuta tu ambayo ni karibu 270M,
Sasa mnaolalamika Rais katumia gharama kubwa sikieni hii,Emirates gharama ya Mtu mmoja kwenda New York na kurudi Dar es salaam kwa Economy Class ni Tsh 2,854,500 kama utakaa huko chini ya Siku 7 ,
Sasa kwa kadirio la juu kabisa tufanye mama ameenda na watu|deligates 50 japo naamini ameenda na chini ya hawa,
Chukua 2,854,500 7X 50 Utapata jumla ya Tshs 142,725,000 ,
Chukua gharama ya mafuta ya Boing 787-8 ya kwenda New York na kurudi Dar es salaam ambayo ni Tshs 267,306,240 toa 142,725.000 ambayo ni nauli ya watu 50 utapata Salio la Tshs 124,581,240,
( watu 50 ni makadirio ya juu kabisa sio idadi kamili mwenye idadi kamili anaweza kutupa )
Rais Samia anajua umasikini wa watu wake, anajua hakuna madawa, anajua barabara mbovu, anajua watu wanamaisha magumu ndio maana anasafiri na Emirates pamoja na kwamba Tanzania tunazo ndege mpya 11,
Mnaotaka rais aende na dreamliner New York rudieni kusoma uchambuzi huu, Mnaosema rais anatumia gharama kubwa kwenda New York angalieni hii nia ya Rais katika kukwepa gharama zisizo za lazima,
NB, Kitendo cha Rais Samia kwenda na usafiri wa umma amepunguza gharama ya Safari kwa 50% na kwahaki nchi ilimsubiri kiongozi wa aina hii kwa muda mrefu,
"RAIS MZALENDO SAMIA SULUHU HASSAN AKISHUKA KWENYE USAFIRI WA UMMA"