Mafuta ya Dizeli, Petroli yashuka Bei Dar, Tanga, Arusha na Kilimanjaro

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,118
1688498031742.png

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), inatangaza bei kikomo za bidhaa za mafuta ya petroli hapa nchini. Bei hizi zitaanza kutumika kuanzia Jumatano, tarehe 5 Julai 2023 saa 6:01 usiku. Pamoja na kutambua bei hizo, ni muhimu kuzingatia yafuatayo:

(a) Bei za rejareja za mafuta ya petroli na dizeli yaliyopokelewa kupitia Bandari ya Dar es Salaam zimeshuka kwa shilingi 137/Lita na shilingi 118/lita, mtawalia, ikilinganishwa na bei za toleo la tarehe 7 Juni 2023. Pia, bei ya
rejareja ya mafuta ya taa kwa Julai 2023 itaendelea kuwa ni ile iliyotangazwa katika toleo la tarehe 7 Juni 2023 kwa kuwa hakuna shehena iliyopokelewa mwezi Juni 2023.
1688498071619.png
(b) Kwa Mikoa ya Kaskazini (Tanga, Kilimanjaro, Arusha na Manyara), bei ya rejareja ya mafuta ya petroli imeshuka kwa Shilingi 188/Lita wakati bei ya mafuta ya dizeli imeongezeka kwa shilingi 58/lita ikilinganishwa na bei za toleo la tarehe 7 Juni 2023.

(c) Kwa Mikoa ya Kusini (Lindi, Mtwara, na Ruvuma), hakuna shehena ya bidhaa za mafuta iliyopokelewa kupitia Bandari ya Mtwara kwa Juni 2023. Hivyo basi, bei ya rejareja ya dizeli kwa mwezi Julai 2023 itaendelea kuwa ni ile iliyotangazwa katika toleo la tarehe 7 Juni 2023.

Kutokana na upungufu wa bidhaa ya petroli katika maghala ya kuhifadhi mafuta yaliyopo Mtwara, waendeshaji wa vituo vya mafuta katika mikoa ya Kusini wanashauriwa kuchukua mafuta hayo kutoka katika bandari ya Dar es Salaam. Hivyo basi, bei za rejareja za mafuta ya petroli katika mikoa hiyo zitazingatia bei kikomo ya rejareja ya Dar es Salaam na gharama za usafirishaji mpaka mikoa husika.

(d) Aidha, kwa kuwa hakuna mafuta ya taa katika maghala yaliyopo katika 2 Bandari za Tanga na Mtwara, waendeshaji wa vituo vya mafuta katika mikoa ya Kaskazini na Kusini wanashauriwa kuchukua mafuta hayo kutoka katika Bandari ya Dar es Salaam na hivyo bei za rejareja za mafuta ya taa katika mikoa hiyo zitazingatia bei kikomo ya rejareja ya Dar es Salaam na gharama za usafirishaji mpaka mikoa husika.
1688498106725.png
 

Attachments

  • BEI-KIKOMO-ZA-BIDHAA-ZA-MAFUTA-YA-PETROLI-KUANZIA-JUMATANO-TAREHE-5-JULAI-2023.pdf
    398.3 KB · Views: 2
Wale tunaoendaga "sheli" kujaza mafuta mambo ni nzuri.

Licha ya tozo Mpya ya Shilingi 100 Bado bei ya mafuta imeshuka..


My Take
Mwezi ujao bei zinaweza kupanda maana wale wehu Saidi Arabia na Russia wametangaza kupunguza uzalishaji Ili kupandishwa bei hamkawii kuja kusingizia tozo.
 
Hivi tozo za miala ya simu kwa mwaka wa fedha uliopita zikikusangwa shilingi ngapi na matumizi ya fedha hizo yapoje?

Lengo, nikujua kama Kuna haja Tena ya kugawa kitega Uchumi chetu muhimu kwa wawekezaji wenye mashaka(rejea Djibout vs. DP world).
Kwani zilikuwa na Mfuko wake maalumu?
 
Wale tunaoendaga "sheli" kujaza mafuta mambo ni nzuri.

Licha ya tozo Mpya ya Shilingi 100 Bado bei ya mafuta imeshuka..


My Take
Mwezi ujao bei zinaweza kupanda maana wale wehu Saidi Arabia na Russia wametangaza kupunguza uzalishaji Ili kupandishwa bei hamkawii kuja kusingizia tozo.

Sheria ya tozo haijaanza kutumika mpk mwezi wa 8, lazima itangazwe kwenye gazeti la serikali kwanza baada ya kusainiwa
 
Matumizi yake Yako dhahiri kabisa.Viongozi wetu Sasa wanatembelea VX ya 600M.Misafara imeongezeka.Endelea kulipa kodi
 
Kuna kahela flani nakasikilizia nakamalizia sheli. haya ya videbe yanaumiza kila ukiendesha km2 macho automatic yanarudi kwenye geji
 
Sirikali ya wavivu,

Waliposhindwa kudhibiti uchakachuaji wa mafuta, Bei ya mafuta ya taa, ilipandishwa juu kuliko mafuta yoyote.

Waliposhindwa kuzuia wizi bandarini, wanaigawa Bure Kwa waarabu.

Ukishindwa kuwajibika, unawajibishwa.

CCMM must go!!!
 
View attachment 2678722
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), inatangaza bei kikomo za bidhaa za mafuta ya petroli hapa nchini. Bei hizi zitaanza kutumika kuanzia Jumatano, tarehe 5 Julai 2023 saa 6:01 usiku. Pamoja na kutambua bei hizo, ni muhimu kuzingatia yafuatayo:

(a) Bei za rejareja za mafuta ya petroli na dizeli yaliyopokelewa kupitia Bandari ya Dar es Salaam zimeshuka kwa shilingi 137/Lita na shilingi 118/lita, mtawalia, ikilinganishwa na bei za toleo la tarehe 7 Juni 2023. Pia, bei ya
rejareja ya mafuta ya taa kwa Julai 2023 itaendelea kuwa ni ile iliyotangazwa katika toleo la tarehe 7 Juni 2023 kwa kuwa hakuna shehena iliyopokelewa mwezi Juni 2023.
(b) Kwa Mikoa ya Kaskazini (Tanga, Kilimanjaro, Arusha na Manyara), bei ya rejareja ya mafuta ya petroli imeshuka kwa Shilingi 188/Lita wakati bei ya mafuta ya dizeli imeongezeka kwa shilingi 58/lita ikilinganishwa na bei za toleo la tarehe 7 Juni 2023.

(c) Kwa Mikoa ya Kusini (Lindi, Mtwara, na Ruvuma), hakuna shehena ya bidhaa za mafuta iliyopokelewa kupitia Bandari ya Mtwara kwa Juni 2023. Hivyo basi, bei ya rejareja ya dizeli kwa mwezi Julai 2023 itaendelea kuwa ni ile iliyotangazwa katika toleo la tarehe 7 Juni 2023.

Kutokana na upungufu wa bidhaa ya petroli katika maghala ya kuhifadhi mafuta yaliyopo Mtwara, waendeshaji wa vituo vya mafuta katika mikoa ya Kusini wanashauriwa kuchukua mafuta hayo kutoka katika bandari ya Dar es Salaam. Hivyo basi, bei za rejareja za mafuta ya petroli katika mikoa hiyo zitazingatia bei kikomo ya rejareja ya Dar es Salaam na gharama za usafirishaji mpaka mikoa husika.

(d) Aidha, kwa kuwa hakuna mafuta ya taa katika maghala yaliyopo katika 2 Bandari za Tanga na Mtwara, waendeshaji wa vituo vya mafuta katika mikoa ya Kaskazini na Kusini wanashauriwa kuchukua mafuta hayo kutoka katika Bandari ya Dar es Salaam na hivyo bei za rejareja za mafuta ya taa katika mikoa hiyo zitazingatia bei kikomo ya rejareja ya Dar es Salaam na gharama za usafirishaji mpaka mikoa husika.
Mwezi ujao wapandishe tena, Ewura matapeli tu
 
Back
Top Bottom