Nishati: Petroli yashuka kwa Tsh. 116, Dizeli Tsh. 148 Dar, Mafuta ya Taa yabaki palepale

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,118
1701802408788.jpeg

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), imetangaza bei kikomo za Mafuta ya Petroli zitakazotumika kuanzia Desemba 6, 2023 ambapo Dar es Salaam Petroli ni Tsh. 3,158, Tanga Tsh. 3,204 na Mtwara Tsh. 3,231 kwa Lita moja ya Mafuta.

Dizeli Dar es Salaam itauzwa kwa Tsh. 3,226, Tanga Tsh. 3,377 na Mtwara Tsh. 3,546. Mafuta ya Taa yamesalia kwenye bei za Novemba ambazo ni Tsh. Dar es Salaam 3,423, Tanga Tsh. 3469 na Mtwara Ths. 3,495 kwa Lita moja ya Mafuta.

EWURA imesema Bei za Mafuta (FOB) kwa mwezi Desemba zimepungua kwa wastani wa 0.86% kwa Petroli na 9.11% kwa Dizeli. Pia, gharama za uagizaji Mafuta kwa Bandari ya Dar zimepungua kwa 24% kwa Petroli, 30% kwa Dizeli. Tanga gharama za kuagiza Petroli zimeshuka kwa 30% na 17% kwa Dizeli.

==========

1701802455940.png

1701802478010.png
 
Hii si taarifa nzuri kwa wapiga dili waliopandisha nauli kwa ajili ya maslai yao Kama Zee la Fuko la Mifedha nchini lenye mibasi yenye jina la jinsia ya kike.
 
Kama ni hivyo mbona nauli tarehe 08.12.2023 inatangazwa rasmi kupanda kwa hali ya juu kuliko kipato cha mwananchi wa kawaida ambaye ndio anasafiri kila siku kutafuta mkate wa ka siku ???
 
EWURA,Mbona mnaishia hiyo mikoa minne tu? Tuambie mkoa Kagera mchanganuo ukoje?
Au wafanyabiashara wa mafura wajikadirie!
 
Back
Top Bottom