Utumishi Kupeleka Interview Dodoma ni kuwanyima watoto wa masikini nafasi ya kushiriki

Sensei Tai

Senior Member
May 26, 2022
126
359
Hili suala kiukweli linafikirisha sana

Hii inakua ni kama upendeleo kwa wakazi wa Dodoma pekee na kuwanyima nafasi ya kushiriki watoto wa masikini wanaotokea mikoa mingine

Juzi juzi niliona Waziri Jenister Muhagama akiongelea kwamba wameona ni bora kila mtu afanye usaili kwenye mkoa wake ili kupunguza gharama lakini hatuelewi huu mchakato umefikia wapi mana watoto wa masikini ndio tunaoumia kwa kukosa nauli za kwenda Dodoma pamoja na hela za accommodations.

Kuna haja serikali kuangalia kwa jicho la tatu hili suala mana wanaoumia ni watoto masikini, kushiriki usaili tunataka lakini tunakwamishwa na ukosefu wa nauli za kwenda na kurudi Dodoma.

Sijajua kama kupeleka saili Dodoma ni moja tu ya mbinu ya kupunguza watu au la, kama ni mbinu ya kupunguza watu basi hawatendi haki sababu written interview peke yake inatosha kabisa kupunguza watu kuliko hiki wanachokifanya cha kulazimisha saili zote zifanyikie Dodoma.

Serikali tunaomba muangalie upya hili suala la saili zote kufanyikia Dodoma mana dunia ipo Digital lakini sisi bado tunaendelea kukumbatia analog.

Tekelezeni kwa vitendo hili suala la kila muomba ajira kufanyia kwenye mkoa wake mana kwa kufanya hivyo mtakua mmempa kila muombaji haki ya kushiriki.

Asanteni
 
Mimi mwenyewe nilijiuliza nauli ya kwenda Arusha na kurudi elf 50 hapo hujala hujalala guest nafasi za ajira mbili mko 80 si nikaachana na biashara hiyo niliona ni hasara sana kwa mtu alie na wazazi masikini haswa wakulima, suala hili lingefanyiwa research namna ya kuwa na ukweli kwa msaili na msailiwa wakati wa kufanya usaili ikiwezekana mitihani ifanyikie wilayani au jimboni happy mtu anaweza kwenda kwa miguu, baskeli au kwa usafiri mwingine kwa gharama nafuu kulingana na ukijijini. Tuko vijijini sehemu ambazo mtu anakunywa soda sikukuu mpaka sikukuu.
 
Mimi mwenyewe nilijiuliza nauli ya kwenda Arusha na kurudi elf 50 hapo hujala hujalala guest nafasi za ajira mbili mko 80 si nikaachana na biashara hiyo niliona ni hasara sana kwa mtu alie na wazazi masikini haswa wakulima, suala hili lingefanyiwa research namna ya kuwa na ukweli kwa msaili na msailiwa wakati wa kufanya usaili ikiwezekana mitihani ifanyikie wilayani au jimboni happy mtu anaweza kwenda kwa miguu, baskeli au kwa usafiri mwingine kwa gharama nafuu kulingana na ukijijini. Tuko vijijini sehemu ambazo mtu anakunywa soda sikukuu mpaka sikukuu.
Bora ww umejiongeza.. maana watu mia 8 nafasi 1.. inamaana %risk ya kukosa ni 99.999999999 na 0.0000000001😂😂😂 hapo bado hujakandwa na Lile libaridi la Arusha.
Jobsekeers wote tufanye juu chini tuhamie tu Dodoma.
Utumishi ni Masela sana😂
 
Msije Jutia ombi lenu likikubaliwa muanze kulalamika watu ni wengi

Amini ya kwamba nafasi moja wanayoomba watu 500 Dodoma itafikia watu elf 10 kukiwa na usaili Kila mkoa.

Pia mitihani kuvuja itakuwa kawaida.

Sasa mpime mzani wenyewe hapo, mitihani iendelee kufanyiwa Dodoma mkiwa wachache ama Kila mkoa ufanye muwe utitiri
 
Sambamba na utekelezaji wa hili, nadhani wajitahidi na kuongeza na hizo nafasi zenyewe. Sipati picha usaili wa kumtafuta mtu mmoja wa kujaza nafasi ukifanywa mikoa yote Tanzania. Japo lengo ni kuleta usawa, ila inafikirisha sana.
 
Msije Julia ombi lenu likikubaliwa muanze kulalamika watu ni wengi

Amini ya kwamba nafasi moja wanayoomba watu 500 Dodoma itafikia watu elf 10 kukiwa na usaili Kila mkoa.

Pia mitihani kuvuja itakuwa kawaida.

Sasa mpime mzani wenyewe hapo, mitihani iendelee kufanyiwa Dodoma mkiwa wachache ama Kila mkoa ufanye muwe utitiri

Nakuunga mkono mkuu, na bado hongo pamoja na rushwa zitazidi kushika kasi.
 
Msije Jutia ombi lenu likikubaliwa muanze kulalamika watu ni wengi

Amini ya kwamba nafasi moja wanayoomba watu 500 Dodoma itafikia watu elf 10 kukiwa na usaili Kila mkoa.

Pia mitihani kuvuja itakuwa kawaida.

Sasa mpime mzani wenyewe hapo, mitihani iendelee kufanyiwa Dodoma mkiwa wachache ama Kila mkoa ufanye muwe utitiri
Umeongea kweli mzee bora t kwend huko dodoma
 
Kipindi interviews zinafanyika dar es salaam je? ..tumeshasahau moja wapo iljaza uwanja wa mpira...tatizo la ajira ni kubwa beyond location for interview.
 
Bora hukohuko Dodoma aiseeh kuliko huku mikoani mfano mzur ni mchakato wa sensa na anuani za makazi zilikuwa ni ajira za muda but mbilinge lake lilikiwa lakufa mtu
Cha msing kama uliomba ukaitwa na nauli unayo ni kutimba tu huko Dom na kama huna nauli basi syo riziki yako.Mi binafsi kama nimeitwa huko hata nafasi ni moja nikiwa na pesa ya nauli napambana niende na kama sina nakausha tu huku nikisaka nauli za saili zjazo.
 
Kuna MTU amewahi kufanya interview ya examination officer Secretariat ya ajira? Naomba dondoo.
 
Back
Top Bottom