Usaili wa ajira za utumishi wa umma ni bora uendelee kufanyika Dodoma. Mambo ya kikanda sijui kufanyika taasisi husika haijakaa sawa

mazaga one

JF-Expert Member
Apr 16, 2015
2,463
3,932
Habari wana bodi!

Mimi nikiwa mmoja ya vijana mtafuta ajira, mnaweza kuwa mashahidi wa ajira za utumishi zikifanyikia Dodoma zinakuwa fair sana kuliko zikifanyikia kwenye taasisi husika. Mfano ajira za vyuo vingi, zimefanyikia kwenye taasisi husika. Watu wengi nimesikia wakilalamika ya kuwa kuna upendeleo kwa waliosoma kwenye vyuo husika.

Mimi binafsi nashauri usaili Uendelee kufanyika Dodoma, kwani sio kwa ubaya. Dodoma ni rahisi kwa kila mtu kufika na gharama pia sio kubwa. Msailiwa yeyote anaweza kulala hata Chuo Kikuu cha DODOMA pale bure.

Lakini pia mazingira ya usaili yanakuwa ni fair kwa kila msailiwa. Yale mambo ya kusema kikanda, sijui usaili ufanyike kwenye taasisi husika iliyoajiri kama saili za vyuo zilivyofanyika, binafsi naona hayana afya kabisa.

Kiufupi nimefuatilia hata mahudhurio ya saili zilizofanyika kwenye taasisi husika mahudhurio ya wasailiwa yamekuwa hafifu sana. Mfano usaili wa SUA, Mzumbe, OUT na kwingineko wasailiwa wengi hawakufika kwenye saili na hii ni ishara tosha ya wengi wao kukata tamaa kutokana na usaili kufanyika kwenye taasisi husika kuliko Kufanyikia Dodoma.

Mimi napendekeza Dodoma saili za ajira ziendelee kufanyika kutokana na sababu nyingi nzuri na ambazo zinaweka mazingira ya usawa kwa wasailiwa wote.

Lakini pia ule utaratibu wa Utumishi kufanya usaili siku za weekend, labda Jumamosi na Jumapili, ikienda sana basi ni Jumatatu, ungeendelea kuliko sasa wanavyofanya siku za kazi.

Nawasilisha,
Ni mazaga One,
Kwa Sasa Dodoma,
Wale mnaokuja Dodoma kwenye usaili tukutane, nami Utumishi wameniita usaili Dodoma.
 
All is rubbish! Huwezi kusaili watu zaidi 200 a day, written,ukasahihisha then kama una akili ukasema usaili unafanyika kwa haki!
 
Mimi sio Mgogo,nasema kwa ajili ya Vijana wenzangu....
Mpango wa usaili kufanyika kikanda NI mawazo ya vijana WA kitanzania ili kuwapunguzia ukali WA maisha , wewe unakuja na ngojera za kigogo kisa unaishi sijui kibaigwa, Una akili za ajabu Sana , hivi huwezi kufikiria hata usaili WA mahakama ulivyofanyika vizur.
 
Habari Wana Bodi !Mimi nikiwa mmoja ya Vijana mtafuta Ajira na Ajira. Mnaweza kuwa mashahidi wa Ajira za Utumishi zikifanyikia Dodoma zinakuwa Fair sana kuliko Zikifanyikia kwenye Taasisi Husika. Mfano Ajira za Vyuo vingi,zimefanyikia kwenye Taasisi Husika. Watu wengi nimesikia wakilalamika ya kuwa Kuna upendeleo kwa waliosoma kwenye vyuo husika.

Mimi binafsi nashauri Usaili Uendelee kufanyika DODOMA, kwani sio kwa Ubaya. Dodoma ni rahisi kwa kila mtu kufika na gharama pia sio Kubwa,msailiwa yeyote anaweza kulala hata chuo kikuu Cha DODOMA pale Bure,lakini pia mazingira ya Usaili yanakuwa ni fair kwa kila msailiwa.Yale mambo ya kusema Kikanda, sijui usaili ufanyike kwenye Taasisi Husika iliyoajiri kama saili za Vyuo zilivyofanyika,binafsi naona hayana Afya kabisa Kiufupi nimefuatilia hata mahudhurio ya saili zilizofanyika kwenye Taasisi Husika mahudhurio ya wasailiwa yamekuwa Hafifu sana. Mfano Usaili wa SUA,Mzumbe,OUT na kwingineko wasailiwa wengi hawakufika kwenye saili na hii ni ishara tosha ya wengi wao kukata tamaa kutokana na Usaili kufanyika kwenye Taasisi Husika kuliko Kufanyikia DODOMA.

Mimi napendekeza DODOMA saili za Ajira ziendelee kufanyika kutokana na sababu nyingi nzuri na ambazo zinaweka mazingira ya usawa kwa wasailiwa wote.

Nawasilisha.
Ni mazaga One,
Kwa Sasa Dodoma,
Wale mnaokuja DODOMA kwenye usaili Tukutane.Nami Utumishi wameniita usaili DODOMA
Sio kila unachokiwaza ni lazima ukiandike humu,, vingine jaribu kunyamazia!!,

Kukaa kwako dodoma kusikufanye uwaze hayo!!,
 
Habari Wana Bodi !Mimi nikiwa mmoja ya Vijana mtafuta Ajira na Ajira. Mnaweza kuwa mashahidi wa Ajira za Utumishi zikifanyikia Dodoma zinakuwa Fair sana kuliko Zikifanyikia kwenye Taasisi Husika. Mfano Ajira za Vyuo vingi,zimefanyikia kwenye Taasisi Husika. Watu wengi nimesikia wakilalamika ya kuwa Kuna upendeleo kwa waliosoma kwenye vyuo husika.

Mimi binafsi nashauri Usaili Uendelee kufanyika DODOMA, kwani sio kwa Ubaya. Dodoma ni rahisi kwa kila mtu kufika na gharama pia sio Kubwa,msailiwa yeyote anaweza kulala hata chuo kikuu Cha DODOMA pale Bure,lakini pia mazingira ya Usaili yanakuwa ni fair kwa kila msailiwa.Yale mambo ya kusema Kikanda, sijui usaili ufanyike kwenye Taasisi Husika iliyoajiri kama saili za Vyuo zilivyofanyika,binafsi naona hayana Afya kabisa Kiufupi nimefuatilia hata mahudhurio ya saili zilizofanyika kwenye Taasisi Husika mahudhurio ya wasailiwa yamekuwa Hafifu sana. Mfano Usaili wa SUA,Mzumbe,OUT na kwingineko wasailiwa wengi hawakufika kwenye saili na hii ni ishara tosha ya wengi wao kukata tamaa kutokana na Usaili kufanyika kwenye Taasisi Husika kuliko Kufanyikia DODOMA.

Mimi napendekeza DODOMA saili za Ajira ziendelee kufanyika kutokana na sababu nyingi nzuri na ambazo zinaweka mazingira ya usawa kwa wasailiwa wote.

Nawasilisha.
Ni mazaga One,
Kwa Sasa Dodoma,
Wale mnaokuja DODOMA kwenye usaili Tukutane.Nami Utumishi wameniita usaili DODOMA
Acha kuchafua taasisi kwa hisia usizoweza kuthibitisha. Hakuna cha upendeleo wa sijui huyu katoka chuo gani, bali uwezo wako tu. Ninavyofahamu panels zinakuwa na watu wa nje na wa ndani ya taasisi. Sasa sijui upendeleo unakujaje hapa. Mimi nilikuwa mmojawapo wa wasailiwa, niliridhika sana na diversity ya panelists baada ya kujitambulisha. Kingine unachopaswa kuelewa ni kwamba si saili zote zinafaa kufanyika Dodoma. Mfano hizi za vyuo unazozisemea, ni lazima zifanyike ktk taasisi husika kwani ndiko kuna wataalamu wa kukupima kama unafaa mfano kuwa mhadhiri. Wewe unaona maafisa utumishi wa wizara wenye elimu za level ya bachelor degree wanaweza kusaili wahadhiri wa vyuo? Tuache lawama zisizo na mashiko ndugu.
 
Mtu atoke Kigoma kufuafa usahili Dodoma? Pumbavu kbs ww
Jamaa yangu katoka kigoma,Kesho ana usaili DODOMA.Na nilikutana nae usaili DSM,anasema yeye usaili ataoenda ni WA Dodoma.Na kweli kaitwa Dodoma anaenda.Dodoma imekaa vyema sana
 
Pale Utumishi Kuna watu wa kila aina.Acha kuwa na mashaka na watu wa Utumishi wewe.Mimi naona Dodoma imekaa poa kuliko kufanyika mikoani huku
 
Back
Top Bottom