Ntemii
JF-Expert Member
- May 25, 2022
- 290
- 525
Wakuu natumai mu wazima
Tangu kuanzishwa kwa mfumo wa kidigitali wa uhamisho kwa watumishi wa umma, lengo likiwa kupunguza urasimu na paperwork katika kufanikisha suala la uhamisho kwa watumishi.
Pamoja na lengo hilo zuri mfumo huu tangu uanze umekua ni kero na kizungumkuti cha hali ya juu kwa watumishi wanaoomba uhamisho mbalimbali kupitia mfumo huu.
Watumishi wanaoomba uhamisho wa kubadilishana ili mfumo uweze kukubali maombi yao lazima wote wawe wa kada moja na daraja moja kiutumishi tofauti na hapo mfumo hauwezi kubali maombi yao, kwamfano tabibu daraja la 2 hawezi badilishana kituo cha kazi na tabibu daraja la 1, hili suala ni kikwazo sana kwa watumishi wa idara moja na kada moja kupata nafasi hii ambapo kabla ya mfumo huu hili suala liliwezekana.
Licha ya changamoto nyingi za kimfumo ikiwepo server kuwa down kila mara, kutokupata incoming request, kusema ukweli utumishi muweke wazi kama mfumo umewashinda basi turudi kwenye analogia kuliko haya mateso mnayowapatia watumishi wa umma.
Tangu kuanzishwa kwa mfumo wa kidigitali wa uhamisho kwa watumishi wa umma, lengo likiwa kupunguza urasimu na paperwork katika kufanikisha suala la uhamisho kwa watumishi.
Pamoja na lengo hilo zuri mfumo huu tangu uanze umekua ni kero na kizungumkuti cha hali ya juu kwa watumishi wanaoomba uhamisho mbalimbali kupitia mfumo huu.
Watumishi wanaoomba uhamisho wa kubadilishana ili mfumo uweze kukubali maombi yao lazima wote wawe wa kada moja na daraja moja kiutumishi tofauti na hapo mfumo hauwezi kubali maombi yao, kwamfano tabibu daraja la 2 hawezi badilishana kituo cha kazi na tabibu daraja la 1, hili suala ni kikwazo sana kwa watumishi wa idara moja na kada moja kupata nafasi hii ambapo kabla ya mfumo huu hili suala liliwezekana.
Licha ya changamoto nyingi za kimfumo ikiwepo server kuwa down kila mara, kutokupata incoming request, kusema ukweli utumishi muweke wazi kama mfumo umewashinda basi turudi kwenye analogia kuliko haya mateso mnayowapatia watumishi wa umma.