Utetezi wangu wa wazi wa William Ngeleja - The use of Emergency Powers Act 1986

hili halina shaka lakini Ngeleja anacho kile tu ambaco amepewa. Kumuwekea mtu malengo ya kufikia kitu fulani halafu humpi nyenzo za kufikia malengo hayo kunawanyima waliompa malengo hayo kumdai kwanini hajayatimiza.
Mzee Mwanakijiji, nakubaliana na utetezi wako kwa kiasi fulani kuwa Ngeleja anacho tuu kile alichopewa, jee wakati anapewa hicho alichopewa, alipangiwa malengo?, kama alipangiwa malengo na akanyimwa nyenzo za kuyatekeleza, aliwaambia hao wapanga malezo jee nyenzo vipi?.

Lakini vile vile wale wanaoweka malengo wanamuwekea malengo ya namna gani?
Hapa sasa ndipo tulipotaka Ngeleja aonyeshe uwezo, unawekewa malengo na unakubali kuyatekeleza only kama unao uwezo huo, serikali yetu inatumia utaratibu wa OPRAS, unakaa na mkubwa wako (rais), unapangiwa malengo, mnajadili utekekelezaji within specific time frame. Mkifika katikati, mnafanya MTR (Mid Time Review) na hapa ndipo una determine kama utatimiza malengo at the end of the time kama hutatimiza unasema na unatoa na sababu, Ngeleja aliyafanya haya?.
Huwezi kumwambia Ngeleja atatue tatizo la umeme wakati uhuru wa kufanya hivyo unaamuliwa na Baraza la Mawaziri.
Ni kweli ni Baraza ndilo huamua, lakini Ngeleja alikwenda with a plan huko baraza na ikakataliwa?. Kwa mwananchi wa kawaida, we don't care about the means, we want results, kwetu sisi ni "The end, justify the means", at the end of the day, hatuna umeme, tunataka uwajibikaji, kwa maoni yangu sio Ngeleja tuu, wananchi tunamtaka JK awajibike kwa hili, 2015 is too far!.

Kama huko cabinet wana vichwa vyote hivyo, kina Magufuli, kina Mwandosya, kina Sitta, etc. etc wamefanya nini kwenye hili?. Aren't they are all nothing?!.
 
Mzee mwanakijiji,

Ama kweli leo umeturudisha ktk JF ileee ambayo wengine tumeikosa kwa muda mrefu sana.... bravo!
Na nashukuru sana umeweza kwenda deep ktk swala zima la mh. Ngeleja na hali halisi iliyopo hivyo kujaribu kuwakumbusha Watanzania historia fupi ya kichwa cha mada hii. Na binafsi nakubaliana nawe mia kwa mia kwa sababu kichwa cha mada nzima ni ukosefu wa Umeme ambao kama kweli wananchi tunatafuta solution, Ngeleja ni bangusilo pamoja na kwamba HAFAI... Lakini vile vile ni mawaziri wachache sana wa JK ambao - WANAFAA kushika nyadhifa walizoshika.

mengi umeyazungumza isipokuwa mimi nitatofautiana na wewe pale unapomtaka JK achukue maamuzi magumu..Sijui kama ndio haya alokuwa akizungumzia Lowassa ama yale yanayomhusu yeye mwenyewe na kambi yake ya magamba. Hapa nitarudi ktk usemi wangu wa kila siku -WATU na MAZINGIRA.. Ni kina nani unataka wachukue jukumu hilo? jibu lake bila kuficha wala kumung'unya maneno - MAFISADI.....

Watanzania kwa uhakika sisi ni wavivu wa kufikiri na pengine tusiwalaumu CCM peke yake kwa sababu sisi wote tunafahamu mapungufu hayo toka mwaka 1985 baada ya kuingia Mwinyi tulianza na mgao wa hapa na pale kama dalili ya cancer, lakini kwa mapenzi yetu wenyewe tuliwachagua CCM ktk uchaguzi wa mwaka 1995 pamoja na kwamba Mrema alituasa, baada ya hapo wakaingia CUF na CDM wakimuunga mkono mchumi kama Lipumba na wananchi tukamwona mchawi na hivi majuzi Dr.Slaa....

CCM wasingekuwa na maamuzi haya mabaya kama wangejua wananchi hatutaki kudanganywa, wananchi hatutaki kuzawadiwa khanga, T-shirt na kofia bali tunataka maisha bora kama alivyotuahidi JK ambaye alikuja na mkwara mzito kuhusiana na nishati...Matatizo mengi tumejitakia sisi wenyewe na hakika leo tunavuna tulichopanda. Leo cancer limetushika pabaya tunataka maamuzi ya kukata mguu, kehso itakuwa mkono ili hali hatuna dawa isipokuwa tunaongeza muda wa kuishi..

Sasa nirudi ktk kupinga hoja ya JK achukue maamuzi magumu ingawa wewe umesema hatua ngumu..kwani binafsi naamini desperate measure ni maamuzi ambayo yana carry some risks, na unayafanya kwa sababu huna njia ya kutokea isipokuwa unafumba macho na kujaribu. Pia ni katika maamuzi ambayo ktk hali ya kawaida usingeyafanya. Sasa JK na hali hii mimi nashindwa kumweka popote maanake hana kawaida wala haikuwa ktk akili yake kwamba Umeme ndio roho ya uwekezaji iwe ktk viwanda, madini na makuzi yoote ya uchumi wa nchi. hakuona haya leo MTU huyu unategemea nini toka kwake?

Kitu kimoja tu tukumbuke ni kwamba JK ni ktk viongozi walioshindwa, ni viongozi wanaoshiriki ktk Ufisadi wa nchi yetu toka mikataba ya madini hadi uuzaji wa ardhi na uwekezaji nchini, leo unamtaka yeye achukue desperate measures wakati Bongo haina umeme kaenda South na karudi kujirusha ktk harusi ya ndugu yake B'moyo. Hivyo ni sawa na Julius Kaizali ambaye aliambiwa janga la njaa na kwamba wananchi wake wanakufa njaa yeye akasema wagawiwe cake (as a desperate measure) wakati yeye na maseneta wake wakioga maziwa.


Binafsi, siamini na wala sintaamini JK ambaye alijua wazi kwamba Tanzania tuna tatizo la Umeme na akaja na desparate measure wakati ule kumbe katuletea Richmond na hadi leo hii hakubali makosa yalifanyika. Kwa akili zake, Msabah na Lowassa wameonewa na hakika maamuzi ya kujiuzulu watu hawa yanamuuma hadi leo.. can U imagine? yaani kujizulu kwa Msabah kunamuuma kuliko adha alowaaachia wananchi leo unamtaka achukue measures nyingine ambazo zinapelekea kule kule ktk kuleta mitambo chakavu ktk mikataba feki, leo wewe mwananchi unachukua desprate measures za kumkabidhi (panga jambazi) mamlaka yale yale yalopelekea tuwe hapa tulipo leo...

What makes u think JK ataleta mitambo chakavu kwa bei nafuu na kwa muda wa siku au miezi michache leo hii ikiwa kashindwa muda wote wa miaka sita alokaa madarakani. Jamani Tanzania wenye kupata umeme ni asilimi chini ya 15 hilo pekee ni tatizo kubwa ambalo kiongozi yeyote mwenye busara na utashi wa kazi angelitazama kwanza ikiwa anataka kualika wageni wawekezaji. Kama alishindwa kulitazama hilo mahala ambapo taifa linaingiza fedha leo aje kuwekeza ktk mitumba ati kwa sababu wananchi asilimia 15 wameingia ktk mgao?...

Mtanisamehe lakini ktk hili hakuna njia zaidi ya sisi wananchi wenyewe kumtaka JK ajiuzulu pamoja na baraza lake la mawaziri. CCM wameshindwa kutuletea maendeleo na yawezekana chini ya maamuzi magumu ambayo unayazungumzia nadhani ni wananchi ambao wanatakiwa kuchukua maamuzi hayo. Aidha wananchi wamalazimishe JK kuchukua hatua 1,2,3 au laa sivyo ajiuzulu yeye pamoja na baraza lake, Ama afanye mabadiliko ktk wizara hii na kazi hiyo akabidhiwe Magufuli, Mwanri au hata January Makamba ambaye najua pamoja na uchizi wake anaweza kazi - he can deliver!
Nina hakika kesho akiondolewa Ngeleja basi sifa zitamwangukia JK kama rais asiyetaka mzaha, wakati shida yetu imesimama pale pale. Nawajua Wadanganyika maana tumeona kwa Lowassa, Chenge na majuzi Rostam sifa zinamfuata JK na kina Nnauye! Ni sifa gani haswa...Oooh magamba wamejiuzulu!

Mwisho wa yopte haya wananchi tunatakiwa kujifunza kutokana na makosa tuloyafanya nyuma. Kuendelea kuwachagua CCM kwa kufikiria ndani ya CCM ndiko solution inaweza patikana, ni kujidanganya zaidi kiasi kwamba inaonyesha hata sisi Wadanganyika hatufahamu tunachokitaka. Mtanisamehe kusema tena sisi ni wanafiki kama viongozi wetu, ni sawa na bwana/ mke anayemkandya mkewe/mumewe lakini wameishi kwa miaka 40 kisha kuna watu wanaamini kabisa kwamba pale hakuna mapenzi isipokuwa ni mazoea yamewaweka pamoja! - Thats bull!
 
Pasco, kwanini watu hawataki Rais na Baraza zima lijiuzulu turudi kwenye uchaguzi?
Mzee Mwanakijiji kwenye hili la kuitisha uchaguzi sasa, naomba tuwe realistic, ni jambo ambalo haliwezekani!. Hata kichaa asinge kubali!. It would be adding an insult to an injury.
 
Mzee Mwanakijiji kwenye hili la kuitisha uchaguzi sasa, naomba tuwe realistic, ni jambo ambalo haliwezekani!. Hata kichaa asinge kubali!. It would be adding an insult to an injury.

Sasa si ndio demokrasia; vipi kuhusu Rais kutangaza rasmi hali ya dharura na kutumia madaraka yake kama Amiri Jeshi Mkuu -- au hicho cheo watu wanafikiria ni cha mapambo tu?
 
Notwithstanding makosa ya waliokuwepo Wizara hii.............Ngeleja is to blame as well...........kwa sababu ktk kipindi chake ameendelea na business as usual...........Wizara hii ni critical...........inahitaji mtu aliye na "balls" za kufanya maamuzi juu ya kutatua tatizo la umeme nchini for good...............short of that......unajiuzulu............

Ninamuomba mwenyezi Mungu anipe uhai zaidi ili nije shuhudia mradi wa Stiegler's Gorge.....walau ukianza........
 
Mzee Mwanakijiji kwenye hili la kuitisha uchaguzi sasa, naomba tuwe realistic, ni jambo ambalo haliwezekani!. Hata kichaa asinge kubali!. It would be adding an insult to an injury.
Pasco hakuna mageuzi au maendeleo yasiyo na gharama. Watanzania ni lazima tujifunze kwa vitendo, kama ni nadharia tumeshindwa. Tusingewarudisha madarakani waliotufikisha hapa iwe kwa kura au kuchakachua.

Uchaguzi si ghali, utagharimu si zaidi ya bilioni 150. Kampuni ya Pan Africa imeingia mkataba na TPDC tukapoteza 100B, Zantel 300B, Kagoda 40B, BAE 70B. Gharama za kuandaa bajeti ya Ngeleja haijulikani. Kwanini tuone kurudia uchaguzi ni ghali kuliko pesa zinazopotea na hatuhoji?

Mfumo wa chama kimoja unasemekana haukuwa wa demokrasi, sasa huu wa demokrasi kwanini tuogope kuu enzi? Wabunge warudi kuuliza wapiga kura, je hii ndio serikali waliotaraji na je wanaridhika na wawape ridhaa tena? Si ndio demokrasi yenyewe.
Kama wananchi hatutafanya maamuzi magumu watachezea akili zetu kila siku huku tukiumia. Tunaweza kuwa vichaa wa mwezi mmoja lakini tukapata dawa ya kudumu ya matatizo yetu.
 
Watu tuna kumbukumbu fupi sana na ukweli huu umejidhihirisha hivi sasa kwenye haya matatizo ya umeme. Waziri Ngeleja anaoneka ndiye kama vile amesababisha matatizo yote haya wakati ukweli wa mambo umeme wa uhakika umekuwa tatizo sugu Tanzania.

Sasa iweje Ngeleja leo abebeshwe msalaba wa lawama na shutuma wakati mawaziri wa nishati na serikali zilizopita zimemrithisha tatizo? Hiyo si haki hata kidogo. Jaribuni tu kurudi nyuma miaka 20 iliyopita muone ni kina nani waliweza kupata fursa ya kuongoza wizara hiyo na walifanya nini kuhakikisha tatizo linakuwa historia.

I cut him some slack!!

Mkuu pamoja na utetezi huo makini bado kuna jambo linasahaulika! Uwajibikaji! Wakati wa uchaguzi serikali iliyo madarakani ilitoa ahadi ya 'kulifanya tatizo la umeme kuwa historia' the exact wording quoted, sera zilizoenda shule zilimwagwa, haswa kule kwa jamaa zetu Kigoma ambako umeme ni lulu! Je haileti maana ukiwa umepanga mikakati ukae chini na kutathmini, kisha ukiona inakwenda kinyume na matarajio ukabadili mbinu? Wewe mwenyewe unashuhudia jinsi mikakati invyowekwa wazi kwa faida za kisiasa tu wakati ukweli upo wazi kwamba umeme siyo tatizo tatizo ni utekelezaji wa mipango? Hata leo ukitafuta nyaraka za serikali zinazoelezea mikakati mahsusi ya kulitatua hili janga ipo wazi but why can't somebody be responsible and act(Give results). By profession mimi ni Mhandisi and i read and read and know hakuna tatizo la umeme hapa, tatizo ni ahadi, unapotoa ahadi it is an oath that one should abide to governing rules, like you said kwenye ile issue ya kuapa, sasa unamtoa vipi huyu ndugu kwenye ahadi alizoziweka mwenyewe huku wananchi wakimshangilia na kumpepea, sasa yanamtokea puani , do we question if he deserves kutetewa, hell no, rudi kinyumenyume utajua kwa nini yeye anakaliwa kooni zaidi! otherwise i give you guys much regards!
 
Kweli mwanakijiji kwa kutetea wakristo wenzake anaongoza, unamtetea kwakuwa wiliam au una lingine?

Alipokuwa Idrisa Rashid anashauri tununue mitambo ya doawns chakavu ulimpinga hadi mapofu yanakutoka!!!! unafikiri kidini dini

Eti uchaguzi ufanyike? wa nini? tunatakiwa kuchukua hatua rahisi na fupi..ondoa mtu asiye perfom ngeleja period!
 
Kwani hawajatokea watu wenye balls? majuzi tu Magufuli alifanya operation bomoa bomoa akaambiwa asimamishe zoezi hilo na mkulu, hakujiuzulu tena wabunge wakaingia bungeni kupinga maamuzi yake, leo hii vibanda vinaongezeka na mwisho wa siku majuto ni mjukuu. Mama Tibaijuka alipandisha mashetani yake akazimwa yaani haya mambo mnayoyataka, hayawezekani ndani ya utawala huu bado hamuelewi kitu jamani.

Ngeleja hafai na hafai toka achaguliwe kwa kutazama malengo yetu sisi wananchi isipokuwa anafaa sana ktk kuficha siri na mikataba mibovu ilokwisha sainiwa na utawala uliopo, hivyo anatakiwa mtu anayeaminika na mafisadi. Looking from that angle, Ngeleja anafaa na yupo ktk kundi la magamba..hafai kwetu lakini anafaa sana kwao..kwa hiyo tunataka ajionzulu kwa sababu gani haswa.. kutokana na mgao wa umeme au ile barua ya Jairo? ama yote kwa ujumla wake inamlazimu ajiuzulu kwa sababu yupo katikati ya scandal hizi.

Haya matatizo yalijulikana na sii mara ya kwanza mvua kugoma miezi hii nadhani huu utakuwa mwaka wa 10 kama sikosei tukiwa na shida kubwa ya maji pale bwawa la Mtera. na mnataka Ngeleja ajiuzulu lakini mmesahau kwamba magamba bado wanashika mamlaka yote ktk Ufisadi wao na hakika hiyo barua ya Jairo ni ktk kuficha kombe mwanaharamu apite. Unapotaka mtu mbovu ajiuzulu ni kwa sababu unahakika atachaguliwa mbora lakini kutaka Ngeleja ajiuzulu hali mnajua atakuja msanii mwingine nani hapa anajidanganya!

Leo hii hadithi bungeni ni Jairo na Ngeleja mabangusilo wanaotakiwa kutolewa kafara ili hali hakuna kiongozi yeyote iwe Magufuli ama Mwandosya wangeweza kufanya lolote kwani hata hawa wamewahi kuwa ktk wizara nyeti na walishindwa kufanya la maana zaidi ya kuonyesha kwamba wangeweza isipokuwa hawana jinsi...tunabakia na WANGE... NINGE. Sasa kama wabora wanashindwa kwa kutokuwa na jinsi iweje tuwe na tumaini jingine kwa kupitia njia ile ile..Uwajibikaji unatakiwa kwa serikali nzima ILOSHINDWA na kushindwa kwa CCM kuleta maendeleo hakutokani na Ngeleja bali chama kizima kimeshindwa..mwenye ushahidi kinyume cha maelezo yangu anipe!

Labda turudi ktk sababu za awali zilizotokana na kutokea umeme na mgao huu maanake nadhani ndio sababu ya kwanza kusikia habari za Ngeleja ajiuzulu..Maaana sidhani kama tatizo ni ukosekanaji wa nguvu za umeme za kutosheleza uzalishaji kwani hizo kama alivyokwisha sema Mwanakijiji mapungufu hayo yapo kwa zaidi ya miaka 20. Hoja ya Ngeleja inatokana na mgao wa umeme uliopo hivyo chanzo chake ni nini haswa!

Je, ni kusimama kwa mitambo ya IPTL? nasikia sababu ni kwamba IPTL hawana mafuta au hawana fedha za kununulia mafuta...IPTL ni shirika huru ambalo halipo chini ya wizara yake afanye nini hali mkataba unasema wazalishe wasizalishe ni lazima walipwe!..hakuna sheria inayowafunga IPTL iasi kwmaba unaweza kusema Ngeleja ANGE....
Haya nimesikia kwamba sijui Transformer ililipuka huko Ubungo, hii ni swala la Tanesco ambao walitakiwa kufanya ukarabati na pengine hawana fedha kutokana na kwamba serikali haikuwapa za kutosha na shirika limekuwa likiendeshwa kwa hasara toka enzi.. Haya nipeni sababu nyingine za mgao kisha tumjadili Ngeleja laa sivyo isiwe hiyo barua ya jairo kuwa sababu kubwa ya waziri kujiuzulu hali tatizo letu sisi wananchi ni ukosefu wa umeme.

Lobbying wanafanya kila bajeti na kama nilivyosema wewe sikiliza bunge utasikia vikao vya wizara na mialiko ikitolewa na Spika kila siku anapolifunga bunge. Na Wabunge wote hupenda kuhudhuria vikao hivi kwa sababu kuna posho ya buree ambayo leo mnaikubali kama ni rushwa! Posho za vikao ni rushwa siku zote isipokuwa leo imeandikwa ktk lugha ambayo hamuifahamu ndio mnafikiria hiki ni kitu kigeni..Mara ngapi mmesikia Pinda akiitisha vikao vya wanaCCM wakiwa bungeni kisha kesho yake wote wanapitisha hoja kwa kura nyingi. CDM kunyimwa kamati za Upinzani haikuwa bahati mbaya hata kidogo ila ilipangwa pale pale bungeni na watu wakavuta kama kawa..

Na labda niwataarifu tu kwamba sii kweli wananchi na wana CCM wanamapenzi na chama chao kiasi hicho bali ndani ya CCM kuna KULA..ukitaka kutajirika haraka kuwa mwana CCM na hilo huondoa imani za watu kiasi kwamba wapo tayari kukutoa roho kama utakata mirija yao. Na sisi wananchi tunashangaa kuona Jairo kaomba mamillioni watu mmeshtuka mkidhania ni nyingi sana hali kwa hawa wabunge 200 na zaidi ni vijisenti! kupitisha bajeti inayotazama wilaya nne tu.
 
Umeongea pointi kwa kwenda mbele..kwanini usiwe na consultancy yako..ulitakiwa uwe unaenda kuwapiga msasa wabunge Dodoma..walejamaa wangekupa mshiko mrefu..jamaa wanamihela kibao lakini kichwani ovyo tu.
 
Tukubali ya kwamba hatuhitaji kumlaumu ngeleja kwa yaliyopita.
Je aliposhika uongozi alikuwa na mtaji kiasi gani na ameweza kuuongeza kiasi gani, au je amedidimiza huo mtaji kwa asilimia ngapi.
Tatizo la umeme katika kipindi chake limeonyesha ubora upi au limeonyesha magumu zaidi.
Kama ngeleja hastahili kulaumiwa basi tatizo hili haliwezi kutatuliwa hapa tanzania tulipeleke nje ya sayari kwa ufumbuzi, tuingie makanisani na misikitini tufunge mikono na tusubiri miujiza.
 
Wakati wa Mchakato wa wabunge G55 Nyerere alitaka Waziri mkuu, ajiuzulu kwa sababu aliamshauri raisi vibaya, akajenga hoja kwamba Raisi kujiuzulu siyo jambo dogo kwani nchi itayumba, leo pia the same hoja inaweza kuwa applied kwa Kikwete na Ngeleja, ni dhahiri Raisi akijiuzulu nchi Itayumba, ila mshauri wake Bwana Ngeleja ambaye ni mwenye dhamana ya Umeme hana budi kujiuzulu either (1) kwa kutomshauri Raisi mbinu bora na za haraka za kuondoa tatizo hili AU (2) Kamshauri raisi lakini raisi kampuuza.

Kikwete Kachaguliwa na Watu, na wakati anachaguliwa Tatizo la umeme lilikuwa palepale kwa hiyo ni dhahiri wananchi wanaimani na Kikwete la sivyo wasingemchagua tena mwaka 2010, mojawapo ya sababu ya kumchagua ni katika kuamini kwamba atatatua tatizo la umeme, sasa ni dhahiri basi Mtu aliyewekwa Incharge ya kuondoa tatizo hilo Bwana Ngeleja, ameshindwa, inabidi ajiuzulu!.
Raisi hawezi kujiuzulu kwa sababu ya incompetency ya waziri mmoja mmoja, Ifahamike Mawaziri wanafanya kazi waliyopewa na Raisi, wakishindwa haondoki raisi kwanza, bali inabidi aondoke aliyeshindwa ambaye katumwa na raisi. Sisi wananchi kazi yetu iwe ni katika mambo mawili (1) Kumshinikiza Ngeleja aondoke kwa hiyari yake mwenyewe (2) Kumshinikiza Raisi amwajibishe ngeleja kwa kumuondoa katika nafasi yake ya uwaziri.

Kumtaka raisi ajiuzulu hivi sasa kwa sababu ya sakata la umeme wakati wananchi wamemchagua juzi tu tukiwa ndani ya tatizo la umeme ni kutokuwa realistic!
 
Sasa si ndio demokrasia; vipi kuhusu Rais kutangaza rasmi hali ya dharura na kutumia madaraka yake kama Amiri Jeshi Mkuu -- au hicho cheo watu wanafikiria ni cha mapambo tu?
Viongozi wa Afrika wanafuata misingi ya demokrasia ya kweli ni wachache, JK angependa demokrasia ya kweli, angewateua Lipumba na Dr. Slaa kuwa wabunge kwenye zile nafasi zake za uteuzi. Hata hili la vyama vingi, tumelikubali because we had no choice. Wengi wa viongozi wetu wangependa kufuata African Democracy kama ya Libya na Zimbabwe.

Hili la kutangaza hali ya hatari, nalo pia haliwezekani, akifanya hivyo ni admission ya weakness ambayo rais wetu JK kamwe hawezi kukubali. Yeye anapenda songs of praise, makofi, hongera na mapambio, he is a perfect president who does no wrong na ndio ametufikisha hapa tulipo with smilling face!.

Naamini hata ile deal ya kwanza he had his cut, ndio maana EL kajinyamazia kimya bila kuingia kwa undani what was his role, ni kusave face ya band mate wake kwenye Boys II Men!.

Kwake hiki kilio cha umeme is not a big deal, ni Watanzania tuu kutaka kujidekeza, mbona wote wamezaliwa vijijini na hakuna umeme?, mbona mpaka leo wanaofaidi matunda ya umeme ni asilimia 20% wa mijini na asilimia 80 wa vijijini hawaujui hata huo umeme?, hivyo kwake umeme ni luxury, tangu lini luxury ikawa Janga la taifa!?.
 
unaijua hali ya dharura ya JK, bora akae kimya hivyo hivyo, maana anaweza tangaza kisha akaiita mashehe na maskofu jangwani kuiombea mvua, si utapiga kichwa ukuta kwa hasira.
Nani anayetengeneza sera ya Nishati nchini? Kuna ubaya gani kwa Rais kutangaza hali ya dharura hata kesho na kutumia madarka aliyonayo kutatua tatizo la umeme?
 
SG project ilikuwapo muda mrefu, matayarisho ya mwanzoni yalishafanywa, sote tunajua huu mradi is being pushed aside for selfishness!!! Ngereja hawezi kuepuka hili mkuu MKJJ!!!

Kwa ufupi the whole CCM group will never come clean on this!!! The truth is, SG is the only solution to this problem!!!

Kama SG ndio suluhisho la matatizo yetu ya umeme ambayo yamedumu kwa muda mrefu kwa nini sasa mradi huu hautekelezwi? ni kwa maslahi ya nani hautekelezwi?,tunapaswa kumfahamu ili tumuwajibishe.
 
Wabunge badala ya kukubaliana kumlaumu Ngeleja, wakubaliane kumpa Ngeleja mzigo wa kuanza ujenzi wa Stielger’ Gorge kwa kushirikiana na RUBADA.
Nakupongeza sana mwanakijiji umechambua kwa umakini na upana wa mawazo lakini napingana nawewe kwa jambo moja tu. Kumpa kazi mtu ambaye hajawahi kuwaza mbinu zakuifanya nikupoteza muda wako kama wewe uliye nje ya wizara umeweza kufikiri nakutoa huo ushauri lakini yeye aliye waziri mwnye dhamana anawaza kudanganya wananchi kwakuwatajia miradi lukuki ili awachanganye kitakwimu na kuwafariji kwamba anatatua tatizo pasipo ukweri hatakidogo ataaminika vipi? kajua kwamba ana bajeti ya ulaghai akajaribu kuhonga ipite unadhani analengo zuri ukimkabidhi mradi kama huo atadanganya umeanza kumbe haujaanza alidanganya mwanza itazalisha mw 60 kufikia june leo tunaelekea july hakuna kitu mwanza nakusihi muone ngeleja kama ukoma hakuna anacho weza zaidi yakuandaa rushwa kuhonga wabunge.
 
Back
Top Bottom