Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Na. M. M. Mwanakijiji
Utangulizi
Tatizo la upungufu wa nishati nchini linatafutiwa kisingizio. Naam, limetafutiwa kisingizio na kisingizio hicho kinazidi kukuzwa mbele ya macho yetu na kufanywa ndio sababu. Kwamba, hali ya upungufu wa nishati ya umeme nchini inatokana, imesababishwa, imeongezwa na kudumishwa na Waziri wa Nishati na Madini Bw. William Ngeleja. Hivyo - hitimisho linapendekezwa - kwamba Waziri Ngeleja awajibishwe na hata wengine wamefikia mahali pa kutaka baraza zima la mawaziri lijiuzulu.
Utetezi wangu huu una lengo moja nalo ni kutaka sababu ya tatizo la upungufu wa nishati nchini iwekwe wazi, ikubaliwe na iwajibishwe. Badala ya watu kuzunguka mbuyu na kuuimbia kama wanga, wasimame na kuungoa mbuyu huo. Utetezi huu haumhusu Ngeleja kama mtu - kwani sina ujamaa, undugu, au hata urafiki wa karibu - bali yeye kama Waziri mwenye dhamana ya Nishati na Madini. Kwamba, ninachosema na kupendekeza kwako msomaji ni kuwa wakosoaji wa Ngeleja wanataka kumkosoa na kumbembesha mzigo ambao mwenye kuustahili haugusi wala kuonesha anawajibika kwao.
Sitojaribu hata kidogo kuingia kwa undani kuchambua historia, sera mbalimbali au hata kuingia kufafanua mambo mengine mengi yanayohusiana na tatizo hili kwani ninayachukulia kwamba msomaji wangu atakuwa ana uelewa wa kutosha na anaweza kufanya mwenyewe utafiti kudogo kujibu maswali mbalimbali ambayo yanaweza kubakia katika fikra zake.
Ngeleja amekuta tatizo la umeme Tanzania.
Kwa mtu yeyote ambaye amewahi kuchukua muda kidogo kufanya utafiti wa hali ya nishati nchini na hususan nishati ya umeme atakuwa ametambua jambo moja dhahiri kuwa tatizo la nishati hiyo nchini halikuanza mwaka 2011. Naam, halikuanza mwaka 2005 au hat amwaka 2000. Ni tatizo ambalo kukua kwake kumekujalikana kwa karibu miaka ishirini sasa. Upungufu wa nishati ya umeme haujatokea nchini kama mvua ya jua kali ambayo inatokea bila kuwa na mawingu! Kweli, tatizo hili halijatokea kwa sababu kuna mtu alitupiga dawa ya usingizi taifa zima na tulipoamka tukakuta kuna upungufu wa umeme
Hadi tumefika mahali taifa zima tunapigishwa magoti mbele ya hali mbaya ya tatizo la nishati tujue kuwa imechukua karibu miaka 25 kufika hapa. Tumefikishwa hapa siyo na njama toka kuzimu bali kutokana na maamuzi mbalimbali na kati ya maamuzi hayo hakuna ambalo lilifanyika bila kujua hali ya umeme nchini.
Ninachopendekeza ni kuwa hatuwezi kutenganisha tatizo la nishati nchini leo hii, matokeo yake mabaya katika maisha ya kiuchumi ya taifa letumna athari zake za moja kwa moja katika kupiga hatua kubwa mbele (The Great Step Forward) ya maendeleo kwetu sisi wa kizazi hiki na uzao wetu huko mbeleni na uongozi wa sera na kisiasa pamoja na utawala wa Chama cha Mapinduzi. Kwamba, matatizo ya nishati nchini yana uhusiano wa moja kwa moja na sera pamoja na utekelezaji wa sera hizo katika miaka thelathini iliyopita. Naomba mniruhusu nipitie tu baadhi ya sera na miongozi ya kisiasa chini ya Chama cha Mapinduzi.
Mwongozo wa CCM wa 1981
Mwaka huu ni miaka thelathini ya mojawapo ya nyaraka muhimu za kisiasa nchini. Kama Azimio la Arusha lilipanga miaka ya sitini, na Siasa ni kilimo pamoja na Ujamaa vijijini vilipamba siasa za miaka ya sabini, naweza kusema kuwa Mwongozo wa CCM wa mwaka 1981 ulipamba sehemu kubwa ya nusu ya kwanza ya miaka hiyo. Ni nyaraka ambayo hata leo bado nguvu ya hoja zake inasimama.
Mwongozo ulisema hivi Suala la nishati ni la msingi kwa maendeleo ya Taifa letu. Pamoja na kuendelea kutafuta mafuta, Chama kitahakikisha kuwa serikali inazidisha mipango thabiti itakayoliwezesha Taifa kuanza kutumia nguvu za maji, makaa, upepo na jua. Pamoja na miradi mikubwa ya nguvu za maji kuna haja ya kutia maanani miradi midogo midogo ya nguvu za maji. Suala la kuni itabidi lipewe umuhimu mkubwa kwa kuwa na mipango kamambe ya kupanda miti vijijini na miradi ya Mikoa na Taifa. Chama kiihimize Serikali kuendelea na kutafuta mbinu za kutumia makaa ya mawe tuliyonayo kusukuma uchumi wetu. Umuhimu wa suala la nishati utahitaji sera maalum
Ni wazi kuwa haja ya kuendeleza vyanzo vya nishati si jambo ambalo limeanza wiki iliyopita Bungeni. Lina miaka thelathini chini ya watu wale wale, chama kile kile chenye sera zile zile. Inashangaza watu wanashangaa kukutana na matokeo yale yale.
Azimio la Zanzibar 1991
Kama kuna maamuzi ya kisiasa ambayo mrindimo wa mwangwi wake unaendelea kusikika hadi leo hii ni maamuzi ya Zanzibar ya mwaka 1991. Maamuzi yale yalibadilisha mwelekeo wa kiuchumi wa taifa letu na kwa namna moja au nyingine (nitawaacha wengine waamue hili) ulikoleza kuibuka kwa mgongano kati ya watawala na watawaliwa, na kuibuka kwa tabaka la kinyonyaji la mafisadi. Maamuzi ya Zanzibar hayakuanisha sana suala la haja ya kushughulikia tatizo la nishati. Yalihusu zaidi umiliki wa mali za uchumi na kulegeza masharti ya uongozi ikiwemo kutengeneza msingi wa ubinafsishaji wa mashirika ya umma ambao ulikuja kufanyiwa kazi sana na Rais Mkapa baadaye.
Sera ya Nishati ya 1992
Tukiwa njiani kutoka mfumo wa chama kimoja cha kisiasa kwenda vyama vingi na tukiwa chini ya uongozi wa chama hicho kimoja tuliandaliwa sera ya nishati ya taifa. Sera hii ilitolewa na Wizara ya Maji, Nishati na Madini ambayo wakati huo ilikuwa ikiongozwa na mmoja wa viongozi wasomi ambao walikuwa wameingia tu umri wa kati lakini mwenye sura na mvuto wa Ujana Jakaya Kikwete. Sera hiyo ya nishati ilisema mambo mengi lakini hakuna lolote mabalo linasemwa kwenye sera hilo ambalo laweza kuwa geni kwenye masikio ya Watanzania.
Sera hiyo ilitudokeza jinsi mpango wa Kufufua uchumi wa miaka ya themanini ulivyokuwa na malengo makubwa matano. Malengo yote matamu hayakuhusisha moja kwa moja kuongeza nishati kama njia ya kusisimua uchumi zaidi. Kwa kiasi kikubwa mipango yote ya wakati ule ilikuwa na lengo la kutimiza kile tulichokiita ruksa ambapo mikopo ya kigeni iliweza kuingia zaidi, uchumi kufunguliwa n.k. Chama cha Mapinduzi wakati huo hakikuweka msingi wa kuongeza uzalishaji wa nishati kama Mwongozo wa 1981 ulivyodokeza.
Kwa ufupi utawala wa Rais Mwinyi, japo unasifiwa kwa kufungua uchumi na kuwezesha vitu vingi kufurika kwenye maduka yetu (kufuatia uhaba wa bidhaa wa mwanzoni mwa miaka ya themanini) ulishindwa kulifanyia taifa jambo moja kubwa na la msingi kuliruhusu kuwa na uhuru wa kiuchumi. Hakukuwa na ruksa ya kuzalisha umeme na ziada. Chama cha Mapinduz hakikusimamia serikali yake wala kuisukuma kutekeleza sera ya uhuru wa nishati.
Sera ya Ubinafsishaji ya Mkapa
Rais Mkapa, alipoingia na uongozi wake hasa ngwe ya kwanza alisimamia na kusukumiza ubinafsishaji wa mashirika mbalimbali ya umma. Nimepitia juzi orodha ya makampuni mbalimbali (makubwa na madogo) ambayo yalikuwa yametaifishwa na seriakali wakati wa Mkapa hadi ilipofika mwaka 2003. Hadi Juni 2003, kulikuwa na mashirika 138 yaliyobinafsishwa kwa Watanzania kwa asilimia 100; mashirika 20 yaliyomilikishwa wageni kwa asilimia 100; na mashirika 42 kwenye ubia.
Mojawapo ya vitu vinavyonishangaza sana ni jinsi gani wataalamu wetu wa ubinafsishaji walivyopima hali ya nishati nchini kiasi cha kuweza kuuza makampuni mbalimbali ambayo walitarajia yangeweza kutengenezwa na kurudishwa katika uzalishaji karibu yote kwa wakati mmoja. Tukumbuke kuwa makampuni mengi yaliyokufa au kuwa na hali ngumu yalikuwa hayatumii nishati zaidi kama zamani. Kitendo cha kuyauza na kuhimiza kuyarudisha kwenye uzalishaji ni wazi kingesababisha ongezeko la mahitaji ya nishati ya umeme nchini.
Kosa kubwa ambalo lilitokea katika sera ya ubinafsiji hususan suala la nishati linapokuja ni kutokuendeleza vyanzo vya nishati kukidhi mahitaji ya makampuni ambayo yalikuwa yanarudishwa kwenye uzalishaji au yaliyokuwa yanaanza kuzalisha bidhaa nyingine na kujipanua zaidi. Najenga nadharia (ningependa kuwaachia wataalamu wetu kupima kama ina ukweli) kwamba sera ya ubinafsishaji iliyotukuzwa kwa mafanikio yake na Dr. Kigoda mwaka 2004 imechangia kwa kiasi chake kusababisha upungufu wa nishati. Kwamba kisima cha nishati kilichokuwepo kilitosha watu wachache waliokuwepo na hasa wazee wachache, lakini tulipopata mwamko wa kuleta wanafamilia, jamaa na marafiki kijijini tulijikuta kisima chetu kikishindwa kuwahudumia vya kutosha.
Serikali ya CCM wala Wabunge wake hawakuisukumiza serikali kuendeleza nishati ili kuzalisha zaidi na ziada kuweza kukidhi mahitaji ya viwanda vinavyobinafsishwa, vipya na vya uwekezaji.
Sera ya Kikwete ya Uwezekaji
Rais Kikwete alipoingia madarakani aliingia akiwa na credentials labda kuliko kiongozi mwingine yoyote nchini. Kati ya wizara nyeti nchini ni moja tu haikuishika yaani ile ya Ulinzi na JKT lakini kwa kuwa ni mmoja wa makamisaa wa zamani wa kijeshi naweza kusema hiyo pia ilikuwa ni sifa nyingine. Wizara alizoshikilia kabla ya Urais ni Wizara ya Maji, Nishati na Madini, Wizara ya Fedha, na Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje.
Sifa hizo zingemfanya kuwa kiongozi ambaye ana maono mapana ya kuelewa matatizo ya Watanzania na vile vile kuweza kuelewa baadhi ya masuluhisho. Alipoingia madarakani alitekeleza kile ambacho sisi wengine tumekibeza nacho nacho ni kutukuza wawekezaji. Ugomvi mkubwa kati yetu wakosoaji wake ni zile safari zake na mipango yake ya kualika wawekezaji wa nje kuja kuwekeza. Tatizo ni lile lile ambalo tunaliona kwenye sera ya ubinafsishaji ya Mkapa - wote wawili wakiwa ni wana CCM na wakiongoza Mabunge ya CCM na serikali ya CCM!
Kwa kualika na kufungulia mlango kwa wawekezaji wa kigeni nchini CCM na serikali yake imeongeza tatizo la nishati. Tukumbuke kuwa kanuni za fizikia zinafanya kazi. Kuongezeka kwa shughuli mbalimbali za kiuchumi za kawaida tu, na kuongezekana kwa viwanda na huduma nyingine mbalimbali kumesababisha ongezeko la mahitaji (demand) ya nishati nchini. Wengine wanasema kukua kwa uchumi ndio kumesababisha hali hii, naomba nitofautiane nao kiufundi tu - kwamba ni ongezeko la mahitaji ya nishati kutokana na sera za ubinafsishaji na uwekezaji zisizoendana na ongezeko la uzalishaji wa umeme ndio vimechangia sana tatizo la umeme la sasa.
Mfano mzuri wa kuelewa ni kushikilia rubber band kati ya vidole viwili - upande mmoja kuna uwekezaji mkubwa, upande wa pili kuna ubinafsishaji na makampuni ya ndani na katikati yake shughuli nyingine zote za uzalishaji mali. Kwa kadiri shughuli zinakua zinatanua mpira ule ambao unawakilisha uwezo wetu wa nishati. Ndugu zangu, rubber band unaweza kuitanua hadi kiasi kwamba kutanua zaidi kutasababisha ikatike. Ni jambo ambalo linaweza kuoneshwa kimahesabu (nitawaachia wengine kuweza kugundua ni kwa kiasi gani tunaweza kutanua uwezo wetu wa nishati kabla hatujashindwa). Ninaamini hali ya sasa imefikia mahali ambapo hatuwezi kutanua zaidi bila kusababisha matatizo kwenye uchumi.
Hivyo basi, tunaweza kusema pasipo shaka yoyote ile, tatizo la nishati nchini limetokana, kutengenezwa na kudumishwa kwa muda mrefu na kutotekelezwa kwa sera bora za nishati nchini. Na hili lote linarudisha mzigo kwanza kabisa kwa Chama cha Mapinduzi kwani ndicho kwa miaka hamsini kimeshikilia utawala wa nchi, na ndicho ambacho kimepanga safu yote ya viongozi wa kisiasa na kutoka kwao viongozi wa serikali nchini. Lakini pili, lawama zinawaendea moja kwa moja wabunge wote wa Chama cha Mapinduzi - siyo Ngeleja peke yake - kwa kushindwa kusimamia serikali na kutoa uongozi unaostahili kwenye suala la nishati. Wabunge ndio wanatunga sheria, ndio wanatenga bajeti na ndio wanasimamia serikali.
Inanishangaza kuona wabunge wa CCM wanakuja juu dhidi ya Ngeleja. Kama wangetaka kutatua tatizo la nishati wangeweza kufanya hivyo miaka ishirini iliyopita. Hata kesho wakitaka wanaweza kuondoa tatizo hili kwa kiasi kikubwa. Wabunge wa CCM na Chama chao hawana udhuru wala uwezo wa kukwepa lawama za moja kwa moja. Ngeleja katika hili ni ni punje tu ya mtama ghalani! Tatu, tukubaliane kuwa serikali imeshindwa kwa njia za kawaida kutatuta tatizo la nishati.
Hivyo basi, tunabakiwa na kile ambacho naweza kusema kutumia njia zisizo za kawaida kupata ufumbuzi wa muda wakati tunajiandaa na ufumbuzi wa muda mrefu. Kwenye Kiingereza wanasema desperate situation calls for desperate measures yaani wakati mgumu unahitaji hatua ngumu. Ndugu zangu, tatizo la nishati nchini linaweza kuondolewa kwa njia ya dharura ndani ya kati ya siku 30 na 60. Lakini hili litahitaji uongozi na uthubutu hasa wa wanasiasa wa CCM.
Hatua zifuatazo:
Hatua ya Haraka ya Muda Mfupi
Emergency Powers Act 1986
1. Huu ni Uamuzi wa Nyuklia (Nuclear Option) - ninachokiita uamuzi wa nyuklia sizungumzii matumizi ya nishati ya nyuklia bali uamuzi wa kikatiba wa kutangaza hali ya hatari chini ya Sheria ya Madaraka ya Rais wakati wa Dharura ya Mwaka 1986 (Emergency Powers Act). Hivyo, la kwanza kufanyika ni kwa wabunge kumtaka Rais Kikwete atangaze hali ya hatari/dharura nchini chini ya Ibara ya 32 ya Katiba. Rais akitangaza hali ya dharura nchini kutakuwa na matokeo mbalimbali ya kisheria na kiutendaji kwani yeye pekee atakuwa na madaraka ambayo mtu mwingine au chombo kingine chochote hakina.
2. Kutokana na hilo la 1 Rais Kikwete atakuwa mtu mwenye nguvu katika lile jambo aliloliamua yaani kushughulikia tatizo la nishati. Atakuwa na madaraka ya kusimamisha sheria na kanuni mbalimbali (suspending the law) na hivyo kuondoa haja ya kufanya mabadiliko ya sheria ya manunuzi ili kuruhusu mitambo iliyotumika kuingizwa nchini. Chini ya Ibara ya 18 ya Sheria ya Madaraka Wakati wa Dharura Rais ataweza kusimamisha sheria hiyo hadi tamko la hali ya dharura litakapoondolewa.
3. Rais akishatangaza hali ya hatari na kusimamisha sheria kadhaa au vipengele kadhaa vya sheria hususana kwenye jambo hili la nishati (katika hoja yetu sheria ya manunuzi ya Umma -PPA na hata sehemu ya sheria ya fedha) Rais ataweza kujadiliana moja kwa moja na watengenezaji wa majenereta na kuagiza kutoka kwao moja kwa moja bila kusubiri kamati, vikao au baraka za Bunge - Bunge bado lina uwezo wa kupitia uamuzi huo baadaye. Kwa kutangaza hali hiyo ya dharura siyo tangazo lisilo na nguvu la janga la kitaifa Rais atakuwa amejipa jukumu ambalo Watanzania wanatamani waone analichukua nalo ni kuondoa tatizo la nishati. Kwa kususpend sheria hii Rais anaweza kuunda timu maalum kumshauri - ufundi na bajeti - kuweza kupata dili nzuri bila kutumia kuwadi yeyote. Wabunge wanaweza wakatoa wito huo na Rais afanye uamuzi badala ya kukaa pembeni kama vile hausiki au kuwaachia wengine. Hili ni jukumu lake kubwa na la msingi wakati huu. Badala ya kwenda kuwaita wawekezaji atumie muda kutatua tatizo la nishati vinginevyo anajitahidi kutanua rubber band yetu halafu anakaa pembeni kuangalia itakatika vipi!
Hilo litaondoa tatizo la wakati huu kwani chini ya hicho nilichopendekeza tunaweza kuingiza majenereta ndani ya miezi miwili tu.
4. Chini ya Sheria hiyo hiyo ikifanyika wakati wa dharura Rais anaweza kunegotiate bei na hata kuamua bei ya kulipa mafuta kwa sababu ni hali ya hatari badala ya kulipa bei ya soko - kwa vyanzo vya ndani. Hili linawezekana chini ya Ibara ya 12:1 ya sheria hiyo.
Wanaposema kuwa wao ni watu wa utawala wa sheria wajue kuwa mojawapo ya sheria ni hiyo ya wakati wa dharura na ni maoni yangu ya muda mrefu kuwa Tanzania iko katika hali ya dharura na wakati umefika kwa Rais kuitangaza hivyo lakini akitanza hivyo analazimika kutumia madaraka yake ya kisheria ambayo yanamuangukia.
Hatua za Muda mrefu
Sasa tukishashughulikia hatua hizi za muda mfupi tunajikuta tunabakiwa na jukumu moja tu kubwa nalo ni kushughulikia tatizo la muda mrefu. Mapendekezo yangu ni kutupilia mbali kwa wakati huu miradi midogo midogo ya nishati. Hii miradi ya 100MW au 50MW ni kupoteza muda wa taifa hasa wakati huu. Miradi ya namna hiyo inatakiwa ije baadaye sana kama kuongezea mahitaji ya taifa na tunaweza kufanya wakati mzuri ziadi.
Sasa hivi tunahitaji kutenga fedha za kutosha kuanza mradi wa ujenzi wa Stielgers Gorge ambao sehemu yake ya kwanza inaweza kumalizika ikiwa na uwezo wa 500MW hivi. Ni kwa sababu hiyo wabunge wanaolalamikia nishati waamue baada ya kumtaka Rais afanye hayo ya hapo juu wao wenyewe watenge kuanzia kwenye bajeti hii fedha kwa ajili ya kuanza kwa mradi huu kwani hatua zote za awali zimeshafanyika.
picha toka VijanaFM
Kama kweli wabunge wa CCM wanauchungu na kwamba kweli wanataka hatimaye kujiokoa basi waamue - kwani wao ndio watunga sheria na ndio wanapanga fedha - kupeleka fedha zaidi kwa ajili ya kuanza kwa ujenzi wa mradi huu. Tukumbuka kuwa miaka mitano iliyopita ni Rais Kikwete aliyeahidi kwenye Bunge hilo hilo kuanza kwa mradi huu mkubwa ambao ungeweza kuzalisha zaidi MW 2000 za umeme na ukiongeza na vyanzo vilivyopo kuweza kujikuta tunazalisha umeme zaidi. Jukumu litakalobakia liwe la kusambaza zaidi na kuboresha zaidi mitambo na njia za umeme.
Wabunge badala ya kukubaliana kumlaumu Ngeleja, wakubaliane kumpa Ngeleja mzigo wa kuanza ujenzi wa Stielger Gorge kwa kushirikiana na RUBADA. Mradi huu umechelewa kwa miaka thelathini na wakati umefika kwa wabunge kuamua. Binafsi nashangaa kwanini wabunge wa upinzani hawasukumizi kuanza kwa mradi huo sasa hivi na nina uhakika wana CCM watawaunga mkono vile vile kwani vyama vyote vilikuwa na ajenda hiyo.
Mwisho
Ndugu zangu, nilichokisema ni kwamba tatizo la nishati nchini linatatulika na utatuzi wake hauitaji malaika kutoka mbinguni. Linaweza kutatuliwa kwa kuwepo kwa utashi wa kisiasa, uthubutu wa wabunge na ushiriki wa moja kwa moja wa Rais Kikwete. Badala ya kumsulubu Ngeleja na kumbana wabunge waamue kufanya kilicho ndani ya uwezo wao - wamtake Rais afanye sehemu yake (kwenye utatuzi wa muda mfupi) na wao wafanye kilicho sehemu yao.
Ni matumaini yangu kuwa Ngeleja atakapozungumza kujibu hoja mbalimbali za Wabunge atawaambia jambo hili kama kweli wanataka wanachokitaka waidhinishe fedha za kutosha ili mradi wa Stielgers Gorge uanze. Na katika kukubali huko wawe tayari kupunguza gharama nyingine za msingi ikiwemo posho, matumizi mengine ya anasa. Hapa ndio tutajua ni kina nani kweli wanataka tatizo la nishati liishe au liendelee. Wawe tayari kukatwa mishahara, posho na matumizi mengine ya anasa au yasiyo ya lazima ili Taifa liunganike pamoja kutatuta tatizo hili. Siyo wao peke yao bali na wananchi wote wawe tayari kukubali kutoa sadaka hiyo. Lakini, mfano lazima uanzie Bungeni!
Haitoshi kuzungumza kwa jazba!
Twende tupige hatua kubwa mbele - lets make the great step forward!
We too Can! - Nasi Tunaweza Pia!
Niandikie: mwanakijiji@jamiiforums.com
Utangulizi
Tatizo la upungufu wa nishati nchini linatafutiwa kisingizio. Naam, limetafutiwa kisingizio na kisingizio hicho kinazidi kukuzwa mbele ya macho yetu na kufanywa ndio sababu. Kwamba, hali ya upungufu wa nishati ya umeme nchini inatokana, imesababishwa, imeongezwa na kudumishwa na Waziri wa Nishati na Madini Bw. William Ngeleja. Hivyo - hitimisho linapendekezwa - kwamba Waziri Ngeleja awajibishwe na hata wengine wamefikia mahali pa kutaka baraza zima la mawaziri lijiuzulu.
Utetezi wangu huu una lengo moja nalo ni kutaka sababu ya tatizo la upungufu wa nishati nchini iwekwe wazi, ikubaliwe na iwajibishwe. Badala ya watu kuzunguka mbuyu na kuuimbia kama wanga, wasimame na kuungoa mbuyu huo. Utetezi huu haumhusu Ngeleja kama mtu - kwani sina ujamaa, undugu, au hata urafiki wa karibu - bali yeye kama Waziri mwenye dhamana ya Nishati na Madini. Kwamba, ninachosema na kupendekeza kwako msomaji ni kuwa wakosoaji wa Ngeleja wanataka kumkosoa na kumbembesha mzigo ambao mwenye kuustahili haugusi wala kuonesha anawajibika kwao.
Sitojaribu hata kidogo kuingia kwa undani kuchambua historia, sera mbalimbali au hata kuingia kufafanua mambo mengine mengi yanayohusiana na tatizo hili kwani ninayachukulia kwamba msomaji wangu atakuwa ana uelewa wa kutosha na anaweza kufanya mwenyewe utafiti kudogo kujibu maswali mbalimbali ambayo yanaweza kubakia katika fikra zake.
Ngeleja amekuta tatizo la umeme Tanzania.
Kwa mtu yeyote ambaye amewahi kuchukua muda kidogo kufanya utafiti wa hali ya nishati nchini na hususan nishati ya umeme atakuwa ametambua jambo moja dhahiri kuwa tatizo la nishati hiyo nchini halikuanza mwaka 2011. Naam, halikuanza mwaka 2005 au hat amwaka 2000. Ni tatizo ambalo kukua kwake kumekujalikana kwa karibu miaka ishirini sasa. Upungufu wa nishati ya umeme haujatokea nchini kama mvua ya jua kali ambayo inatokea bila kuwa na mawingu! Kweli, tatizo hili halijatokea kwa sababu kuna mtu alitupiga dawa ya usingizi taifa zima na tulipoamka tukakuta kuna upungufu wa umeme
Hadi tumefika mahali taifa zima tunapigishwa magoti mbele ya hali mbaya ya tatizo la nishati tujue kuwa imechukua karibu miaka 25 kufika hapa. Tumefikishwa hapa siyo na njama toka kuzimu bali kutokana na maamuzi mbalimbali na kati ya maamuzi hayo hakuna ambalo lilifanyika bila kujua hali ya umeme nchini.
Ninachopendekeza ni kuwa hatuwezi kutenganisha tatizo la nishati nchini leo hii, matokeo yake mabaya katika maisha ya kiuchumi ya taifa letumna athari zake za moja kwa moja katika kupiga hatua kubwa mbele (The Great Step Forward) ya maendeleo kwetu sisi wa kizazi hiki na uzao wetu huko mbeleni na uongozi wa sera na kisiasa pamoja na utawala wa Chama cha Mapinduzi. Kwamba, matatizo ya nishati nchini yana uhusiano wa moja kwa moja na sera pamoja na utekelezaji wa sera hizo katika miaka thelathini iliyopita. Naomba mniruhusu nipitie tu baadhi ya sera na miongozi ya kisiasa chini ya Chama cha Mapinduzi.
Mwongozo wa CCM wa 1981
Mwaka huu ni miaka thelathini ya mojawapo ya nyaraka muhimu za kisiasa nchini. Kama Azimio la Arusha lilipanga miaka ya sitini, na Siasa ni kilimo pamoja na Ujamaa vijijini vilipamba siasa za miaka ya sabini, naweza kusema kuwa Mwongozo wa CCM wa mwaka 1981 ulipamba sehemu kubwa ya nusu ya kwanza ya miaka hiyo. Ni nyaraka ambayo hata leo bado nguvu ya hoja zake inasimama.
Mwongozo ulisema hivi Suala la nishati ni la msingi kwa maendeleo ya Taifa letu. Pamoja na kuendelea kutafuta mafuta, Chama kitahakikisha kuwa serikali inazidisha mipango thabiti itakayoliwezesha Taifa kuanza kutumia nguvu za maji, makaa, upepo na jua. Pamoja na miradi mikubwa ya nguvu za maji kuna haja ya kutia maanani miradi midogo midogo ya nguvu za maji. Suala la kuni itabidi lipewe umuhimu mkubwa kwa kuwa na mipango kamambe ya kupanda miti vijijini na miradi ya Mikoa na Taifa. Chama kiihimize Serikali kuendelea na kutafuta mbinu za kutumia makaa ya mawe tuliyonayo kusukuma uchumi wetu. Umuhimu wa suala la nishati utahitaji sera maalum
Ni wazi kuwa haja ya kuendeleza vyanzo vya nishati si jambo ambalo limeanza wiki iliyopita Bungeni. Lina miaka thelathini chini ya watu wale wale, chama kile kile chenye sera zile zile. Inashangaza watu wanashangaa kukutana na matokeo yale yale.
Azimio la Zanzibar 1991
Kama kuna maamuzi ya kisiasa ambayo mrindimo wa mwangwi wake unaendelea kusikika hadi leo hii ni maamuzi ya Zanzibar ya mwaka 1991. Maamuzi yale yalibadilisha mwelekeo wa kiuchumi wa taifa letu na kwa namna moja au nyingine (nitawaacha wengine waamue hili) ulikoleza kuibuka kwa mgongano kati ya watawala na watawaliwa, na kuibuka kwa tabaka la kinyonyaji la mafisadi. Maamuzi ya Zanzibar hayakuanisha sana suala la haja ya kushughulikia tatizo la nishati. Yalihusu zaidi umiliki wa mali za uchumi na kulegeza masharti ya uongozi ikiwemo kutengeneza msingi wa ubinafsishaji wa mashirika ya umma ambao ulikuja kufanyiwa kazi sana na Rais Mkapa baadaye.
Sera ya Nishati ya 1992
Tukiwa njiani kutoka mfumo wa chama kimoja cha kisiasa kwenda vyama vingi na tukiwa chini ya uongozi wa chama hicho kimoja tuliandaliwa sera ya nishati ya taifa. Sera hii ilitolewa na Wizara ya Maji, Nishati na Madini ambayo wakati huo ilikuwa ikiongozwa na mmoja wa viongozi wasomi ambao walikuwa wameingia tu umri wa kati lakini mwenye sura na mvuto wa Ujana Jakaya Kikwete. Sera hiyo ya nishati ilisema mambo mengi lakini hakuna lolote mabalo linasemwa kwenye sera hilo ambalo laweza kuwa geni kwenye masikio ya Watanzania.
Sera hiyo ilitudokeza jinsi mpango wa Kufufua uchumi wa miaka ya themanini ulivyokuwa na malengo makubwa matano. Malengo yote matamu hayakuhusisha moja kwa moja kuongeza nishati kama njia ya kusisimua uchumi zaidi. Kwa kiasi kikubwa mipango yote ya wakati ule ilikuwa na lengo la kutimiza kile tulichokiita ruksa ambapo mikopo ya kigeni iliweza kuingia zaidi, uchumi kufunguliwa n.k. Chama cha Mapinduzi wakati huo hakikuweka msingi wa kuongeza uzalishaji wa nishati kama Mwongozo wa 1981 ulivyodokeza.
Kwa ufupi utawala wa Rais Mwinyi, japo unasifiwa kwa kufungua uchumi na kuwezesha vitu vingi kufurika kwenye maduka yetu (kufuatia uhaba wa bidhaa wa mwanzoni mwa miaka ya themanini) ulishindwa kulifanyia taifa jambo moja kubwa na la msingi kuliruhusu kuwa na uhuru wa kiuchumi. Hakukuwa na ruksa ya kuzalisha umeme na ziada. Chama cha Mapinduz hakikusimamia serikali yake wala kuisukuma kutekeleza sera ya uhuru wa nishati.
Sera ya Ubinafsishaji ya Mkapa
Rais Mkapa, alipoingia na uongozi wake hasa ngwe ya kwanza alisimamia na kusukumiza ubinafsishaji wa mashirika mbalimbali ya umma. Nimepitia juzi orodha ya makampuni mbalimbali (makubwa na madogo) ambayo yalikuwa yametaifishwa na seriakali wakati wa Mkapa hadi ilipofika mwaka 2003. Hadi Juni 2003, kulikuwa na mashirika 138 yaliyobinafsishwa kwa Watanzania kwa asilimia 100; mashirika 20 yaliyomilikishwa wageni kwa asilimia 100; na mashirika 42 kwenye ubia.
Mojawapo ya vitu vinavyonishangaza sana ni jinsi gani wataalamu wetu wa ubinafsishaji walivyopima hali ya nishati nchini kiasi cha kuweza kuuza makampuni mbalimbali ambayo walitarajia yangeweza kutengenezwa na kurudishwa katika uzalishaji karibu yote kwa wakati mmoja. Tukumbuke kuwa makampuni mengi yaliyokufa au kuwa na hali ngumu yalikuwa hayatumii nishati zaidi kama zamani. Kitendo cha kuyauza na kuhimiza kuyarudisha kwenye uzalishaji ni wazi kingesababisha ongezeko la mahitaji ya nishati ya umeme nchini.
Kosa kubwa ambalo lilitokea katika sera ya ubinafsiji hususan suala la nishati linapokuja ni kutokuendeleza vyanzo vya nishati kukidhi mahitaji ya makampuni ambayo yalikuwa yanarudishwa kwenye uzalishaji au yaliyokuwa yanaanza kuzalisha bidhaa nyingine na kujipanua zaidi. Najenga nadharia (ningependa kuwaachia wataalamu wetu kupima kama ina ukweli) kwamba sera ya ubinafsishaji iliyotukuzwa kwa mafanikio yake na Dr. Kigoda mwaka 2004 imechangia kwa kiasi chake kusababisha upungufu wa nishati. Kwamba kisima cha nishati kilichokuwepo kilitosha watu wachache waliokuwepo na hasa wazee wachache, lakini tulipopata mwamko wa kuleta wanafamilia, jamaa na marafiki kijijini tulijikuta kisima chetu kikishindwa kuwahudumia vya kutosha.
Serikali ya CCM wala Wabunge wake hawakuisukumiza serikali kuendeleza nishati ili kuzalisha zaidi na ziada kuweza kukidhi mahitaji ya viwanda vinavyobinafsishwa, vipya na vya uwekezaji.
Sera ya Kikwete ya Uwezekaji
Rais Kikwete alipoingia madarakani aliingia akiwa na credentials labda kuliko kiongozi mwingine yoyote nchini. Kati ya wizara nyeti nchini ni moja tu haikuishika yaani ile ya Ulinzi na JKT lakini kwa kuwa ni mmoja wa makamisaa wa zamani wa kijeshi naweza kusema hiyo pia ilikuwa ni sifa nyingine. Wizara alizoshikilia kabla ya Urais ni Wizara ya Maji, Nishati na Madini, Wizara ya Fedha, na Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje.
Sifa hizo zingemfanya kuwa kiongozi ambaye ana maono mapana ya kuelewa matatizo ya Watanzania na vile vile kuweza kuelewa baadhi ya masuluhisho. Alipoingia madarakani alitekeleza kile ambacho sisi wengine tumekibeza nacho nacho ni kutukuza wawekezaji. Ugomvi mkubwa kati yetu wakosoaji wake ni zile safari zake na mipango yake ya kualika wawekezaji wa nje kuja kuwekeza. Tatizo ni lile lile ambalo tunaliona kwenye sera ya ubinafsishaji ya Mkapa - wote wawili wakiwa ni wana CCM na wakiongoza Mabunge ya CCM na serikali ya CCM!
Kwa kualika na kufungulia mlango kwa wawekezaji wa kigeni nchini CCM na serikali yake imeongeza tatizo la nishati. Tukumbuke kuwa kanuni za fizikia zinafanya kazi. Kuongezeka kwa shughuli mbalimbali za kiuchumi za kawaida tu, na kuongezekana kwa viwanda na huduma nyingine mbalimbali kumesababisha ongezeko la mahitaji (demand) ya nishati nchini. Wengine wanasema kukua kwa uchumi ndio kumesababisha hali hii, naomba nitofautiane nao kiufundi tu - kwamba ni ongezeko la mahitaji ya nishati kutokana na sera za ubinafsishaji na uwekezaji zisizoendana na ongezeko la uzalishaji wa umeme ndio vimechangia sana tatizo la umeme la sasa.
Mfano mzuri wa kuelewa ni kushikilia rubber band kati ya vidole viwili - upande mmoja kuna uwekezaji mkubwa, upande wa pili kuna ubinafsishaji na makampuni ya ndani na katikati yake shughuli nyingine zote za uzalishaji mali. Kwa kadiri shughuli zinakua zinatanua mpira ule ambao unawakilisha uwezo wetu wa nishati. Ndugu zangu, rubber band unaweza kuitanua hadi kiasi kwamba kutanua zaidi kutasababisha ikatike. Ni jambo ambalo linaweza kuoneshwa kimahesabu (nitawaachia wengine kuweza kugundua ni kwa kiasi gani tunaweza kutanua uwezo wetu wa nishati kabla hatujashindwa). Ninaamini hali ya sasa imefikia mahali ambapo hatuwezi kutanua zaidi bila kusababisha matatizo kwenye uchumi.
Hivyo basi, tunaweza kusema pasipo shaka yoyote ile, tatizo la nishati nchini limetokana, kutengenezwa na kudumishwa kwa muda mrefu na kutotekelezwa kwa sera bora za nishati nchini. Na hili lote linarudisha mzigo kwanza kabisa kwa Chama cha Mapinduzi kwani ndicho kwa miaka hamsini kimeshikilia utawala wa nchi, na ndicho ambacho kimepanga safu yote ya viongozi wa kisiasa na kutoka kwao viongozi wa serikali nchini. Lakini pili, lawama zinawaendea moja kwa moja wabunge wote wa Chama cha Mapinduzi - siyo Ngeleja peke yake - kwa kushindwa kusimamia serikali na kutoa uongozi unaostahili kwenye suala la nishati. Wabunge ndio wanatunga sheria, ndio wanatenga bajeti na ndio wanasimamia serikali.
Inanishangaza kuona wabunge wa CCM wanakuja juu dhidi ya Ngeleja. Kama wangetaka kutatua tatizo la nishati wangeweza kufanya hivyo miaka ishirini iliyopita. Hata kesho wakitaka wanaweza kuondoa tatizo hili kwa kiasi kikubwa. Wabunge wa CCM na Chama chao hawana udhuru wala uwezo wa kukwepa lawama za moja kwa moja. Ngeleja katika hili ni ni punje tu ya mtama ghalani! Tatu, tukubaliane kuwa serikali imeshindwa kwa njia za kawaida kutatuta tatizo la nishati.
Hivyo basi, tunabakiwa na kile ambacho naweza kusema kutumia njia zisizo za kawaida kupata ufumbuzi wa muda wakati tunajiandaa na ufumbuzi wa muda mrefu. Kwenye Kiingereza wanasema desperate situation calls for desperate measures yaani wakati mgumu unahitaji hatua ngumu. Ndugu zangu, tatizo la nishati nchini linaweza kuondolewa kwa njia ya dharura ndani ya kati ya siku 30 na 60. Lakini hili litahitaji uongozi na uthubutu hasa wa wanasiasa wa CCM.
Hatua zifuatazo:
Hatua ya Haraka ya Muda Mfupi
Emergency Powers Act 1986
1. Huu ni Uamuzi wa Nyuklia (Nuclear Option) - ninachokiita uamuzi wa nyuklia sizungumzii matumizi ya nishati ya nyuklia bali uamuzi wa kikatiba wa kutangaza hali ya hatari chini ya Sheria ya Madaraka ya Rais wakati wa Dharura ya Mwaka 1986 (Emergency Powers Act). Hivyo, la kwanza kufanyika ni kwa wabunge kumtaka Rais Kikwete atangaze hali ya hatari/dharura nchini chini ya Ibara ya 32 ya Katiba. Rais akitangaza hali ya dharura nchini kutakuwa na matokeo mbalimbali ya kisheria na kiutendaji kwani yeye pekee atakuwa na madaraka ambayo mtu mwingine au chombo kingine chochote hakina.
2. Kutokana na hilo la 1 Rais Kikwete atakuwa mtu mwenye nguvu katika lile jambo aliloliamua yaani kushughulikia tatizo la nishati. Atakuwa na madaraka ya kusimamisha sheria na kanuni mbalimbali (suspending the law) na hivyo kuondoa haja ya kufanya mabadiliko ya sheria ya manunuzi ili kuruhusu mitambo iliyotumika kuingizwa nchini. Chini ya Ibara ya 18 ya Sheria ya Madaraka Wakati wa Dharura Rais ataweza kusimamisha sheria hiyo hadi tamko la hali ya dharura litakapoondolewa.
3. Rais akishatangaza hali ya hatari na kusimamisha sheria kadhaa au vipengele kadhaa vya sheria hususana kwenye jambo hili la nishati (katika hoja yetu sheria ya manunuzi ya Umma -PPA na hata sehemu ya sheria ya fedha) Rais ataweza kujadiliana moja kwa moja na watengenezaji wa majenereta na kuagiza kutoka kwao moja kwa moja bila kusubiri kamati, vikao au baraka za Bunge - Bunge bado lina uwezo wa kupitia uamuzi huo baadaye. Kwa kutangaza hali hiyo ya dharura siyo tangazo lisilo na nguvu la janga la kitaifa Rais atakuwa amejipa jukumu ambalo Watanzania wanatamani waone analichukua nalo ni kuondoa tatizo la nishati. Kwa kususpend sheria hii Rais anaweza kuunda timu maalum kumshauri - ufundi na bajeti - kuweza kupata dili nzuri bila kutumia kuwadi yeyote. Wabunge wanaweza wakatoa wito huo na Rais afanye uamuzi badala ya kukaa pembeni kama vile hausiki au kuwaachia wengine. Hili ni jukumu lake kubwa na la msingi wakati huu. Badala ya kwenda kuwaita wawekezaji atumie muda kutatua tatizo la nishati vinginevyo anajitahidi kutanua rubber band yetu halafu anakaa pembeni kuangalia itakatika vipi!
Hilo litaondoa tatizo la wakati huu kwani chini ya hicho nilichopendekeza tunaweza kuingiza majenereta ndani ya miezi miwili tu.
4. Chini ya Sheria hiyo hiyo ikifanyika wakati wa dharura Rais anaweza kunegotiate bei na hata kuamua bei ya kulipa mafuta kwa sababu ni hali ya hatari badala ya kulipa bei ya soko - kwa vyanzo vya ndani. Hili linawezekana chini ya Ibara ya 12:1 ya sheria hiyo.
Wanaposema kuwa wao ni watu wa utawala wa sheria wajue kuwa mojawapo ya sheria ni hiyo ya wakati wa dharura na ni maoni yangu ya muda mrefu kuwa Tanzania iko katika hali ya dharura na wakati umefika kwa Rais kuitangaza hivyo lakini akitanza hivyo analazimika kutumia madaraka yake ya kisheria ambayo yanamuangukia.
Hatua za Muda mrefu
Sasa tukishashughulikia hatua hizi za muda mfupi tunajikuta tunabakiwa na jukumu moja tu kubwa nalo ni kushughulikia tatizo la muda mrefu. Mapendekezo yangu ni kutupilia mbali kwa wakati huu miradi midogo midogo ya nishati. Hii miradi ya 100MW au 50MW ni kupoteza muda wa taifa hasa wakati huu. Miradi ya namna hiyo inatakiwa ije baadaye sana kama kuongezea mahitaji ya taifa na tunaweza kufanya wakati mzuri ziadi.
Sasa hivi tunahitaji kutenga fedha za kutosha kuanza mradi wa ujenzi wa Stielgers Gorge ambao sehemu yake ya kwanza inaweza kumalizika ikiwa na uwezo wa 500MW hivi. Ni kwa sababu hiyo wabunge wanaolalamikia nishati waamue baada ya kumtaka Rais afanye hayo ya hapo juu wao wenyewe watenge kuanzia kwenye bajeti hii fedha kwa ajili ya kuanza kwa mradi huu kwani hatua zote za awali zimeshafanyika.
picha toka VijanaFM
Kama kweli wabunge wa CCM wanauchungu na kwamba kweli wanataka hatimaye kujiokoa basi waamue - kwani wao ndio watunga sheria na ndio wanapanga fedha - kupeleka fedha zaidi kwa ajili ya kuanza kwa ujenzi wa mradi huu. Tukumbuka kuwa miaka mitano iliyopita ni Rais Kikwete aliyeahidi kwenye Bunge hilo hilo kuanza kwa mradi huu mkubwa ambao ungeweza kuzalisha zaidi MW 2000 za umeme na ukiongeza na vyanzo vilivyopo kuweza kujikuta tunazalisha umeme zaidi. Jukumu litakalobakia liwe la kusambaza zaidi na kuboresha zaidi mitambo na njia za umeme.
Wabunge badala ya kukubaliana kumlaumu Ngeleja, wakubaliane kumpa Ngeleja mzigo wa kuanza ujenzi wa Stielger Gorge kwa kushirikiana na RUBADA. Mradi huu umechelewa kwa miaka thelathini na wakati umefika kwa wabunge kuamua. Binafsi nashangaa kwanini wabunge wa upinzani hawasukumizi kuanza kwa mradi huo sasa hivi na nina uhakika wana CCM watawaunga mkono vile vile kwani vyama vyote vilikuwa na ajenda hiyo.
Mwisho
Ndugu zangu, nilichokisema ni kwamba tatizo la nishati nchini linatatulika na utatuzi wake hauitaji malaika kutoka mbinguni. Linaweza kutatuliwa kwa kuwepo kwa utashi wa kisiasa, uthubutu wa wabunge na ushiriki wa moja kwa moja wa Rais Kikwete. Badala ya kumsulubu Ngeleja na kumbana wabunge waamue kufanya kilicho ndani ya uwezo wao - wamtake Rais afanye sehemu yake (kwenye utatuzi wa muda mfupi) na wao wafanye kilicho sehemu yao.
Ni matumaini yangu kuwa Ngeleja atakapozungumza kujibu hoja mbalimbali za Wabunge atawaambia jambo hili kama kweli wanataka wanachokitaka waidhinishe fedha za kutosha ili mradi wa Stielgers Gorge uanze. Na katika kukubali huko wawe tayari kupunguza gharama nyingine za msingi ikiwemo posho, matumizi mengine ya anasa. Hapa ndio tutajua ni kina nani kweli wanataka tatizo la nishati liishe au liendelee. Wawe tayari kukatwa mishahara, posho na matumizi mengine ya anasa au yasiyo ya lazima ili Taifa liunganike pamoja kutatuta tatizo hili. Siyo wao peke yao bali na wananchi wote wawe tayari kukubali kutoa sadaka hiyo. Lakini, mfano lazima uanzie Bungeni!
Haitoshi kuzungumza kwa jazba!
Twende tupige hatua kubwa mbele - lets make the great step forward!
We too Can! - Nasi Tunaweza Pia!
Niandikie: mwanakijiji@jamiiforums.com