KAMWE, KWAMWE, KAMWE, usikae ufikirie kwenda kutafuta uchawi ili kutajirika. Ni ujinga mtupu. Hata ukipata pesa nyingi saaaana, unadhani utabadilika nini? Kitanda utalala kimoja tu, hata ukila chakula kitamu kuliko vyote, bado ukishashiba huwezi kuendelea kula tena. Na chote kitatoka baada ya masaa kadhaa. Hata ukimchukua mwanamke unayemwona ndio bora kuliko wote, utakuwa tu sawa na mtu mwingine yeyote aliye na mwanamke anayempenda. Hata ukinunua magari kumi ya bei mbaya, bado utaendesha moja tu kwa wakati mmoja. Ukijenga majumba lukuki, watalala wengine.
Sana sana , tafuta tu kipato ujenge nyumba, usomeshe watoto, uwe na kausafiri kako kanakoridhisha, na wewe na familia yako muwe mnavaa vizuri na kula vizuri. Zaidi ya hapo ni UBATILI TU.