Utajiri wa kufa na kuoza ndio pesa ije

Utajiri wa kufa na kuoza ndio pesa ije

Ni aina mojawapo ya uchawi wa kupata utajiri ukiacha huu wa ;
kuua ndugu
Kuwafanya wanafamilia ndondocha
Kuwekwa kidonda mwilini
Kupewa masharti ya chakula nguo na magari nk nk
Huu una mambo yake ya ajabu, unapewa dawa ambayo utamshirikisha mkeo tuu....ukishakunywa hiyo dawa unakufa na kuoza kabisa mpaka kutoa funza wengi
Sasa mkeo kazi yake kila siku itabidi awafagie hao funza na kuwaweka kwenye ndio kwa mpaka siku ya saba utakapofufuka..... utajiri wako utategemea na wingi wa funza watakaokusanywa kwa siku
Ukishamaliza siku Saba utafufuka na biashara zako zitaanza kuchanganya
Onyo na tahadhari
-hutakiwi kuwa na mwanamke mwingine
-mkeo hapaswi kushtuka mara ya kwanza akiwaona funza utakufa moja kwa moja
-so wewe wala mkeo mnapaswa kutoa siri hii kwa yeyote hata chini ya mtutu wa bunduki
-Ishu ya kufa wiki nzima na kuoza utaifanya kila biashara zinapoyumba
Kama bado unataka utajiri kwa njia za mkato fikiria mara mbili kabla hujamua
Acha hizo!
Kuwaingiza watu kwenye utumwa wa kishirikina.
Halafu watu wakixipata hixo hela wanaishije, kama wanyama wa kufugwa tu.
Mtumainie Yesu kwa mafanikio mema!
 
pambeetyu:Kweli kabisa kiongozi hizimambo zisie tu! kwa watu unaweza kuwa na miji pesa alafu ukawa hauwezi kufaa unacho penda , kula unacho penda , kunywa ukitakacho nk sasa ndio ujiulize pesa hizo nizanini sibora ukapuku kuliko kuwa na pesa usizo zifurahiya.
 
Hiyo ya kuku na punje za mahindi ipoje,,naomba unijuze great thinker
Nilihadithiwa unaenda kwa mganga then usiku mnatoka na mganga ameshika kuku ww umeshika punje za mahindi katika mikono yako unamwaga uwanjani kuku anakula. Punje atakazo kula ndio urefu wa maisha yako ie akila 10 unakaa miaka 10 ya utajiri wa kutupwa etc
Naskia kwa wakinga iko common sana
 
Back
Top Bottom