Utajiri wa kufa na kuoza ndio pesa ije

Utajiri wa kufa na kuoza ndio pesa ije

KAMWE, KWAMWE, KAMWE, usikae ufikirie kwenda kutafuta uchawi ili kutajirika. Ni ujinga mtupu. Hata ukipata pesa nyingi saaaana, unadhani utabadilika nini? Kitanda utalala kimoja tu, hata ukila chakula kitamu kuliko vyote, bado ukishashiba huwezi kuendelea kula tena. Na chote kitatoka baada ya masaa kadhaa. Hata ukimchukua mwanamke unayemwona ndio bora kuliko wote, utakuwa tu sawa na mtu mwingine yeyote aliye na mwanamke anayempenda. Hata ukinunua magari kumi ya bei mbaya, bado utaendesha moja tu kwa wakati mmoja. Ukijenga majumba lukuki, watalala wengine.

Sana sana , tafuta tu kipato ujenge nyumba, usomeshe watoto, uwe na kausafiri kako kanakoridhisha, na wewe na familia yako muwe mnavaa vizuri na kula vizuri. Zaidi ya hapo ni UBATILI TU.
Daah, ni heri kufa maskini kuliko kufanya huo ujinga, ila nmegundua kitu kimoja, ukishaanza kufanya hayo hutakiwi kuacha na hilo ni sharti, baada ya kufanya starehe zote watu wa namna hiyo hutamani kuacha ili wawe huru kama wengne, mana huona hamna kitu cha ziada, wanawake ni wale wale, majumba ni yaleyale, magari ni yaleyale, ulaya ni ileile, tatizo linakuja gharama ya kuacha ni maisha yao, hvyo huamua kusonga mbele huku wakiwa na stress sana,
Uhuru aliotupatia Mungu ni wa thamani sana, ni ujinga wa hali ya juu kuuza uhuru ulio nao, nina hakika kabisa mtu ukipambana mtaani huwez kosa hela ya kula, kujenga nyumba nzuri, Kuvaa vizuri, kupata usafir, kusomesha watoto, japo utakuwa unahangaika lakni huwez kukosa....zaidi ya hapo ni majaaliwa, hakuna haja ya kuforce mpak unauza utu wako aisee
 
Utajiri wa aina hii upo Njombe,mbeya,iringa kwa 90% kuna mganga maarufu mwandulami ndio anaetoa hii
DASM
instanbul
idawa

Mimi nipo Njombe na hapa ndio nasikia hii habari, nani Njombe ambaye ana utajiri huu? Anyway, kuna tetesi nyingi za wakinga kufanya hivi lakini usi-generalize kuwa ni Njombe, Njombe kuwa wapangwa, Wabena na wahehe pia na biashara zao ni za kawaida na zinaonekana!
 
Kufa mpaka uoze na utoke funza inamaana ushapotea.
sasa huko kufufuka kinakuwa ni kitu kingine yaani ni kama wewe lakini si wewe.
Umewaza vyema kuna kaukweli fulani! Nadhani wake za hao waume wangetupa ushuhuda baada ya kufufuka waume zao kuna badiliko lolote?
 
Kuna utajir upo hv niliambiwa na bibi, yani unakwenda kwa mganga afu zinatupwa punje za mtama. Jogoo atafunguliwa kama akila punje 100 bhs utaish miaka 100 then utakufa au akila 5 bhs miaka ako mitano inakuhusu[emoji23][emoji23]. Ila hakuna mashart mengine, mashart ni ww na kuku tu
 
Back
Top Bottom