Utajiri wa kufa na kuoza ndio pesa ije

Utajiri wa kufa na kuoza ndio pesa ije

Loooh kweli pesa ilimuua hadi Yesu hapana kwa kweli. Sasa mwanamke akitaka huu uchawi anamwambia mumewe? Na kama mtu upo single sijui utamwambia nani aje apanguse funza looh
 
Ni aina mojawapo ya uchawi wa kupata utajiri ukiacha huu wa ;
kuua ndugu
Kuwafanya wanafamilia ndondocha
Kuwekwa kidonda mwilini
Kupewa masharti ya chakula nguo na magari nk nk
Huu una mambo yake ya ajabu, unapewa dawa ambayo utamshirikisha mkeo tuu....ukishakunywa hiyo dawa unakufa na kuoza kabisa mpaka kutoa funza wengi
Sasa mkeo kazi yake kila siku itabidi awafagie hao funza na kuwaweka kwenye ndio kwa mpaka siku ya saba utakapofufuka..... utajiri wako utategemea na wingi wa funza watakaokusanywa kwa siku
Ukishamaliza siku Saba utafufuka na biashara zako zitaanza kuchanganya
Onyo na tahadhari
-hutakiwi kuwa na mwanamke mwingine
-mkeo hapaswi kushtuka mara ya kwanza akiwaona funza utakufa moja kwa moja
-so wewe wala mkeo mnapaswa kutoa siri hii kwa yeyote hata chini ya mtutu wa bunduki
-Ishu ya kufa wiki nzima na kuoza utaifanya kila biashara zinapoyumba
Kama bado unataka utajiri kwa njia za mkato fikiria mara mbili kabla hujamua
Sasa kama masharti ni kutokuwa na mwanamke zaidi ya mmoja, na itakuwa vipi mkeo bahati nzuri au mbaya kafariki? hahahaha
 
nina jamaa namjua tajiri ila aliupata ghafla, barazani kwake kwa juu kuna nyuki wamjenga kinyumba na wanang'ata watoto wake hata wageni lakini hata haahangaiki kuwatoa, ni uchawi gani huo?
Uchawi wa wadudu wengine ni kunguni siafu mende mchwa inzi ndorobo nk, unakuta nyumba nzuri safi kweli lakini haikosi mojawapo ya hizo viumbe tena kwa wingi
 
Tatizo wabongo wakishapata huyo utajiri wanawaza ngono tu,ina mana lazima sharti watavunja!!!I'd rather stay broke for the rest of my life[emoji24] [emoji24] [emoji24]
 
Siyo kwenda na kuku ila utamkuta hukohuko kwa mtaalamu si wote wanamudu hizi mambo ina bidi uwe na roho ngumu kama chuma..ndomana waganga wengi huwa wanawajaribu wateja wao kabla ya kuwapa masharti kuona kama wana mudu au laah!
Ingekuwa unaenda nae, me namfungia wiki bila msosi akifika kule lazima adonoe hata mahindi 200 mkuu
 
Kwa huyu mke wangu ninavyomjua mmmmh acha tu tufe na umasikini, kama akiona nanhii tu amabayo kila siku anaiona hushtuka hao funza si ndo atashtuka na kudhirai kabisa na mm nisiuone ugali tembele teeena
Funguka mbona umejibana akiona nini?kiukweli hayo mambo yapo ila hayafai coz huna raha na tatizo kila siku masharti yanabadilika ndo inafika huko mara ujamiiane na nduguyo na damu kama wakienda mbele basi bimkubwa hapo pana nini tena?
 
Mwaka2001 Nina Jamaa Yangu Wa Karibu Alikufa Kwa UKIMWI Lakn Historia Ya Mareheumu Ilisema Kafa Kwa Saratani Ya Utumbo.
Mungu anisamehe ila mwaka 2013 kaka yangu alifariki kwa ukimwi lakini Mimi msoma hotuba nikasema mbele ya umati wa watu kwamba amefariki kwa pneumonia na maradhi ya tumbo...hivyo wengi kusema Pepe kafariki kwa shinikizo la moyo ni sahihi kwani kwa wadhifa wake wasingeweza kusema amefariki kwa mambo ya kishirikina...
 
Mungu anisamehe ila mwaka 2013 kaka yangu alifariki kwa ukimwi lakini Mimi msoma hotuba nikasema mbele ya umati wa watu kwamba amefariki kwa pneumonia na maradhi ya tumbo...hivyo wengi kusema Pepe kafariki kwa shinikizo la moyo ni sahihi kwani kwa wadhifa wake wasingeweza kusema amefariki kwa mambo ya kishirikina...
[emoji3] [emoji3] [emoji3] [emoji3] [emoji3] Yani Kama Mi Ningekuwa Mungu Nisingekusamehe Hata Kidogo [emoji3] [emoji3] [emoji3]
 
Back
Top Bottom