Yani mtu anayejua fizikia kuliko wewe anakwambia hapa juu sana huwezi kuruka ukabaki salama, halafu wewe ambaye hujui fizikia vizuri umbishie ukatae kujifunza ukweli kwa sababu hutaki kuwa mdogo?
Kuna sehemu unatakiwa kukubali kuwa mdogo, ujifunze.
Na kukataa kuwa mdogo kwa confidence tu hata kama hauko sawa, kunaweza kukuua.
Kiongozi uko sahihi kabisa, unatembea sambamba na maandiko...
Luka 6:40: "Mwanafunzi hawezi kuwa mkubwa kuliko mwalimu wake, lakini kila mwanafunzi aliyekamilika atakuwa kama mwalimu wake."
Kuukataa ukweli au uhalisia ni kiburi na upumbavu, hata sio ujinga ( not even foolishness Sir).
Kwa mtizamo wangu, hapa tatizo kubwa ni ile hali ya unyonge na kujiona duni.
Kwenye mfano wako, ntakua zaidi ya juha kugoma kuelekezwa na mtu kitu ambacho sikijui kwa ukaidi kwamba naelewa. Natakiwa kuwa mpole ili niweze kujifunza.
Hapa ni ile kuifanya potential yako kuwa haiwezi, unaniambia bwana mdogo Monk njoo nikupe kipindi hapa uelewe mambo ya stock na uwekezaji yanavyoenda, mue hapo ndani najiona siwezi na aibu kwamba kwanini sifahamu kama wewe, napoteza ujasiri hata wa kuwa na shauku ya kujifunza, naanza dharau au kupingana na ukweli kwamba nikiwa mtulivu ukanipiga kipindi, ntaelimika na kuongeza kitu.
Mwalimu ana mchango mkubwa katika kuumba mtazamo na maisha ya mwanafunzi, hivyo kujifunza kunahitaji unyenyekevu na utii.
Mfano hai ni mimi ambavyo nimekua nikisema mara kwa mara kwamba, kuna vitu vingi nimejifunza kwako.