Usikubali kufanywa mdogo na yeyote

Usikubali kufanywa mdogo na yeyote

ShesRise_1

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2025
Posts
18,058
Reaction score
42,755
Kwa dunia ya sasa, nadhani si mwanaume wala mwanamke asiyeweza kujua ni kitu gani anachohitaji
Nadhani kila mtu anajua thamani yake

Huwa nashangaa sana ninapoona mtu akitumia nguvu kubwa kumfanya mtu mwingine ajihisi au ajione mdogo

Na kisha huyo mtu anakubali kabisa na kuanza kujiona mdogo na kujishusha thamani

Mbinu hii ya kutaka kuwafanya wengine wajihisi wadogo hutumiwa na watu wadogo wanapotaka kuweka mizani sawa

Huna haja ya kukubali hizi mbinu zisizo na maana yeyote

Ni ukweli usiopingika kwamba duniani tupo katika viwango tofauti sana
Kuna watu walio kwenye high level, kuna walio kwenye low level, na kuna walio kwenye average level

Lakini licha ya yote hayo, confidence inaweza kumbeba sana mtu

Yes hata ukiwa mtu wa kiwango cha chini kiasi gani
Ukiwa na confidence unaweza kufanya vingi na vitu postitive
Unaweza kuitwa kwenye interview, ukaweza kujieleza vizuri bila hofu na ukafaulu

Unaweza kuanzisha biashara ndogo na ukafanikiwa

Watu wanasema bila pesa huwezi kuwa na confidence
Mimi hilo sioni kuwa ni kweli, au kama kuna ukweli ndani yake, basi ni mdogo sana

Ukiwa na confidence, uwezekano wa kuzipata pesa unakuwa mkubwa pia


Watu waoga waoga huwa wanachukua muda mrefu sana kufikia malengo au wasifikie kabisa matamanio yao

Ujumbe wangu wa leo ni huu:
No matter what, huna haja ya kukubali kufanywa mdogo na yeyote

Hasa sisi wanawake, huna haja ya kujiona wa kawaida
Na hii si kiburi wala jeuri ni moja ya njia za kujiwekea kiwango na mipaka ambayo si kila mtu anaweza kuvuka

Mimi : ShesRise_1
hupendelea kusema:👇

Mimi si wa kawaida, ila wewe unaponitazama mimi na ukaniona wakawaida
wewe ndiyo wa kawaida sana kiasi kwamba huwezi kuona viwango vyangu.

Wewe mdau umewahi kujihisi mdogo?
Nini kili rudisha confidence yako?

ShesRise_1 🤚
 
Sawa
downloadfile-10.png
 
Hakika mkuu hakika anguko la mtu huanza tu punde anapoamua kujidogosha mwenyewe
Methali 23:7 inasema: "Maana aonavyo nafsini mwake, ndivyo alivyo."

Pia imeandikwa katika Hesabu 13:33

"Kisha huko tuliwaona Wanefili, wana wa Anaki, waliotoka kwa hao Wanefili; tukajiona nafsi zetu kuwa kama mapanzi, nao ndivyo walivyotutazama."

Mtazamo na mawazo unayoyahifadhi moyoni mwako ndiyo yanayotengeneza uhalisia wa maisha yako na jinsi unavyojiweka mbele za watu au kukabiliana na changamoto.
 
Back
Top Bottom