Ushauri wenu juu ya siri hii inayonitesa kwa muda mrefu

Huwezi kuepuka madhara..ingawa ukweli utakuweka huru, ongea na wazazi wako.
mimi kama mimi itakua ngum kuwaambia labda nitumie wazee wenye busara wawaanzie mbali kabla yakuwaambia chochote.
 
nyege....hazijawahi kumuacha mtu salama...nina amini unajuta sana hapo ulipo...ila usisahau kuwa maji umeshayavulia nguo hayo
najuta sana mkuu bt kinachoniumiza sana nawaza mwisho wa jambo hili utakuwaje, maana shangazi anaweza kasirika na kutoa maneno mbovu kwa kusema "umediriki kunilala ukavunja miiko yetu" na hapo ndo timbwili litaanzia pia hofu nyingine inatokana na vile mashngaz wengi wakiwa na vinyongo anaweza kukulaani kimya kimya na hapa ndo nadata kabisa mkuu.
 
Mpaka wamempatia mwanao jina lako maana yake walijua na wakakutangulia mbele kifikra maana waliona mbali sana kuliko wewe

Maisha yako hivi; pale mtaani unako ishi unaweza ukaibiwa TV yako nzuri na kubwa mchana kweupe kabisa na ukalalamika kila ukiuliza utaambiwa hakuna alie muona mwizi

Likini usiku ukaingiza mke wa mtu kwako na mkafanya yenu watu watajua tu maana wanasema hata majani yanaona
 
Mpaka wamempatia mwanao jina lako maana yake walijua na wakakutangulia mbele kifikra maana waliona mbali sana kuliko wewe

Maisha yako hivi; pale mtaani unako ishi unaweza ukaibiwa TV yako nzuri na kubwa mchana kweupe kabisa na ukalalamika kila ukiuliza utaambiwa hakuna alie muona mwizi

Likini usiku ukaingiza mke wa mtu kwako na mkafanya yenu watu watajua tu maana wanasema hata majani yanaona
kwa navyowajua wale wazee wangeshajua wangeshakisanua zamani mkuu
 
[SUP]Waliompa jina lako wanajua wewe ndo Baba wana Ku enjoy tu[/SUP]
wazee wale ni watata sana mkuu laiti wangejua ingeshakua noma, jambo hili halinitesi mimi pekee bt hata binam pia hua tunajiwazia mambo yakijulikana tutaweka wapi nyuso zetu mbele za wana ukoo?
 
Nawaza tu mfano huyo mtoto aje kulana na mwanao wapeane na mimba pia maana si anajua we ni mjomba hivyo atajua ni binamu yake,,

Bora tu ijulikane we ni baba,sawa itakuwa aibu ila mwisho wa siku watazoea na wewe utazoea tu maisha mengine yataendelea
 
Imagine kuna ndugu yako humu kasoma hii siri yako anaunga madoti tu sasa hivi
ukiwaza negatively ni ngum sana kusaidika mkuu, huku kidogo kuna uficho na nirahisi kusaidika, kama kuna ndugu basi itakua emergency isiyoepukika.
 
Tafuta hela mkuu,
Tembeza hela kwa watata wote wa familia,jifanye mwema sana kwao,wape misaada ya nguvu,fanya hivi kwa miezi kama 3 mpaka 6 kisha mwaga siri kwa gia ya kuomba msamaha na kutubia,

Mwenye hela hua hanuniwi hata siku moja.
 
Nawaza tu mfano huyo mtoto aje kulana na mwanao wapeane na mimba pia maana si anajua we ni mjomba hivyo atajua ni binamu yake,,

Bora tu ijulikane we ni baba,sawa itakuwa aibu ila mwisho wa siku watazoea na wewe utazoea tu maisha mengine yataendelea
nitafanyia kazi ushauri wenu na nitaleta mrejesho.
 
Chukuwa mtoto,,mlee kwa kisingizio cha kupewa jina lako,,na kumsaidia ulezi hyo binamu yako,,mwisho wa siku utakuwa kama baba mlezi...sababu baba ni wewe..hakuna wala hatotokea mwengine ..
 
Tafuta hela mkuu,
Tembeza hela kwa watata wote wa familia,jifanye mwema sana kwao,wape misaada ya nguvu,fanya hivi kwa miezi kama 3 mpaka 6 kisha mwaga siri kwa gia ya kuomba msamaha na kutubia,

Mwenye hela hua hanuniwi hata siku moja.
kuna ushauri huu nilipewa je unafaa? niliambiwa niitishe kikao cha familia yangu nikiwa na wazee wengine hata wa 3 then niwaeleze then wakipanic wale wazee ndo wasawazishe mambo.
je, naweza tumia njia hiyo ikafaa?
 
kuna ushauri huu nilipewa je unafaa? niliambiwa niitishe kikao cha familia yangu nikiwa na wazee wengine hata wa 3 then niwaeleze then wakipanic wale wazee ndo wasawazishe mambo.
je, naweza tumia njia hiyo ikafaa?
Kabla ya kufanya kikao chochote hakikisha unatengeneza mazingira mazuri kwanza,ndio maana nikakwambia mwaga fedha ili kujitengenezea njia,

Penye udhia pitisha rupia.
 
Mimi nakushangaa kitu kimoja mkuu,

Unasema umeoa na huyo binamu yako kaolewa,lakini huonyeshi dalili zozote zakumuhofia mkeo au mume wa huyo binamu yako!

Yaani unachohofia ni mila tu ambazo ni kama mazowea tu.
 
Kama ingekua ni vibaya, basi asingejifungua salama, lingetokea linyama tu, hizo ni imani zilizopitwa na wakati.
Kwa hiyo wakijua ndio mtoto atayeyuka?
 
Natumai hamjambo wakuu.

Miaka 7 iliyopita nili-date na binamu yangu, bahati mbaya alipata ujauzito nikamtaka autoe akakataa katakata. Nilimtaka autoe sababu mila zetu haziruhusu mahusiano ya kimapenzi na binamu, nyumbani aliwaambia aliyempa mimba ni mtu wa mbali ambaye walikutana shule na hawana mawasiliano tena.

Baada ya kukataa kuitoa ilibidi tufanye kiapo cha kutunza siri ili tusije leta ugomvi katika familia, alipojifungua mtoto alifanana na mimi kila kitu, wazazi wake wakaamua kumpa jina langu eti kafanana na mjomba ake.

Mila zetu zinasema ukilala na mtoto wa shangazi/mjomba ni sawa na kulala na shangazi/mjomba wako, na hapa ndo panaleta ugumu wa suluhu wa hii siri ya muda mrefu.

Wakuu nawaombeni kwa busara zenu mchangie mawazo ambayo huenda yakazaa suluhu ya jambo hili kwa hekima bila kuleta mtafaruku kifamilia.
jamaa bhana! umesema "mila yenu hairuhusu kuoa." sawa.... je! kuzaa?

kwanza huyo binamu ni jasiri kuliko wewe tena sana.
pili hizo habari za mila unaweza kuzivunja na kuamua kuishi maisha unayoona yanafaa.
sheria zingine za kimila zimewekwa ila ni za kipumbavu sana
 
Back
Top Bottom