Ushauri: Rais Samia na wapinzani, kubalini kuelewana kwenye hili la Katiba Mpya

Mzalendo Uchwara

JF-Expert Member
Jan 26, 2020
3,716
11,704
Facts
- Ni wazi kuwa wapinzani (wa kweli), wanaharakati, CCM Zanzibar, CCM wapenda mabadiliko bara na watanzania wengi kwa ujumla wao wanataka mabadiliko ya katiba ili kuondoa changamoto nyingi za kisheria na kiutawala zilizopo sasa.

- Ni wazi kuwa wazanzibari wengi (Mh. Rais akiwemo) wanatamani mabadiliko ya katiba ili kujaribu kutafuta ufumbuzi wa zinazoitwa kero za muungano.

- Ni wazi kabisa kuwa Rais Samia hawezi kuanzisha mchakato wa katiba mpya katika ungwe yake ya kwanza, itakuwa ni political suicide. Hivyo basi kuna uwezekano mkubwa zaidi wa kufufua mchakato akiwa katika ungwe yake ya mwisho (inshaallah).

- Ni wazi kuwa wapinzani wa kweli wamedhamiria kutoshiriki uchaguzi wowote nchini ambao utakua chini ya tume hii ya taifa ya uchaguzi (ya uchafuzi). Vilevile hawatoshiriki uchaguzi utakao simamiwa na ule mfumo kichekesho wa kusimamia uchaguzi wa serikali za mitaa kupitia waziri wa TAMISEMI. Jambo hili ni doa na hatari kwa ustawi wa nchi.

Ushauri
Lazima mchakato wa mabadiliko ya katiba uanzie mahali fulani, hivyo basi Mheshimiwa Rais nakuomba kwa unyenyekevu ukutane na wadau wote kwenye swala hili ikiwa ni pamoja na vyama vya siasa (hususani CDM), kisha mkubaliane kwa kuanza na marekebisho ya sheria ya uchaguzi ikiwa ni pamoja na kuirekebisha tume ya uchaguzi.

Hii itawezesha uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu 2025 kufanyika kwa uhalali machoni pa watanzania na jumuiya za kimataifa na vyama vyote vitaweza kushiriki. (Wewe Mheshimiwa sana utashinda ili uongoze kwa awamu ya pili).

Pia, CDM na wapinzani wengine watashinda viti vya kutosha bungeni na kwenye udiwani. Mheshimiwa Rais, utawahitaji sana watu hawa pindi utakapo fufua mchakato wa katiba mpya.

Hata wewe mwenyewe Mheshimiwa sana ukweli unaujua, upinzani wa mabadiliko ya katiba unaletwa na wana CCM wahafidhina kutoka Tanzania bara. Hivyo basi support ya vyama vya upinzani ni muhimu sana pamoja na ile ya wale CCM 'moderates' wa bara na CCM Zanzibar.

Kwenye hili lazima pande zote zikubali ku 'compromise' ili tupate pa kuanzia.
 
Hao wanaojiita wapinzani ndio hawasomeki Rais kawaambia wasubiri consern yao itakuwa dealt eti wanakuja na vitisho,who are they? Wapigwe pin tuu wanahemka sana
Wanaeleweka sana, hiyo ni negotiation tactic. Unaanzia mbali na unakomaa kweli, lakini ukweli unaujua kuwa madai yako yote hayawezi kukubaliwa lakini mwisho wa siku utapata kitu fulani. Wako sahihi kabisa.

Ukimya wa Mheshimiwa Rais na kuwaambia 'wangoje' ndio tatizo, labda kama na yeye anatumia mbinu ya 'hard to get'.
 
Tuliyoyaona na Kuyasikia Chini ya Utawale Ule, Inatosha Kusema katiba Mpya na Tume huru ya Uchaguzi is a Must. Nadhani lisipofanyika hili basi Tujue Nchi imewekwa Rehani; Tuliyoyashuhudi Kipindi Kilichopita Hakifai na Kisirudiwe".

Nchi Ilikuwa Kama Familia ya Mtu Mmoja" Neno lake iligeuka kuwa Sharia na Walio wake walineemeka, Kijiji Kikageuzwa kuwa Jiji na Ikulu; watu wakagawanywa kimafugu kama ya Dagaa na Kambale.

Dhurumati , Utesaji, Ubambikiaji, Ufitini na Ukora wa rangi zote Tulipata kuuona, Simba alipounguruma wote tuliufyata Mkia, Hakuna aliyejitokeza Kukemea Isipokuwa Wasifiaji waliongezeka ILA ni Mtu mmoja tu TUNDU LISSU Aliyebaki Kupambana na Mungu Mtu yule ( kwa hisani ya Prof. wa Jalalani).
 
Yaliyotupata Watanzania Chini ya Utawale Ule, Inatosha Kusema katiba Mpya na Tume huru ya Uchaguzi is a Must.
Ndani ya muhula wa kwanza ni rahisi zaidi kupata mabadiliko ya tume, hakuna kisingizio cha gharama kwani ni muswada wa sheria tu kama sheria nyingine.

Kwenye ungwe ya pili katiba inawezekana kupatikana. Huo ndio uhalisia wa mambo.

Kwahiyo wanaweza kukubaliana kuanza na tume kisha katiba ikafuata.
 
Hao wanaojiita wapinzani ndio hawasomeki Rais kawaambia wasubiri consern yao itakuwa dealt eti wanakuja na vitisho,who are they? Wapigwe pin tuu wanahemka sana
Usichokijua ni kwamba wananchi wakiamua, wana uwezo wa kpiga pini Rais na Serikali yake. Kila upande ni muhimu kwaajili ya mstakabali wa Taifa.

Serikali ina polisi, mabomu na bunduki, wapinzani wana akili ja weledi.

Magufuli alikuwa na vyote bavyo Samia anavyo lakini mapambano yake na vyama vya upinzani, aliangukia pua. Angekuwa hai, siku moja kama angehojiwa angeeleza wazi jinsi CHADEMA ilivyomwendesha. Serikali ya Magufuli ilifikia hatua mpaka ya kwenda kukopa kwenye mabenki ya biashara baada ya kuishiwa mbinu zote.

Wajinga walimwona Magufuli ni mwamba lakini Magufuli alibanwa mbavu kila sehemu. Hakuna alichopanga kilichofanikiwa. Utekelezaji wa bajeti ukawa unacheza kati ya 35 na 40%. Akabakia kutawala akiwa na frustration.

Baada ya kushindwa mbinu zote, akaamua kutumia njia ovu kutawala. Baadaye akaamua kujishughulisha na vitu vidogo vidogo maana vikubwa ikawa ngumu kuvimaliza. Pesa kidogo aliyokusanya na kupora watu, akaamua kuitumia kwenye miradi midogo midogo kama vile visima vya maji, vipande vya barabara za mijini, ujenzi wa masoko na stand, huku miradi mikubwa akisubiria mikopo.

Rais Samia, nia yake njema ya kufufua uchumi itakuwa ngumu sana kutekelezeka, akishindwa kuvifanya vyama vya upinzani kuungana naye kwenye ajenda za kitaifa.
 
Usichokijua ni kwamba wananchi wakiamua, wana uwezo wa kpiga pini Rais na Serikali yake. Kila upande ni muhimu kwaajili ya mstakabali wa Taifa.

Serikali ina polisi, mabomu na bunduki, wapinzani wana akili ja weledi...
Naam, umenena vyema mkuu.
 
Werema, Warioba na sasa Uamsho wameunga mkono harakati za kudai katiba mpya. Tutaipata tu.
Haizuiliki, ni ajenda ya wananchi. Mheshimiwa rais awe makini na akubali maelewano, vyama vya upinzani wamempa mkono wa heri kwa kuomba kukutana naye lakini amejikausha mpaka sasa.
 
Usichokijua ni kwamba wananchi wakiamua, wana uwezo wa kpiga pini Rais na Serikali yake. Kila upande ni muhimu kwaajili ya mstakabali wa Taifa.

Serikali ina polisi, mabomu na bunduki, wapinzani wana akili ja weledi...
Ndio mpaka wananchi waamue sasa,CDM mumekataliwa na wananchi sasa mnajifanya kuwasemea,waliwatuma lini?
 
Wanaeleweka sana, hiyo ni negotiation tactic. Unaanzia mbali na unakomaa kweli, lakini ukweli unaujua kuwa madai yako yote hayawezi kukubaliwa lakini mwisho wa siku utapata kitu fulani. Wako sahihi kabisa.

Ukimya wa Mheshimiwa Rais na kuwaambia 'wangoje' ndio tatizo, labda kama na yeye anatumia mbinu ya 'hard to get'.
Hapana. Hawa watu ni mafedhuli wasio na staha wala busara.

Mheshimiwa rais aliwaambia vizuri tu kwamba wasubiri hiyo issue ataishughulikia. Kisa cha kuanza kumporomoshea matusi ni nini? Wengine ndio wamo humu humu JF kazi yao kutukana tu.

Watu tunaowategemea kama wapinzani wanakaa na kutoa kauli za ajabu ajabu kwa rais. Hii haikubaliki, hamjifunzi??? How do you really want to be treated you guys??

Anyway, walisema watamlazimisha atake asitake. Sasa ok, kila mtu na ashinde mechi zake!

Impitie: Extrovert
Jumbe Brown
 
Watanzania wengi wanaitaka. Lakini Mh. Rais ni miongoni mwa wanufaika wa katiba hii ya sasa, lazima awe na kigugumizi. Hivyo ni muhimu kwa pande zote kuelewana.
Tunaposhindwa kuelewa ni kwamba hata CCM tunaitaka katiba mpya.

Uhalisia ni tofauti, kuna mengi ya kufanyika kabla hata huo mchakato haujaanza. Ndio maana Mheshimiwa Rais akasema tusubiri. Sasa Sisi na ujuaji wetu ambao in fact hatujui kitu tunatoka majukwaani tunaanza kumtukana rais.

Haya tuendeleeni labda ndio tutaipata.
 
Back
Top Bottom