Ushauri mpya kuhusu uvaaji wa Barakoa (Masks) kujikinga na maambukizi ya Covid-19: Tujielimishe ili tuamue vema

Dr Mathew Togolani Mndeme

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
201
808
Ushauri wa barakoa na mkanganyiko wake

Jana Marekani na Uingereza, ambazo ni nchi zenye nguvu kiuchumi na kuongoza katika ugunduzi na tafiti za kisayansi, zimetoa kauli zinazokinzana kuhusu uvaaji wa barakoa (masks) kama njia ya kujikinga na maambukizi ya ugonjwa wa Corona kwa mtu ambaye hajaambukizwa (mass masking).

Nina hofu kwamba maamuzi yao (hasa ya Marekani) yanakwenda kuongeza taharuki Afrika katika janga la Corona. Hii ni kwa sababu hadi sasa ushahidi unaonesha kwamba nchi nyingi Afrika zinaparamia mapendekezo au maamuzi yanayochukuliwa na nchi za Maghararibi bila kutazama mazingira ya utekelezaji wake katika nchi zetu.

Walichokisema kinaweza kabisa kuchukuliwa kama ushahidi wa kisayansi na nguvu zote zikahamishiwa kwenye uvaaji wa barakoa. Naomba nielezee mkanganyiko huu kwa kifupi, maana yake na tunavyoweza kuutumia.

1585960340949.png

Hadi juzi, taasisi ya udhibiti wa magonjwa ya Marekani (CDC) walikua na msimamo kwamba uvaaji wa barako hauna msaada kumkinga mtu kupata maambukizi. Ila jana walisema watapitia upya mapendekezo (recommendations) yao maana kuna dalili kwamba zinaweza kuwa na msaada. Leo wameibuka na mapendekezo mpya kwamba watu wanaweza kuvaa barakao zisizo za tiba kama njia ya kujikinga na maambukizi. Hata hivyo rais Trump yeye kasema hatava barakoa maana hayo ni mapendekezo tu.

Wakati huohuo, serikali ya Uingereza imeendelea na msimamo uliokua unajulikana katika viunga vya wanasayansi kwamba hakuna msaada kwenye kuvaa barakoa kwa mtu mzima. Katika kuweka msisitizo, wamesema wamewasiliana na watafiti wenzao kule Hong Kong (watu wanaposingizia barakoa zimesaidia) na wamewathibitishia kwamba hakuna ushahidi wa kisayansi kwamba zina msaada.

Nini msingi wa hoja za kisayansi kwa jambo hili?
Tangu maambukizi ya Corona yaliposhika kasi, kumekua na mjadala mkubwa wa matumizi ya barakoa kama moja ya vitu vinavyoweza kusaidia mtu kujikinga na maambukizi. Baadhi ya wanasayansi/watafiti wamekua wakijenga hoja kwamba barakoa zina msaada na hivyo watu washauriwe kuvaa. Hata hivyo nchi nyingi pamoja na Shirika la Afya Duniani (WHO) wamekua wakishauri kwamba uvaaji wa barakoa hauna msaada kumkinga mtu anayehudumia wenye maambukizi pekee
(TAZAMA HAPA). Wanashauri parakoa kuvaliwa na mwenye maambukiki kupunguza uwezo wake wa kusambaza virusi anapokosa, kuongea au kupiga chafya.

Ukiachilia mbali hoja za kisayansi, wanananchi wa kawaida wamekua na mtizamo kwamba barakoa zinazuia kuambukizwa Corona. Fikra hii inahusishwa na ukweli kwamba tangu Corona ilipoanza kilichokua kinaonekana kule China ni watu waliozivaa kila mahali. Hii ikachukuliwa moja kwa moja kwamba ile ni kinga ya Corona. Ila ukweli uliopo ni kwamba uvaaji wa barako kwa China na hata Hong Kong ni utamaduni wa kila siku unaosababishwa na uchafuzi mkubwa wa hali ya hewa. Barakoa zinajulikana kitaalamu kwamba zina uwezo wa kusaidia kupunguza uvutaji wa hewa chafu. Hivyo kule China kutokuvaa barakao hasa kwenye miji mikubwa inachukuliwa kama uzembe (being irresponsible). Corona imewakuta wachina wakivaa barakoa na sio kwamba barakoa zimeanza kuvaliwa kama kinga ya Corona.

Lakini hata tukichukulia kwamba wachina walizivaa kujikinga na Corona, bado sio njia sahihi ya kuhitimisha kwamba ni kinga. Tukumbuke wao walipata ugonjwa huu wakiwa hawajui unatoka na nini na unaambukizwaje. Hivyo kwa taharuki waliyokua nayo walijaribu kila njia kutafuta kujikinga bila kujali njia hizo zina tija au la kwa sababu mwenye njaa hachagui chakula. Ila kwa sasa ulimwengu una uelewa mpana kwa kiasi fulani kuhusu ugonjwa wa Corona na unavyoenea hivyo sio sahihi kuendelea kuchukua hatua kwa taharuki au kubahatisha iwapo kuna nafasi ya kutumia akili na ushahidi wa kisayansi.

Kuna machapisho mengi ya kisayansi yanayojadili jambo hili ila katika ujumla wake, yanakubaliana kwamba hadi sasa hakuna ushahidi wowote wa kitafiti kuthibitisha kwamba barakoa zina uwezo wa kumkinga mtu mzima na maambukizi ya Corona. Kama zingekua kinga, ni wazi China wangeweza kuudhibiti ugonjwa mapema sana maana wao kuzivaa ni utamaduni. Pia nchi ambazo zinavaa kwa wingi kama Hong Kong na Korea zisingekua zinatoa taarifa ya wagonjwa wapya na vifo kila siku kama tunavyoona. Wanasayansi wanaotetea uvaaji wa barakoa, wanasema kutokuwepo kwa ushahidi wa kwamba zinasaidia, haimaanishi kuwa ni uthibitisho wa kutokua na msaada. Nikitafsiri hoja yao katika mazingira yetu nitasema: wewe ukisema hujawahi kuona paka anayepaa, haiwezi kutumika kama ushahidi kwamba hakuna paka anayepaa. Inawezekana kabisa tukiendelea kuchunguza paka wote tukakuta yuko anayepaa.

Nini ushahuri wangu?
Nina mambo makuu mnne ya kugusia kwenye jambo hili kama ushauri.

  1. Hakuna ushahidi kwamba barakao zinasaidia kujikinga na maambukizi. Haijalishi nani katoa mapendekezo, ila kisayansi na tiba, maamuzi hata kama yanaonekana ni mazuri kama hayana ushahidi wa kutosha wa kitafiti. Sio mapendekezo yote yanatumia ushahidi wa kisayansi. Mengine yanatolewa kulingana na mazingira hasa watu wanapokua kwenye taharuki au hawana njia mbadala ya kuitegemea. Tusichukulie mapendekezo ya CDC kama vile ndio amri ya 11 tukaanza kukimbizana na barakoa tukazua mengine na tija tusipate. Bado nafuatilia kujua CDC wamechukua ushahidi gani kufikia mapendekezo haya (bado natafuta desa walilotumia).
  2. Kuna baadhi ya tafiti za kisayansi zimeonesha kwamba uvaaji wa barakoa kwa wananchi (mass masking) unaweza kuwa na msaada wa kisaikolojia. Bila kujali kwamba zina kinga au vinginevyo, tafiti zimeonesha kuna watu hujisikia salama au wamekingwa kwa kiasi fulani wao wenyewe wanapokua wamevaa barakoa au/na watu wengine wanaowazunguka wamevaa pia. Hivyo, kwa kuwa jamii nzima ina taharuki na madhara ya kisaikolojia ya ugonjwa huu ni makubwa sana, tiba ya kisaikolojia inahitajika pia. Hivyo, kama mtu au watu wanajisikia salama zaidi wakivaa barakoa, wavae na watu wengine wasiwashangae wala kuwakosoa wakizivaa.

  3. Ninafahamu serikali inafanya kazi kubwa ya kutoa elimu hukusu mlipuko wa Corona. Ila ninawashauri wahusika waendelee kutoa elimu zaidi kwenye eneo hili kuhusu uhalisia wa msaada wa barakoa. Walizungumzie katika dhana ya kinga (based on existing scientific evidence) na katika dhana ya tiba ya kisaikolojia (mitigating psychological effects). Watu wajue kwamba sio lazima kuvaa lakini kama wanaona kuvaa kunawapa amani ya moyo zaidi, basi wavae. Elimu hii ni muhim sana kwani iwapo watu wengi watazivaa huku wakiwa hawana uelewa wa kitaalamu wa namna bora ya kuzivaa, kuzitumia, kuzitunza, na usafi wake, ni wazi zinaweza kuwa sababu ya maambukizo zaidi au kuleta madhara mengine ya kiafya.

  4. Kwa kuwa Marekani wamebadilisha mapendekezo yao, na tunajua nguvu yao kwenye taasisi ya kimataisa, kuna uwezekano mkubwa kabisa kwmaba WHO nao watabadilisha mapendekezo yao na kuhamasisha uvaaji wa Barakoa. Jana nimesikia afisa mmoja wa WHO akikaririwa kusema nao watapitia upya mapendekezo yao kuhusu barako baada ya Marekani kubadili. Tusishangae tukiona nao wanaaza kutushawishi kuvaa barakoa. Bado tukumbuke, sio kila mapendekezo tupewayo ni sahihi na yatatekelezeka.

    Imeandikwa na MM Togolani (mmtogolani@gmail.com)
    Mtafiti wa mifumo ya digitali katika ufuatiliaji na udhibiti wa magonjwa
 
Asante kwa andiko. Tukitumia ukweli huu ...nitakaosema yaani Mita 1+barakoa (ya aina yoyote)+kunawa mikono chance ya maambukizi itakuwaje? Naamini barakoa haijawa recommended sana kwa sababu ya uchache na upatikanaji wake.
 
Nchi nyingi pamoja na Shirika la Afya Duniani (WHO) wamekua wakishauri kwamba uvaaji wa barakoa una msaada kumkinga mtu anayehudumia wenye maambukizi pekee. Pia, ni vema kuvaliwa na mwenye maambukiki kupunguza uwezo wake wa kusambaza virusi anapokosa, kuongea au kupiga chafya.
Para hiyo imemaliza kila kitu.

Kwa vile tangu mtu kuambukizwa hadi kuonyesha simptoms ni 14 days, huwezi jua nani ameambukizwa na nani bado, hivyo to be on a safe side, barakoa zivaliwe na wote!

Sisi Tanzania anaetulinda ni Mungu tuu kufuatia kuushtukia Corona ni shetani hivyo rais wetu Magufuli akaikabidhi shetani Corona kwa kiboko ya shetani ambaye ni Mungu mwenyewe vinginevyo...!

P
 
Para hiyo imemaliza kila kitu

Kwa vile tangu mtu kuambukizwa hadi kuonyesha simptoms ni 14 days, huwezi jua nani ameambukizwa na nani bado, hivyo to be on a safe side, barakoa zivaliwe na wote!
P
Asante kaka kwa kuonesha hilo... kulikua na spelling error kwenye hiyo sentensi. Neno sahihi ni HAUNA MSAADA na sio UNA msaada. Nimerekebisha
 
Kama ukweli ni ukiambukizwa ndani ya dakika chache na wewe una anza kuambukiza, barakoa ni muhim Sana maana chanzo cha maambukizi ni pua na mdomo. Pia kusema china wana utamaduni wa kuvaa barakoa sidhani kama ni Sahihi!
Kwenye wa china 10,000 kabla ya ugojwa unaweza mkuta mmoja tu kavaa. Serikali ya China tuliona sana ikisisitiza uvaaji wa barakoa na Mimi pia kwa ufaham wangu Nina pendekeza uvaaji wa Barakoa!!

Tusiwaamini Sana hawa wanao jiita wa kubwa wana mengi juu yetu. Wao wana gombania barakoa Sisi tusivae!!!
Adi Muda huu ni Mungu ana tulinda. Waruke vikwazo walivyo weka kwa kupokea barakoa Sisi tusitumie barakoa!!

Putin’s U.S. Virus Aid Flight May Have Carried Sanctioned Goods!
 
Hahahahaha

Wote waliokuwa wanapiga vita niqaab na hijab za Kiislam, sasa watafunika nyuso zao wakipenda wasipende.

Allahu Akbar.
Duh!. Saa hizi niludhani watu wa swala 5 wako kwenye swala, kumbe wengine wao wanaswali JF!.
Asante mpenzi FF, tutashauri niqaab na hijab za Kiislamu ziwe ni vazi la taifa na ziwe mandatory.

Mimi binti yangu rafikiye ni Muislamu anavaa uniform zile la Kiislamu shule, binti akaomba na yeye ashonewe, mama yake akamgomea, kuwa ni vazi la Kiislamu, nikamwelimisha hata Yesu alivaa kanzu na kile kitambaa, hata Bikira Maria Mama wa Mungu Mwana, alivaa hijab na walikulia Misri nchi ya Kiislamu. Wazungu ndio wamebadili ila mavazi ya Kiislamu ndio mavazi ya hishma na staha, wife akakubali, tukamshonea na binti akafurahi sana.

Alipovaa shule, akapewa barua kuwa kwa mujibu wa muongozo wa Wizara ya Elimu, mavazi hayo yanaruhusiwa kwa wanafunzi wa Kiislamu pekee, sisi Wakristu haturuhusiwi!, ila home kila akitoka ni hijab kwa kwenda mbele hadi watu wanadhani ni binti wa Kiislamu. Hivi ndivyo Wazungu walivyotufanya vibaya!.

Kwa hili la mavazi namlia timing Prof. Ndalichako. Watu hawajui Yesu Kristo alivaa kanzu na Bikira Maria alivaa hijab!.

Asubuhi njema la Aziz

P
 
Thanks brother for your digital based research.

Binafsi naona kuna haja saana ya kuzipa nguvu taasisi zetu za utafiti zitakazo fanya utafiti na kutoa mapendekezo kulingana na mazingira yetu.

Nadhani kama vilivyo bize vyuo vya wenzetu kufanya tafiti nasisi tulitegemea vyuo vyetu pale udsm conas wawe bize kutafiti... muhimbili bugando udom n.k lakini sijui wanasubiri paka wanasiasa waseme?

Nilitegemea miongozo mingi itoke from them kuliko kutoka kwa wanasiasa. Yani wanasiasa wamekuwa watoaji maelekezo kuliko hata watalaam wa afya?


Kwakweli mapendekezo na tafiti nyingi za hawa mabeberu zinaonekana hazifiti saana kwa sisi Africans mpaka tunafikia kuhisi kama wananjama zidi yetu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
MM Togolani,

Kwanini wanashauri watu wakae 1 m apart,watu wanawe mikono na kutojishika usoni?Ni kwa sababu virus hawa wanaaffect respiratory system, wanaingia kupitia mfumo wa hewa.Kwa akili ya kawaida tu na hata sio mpaka uende medical school, uvaaji wa mask unasaidia sana kweny kujikinga kuvuta hewa yenye infected airdroplets lakini pia kujishika shika usoni ambako kunawez pelekea kuvuta virus kutoka kwenye mikono in case kama umeshika sehem virus hivyo vimeachwa au kama ur infected itasaidia kuepusha the spread.1 m distance apart, kuvaa masks, kunawa mikono na sabuni thouroghly kwa maji tiririka , using hand sanitizers, kuepuka crowded areas...hizi ndio kinga kwetu huku uswahilini. Tusiangalie kitu kimoja tu kwa sababu kujikinga na hii kitu depends on many factor not just a single method.
 
Duh!. Saa hizi niludhani watu wa swala 5 wako kwenye swala, kumbe wengine wao wanaswali jf!.
Asante mpenzi FF, tutashauri niqaab na hijab za Kiislamu ziwe ni vazi la taifa na ziwe mandatory.

Mimi binti yangu rafikiye ni Muislamu anavaa uniform zile la Kiislamu shule, binti akaomba na yeye ashonewe, mama yake akamgomea, kuwa ni vazi la Kiislamu, nikamwelimisha hata Yesu alivaa kanzu na kile kitambaa, hata Bikira Maria Mama wa Mungu Mwana, alivaa hijab na walikulia Misri nchi ya Kiislamu. Wazungu ndio wamebadili ila mavazi ya Kiislamu ndio mavazi ya hishma na staha, wife akakubali, tukamshonea na binti akafurahi sana.

Alipovaa shule, akapewa barua kuwa kwa mujibu wa muongozo wa Wizara ya Elimu, mavazi hayo yanaruhusiwa kwa wanafunzi wa Kiislamu pekee, sisi Wakristu haturuhusiwi!, ila home kila akitoka ni hijab kwa kwenda mbele hadi watu wanadhani ni binti wa Kiislamu. Hivi ndivyo Wazungu walivyotufanya vibaya!.

Kwa hili la mavazi namlia timing Prof. Ndalichako. Watu hawajui Yesu Kristo alivaa kanzu na Bikira Maria alivaa hijab!.

Asubuhi njema la Aziz

P
Hiyo shule wamekosea sana kumzuia mwanao kuvaa Hijab. Hilo ni vazi halali na rasmi la shule bila kujali binti ni dini gani ilmradi mtoto hajavalishwa kwa lazima na wazazi wanaridhia.

Lakini kaka yangu Pascal Mayalla, usiache kumfuatilia kwa karibu huyo bintiyo. Kuna ushahidi mwingi kwa baadhi ya mabinti wanaovaa Hijab, wanazitumia "kuficha" mambo yasiyohitajika shuleni na nyumbani, mfano kufuga nywele ndefu, kuzitia dawa, kuchora tattoo shingoni na mikononi, kuficha vinguo vya kutokea 'out' awapo mtaani na mbaya zaidi kuficha simu.

Chukua tahadhali. Utanishukuru baadae!
 
Hiyo shule wamekosea sana kumzuia mwanao kuvaa Hijab. Hilo ni vazi halali na rasmi la shule bila kujali binti ni dini gani ilmradi mtoto hajavalishwa kwa lazima na wazazi wanaridhia.

Lakini kaka yangu Pascal Mayalla, usiache kumfuatilia kwa karibu huyo bintiyo. Kuna ushahidi mwingi kwa baadhi ya mabinti wanaovaa Hijab, wanazitumia "kuficha" mambo yasiyohitajika shuleni na nyumbani, mfano kufuga nywele ndefu, kuzitia dawa, kuchora tattoo shingoni na mikononi, kuficha vinguo vya kutokea 'out' awapo mtaani na mbaya zaidi kuficha simu.

Chukua tahadhali. Utanishukuru baadae!
Una style nzuri ya kuamrisha maovu! Unataka kusema uovu wa waiba viatu msikitini ufanye watu wasiende kuswali badala ya kutafuta mbinu ya kukomesha wizi na swala ziendelee. Vazi la stara ya kiislamu ni ibada,hata kama waovu wanalitumia kinyume na lengo.
 
Tusipende kuamini vitu vya wazungu kwani wazungu wanachuki kubwa sana dhidi ya waafrika wanatuona kama siyo binadamu. Mfamo jana kuna clip moja niliona madaktari wa ufaransa wanasema sehemu sahihi ya kufannyia majaribio ya chanjo ya huu ugomjwa ni Africa. Kwa mtazamo huo wanaweza hata kuleta madhara makubwa kwa Afrika. Hivyo viongozi wa Afrika inabidi wawe makini sana kwa kipindi hiki dhidi ya vifaa wanavyopokea toka mataifa ya ulyaya n.k.
 
MM Togolani,

Kwanini wanashauri watu wakae 1 m apart,watu wanawe mikono na kutojishika usoni?Ni kwa sababu virus hawa wanaaffect respiratory system, wanaingia kupitia mfumo wa hewa.Kwa akili ya kawaida tu na hata sio mpaka uende medical school, uvaaji wa mask unasaidia sana kweny kujikinga kuvuta hewa yenye infected airdroplets lakini pia kujishika shika usoni ambako kunawez pelekea kuvuta virus kutoka kwenye mikono in case kama umeshika sehem virus hivyo vimeachwa au kama ur infected itasaidia kuepusha the spread.1 m distance apart, kuvaa masks, kunawa mikono na sabuni thouroghly kwa maji tiririka , using hand sanitizers, kuepuka crowded areas...hizi ndio kinga kwetu huku uswahilini. Tusiangalie kitu kimoja tu kwa sababu kujikinga na hii kitu depends on many factor not just a single method.
Sasa baba hata hizo santanaiza hazipatikani si tutakwisha huku baghosha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Una style nzuri ya kuamrisha maovu! Unataka kusema uovu wa waiba viatu msikitini ufanye watu wasiende kuswali badala ya kutafuta mbinu ya kukomesha wizi na swala ziendelee. Vazi la stara ya kiislamu ni ibada,hata kama waovu wanalitumia kinyume na lengo.
Mkuu ndio maana nimetumia kauli mbili kulilinda vazi la Hijab. Ya kwanza, nimesema baadhi ya mabinti. Hawa wanalitumia vazi zuri kwa nia ovu. Hovyo, tunatakiwa tuwe makini nao na tuwakomeshe. Ya pili, nimemshauri mzee mwenzangu amfuatilie kwa karibu bintiye kuhakikisha kwamba analivaa kwa stara zake za ndani na nje na sio vinginevyo. Nipo tayari kusahihishwa Mkuu.
 
Mkuu ndio maana nimetumia kauli mbili kulilinda vazi la Hijab. Ya kwanza, nimesema baadhi ya mabinti. Hawa wanalitumia vazi zuri kwa nia ovu. Hovyo, tunatakiwa tuwe makini nao na tuwakomeshe. Ya pili, nimemshauri mzee mwenzangu amfuatilie kwa karibu bintiye kuhakikisha kwamba analivaa kwa stara zake za ndani na nje na sio vinginevyo. Nipo tayari kusahihishwa Mkuu.
Shukran. Vazi hili huvaliwa mbele ya wanaume wawezao kumuoa,lakini mbele ya baba,kaka,babu mjomba ....atapunguza mavazi yaani kama wavaavyo wasokuwa/ wasiozingatia sheria,hapo mzee mwenzio ana fursa ya kumuona. Halivaliwi mahali pote na muda wote.
 
Asante kaka kwa kuonesha hilo... kulikua na spelling error kwenye hiyo sentensi. Neno sahihi ni HAUNA MSAADA na sio UNA msaada. Nimerekebisha

Ukisema umerekebisha, ina maana mgonjwa wa Corona kuvalishwa mask pamoja na mtaalamu wa afya kuvaa mask havina msaada kwao katika kuambukiza ugonjwa kati yao?

Kwa nini sasa hawa watu wanashauriwa na wataalamu wa afya katika mazingira ambayo mtu ni suspect kuvalishwa/avae mask na mtaalamu wa afya hutakiwa kuvaa mask?

Naunga mkono hoja ya kwamba, kwa kuwa watu/mtu anaweza kupata ugonjwa wa Corona na kulingana na kinga zake asionyeshe dalili au akakaa na ugonjwa siku 14 mpaka 21 ndipo akaonyesha dalili na wakati huohuo anao uwezo wa kusambaza ugonjwa, ni vyema basi tukasema kila mmoja wetu ni "suspect until proven otherwise". Hivyo, ni vyema kuunganisha taratibu ziwe: barakoa+nawa mikono kwa sabuni kwa maji tiririka/sanitizer+social distance inaweza kutusaidia sana.

Sina uhakika kama nchi ikiingia gharama ya kusambaza mask za N95 kwa wananchi(ingawa upatikanaji ni issue) ni sawa au inazidi huduma ya janga hili pale linapoingia kikamilifu ili tuanze kukimbizana na wagonjwa wakati huo hata ventileta 200 hatuna nchi nzima.
 
Back
Top Bottom