Usafiri enzi zile Mwanza yetu

Usafiri enzi zile Mwanza yetu

Ndio bado wako hapo ingawaje kuna watoto wake wawili wa kike walifariki na mjukuu wake wa kike.
Inaelekea tunafahamiana maana enzi hizo sisi tulikuwa tunaishi jirani kabisa na mzee Sadoti.
hapo kwa sadotiwaliokufa ni
Mabinti zake wawili Nyasa na Prisca. Juzijuzi kafa brother Kalori mtoto mkubwa wa mzee sadoti.
 
hapo kwa sadotiwaliokufa ni
Mabinti zake wawili Nyasa na Prisca. Juzijuzi kafa brother Kalori mtoto mkubwa wa mzee sadoti.

eeh na kaka Kalori kafariki? ooh masikini alikuwa anaumwa? .. RIP kaka Kalori
 
Huu uzi ubadalisheni heading, maana naona kama unawahusu mwanza tujuane
 
Kumbe nyie wote mliotoa comment mpaka sasa hivi ni wa juzi tu. Miaka ile ilikuwa hakuna cha minibus wala nini. Tulikuwa tunapanda zile peugeot za kizamani mnarundikwa kama ndizi humu. Station wagon moja ilikuwa inaweza kubeba hadi abiria 8. Zilipotoka hizo ndio zikaja express. I love Mwanza mji niliokulia.

Tiba
Wajemeni tuwekeeni picha basi. Uzi kama huu halafu picha hakuna!
 
Wajemeni tuwekeeni picha basi. Uzi kama huu halafu picha hakuna!

Mkuu enzi hizo mtu kuwa na Kamera ilikuwa issue kupita kiasi. Picha tulikuwa tunapiga studio tu. Halafu pale stendi mjini kulikuwa na kituo cha Polisi na mkuu wa kituo alikuwa anaitwa Kalori, Mzee mmoja mweupe amejaza halafu kapanda juu. Huyu alikuwa anawajua vibaka/vijana wa pick pocket wote. Akimwona mmoja akimwangalia jicho tu inabidi huyo kibaka akimbie kama hana akili nzuri. Mwanza enzi hixo. Mimi nilisoma Mwanza Secondari.

Tiba
 
Kumbe nyie wote mliotoa comment mpaka sasa hivi ni wa juzi tu. Miaka ile ilikuwa hakuna cha minibus wala nini. Tulikuwa tunapanda zile peugeot za kizamani mnarundikwa kama ndizi humu. Station wagon moja ilikuwa inaweza kubeba hadi abiria 8. Zilipotoka hizo ndio zikaja express. I love Mwanza mji niliokulia.

Tiba

wewe uko vizuri, nakumbuka jirani yetu moja alikuwa nayo hii kitu alikuwa anaitwa chakubanga. I will never forget the day katuchukua twende kuogelea kigoto watoto wa mtaani, palichimbika tuliporudi sijawai kuona.
 
Nimepanda magari ya Sadoti enzi hizo dereva akiwa 'kaka Mafyale'.. bahati mbaya sana huyu mzee alifilisika vibaya na kwa sasa amezeeka kweli.

Kuna express moja ilikuwa inapiga route za Mwaloni - mjini inaitwa MAJIRA...

"Mafyele" mtoto wake huyo, mume wa Mwalimu "Bunango" Mwalimu mnoko sanaaaaaaaa
 
ahahahahhh, duh umenikumbusha mbali aisee, mmiliki wa majira tulikuwa tunaishi nae jirani mtaa wa azimio. Mmoja wa watoto wa sadoti alimuoa mwalimu wangu wa hesabu enzi hizo mwenge primary, basi mwalimu alikuwa anajidai huyo babamkwe ana express

Mwenge umesoma enzi zipi, Unamfahamu mwalimu mlagili, mama wa kikurya?
 
  • Thanks
Reactions: ram
Wadau wa rock city enzi zile mnakumbuka Mwanza hapakuwa na usafiri wa vipanya kama leo. Vipanya vilikuwa Mabatini na Kirumba tu lakini Igombe kulikuwa na min bus zikiitwa Toto Tundu, Mayeji na Jalijalalam, Igoma kulikuwa na Last Boy na Mkuyuni air Jordan.

wewe ni wajuzi hupaswi kusema enzihizo. magari ya kwenda Igombe yalikuwa aina ya Combi,Randrover, mabasi yalikuwa ni Subira na Dakiki yaliyokuwa yakienda mpaka Kayenze
 
  • Thanks
Reactions: ram
Mkuu enzi hizo mtu kuwa na Kamera ilikuwa issue kupita kiasi. Picha tulikuwa tunapiga studio tu. Halafu pale stendi mjini kulikuwa na kituo cha Polisi na mkuu wa kituo alikuwa anaitwa Kalori, Mzee mmoja mweupe amejaza halafu kapanda juu. Huyu alikuwa anawajua vibaka/vijana wa pick pocket wote. Akimwona mmoja akimwangalia jicho tu inabidi huyo kibaka akimbie kama hana akili nzuri. Mwanza enzi hixo. Mimi nilisoma Mwanza Secondari.

Tiba

Hongera mzee mwenzangu najua utakuwa unamkumbuka na Mzee Kanyau mzee wa zeze alikuwa na kibwagizo (wekelea kanyau) nyimbozake nyingi zilikuwa za kuisifu Tanzania na Kambarage huku akimponda Idd Amin.
 
Mlio soma Isenga s/msingi vidole juu. niliyo yafanya utotoni niliokota mabox ya viatu ili kutengenezra gari, nimeuza fagio za ndani, nimeokota dagaa, ndozi na kumwagilia ndizi mwaloni Kirumba, nimeuza karanga,dengu,bajia,vitumbua, vibaragala, maandazi, nimeuza ngio za wahindi kabura ya machinga kuwepo Mwanza, nimeponda kokoto na kuzisomba kwa kichwa kutoka mlima wa papa kuzisogeza barabarani mchongomani. etisasa nami naeshimika ktk jamii? kweli Mungu acha aitwe Mungu.
 
  • Thanks
Reactions: ram
Hongera mzee mwenzangu najua utakuwa unamkumbuka na Mzee Kanyau mzee wa zeze alikuwa na kibwagizo (wekelea kanyau) nyimbozake nyingi zilikuwa za kuisifu Tanzania na Kambarage huku akimponda Idd Amin.

Mzee kanyau alikuwa mlevi sana wa gongo, halafu meno ya chini alikuwa KANG'OA.
Huyu mzee niliskia aligongwa na Bus La mwatex ndio ikawa sababu ya kifo chake.

Nani anamkumbuka yule mgambo pale Feri ya kwenda Kamanga?
Alikuwa ana tumbo kubwa sana km Ngoma, anatembea na Rungu lake ameliandika" PIGA LKN USIUWE" na picha ya Kipepe!

Ha ha ha ha ha!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom