USA vs N.Korea Military Power

USA vs N.Korea Military Power

Nadhani ule msako wa mashamba ya bangi uendelee hadi vichwani mwa vijana wetu.

North Korea ni mende tu kwa USA. Hata Iraq ilikua hivyo.

North Korea hawajachapwa hadi sasa kwa sababu ya China na Russia.

Msidhani mnachokipenda basi ndio kilivyo. Unaweza kuichukia USA lakini ina nguvu zaidi ya mara 100 kwa North Korea.
 
Suala siyo uwingi. Cha muhimu ni ubora na uwezo.

Unaweza kuwa na pickup 10 ambazo mzigo zinaoubeba haufikii wa semi trailer moja. Tunatakiwa kujua zaidi kuhusu hivi vifaa kuliko uwingi wake. Sadam Hussein alikuwa na ndege nyingi lakini karibia zote zilimalizwa na ndege chache za wafaransa Jaquar.

Siyo mkono bro. Kwa upande wa majini N. Korea wapo njiema sana. Na upande wa ground wapo na multiple rocket launcher 2400 wakati USA wapo na 1200.
 
Yani kwaakili yako yote huo ndo utafiti unaoona unamuwezesha N Korea kumpiga Marekani. Wewe utakuwa sijui umetoka pangoni Leo. Ulishaona watu wanakimbilia kwenda N Korea? Simply hawa N korea wanachezea kiberiti ndo maana Dunia inawaonya 'USA' akiwa kiongozi. Kwasababu wakiamua tuu wanadetonate hydrogen bomb hapo juu ya anga la N Korea na wanarudi back mwaka 1880. Hakuta kuwa na kitu cha umeme kitakachofanya kazi. Just imagine magari hayawaki wala kifaa chochote chenye Nyaya za umeme kitakuwa kimeunguzwa na EMP attack. Welcome to Star Wars 101.
Mkuu,umekuwa brainwashed kweli na propaganda za wamarekani.Punguza kuangalia movies
 
Siyo mkono bro. Kwa upande wa majini N. Korea wapo njiema sana. Na upande wa ground wapo na multiple rocket launcher 2400 wakati USA wapo na 1200.

Hizi data zako Inaelekea unazitoa kwa babu wa Loliondo
 
Hivi Umesikia silaha zitakazotumika mkuu.. Ni nuclear bombs mkuu.. Hata sisimizi wanakufa labda uwe na nuclear shelter..au nuclear bunker!ukimbilie huko chini ya ardhi ukajihifadhi. Hiyo issue ya ground force haina mantiki.. Labda waamue kuzichapa kikawaida tu!

Mkuu mimi nilikuwa nazungumzia zaidi kuzichapa kikawaida, sasa wakihamua ku resort kwenye matumizi ya nuclear hilo ni suala lingine kabisa, binafsi naona kati ya Trump na Kim dogo huyo wa DPRK ndiye anaweza kukimbila kutumia mabom ya Nuclear, Biological na Chemical mapema zaidi kuliko Trump - hayo yakitokea pande zote mbili zitakuwa affected kwa kiwango kikubwa, lakini kwa upande wa Korea Kasikazini nadhani raia wa kawaida walifundishwa jinsi ya kusurvive nuclear Blasts kwa kujificha kwenye specialised Bunkers ambazo wanaweza kuishi hata miezi sita bila ya kutoka nje, wanajeshi wao ndiyo wanaweza kupata madhara ya mionzi nk lakini siyo raia wao.

Korea na Amerika watumie busara zaidi kumaliza mgogoro huu kidiplomasia kuliko utumiaji wa ubabe na vitisho, wasipo kubaliana wakanza kupigani Amerika ikae ikijua kwamba Uchina na Urusi azitakubali vurugu kwenye backyard yao, watafuta kila njia ya kumsaidia Kim kwa kumpa silaha kali na kutuma wanajeshi wa Kichina kwanda Korea kwa kificho mtu wa kawaida uwezi kutofautisha sura za Kichina na Kikorea wote wanafanana Amerika itajikuta ya ya mwaka 1950-53 yanajirudia!! Amerika ikiwa kiganganizi kutaka kuleta mambo ya Regime change basi Wachina na Warusi wataingia vitani rasmi na kusababisha WW3, watu hawajui tu vurugu za Ras ya Korea ndiyo inaweza kuwa chanzo cha WW3 kuliko Syria au Ukraine.
 
Kwa matumizi ya Atomic (Nuclear) sina taarifa kama kuna taifa jingine zaidi ya USA wamewahi kutumia! (Rejea Hiroshima na Nagasaki) Pia silaha za sumu sidhani kama kuna taifa limewahi kufanya maangamizi kwa kuzitumia kuliko USA! (rejea Vietnam, Cambodia na Iraq) Kwenye suala la maangamizi wakati wa vita USA ni na. 1 hilo sina shaka nalo. Kikubwa tuombe hiyo vita isiwepo kwa sababu itatuathiri sisi tunaotegemea far east kwa mahitaji yetu na biashara. (tukumbuke bahari ndio hiyohiyo) tujiulize vita itachukua siku moja kama ya Iraq? (tuliambiwa hivyo na wengi tukaamini!)

Siwezi kuweka turufu kokote kwani VITA NI MAARIFA NA TIMING! Mwenye silaha kali anaweza kushindwa na mwenye silaha duni au kinyume chake kutokana na maarifa yatakayotumika.
 
Najiuliza kwanini USA
Huomba Washiriki kwenye vita yake
kwanini haendi yeye kama yeye pekee
Kifo cha wengi mkuu....
Gharama za vita zikibebwa na wengi kwake ni nafuu.
Akili ya kijinga ni kudhani hiyo vita ikiwepo haitatuathiri kwetu!!
 
  • Population US 360Million Kore 25Million
  • Budget US $18Trillions Korea $18Billions
  • So Uchumi wa Korea ni Mara mia Moja ya Uchumi wa Marekani
  • Atapigwa mpaka Anye.
 
Najiuliza kwanini USA
Huomba Washiriki kwenye vita yake
kwanini haendi yeye kama yeye pekee
Kabla hujajibiwa swali lako jiulize kwa nini Tembo mnyama mkubwa kuliko wote mwituni hutembea wakiwa kundi?
 
Mimi najiuliza ni kwanini kwenye magwaride ya Kijeshi ya USA huwa haoneshi Makombora yake ya Nyuklia?
 
  • Population US 360Million Kore 25Million
  • Budget US $18Trillions Korea $18Billions
  • So Uchumi wa Korea ni Mara mia Moja ya Uchumi wa Marekani
  • Atapigwa mpaka Anye.
Vita vya kitekinolojia havihihtaj wingi Wa binadamu wala pesa,
Bali ni mbinu za kuzimisha mtu au watu wasipumue!
 
*BREAKING NEWS*.
*Hamorapa aondoka nchini asubuhi ya leo kwenda kusuluhisha mgogoro wa Marekani na Korea kaskazini*
 
wabongo wanaijua n.korea kuliko hata wakorea wenyewe.
 
Nimecheck video hapa chini. Nimegundua USA anambwembwe nyingi sana. Kwa upande wa majini N. Korea iko njema sana. Vile vile kwa upande wa nchi kavu N. Korea wapo vizuri kinoma. Nina shawishika kusema kwamba N. Korea ni tishio kubwa sana kwa USA.

Ninathubutu kusema kwamba Trump anapiga mikwara tu. Na isitoshe kuna vifaavingine vingi vya N. Korea hawavijui. Kwa upande wa anga USA wapo vizuri sana lakini wanaweza kuingia N. Korea yenye uwezo mkubwa majini na nchi kavu?
Torpedo Boats and Missile Craft N. Korea zipo 250 wakati USA 0.
Attack Submarine N. Korea 70 wakati USA 55




Siyo mkono bro. Kwa upande wa majini N. Korea wapo njiema sana. Na upande wa ground wapo na multiple rocket launcher 2400 wakati USA wapo na 1200.

Kuna vitu vingi vya kuangalia mkuu. Kiuwezo wa kijeshi, Marekani wamewaacha sana North Korea. Test za Makombora anazoangaika nazo North Korea sasa hivi, US walishazifanya miaka ya 1950-70 huko. Kwa ufupi kivita North Korea inachakazwa, ila ishu kubwa hapo ni China na kumiliki silaha za nyuklia. North Korea inamtegemea sana China kiuchumi, teknolojia na kidiplomasia. leo hii China ikimpiga chini hana ujanja zaidi ya kuwapiga Japan na South Korea na makombora yake.
 
Nimefuatillia sana comment zenu wadau, ila
naomba kujua hii vita kati ya America na North Korea inasababishwa na kitu gani? pili kati ya America na North Korea na mchokozi ? mwenye majibu Please.
 
Soma historia ya korea.

Ukisoma vizuri historia ya Korea Kaskazini utaona mkono wa China nyuma yake. Marekani kuichukua North Korea ikawa chini ya ushawishi wake kama ilivyo South Korea ni kitu ambacho China haikutaka na haitataka kitokee. North Korea wanasaidiwa sana na China. Bila mkono wa China wasingeleta jeuri hiyo.

Kitu ambacho Marekani amekuwa akisita kuishambulia North Korea ni kuingia vita ambayo itahusisha China may be hata Urusi na silaha za Nyuklia kutumika kwa washirika wake Marekani, South Korea na Japan.
 
Back
Top Bottom