Urais, Halima, Nassari na Kigoma

Urais, Halima, Nassari na Kigoma

Status
Not open for further replies.
Ndugu wanajamvi naomba
niseme kabisa kuwa wote waliyoyakataa maneno yao waliyoyatamka kule
Kigoma pale Lake TANGANYIKA stadium ni wanafiki.Kwa kuwa mimi nilikuwepo
pale uwanjani na ninavideo la tukio lote,Nimeanza kuupload japo ipo
slow but ukweli utajulikana.Nassary ni mnafiki na akizeeka atakuwa
mchawi kwa sababu anakataa maneno aliyeyasema mwenyewe mbele ya umati wa
watu.Zitto,usipoweka video kwa kumlinda Nassary na wanafiki wenzake
mimi nitaweka.Sasa sijui walikuwa wamelewa ile siku pale
jukwaani!

unaweka kwa manufaa gani mkuu? haijalishi nani kasema nani hajasema, lakini Zitto afai kuwa rais....over
 
nafikiri ni swala tu la wenda wazimu wanaofikiri IKULU ni sehemu ya maonyesho ya kuonyesha kwamba wewe ni kijana sana au mzee sana au mwembamba sana, au mtanashati au unasali sana, au kabila lenu ni wazuri sana, watanzania hapa tulipofikia tumekwisha.
 
Mh Zitto,

Una haki zote za kutaka uongozi ngazi yoyote katika nchi hii. Hilo halina ubishi. Mimi, sisemi sisi au watu isipokuwa mimi mwenyewe, tunakupenda sana lakini wewe siyo bidhaa ya kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania. Wazungu wanasema, 'You are not material for presidency'. Ni ukweli huenda ukaona mchungu lakini ndo uhalisi wake. Jaribu kwenda njia yote ndo utaelewa. Usikubali watu wakukatishe tamaa, jitose maana ndo njia pekee ya kuelewa. waswahili husema mtoto akililia wembe mpe. 2015 utajifunza somo zuri. Jitahidi hata ukishindwa kuwa nominated na Chadema unda hata chama chako ukipiganie ili ujifunze.
 
Zitto leta ushahidi wa kwamba waandishi wote na wahariri wanahongwa ispokuwa wa Mwananchi tu. Tutajie pia hao wanasiasa wanaotoa hongo kwa waandishi.

Tatu, kama huna interest yoyote na habari ya mwananchi ilokanushwa na kina Mdee, kwanini ujitokeze kutetea mwananchi na wao wasijibu. Wewe ndo mhariri wa mwananchi? Kitendo cha kuijibia mwananchi tena kwa thread ndefu hivi kinatosha kuwashawishi wenye akili kuamini una interest fulani na habari za hilo gazeti.
 
Hapana Mkuu, sikubaliani na wewe...Zitto hana damu ya kunguni! Matatizo anayoyapata Zitto ni ya kujitakia, kuna wakati anashindwa kupima uzito wa kauli zake, kwa mfano;



Katika mahojiano hayo alielezwa Zitto Kabwe kama The Country's One-Man Backbench! Unadhani Wabunge wenzake huko Upinzani walijisikiaje baada ya hilo tambo? Hilo tuliache ila mwaka 2010 aligombea baada ya habari kuzagaa kwamba aliombwa kufanya hivyo kutoka maeneo mbali mbali na tatizo lake kubwa lilikuwa ni kuchagua agombee kupitia jimbo gani...Dar, Geita, Kigoma na wapi sikumbuki! Huyo ndiye Zitto.

Likaja la vita ya Comoro, haya ndiyo maneno ya Zitto;

Lakini baadaye yakazuka ya wakina Shimbo.
Likaja la utendaji wa Idris Rashid na Tanesco - one of the best CEOs,

Likaja la utendaji wa Kikwete - one of the best Presidents,
Likaja yaliyomo kwenye Ripoti ya Bomani...
na mengine mengi...big up kwa JF na kumbukumbu zake!
Likaja la ununuzi wa miambo chakavu ya Dowans,
Niliwahi kumwonya Zitto hapo zamani;

That was then, this is now...tunarudi kule kuleee!
Mkuu wangu hizi kisiasa tunaziita Zitto's flip -flops. Ni guide to za political facts hivyo unamjua mtu huyu ni wa aina gani. Bongo viognozi wengi wako hivyo kama hawa vijana wetu wametazama mazingira ya sifa hizo wamekana.. Tofauti na Zitto yeye alkisikia jambo hakosi kujibu, hana subira japokuwa ana nia njema..

Kwa Zitto kusema hatagombea ni sababu nzuri sana ku wa throw out watu wanaotaka kummaliza kisiasa. He is smart on that kwa sababu watu wengi wanataka kujua Zitto ana mpango gani kesho. Hawaji kwa kheri bali shari tofauti kabisa na watu watakao kuuliza wewe kama utagombea.. Hizi ndio siasa za Bongo you have to be very smart kuelewa nani rafiki na nani adui yako laa sivyo hutafika popote.. Hilo kajifunza Zitto
 
naweka kwa kuwasaidia wanajf wawajue wanasiasa wanafiki kama Nassary,na kwetu sisi Zitto anafaa kuwa rais
 
UNASEMA MGOMBEA URAIS BADO HAJATANGAZWA WKT UNAJUA DR SLAA NDO MGOMBEA. HII YOTE INAONESHA JINSI ULIVYO KOSA STAHA DR. NA CDM KWA UJUMLA.

KWA KUKOMALIA URAIS HATA KIPINDI TUPO ARUMERU KWNY UCHAGUZI MDOGO.

Sijui wengine wanakuonaje ila mi nakuona ni kijana mnafiki na hatari kwa CHADEMA na TZ na uwepo wako ni faida kwa CCM.
nini maana ya chama cha demokrasia na maendeleo??!!kwi kwi....SLAA kapitishwa lini 2015!
 
Huyu Nassar hana kumbukumbu kabisa. Kipindi yeye anahangaika na na kampeni arumeru pomoja na makamanda, zitto alikua hana habari ndio kwanza akatangaza kuutaka uraisi,hali iliyoleta mtafaruku kwa wanachama, leo ndio amekua mtu wa kwanza kumuunga mkono zitto kuvuruga chama.. Bora tu angeshinda sioi.!
 
Record kubwa sana inaonyesha kuwa wanasiasa wanaokuwa na ndoto za urais kwa muda mrefu hushindwa kufanya majukumu yao vizuri wanapopata nafasi za kuwa rais na mara nyingi huvuruga sana nchi zao. Sababu mojawapo kubwa ya kushindwa huko ni kutokana na kuwa mara nyingi huwa hawana ajenda ya nchi bali ajenda yao biansfi ya kuwa rais tu. Sababu nyingine ni kuwa njia wanazotumia kupata uraisi huwafanya wakose washauri wazuri kwa vile huwa wameshavurugana na watu ambao wangewashauri vizuri.

Richard Nixon (aligombea kwa zaidi ya miaka kumi), Kikwete (alijiandaa kwa zaidi ya miaka kumi+), Bush (alijiandaa kwa miaka minane tang baba yake alivyoshindwa na alitumia pesa nyingi sana kuupata).

Mara zote marais wanaohappen kuwa na ufanisi mkubwa ni wale walioombwa na mashabiki wao kuwa wagombee, na wakapewa support kubwa sana na vyama vyao; wengine huchaguliwa kwa bahati bahati tu kwa vile walikuwa katika position fulani wakiwa hawategemei kupata nafasi hiyo ya urais; utaratibu mzima wa wao kujiandaa kugombea huwa ni muda mfupi sana. Mifano ipo ya kutosha kwa watu wa aina hiyo

Kuanzia mwaka jana (au kabla ya hapo- wakati ulipotuarifu kuwa Kikwete alipendekeza wewe ndiwe uwe rais ajaye), Mheshimiwa Zito umekuwa vocal sana katika kutangaza nia yako ya kugombea urais na mara kadhaa umekwaruzana na wenzako ndani ya chama chako kwa sababu hiyo tu. Kadri siku zinavyokwenda umekuwa unaongeza kasi hiyo ukiwa labda na lengo la ku-preempt watu wengine ndani ya chama chako wasigombee nafasi hiyo. Inawezekana mara zote hizo ni magazeti yanakunukuu vibaya ila kwa vyovyote iwapo umekuwa active kutanganza nia yako ya kugombea urais, basi utaratibu unaotumia, hauna tofauti sana na utaratibu uliotumiwa na Kikwete wakati akitaka kugombea uraisi, na leo hii sote tunajua kuwa Kashindwa kazi hiyo. Ingawa leo hii tunamwona Kikwete ni dhaifu, lakini kila mtu anajua jinsi alivyokuwa thabiti kama wewe ulivyo leo wakati yeye akiwa waziri wa fedha ambapo alibana kabisa mismaha ya kodi na kuwabana sana wafanyabishara waliokuwa wakikwepa kodi. Kwa hali hiyo, kuwa makini na hatua unazofanya sasa hivi kwani zinaweza zisiwe productive kwako binafsi, na huenda kwa chama chako pia. Usitake swala la Zito na Urais ndiyo iwe headline kila siku, kwa sababu ikitokea kuwa hutateuliwa na chama chako kwa njia halali kabisa, basi utakuwa umetia doa kwa chama chako, na kuongeza mwanya wa kushindwa na CCM tena!


Kiongozi mzuri ngazi ya Urais siyo tu yule ambaye yuko vocal bungeni kupambana na serikali, bali ni yule aliyekuwa na busara za kutosha kuangalia mambo kwa mapana kwa faida ya jamii yake. Unapokuwa unafanya mambo ambayo ni wazi yanaishiwa kuwagawa wanachama wa chama chako kwa ajili ya lengo lako la uraisi ni dalili ya kupungukiwa busara hiyo.
 
Mkuu, thread inahusu Zitto Kabwe na wabunge walioenda kushiriki tamasha Kigoma. Kama vipi, anzisha thread ya kuelezea kichefuchefu chako. Unachokifanya hapa ni kuwatia kichefuchefu watu wanaotaka to stick to the topic...
traitor ni traitor tu
paradoxical.jpg
 
Record kubwa sana inaonyesha kuwa wanasiasa wanaokuwa na ndoto za urais kwa muda mrefu hushindwa kufanya majukumu yao vizuri wanapopata nafasi za kuwa rais na mara nyingi huvuruga sana nchi zao. Sababu mojawapo kubwa ya kushindwa huko ni kutokana na kuwa mara nyingi huwa hawana ajenda ya nchi bali ajenda yao. Sababu nyingine ni kuwa njia wanazotumia huwafanya wakose washauri wazuri kwa vile huwa wamahsvurugana na watu ambao wangewashauri vizuri.

Richard Nixon (aligombea kwa zaidi ya miaka kumi), Kikwete (alijiandaa kwa zaidi ya miaka kumi+), Bush (alijiandaa kwa miaka minane tang baba yake alivyoshindwa na alitumia pesa nyingi sana kuupata).

Mara zote marais wanaohappen kuwa na ufanisi mkubwa ni wale walioombwa na mashabiki wao kuwa wagombee, na wakapewa support kubwa sana na vyama vyao; wengine huchaguliwa kwa bahatio bahati tu kwa vile walikuwa katika position fulani wakiwa hawategemei kupata nafasi hiyo. Utaratibu mzima wa wao kujiandaa kugombea huwa ni muda mfupi sana. Mifano ipo ya kutosha kwa watu wa aina hiyo

Kuanzia mwaka jana (au kabla ya hapo- wakati ulituarifu kuwa Kikwete alipendekeza wewe ndiwe uwe rais ajaye), Mheshimiwa Zito umekuwa vocal sana katika kutangaza nia yako ya kugombea urais na mara kadhaa umekwaruzana na wenzako ndani ya chama chako kwa sababu hiyo tu. Kadri siku zinavyokwenda umekuwa unaongeza kasi hiyo ukiwa labda na lengo la ku-preempt watu wengine ndani ya chama chako wasigombee nafasi hiyo. Utaratibu unaotumia, hauna tofauti sana na utaratibu uliotumiwa na Kikwete wakati akitaka kugombea uraisi, na leo hii sote tunajua kuwa Kashindwa kazi hiyo. Ingawa leo hii tunamwona Kikwete ni dhaifu, lakini kila mtu anajua jinsi alivyokuwa thabiti kama wewe ulivyo leo wakati yeye akiwa waziri wa fedha ambapo alibana kabisa mismaha ya kodi na kuwabana sana wafanyabishara waliokuwa wakikwepa kodi. Kwa hali hiyo, kuwa makini kuwa hatua unazofanya sasa hivi zinaweza zisiwe productive kwako binafsi, na huenda kwa chama chako. Usitake swala la Zito na Urais ndiyo iwe headline kila siku, kwa sababu ikitokea kuwa hutateuliwa na chama chako kwa njia halali kabisa, utakuwa umetia doa kwa chama chako.


Kiongozi mzuri ngazi ya Urais siyo tu yule ambaye yuko vocal bungeni kupambana na serikali, bali ni yule aliyekuwa na busara za kutosha kuangalia mambo kwa mapana kwa faida ya jamii yake. Unapokuwa unajaribu kuwagawa wanachama wa chama chako kwa ajili ya uraisi ni dalili ya kupungukiwa busara hiyo.

well said mkuu...

Zitto is very smart, but not a presidential material!! he is not strategic, and most of all, zitto ANAWASHWA-WASHWA SANA na tamaa zisizofichika hadi kuparamia lile mama fisadi ili apate pesa
 
Wakuu binafsi nimechoka kabisa kusikia Au kujadili utoto wake na uroho Wa madaraka! Personal Sioni potential aliyonayo zito mpaka tumzungumzie na kumjadili na kupoteza wakati wetu.

Yafuatayo Ni kweli kuhusu zito:

- Anajiamini na kujithaminisha kuliko ukweli.
- Ni Mroho Wa madaraka na mbinafsi.
- Hana nia Njema na taifa hili.
- Hana lolote, like any other looser.

Kama anabisha aasi Chama aone atakavyoporomoka, Huyu anatengeneza kaburi lake la kisiasa.

Zittoh Wewe Ni mnafiki, haufai.
 
Wakuu binafsi nimechoka kabisa kusikia Au kujadili utoto wake na uroho Wa madaraka! Personal Sioni potential aliyonayo zito mpaka tumzungumzie na kumjadili na kupoteza wakati wetu.

Yafuatayo Ni kweli kuhusu zito:

- Anajiamini na kujithaminisha kuliko ukweli.
- Ni Mroho Wa madaraka na mbinafsi.
- Hana nia Njema na taifa hili.
- Hana lolote, like any other looser.

Kama anabisha aasi Chama aone atakavyoporomoka, Huyu anatengeneza kaburi lake la kisiasa.

Zittoh Wewe Ni mnafiki, haufai.

Zito ana uwezo wa kujenga hoja vizuri sana. tatizo ni hiyo kasoro ya superiority complex aliyo nayo. He believes he is knowledgeable than anybody. katika mambo haya ya vyama team work is very important for a success. Apunguze power mongering. Sawa kila mwanadamu ana hulka ya kutaka madaraka, lakini not at the detriment of the many. kama hakuna hatua za makusudi ataiua CDM, na CCM watampokea kwa kumbeza!!
 
yaani mwandishi umechoaka km mimi...........
ZITTO JANGA LA CDM NA TAIFA NI MTU HATARI SN!
 
Ukweli Wa Zitto:

Miezi ya nyuma nilileta hii mada hapa jukwaani lakini kwa bahati mbaya MODs waliinyofoa dakika 20 baada ya kuiweka. Sina budi kurudisha hii mada baada ya sakata la Zitto Kabwe, Nassari, Halima Mdee pamoja na gazeti la Mwananchi. Kwa muda wa miaka kadhaa sasa, nimekuwa katika tasnia ya habari na lazima nikiri kwamba mengine yanayofanyika katika hii tasnia ni ya kukatiza moyo hasa kazi za wanahabari zinapoingiliwa na wanasiasa. Kwetu sisi wanawake inakuwa ni vigumu sana kukataa kutii haya maagizo ambayo mengine unaona kabisa ni za vitisho

Zitto Kabwe, January Makamba, Bernard Membe na hata Ngeleja kwa siku za nyuma alishiriki sana katika kuingilia kazi za waandishi. Kinara wao akiwa Zitto January na Membe. Hawa viongozi hasa Zitto wamezoea sana kujiandikia makala na hata habari kisha kumlazimisha mwandishi kuzichapisha ukurasa wa mbele kwa gharama yoyote ile. Wanatoa hela nyingi sana kwa waandishi na wahariri. Mbaya zaidi ni kwamba hawa viongozi wanajitengenezea kashfa au kutoka ndani ya vyama vyao.

Matokeo yake kesho wanaitisha waandishi tena kukanusha (kashfa) zao za kujipikia wakati ni wao ndio chanzo cha hizo habari. Lengo lao kubwa ni kutafuta huruma kutoka kwa umma wa kitanzania kwa vitu ambavyo havipo.

Kinachonishangaza ni kwa nini mtu ajichafue kwa kujitengenezea kashfa maadui feki ndani ya chama chake heti ndio wanaomchafua kumbe ni yeye mwenyewe alafu kesho yake akane hizo taarifa? Nadhani tunaelekea kubaya hawa watu wakiendelea nah ii tabia. Moja ya habari hizi ni zile zinazomlaumu Mbowe kam mtazikumbuka..

nawakilisha
 
Zitto ni kirusi hatari sana kwa ustawi wa CDM! Hafai hata kwa mbolea!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom