Kazi tunayo sana watz. Kupata kiongozi ambaye yupo yupo ladhi kufa kwajiri ya wananchi. Mimi kama kijana bado nina wasiwasi na hawa vijana wenzetu ambao wapo kwenye siasa kama wanania ya dhati kuleta mabadiliko au wanatumia mgongo kujinufaisha.
Je kunamtu anaweza simama kwamba ni msafi 100% kati ya hao wote wasemwao kila siku kwenye magazeti yetu? Wanatumia magazeti na redio mbalimbali kujitangaza na kutufanya sisi raia kutopata nn wanakitaka.
Kwani wanashindwa nn kupambana na matatizo tulio nayo leo hii, Madaktari, Walimu, Madini yetu yana chukuliwa bila manufaa yeyote, mbuga zetu ndo balaa kabisa halafu tunakaa na kusema mambo ya Uraisi kweli? Wanasema lisemwalo lipo nakama halipo basi laja.
Hivi tunafaida gani yakuwa na madini, gesi, mafuta (wanasema wanafanya uchunguzi wakati wanachukua na kupeleka nje), Hakuna uzalendo kabisa ktk nchi hii. Mimi nalia na wananchi wa vijijini ambao wanadanganya sana kwa maneno matamu wakati hakuna msaada wowote.