Updates zoezi la kuzima simu bandia

Updates zoezi la kuzima simu bandia

Hata mimi ninayo simu nagu moja ni fake lakini bado inapiga mzigo , network inasoma freeesh
 
Hakuna kitu kama hicho...hawezi kuzimahata simu feki zina IMei feki pia, wakiamua kuzima basi jue hata original zinaweza kuzimika na kuleta madai ya kibiashara...ukizima simu ya mtu mfanya biashara ana haki kudai fidia kubwa tu
Isee huu uanasheria pori utaimaliza tanzania aisee.
 
''Nlikutuma uwashe simu.. si ungesubiri kwanza wiki mpaka hawa jamaa wapite!?''...
Dah! Hakuna namna ya kukwepa mizinga...hiki ni kipind kigum mnooo ,hata namba hazisomeki!!

#R.I.P sim ya Mchepuko Wangu#

BANGO
 
Nadhani zinazimwa kwa awamu maana wengine vimeo vyetu bado vinapiga kazi.!
 
Hiki ndicho kilicho tokea...
a0446268e60ab7b1edcca089b2a5a42f.jpg
 
Nina wasiwasi na uwezo wa mtambo wao wa kubaini simu fake. Yangu ilionyesha IMEI tofauti lakini bado inapiga mzigo kama Kenya. Hata majirani hapa wote waliokuwa na simfake bado zinasoma network. Au labda ilikuwa ni mkwara tu.
 
Mimi ninachofikiria hapa ni kuwa,kama simu yako imetengenezwa kwa wizi wa kutumia teknolojia ya simu nyingine hiyo itaendelea kupiga mzigo,mfano simu yako inaonyesha kuwa ni Tecno lakini teknolojia imetumika ya Samsung nadhani mitambo ya TCRA hapo haiwezi kuizima.lakini zile ambazo wamezitengeneza kimangumashi kwa kutumia teknolojia zao za kutunga zisizo na viwango ndio hizo zitakazozimwa.
 
Tcra wanachofanya ni kuchukua IMEI kutoka kwa makampuni yanayotengeneza simu kwa iyn nokia fake,samsung fake na simu fake kutoka big company km nokia corp,motolola and samsung ndo zitazimwa kwa wingi
 
PLEASE TCRA!! HII TAARIFA NINAYOTOA NIMEOTA LEO USIKU WA MANANE.
======================

Baaada ya mikwara mingi na vitisho vya kutosha juu ya kuzima simu Fake, ndugu zangu wanaofanya kazi TCRA walinialika jana usiku ili niende kujifunza kitu pale zoezi zima la kuzima network ya simu zote ambazo ni Fake likiendelea.

Basi nikaenda pale nikawa nasikilizia nione mambo yatakuaje japo nilikuwa sina imani maana wataalamu wote waliokuwepo pale ni wabongo.

Muda ulipofika jamaa wakaanza kurun program yao inayoitwa PVT (phone Violet Tracer).
Program ilirun pale zaidi ya masaa 3 bila hata mafanikio.

Basi ghafla yule CG wa pale akapigiwa simu na Baba Jescagate. Na maongezi yakawa hivi;

Baba Jescaget: We CG, hayo masimu ya hovyohovyo bado hamjayazima tuu?

CG: Mkuu mtambo umekwama na hadi sasa bado hatujajua tatizo ni nini?

Baba Jescagate : Hiiii wewe hujala chochote kotoka kwa wafanya biashara?

CG: Sijala Mtukufu Mkuu.

Baba Jescaget : Basi ngoja nitafute kaziara kokote hata kakwenda Mskiti wa pale Mbagara. Nikifika huko niwaambie watanzania kwamba mimi Magu siwezi kuzima simu za watanzania wanyonge ambao hawana chochote. Nitawafuatilia wafanya biashara wote wanaoingiza simu bila ushuru maana ni wahujumu uchumi na nilazima nilale nao mbele kwa mbele.

Tanzania ya Magu ni Tanzania ya wanyonge na walifikili nitakuwa nao.

CG: Propaganda nzuri sana hiyo mkuu na utakuwa umetuokoa na Aibu hii.

Baba Jescaget : Haya lala salama na mniombee.

==========$$$======

Ghafla ndikastuka kumbe ulikuwa muda wa kula daku.

Nikakimbilia kucheck simu ya mtu wangu iliyokuwa fake bado inasoma Network. Basi nikahisi hii ndoto itakuwa ya kweli.

By
Kwenyula.
 
Back
Top Bottom