Updates: Hukumu kesi ya Prof Mahalu; ashinda kesi dhidi yake!

Hukumu ndio imeshatolewa lets move on , kuna makosa mengine magumu kuyabaini mahakamani kwa kutumia vielelezo vya Tanzania ndani ya mahakama ya kitanzania wakati kosa limefanyika ughaibuni. Labda hao ma attorney wa serikali wajipange upya in the future maana inaonesha walikumbana na changamoto nyingi sana kwenye hii kesi.
 
Wanafungwa wezi wa kuku bana,sio mtu na fedha yake,kama fedha haiwezi kukutoa kwenye matatizo basi fedha hiyo haina maana.
 
Mkuu kuwa na invoice mbili zenye kiasi kinachotofautiana kwa transaction moja bado nashindwa kujua ameponyokaje.

Jiulize hv hizo invoice mbili hata kama aliziandaa yeye ilikuwaje waziri na Rais wazijue na wakubali hela ilipwe nyingi na ile itakayotumika italy iwe na pesa kidogo? Yet bado mahalu awe na kesi peke yake? Angekutwa amechakachua yeye kama yeye hapo sawa ila haikuwa hivyo ndugu, Mh. Rais alishasema akili za kuambiwa changanya na zako.
 
Unataka kutuambia hawa wote rais amewaonea?

Liyumba visasi, Yona visasi, Ballali visasi, Jeetu Patel visasi, Mramba visasi, Maranda visasi, Farijala visasi, Mgonja visasi?

Kwanini mnaona kama mtu kufikishwa mahakamani ni kitu kibaya? mimi nilitegemea hao wahusika washukuru kwamba wamefikishwa mahakamani ili wapate nafasi ya kujisafisha.

Sasa nijibu nini wakati jibu lipo tayari kweupeeeeee nilisema kitu najua mkuu wangu... sasa hata mate niliyotema chini hayajakauka si umeona matokeo? Hutaki potezea basi!
Ebu nambie kwa nini hukuongeza jina la Andrew chenge kwenye orodha yako na wala jina la Rostam halipo pia? Jina la Manji umesahua linaandikwaje?
Mjinga haaimbiwi jibu ili ashughulishe akili zake.....
 
Mkuu kuwa na invoice mbili zenye kiasi kinachotofautiana kwa transaction moja bado nashindwa kujua ameponyokaje.

Kwa sababu Liwalo na Liwe!! Ulitaka afungwe wakati Dhaifu ni mutual inclusive wa saga zima?Na Hansad inajieleza dhahiri shahiri kwamba there were no mistake in the deal..JK ******
 
Jiulize hv hizo invoice mbili hata kama aliziandaa yeye ilikuwaje waziri na Rais wazijue na wakubali hela ilipwe nyingi na ile itakayotumika italy iwe na pesa kidogo? Yet bado mahalu awe na kesi peke yake? Angekutwa amechakachua yeye kama yeye hapo sawa ila haikuwa hivyo ndugu, Mh. Rais alishasema akili za kuambiwa changanya na zako.
Mahakamani watu huenda kutafuta haki. Ni haki transaction moja kuandaliwa hati za malipo mbili zenye kiasi cha malipo tofauti na hati zote zikawa valid? Hicho ndicho ninachotaka kujua bila kujali kuwa Mahalu alishirikiana na nani katika mchakato huo.
 
Kesi hii ni lazima Mahalu ashinde. Kwa mara nyingine mahakama imeingia kwenye kitendawili au kutoa haki au kusimama na aliyeianzisha mr dhaifu.
Tatizo la kikwete ni mtu wa visasi sana na amehusika sana kuitunga kesi hii na jambo hili ni dhahili wala halina kificho hata chembe.
Kweli kikwete ni dhaifu..

Mazingira ya kuwepo kwa matumizi mabaya ya ofisi yalikuwepo, ila suala kushinda na kutoshinda na jambo lingine. Sidhani kama kulikuwa na tatizo lolote la kufunguliwa kwa kesi hiyo.
 
Hii kitu inaweza kuwa ni stagemanaged na watu humu wanashangilia kama mazuzu.
Ndo kusema huyo jamaa alikua msafi sana au.
Eti jk amepimana ubavu na mkapa WAPI? Ingekua ndo masuala ya kupimana angesema mwacheni mkapa apumzike.suala la kiwira angechomoka vipi huyo mr clean.
Yaani humu kuna ushabiki wa ajabu sana na unakuta jitu zima na kitambi chake lenye wajukuu lakini mambo linayoshabikia ni upuuzi hasa.
 


Waandishi wa habari wakimfuata Balozi Profesa Mahalu akiwa pamoja na Mdogo wake Mirasi Rama wakitoka nje ya Mahakama ya Kisutu Mchana huu mara baada ya kushinda kesi iliyokuwa ikimkabili akidaiwa kununua nyumba ya Ubalozi wa Tanzania nchini Italia, Akisoma hukumu iliyosomwa kuanzia Saa sita leo na Hakimu Mfawidhi mkazi wa mahakama ya Kisutu Mh. Ilivin Mugeta imemtoa Balozi Profesa Mahalu katika hatia na kumwachia huru (PICHA NA PHILEMON SOLOMON WA FULLSHANGWEBLOG)

Balozi Profesa Mahalu akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kushinda kesi yake katika mahakama ya kisutu leo.

Wakili wa Balozi Profesa Mahalu Bw. Alex Mgongolwa akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya mteja wake kushinda kesili iliyokuwa ikimkabili kwenye mahakama ya Kisutu jijini Dar es salaam.

Balozi Profesa Mahalu katikati akitoka nje ya mahaka ya Kisutu huku akiwa ameongozana na mdogo wake Mirasi Rama kulia ni Wakili wa kujitegemea Mabere Nyaucho Marando.

Picha na Full Shangwe Blog
1859130880412241953-8397735442630508199

 
Hivi hamuoni saga yote ni mchezo wa kuigiza, changa la macho kwa Watanzania wakati WOTE lao moja?
 
Hii kitu inaweza kuwa ni stagemanaged na watu humu wanashangilia kama mazuzu.
Ndo kusema huyo jamaa alikua msafi sana au.
Eti jk amepimana ubavu na mkapa WAPI? Ingekua ndo masuala ya kupimana angesema mwacheni mkapa apumzike.suala la kiwira angechomoka vipi huyo mr clean.
Yaani humu kuna ushabiki wa ajabu sana na unakuta jitu zima na kitambi chake lenye wajukuu lakini mambo linayoshabikia ni upuuzi hasa.
Chini ya Marando kesi haikatizi nendeni mahakamani tena kuhusu ile tuhuma ya CDM na usalama wa Taifa
 
Mazingira ya kuwepo kwa matumizi mabaya ya ofisi yalikuwepo, ila suala kushinda na kutoshinda na jambo lingine. Sidhani kama kulikuwa na tatizo lolote la kufunguliwa kwa kesi hiyo.

Ilihitaji akili ya ziada ili kujua kuwa hakukuwa na haja ya kufungua kesi ambayo walijua watashindwa. Hata mtoto wa form two angeweza kutambua hili!
 
Hivi hamuoni saga yote ni mchezo wa kuigiza, changa la macho kwa Watanzania wakati WOTE lao moja?

Pia changa la macho kwa wafadhili kuwa kuna watu wameshtakiwa Tanzania kwa Rushwa...Sasa jitayarisheni ushindi wa kishindo kesi ya Mramba na wenzake
 
Back
Top Bottom