Hivi jamani kuna FISADI hata mmoja aliyewahi kushindwa kesi na akafungwa ama kunyang'anywa mali alizohujumu?.. nauliza tu maanake sijawahi kusikia maamuzi ya kesi yoyote ya juu mtuhumiwa alishindwa kesi.
Mkuu Mkandara, hivi umekaa nje ya bongo hadi kusahau mahakama zetu zinavyofanya kazi? Kushinda kesi inategemea una pesa kiasi gani na kama kama ni kesi inamhusu tajiri, watahongwa kuanzia mwendesha mashtaka, hakimu hadi mashahidi. Hii ndio taswira ya utamaduni wetu kama Taifa, na kwa taarifa yako mtu akipiga dili la mamilioni kazini watu humuona shujaa!
Tatizo ninaloona hapa, JK anataka aonekani haingilii uhuru wa mahakama vinginevyo wahujumu uchumi dawa yao ni kuwaweka KIZUIZINI na mali zao kutaifisha. Hapo hata wapambe wao watawakimbia.
Niliangalia kwenye TV baadhi wanamageuzi wa M4C wakimpongeza Prof. Mahalu kwa vile tu ameshinda kesi dhidi ya serikali wanayoipinga, sijui kama inamaanisha huyu bwana ndio amekuwa msafi?