Unazikumbuka nyimbo za shule ya msingi (e.i. std i - iii)?

Sichakachui tena charminglady
Ngoja namalizia kuongea na CUTE then nakuimbia wimbo mmoja then naongea na Madame B then nakuimbia mwingine halafu nasema faster
.................................................
Mbuga za wanyama wa Tanzania
Ya Kwanza ni Serengetiiii.....Ngorongoro...Manyara na Mikumi
Watanzania oyeeeeeeeee
.........................................................
sikujua kama kuna wakati uko so polite and so romantic like that.....:flypig: lala unono kwa leo kesho useme umeota nini ok
 
mpz umesoma miaka ipi 70's.80's,au kama mm 90's mana ndio izo au wewe hukusoma kitabu cha musa,neema,na baraka na mtakuja primaty school

hahaa,c unajua utofaut wa eneo na eneo bt nyimbo nying ni common!
 
Lol. kwa hizo nyimbo mbona wengi mnaonekana tu
watu wa umri fulani jamani, msinidanganye mimi lakini.

wimbo nakumbuka huu hapa:

Tanzania Tanzania
Nakupenda kwa moyo wote
Nchi yangu Tanzania
Jina lako ni tamu sana
Nilalapo nakuota wewe
Niamkapo ni heri mama wee
Tanzania Tanzania
Nakupenda kwa moyo wote.........
 
Jieleze jieleze,
jieleze jieleze,
jieleze jieleze ntajieleza mama,
Mimi hapa ni Madame,
Mama yangu ni Salima
Baba yangu ni Kikwete.
nshajieleza mama.

Yani huo mwimbo unan'koshaga sana shost Charm na mamito cacico.
tulikuwa tunakatikaje hapo sasa, je ule wa kuruka kamba wa ngurumo, ngurumo, mpaka maputo, sanda na ikweta mamaa ikwetaeee, aineme, ainuke, ainame salome........... nimesahau yeuwiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii tulikuwa tunapigwa na mama kila siku kuchelewa kurudi tuition ya mwalimu mndolwa mlimani primary! khaaaaaaaaa! kuruka kamba! we had some good times kwa kweli. morning chit chatters, morning my sugar Asprin!
 
Last edited by a moderator:
Lol. kwa hizo nyimbo mbona wengi mnaonekana tu
watu wa umri fulani jamani, msinidanganye mimi lakini.

wimbo nakumbuka huu hapa:

Tanzania Tanzania
Nakupenda kwa moyo wote
Nchi yangu Tanzania
Jina lako ni tamu sana
Nilalapo nakuota wewe
Niamkapo ni heri mama wee
Tanzania Tanzania
Nakupenda kwa moyo wote.........
Mamndenyi na huu, tanzania, tanzania
nchi yenye mali nyingi, watu wengi wa ulaya,
wanaililia sana, nimeona ndege wengi,
chini kukatia fora, wanipendeza mlio,
kama mtoto wa nyumbani, ngolo ngololie, ngolo ngololie! khaaaaaaaaaaaaaaaaaa, happy today kwa kuimba hizo nyimbo za uzalendo! watoto wetu sasa hivi watunge za mafisadi kha!
 
Last edited by a moderator:
beibe nasty, Madame B, Erickb52, Raiamwematz Kaizer, Acha Uvivu jaman utoto wa enzi zetu ulikuwa raha kweli mpk nautaman cku moja wanirudishie haja kwa mwez 1 nichezee michezo yooote,niimbe nyimbo za kitoto zoote! watoto wa cku hz hata hawafaidi lolest. . .

Yaani Shost Charm,
watoto wa cku hz hawafaid chochote.

Michezo yote ya hatari tulikuwa tunaicheza sisi enzi zetu: Kujilipua,
Ukuti,
Kibaba baba,
Kuruka majoka,
Kubaka balale,
Kutega kambale,
Kuchimbua Nyotera(viazi vitamu vinapoanza kuchipua),
Kupitia madirishani enzi unatoroka pindi la Hisabati,
Kuwaimba watoto wa walimu kwenye mchaka mchaka.

DA...!! UTOTO RAHAAAA...!!!
Aaagrrhhh...!!!
 
Last edited by a moderator:
itv ndio imeanza mwaka 94, tunaimba class wanawake kuweni wenye furaha, na raha, wakai wote, popote na jessy!
jessy, pedi mpya za kike za jessy, ni nyororo raha kuvaa na kupa kinga thabiti.
wakati wote, popote, na hazina mikanda!
khaaaaaaaaaaaaa! mwalmu akitusikia ni kupiga magoti juani lol! we used kuenjoy!
 
Huna mambo,
Huna nyimbo,
Subiri fimbo.

Anaekubania hayo Mambo unamjua sana,
basi tu.
mambo ninayo tena mazito..katu huwezi kuyabeba bimkubwa..
nina nyimbo mpaka zakumlaza NGAMIA CHINI
fimbo hapa ipo...ni 7" tu ila inachapa mbaaaya.
unataka?
 
Back
Top Bottom