Unakumbuka nini miaka ya 90's kushuka chini?

Unakumbuka nini miaka ya 90's kushuka chini?

Bea Simba, malota soma, DEO njohole, Nico njohole, Raphael Paul, RAMADHANI Lenny , DEO mkuki, peter tino, gebo peter, MOHAMED mwameja, kichochi lemba, HAMISI kinye, zamoyoni mogella.
Mkuu yaani mawazo yangu yameenda mbali sana.hebu endelea kutiririka.
 
Kitabu cha English cha kina baraka, Musa, Neema, Mr& Mrs Daud. Musa na Neema walikuwa wanasoma shule ya msingi mtakuja.
 
Enzi za primary tuliaminishwa kuna 'vinyonya damu'
 
Nakumbuka mama alinunua feni akakodi tax wakati anarudi home akashukia mtaa wa tatu kutoka home akihofia dereva tax akawa jambazi au akawaelekeza majambazi tunapoishi halafu usiku wakalifata, maza alifika na majasho kwa kubeba feni kutoka mtaa wa tatu hadi home ikabidi kulipiga test awashe ajipulizie, nakumbuka bei ya feni na kukodi tax hakukuzidi sh 10, uwezi amini lile feni hadi ilibidi tulitupe tu mwaka 2010 maana halikuharibika lilikuwa kampuni ya National
 
Ahah nakumbuka enzi hizo kila ijumaa wanakuja wana mazingaombwe wakina power nyati wakikosa au basi tunaletewa ngongoti au joyce wowowo au kijebakiingilio sh5. Wale wa shule ya msingi mashujaa miaka ya 80's sinza wananielewa.
 
Nakumbuka mwaka 1985 tukiwa darasa la 6 Muhimbili Primary school na akina Dj Bonny love na Kibonde, alikuja Mwl. Nyerere shuleni kwa shuhuli ya mwenge. Tukaambiwa usipoimba wimbo wa taifa utakufa.. hiyo bidii ya kukariri huo wimbo sitakaa nisahau..
!! Nimecheka sana aisee watoto wa zamani walikuwa wanadanganywa sana
 
Back
Top Bottom