Unakumbuka nini miaka ya 90's kushuka chini?

Unakumbuka nini miaka ya 90's kushuka chini?

Ndiyo na ndilo chimbuko la neno dala dala. Kila ukipanda uda popote pale dala dala.
Ni kwamba asili ya neno daladala ni wakati wa Mwl Julius Nyerere wakati shilingi tano likuwa sawa na dollar moja ya kimarekani hivyo shillingi tano ikawa inaitwa dala na wapiga debe enzi hizo walisema dala -dala-dala kumaanisha kuwa nauli ni dala moja(gwala/shilingi tano) na ndipo lilipoibuka neno daladala.
 
Kitabu cha English cha kina baraka, Musa, Neema, Mr& Mrs Daud. Musa na Neema walikuwa wanasoma shule ya msingi mtakuja.
Hiyo shule ipo pale Kunduchi mpaka leo haikuwa shule ya kubuni tu
 
Wakina mama walikuwa wananunua watoto yaani wadogo zetu Muhimbili au ocean road.
 
Siwezi kusahau vita ya wahujumu uchumi chini ya Waziri Mkuu Edward Moringe Sokoine
 
Operation Maalumu UHAI chini ya vijana wakakamavu wa JWTZ kulinda Tembo walikuwa wanauwawa na majangiri Selou Game Reserve.
 
Itifaki izibgatiwe,

Kuna mambo nmeyakumbuka wkt wa miaka 90's kuja 80's, kwanza kulala ilikuwa saa12 ukionekana nje umeumia. Sukari haikuuzwa dukani tulikuwa tunapanga foleni kununua sehemu fulani zinaitwa ugawaji. Tv mnatizama jumapili tu na ukiwa na TV lazima iwe na kibali.

Wewe unakumbuka nini?
Dah nakumbuka miaka hiyo ya 80's ckuku ya IDD na Pasaka tunajazana kwa Jani kununua bajia na mijeledi huku tunasubiri walioingia kuangalia picha ya kwanza Plaza cinema watoke tuingie picha ya pili 10:30 ya Disco dancer.Mambo ya mo town hayo.
 
Sikuwahi muona au msikia nyerere
Alipokufa ndio nikamjua
 
Nakumbuka wimbo wa" we are the world "(Au U. S. A- AFRICA) mwaka 1985 ulioimbwa ili kuchangia baa LA njaa barani afrika. Wimbo uliimbwa na wakali wa muziki wakina Michael jackson, Leonel Richie.,Diana Rose. Nilikuwa form one mawenzi Sec. Moshi. Siwezi kuandika yote bora niishie hapo.
 
Kweny uzi huu ndipo tutapowabaini watu wazima.
Kuna wengine watabaini mtego huu na kutochangia kumbukumbu zao ili tusiwajue kwamb watu wazima
Kwa nini ukwepe kuitwa mtu mzima (aged?)
 
Nakumbuka mwaka 1985 tukiwa darasa la 6 Muhimbili Primary school na akina Dj Bonny love na Kibonde, alikuja Mwl. Nyerere shuleni kwa shuhuli ya mwenge. Tukaambiwa usipoimba wimbo wa taifa utakufa.. hiyo bidii ya kukariri huo wimbo sitakaa nisahau..
Mmmh darasa LA sita duuh we Senior.shikamoo
 
Ndiyo na ndilo chimbuko la neno dala dala. Kila ukipanda uda popote pale dala dala.
Ndio yaani miaka hiyo ya 80 dollar moja ya marekani ilikuwa sawa na sh. tano ya Tz. Ama kweli kwa sasa shilingi yetu imeshuka thamani!!!
 
Ni kwamba asili ya neno daladala ni wakati wa Mwl Julius Nyerere wakati shilingi tano likuwa sawa na dollar moja ya kimarekani hivyo shillingi tano ikawa inaitwa dala na wapiga debe enzi hizo walisema dala -dala-dala kumaanisha kuwa nauli ni dala moja(gwala/shilingi tano) na ndipo lilipoibuka neno daladala.
Ndiyo na mimi ndivyo nilieleza kabla ya hii comment. Tupo wote. Hakupenda kugeuka jiwe kushu
 
Back
Top Bottom